Featured Post Today
print this page
Latest Post

MTOTO APIGWA NA BABA YAKE MZAZI NA KULISHWA KINYESI CHA MTU MZIMA:

HUYU NDIYE MTOTO ALIPIGWA NA BABA YAKE MZAZI NA KULISHWA KINYESI CHA MTU MZIMA: 



MWALIMU wa Shule ya Msingi Morotonga, wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara, Karata Mugunda, anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa, kwa tuhuma za kumpiga na kumlisha kinyesi mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10. 


Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Wilaya ya Serengeti, Samwel Mewama, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtoto huyo alilishwa kinyesi alichokuwa amejisaidia ndani ya nyumba yao.

Kwa mujibu wa Mewana, tukio hilo la kusikitisha lilitokea Agosti 14, mwaka huu saa 12 alfajiri.

“Chanzo cha tukio hili la kikatili ni mtoto huyo kujisaidia haja kubwa ndani ya nyumba, baada ya kuogopa kutoka nje usiku wa manane.

“Baada ya kujisaidia, baba yake ambaye ni mwalimu, alikasirika na kuamua kumwadhibu kwa kumchapa fimbo sehemu za makalio na kumsababishia majeraha ya kutisha.

“Pamoja na kumwadhibu kwa fimbo, alimlazimisha ale kinyesi chote alichojisaidia kisha akamlazimisha anywe maji kwa wingi,” alisema Mewana.

Akizungumzia jinsi alivyopata taarifa za tukio hilo, alisema ofisi yake ilipigiwa simu na mwalimu mmoja anayefundisha shule moja na mtuhumiwa.

Baada ya taarifa hiyo, alifuatilia ili kujua ukweli wake ndipo alipomkuta mwanafunzi huyo akiwa amejeruhiwa vibaya makalio yake.

“Kwa kweli nilimkuta ana hali mbaya, kwa hiyo nilichokifanya nilimchukua na kumpeleka Kituo cha Polisi Mugumu nikapewa PF 3 kwa ajili ya matibabu hospitalini,” alisema.

Aliongeza kwamba, baada ya polisi kupata taarifa hiyo na kushuhudia majeraha aliyokuwa nayo mwanafunzi huyo kupitia dawati lao la kijinsia, walikwenda kumkamata mwalimu huyo ili hatua zaidi ziweze kufuata.

Daktari wa Zamu katika Hospitali ya Nyerere DDH, Dk. Ohoka Joseph, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo.

Alisema mtoto huyo alijeruhiwa vibaya kwenye makalio yake na kwamba ameathirika kisaikolojia.

“Huyo mtoto ameathirika kisaikolojia, kwa hiyo, kuna haja akafanyiwe uchunguzi kutokana na athari za kipigo na tukio alilofanyiwa.

 

0 comments

Madiwani waliotimuliwa CCM wadai kuwa wako tayari kuhamia CHADEMA.

Madiwani waliotimuliwa CCM wadai kuwa wako tayari kuhamia CHADEMA.

 


MADIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofukuzwa katika Manispaa ya Bukoba, wamesema wako tayari kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kama chama chao kitaendelea na msimamo wa kuwafukuza. 


Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu jana, mmoja wa madiwani hao ambaye alikataa kutaja jina na kata yake, alisema wako tayari kuhamia Chadema muda wowote kama hawatarudishiwa uanachama wao.

Alisema, madiwani wote waliofukuzwa wana msimamo mmoja ambapo wanasubiri vikao vya Kamati Kuu ya CCM ili wajue hatima yao.

Kwa mujibu wa diwani huyo, wanachokifanya wao ni kutetea maslahi ya taifa na wananchi waliowapigia kura, wala siyo kulinda biashara za watu hata kama wanaungwa mkono na uongozi wa CCM.

Msimamo wa madiwani hao, umekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, kuwakaribisha Chadema madiwani wote waliofukuzwa katika manispaa hiyo na kwamba kama wakijiunga na chama hicho, watafundishwa siasa za mageuzi.

Mbowe aliwakaribisha madiwani hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Uhuru Mjini Bukoba juzi, katika mwendelezo wa mikutano ya chama hicho ya mabaraza ya wazi yanayojadili rasimu ya Katiba mpya.

Katika mazungumzo yake, Mbowe alikwenda mbali na kusema chama chake kiko tayari kushirikiana na kiongozi wa CCM anayepinga ufisadi kama anavyofanya Mbunge wa Bukoba Mjini, Khamis Kagasheki.

Alipoulizwa kama wamepata mawazo ya kujiunga na Chadema, baada ya kauli ya Mbowe, diwani huyo alisema wao walishakuwa na mawazo hayo, lakini kauli ya mwenyekiti huyo imewaweka huru zaidi.

“Si kama tumeamua sasa, mawazo ya kuhamia Chadema tulikuwa nayo baada ya uongozi wa mkoa kutangaza kutuvua uanachama, lakini kwa kauli ya Mbowe, kutukaribisha rasmi Chadema, ametujengea moyo zaidi.

“Tatizo letu na meya linafahamika kwamba, ni ufisadi wake tulioulalamikia tangu mwaka jana kwenye vikao vya baraza la madiwani, hatukusikilizwa badala yake tunaonekana wasaliti wa chama.

“CCM wanapaswa kujua kwamba, hoja za wapinzani zikiwa sahihi wananchi wanawaunga mkono, vivyo hivyo na sisi hatuwezi kubeza hoja zao kwa sababu tu ni wapinzani, tutaonekana watu wa ajabu.

“Kimsingi, tumefarijika na kauli ya Mbowe, baadhi yetu tulikuwapo katika mkutano wake jana (juzi) pale Uwanja wa Uhuru, ni suala la muda tu mtasikia Bukoba imezaliwa upya,” alisema diwani huyo.

Balozi Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (CCM), anatajwa kuwa na uhasama wa kisiasa na kada mwenzake, Anatory Amani ambaye awali wawili hao walikuwa na ushirika wa karibu.

Alipotakiwa kuzungumzia suala la kufukuzwa kwa madiwani hao, Kagasheki alisema yeye hakuwepo katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kilichowavua uanachama.

Kuhusu taarifa za kutoelewana na Amani, alisema kila mmoja amekuwa na mtazamo wake juu ya mvutano huo.

“Kila mtu ana maoni yake, siwezi kuzuia hisia na maoni ya watu wengine, kila mtu anaweza kutoa maoni atakavyo, ngoja watu waseme,” alisema Kagasheki.

Madiwani wanane waliofukuzwa wanatuhumiwa kushirikiana na wenzao wa upinzani kusaini hati maalumu na kuiwasilisha kwa mkurugenzi wa manispaa, wakimtaka aitishe kikao ili wapige kura ya kumng’oa madarakani Meya Amani.

Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera kilichokaa Agosti 3 mwaka huu, kiliwafukuza uanachama na uongozi madiwani hao akiwamo Mwenyekiti wake wa Wilaya ya Bukoba, Yusuph Ngaiza na Diwani wa Kata ya Kashai.

Wengine waliofukuzwa ni Diwani wa Kata ya Buhembe, Alexander Ngalinda, Samwel Ruhangisa (Kitendaguro), Dauda Kalumuna (Ijuganyondo), Deus Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe), Richard Gasper (Miembeni) na Murungi Kichwabuta ambaye ni Diwani wa Viti Maalumu.


-Mtanzania 

0 comments

DR.SLAA AWAASA WATANZANIA KUHUSU KATIBA .

DR.SLAA AWAASA WATANZANIA KUHUSU KATIBA .

 

 Elizabeth Kilindi,Tanga
KATIBU  Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Dr Willbroad slaa amewaasa watanzania watambue kuwa katiba ni uhai wa Taifa hivyo wawe huru kutoa maoni ili baadae iweze kuwatetea na kuwalinda.

Dr. Slaa alisema  hayo katika mkutano wenye lengo la kukusanya maoni ya katiba mpya iliyofanyika katika viwanja vya Tangamano jijini hapa  ikiwa  maelfu ya wananchi walikusanyika kutoa maoni ambapo amesema chama hicho kitakusanya maoni si chini ya milioni tano ili kuyapeleka kwa  Jaji Warioba.

Aidha alisema chama chake kimeamua kukusanya maoni kwani katiba si mali ya chama bali ni ya watanzania wenyewe hivyo wameona ni vyema kuwakusanya kwa pamoja kutoa maoni yao ambayo ni haki ya kila mtanzania.

Katibu huyo alisema kuwa wenye mawazo ya kufanana wanauwezo wa kutengeneza katiba hivyo tunaitaji katiba  ambayo itawalinda watanzania na wala sio itakayolinda chama chochote cha siasa.

Katika atua nyengine Dr Slaa alisema katika katiba ya sasa imetumiwa vibaya na viongozi wa sasa walioko madarakani na pamoja na kutowachukulia hatua  wanaovunja maadili kwa kuiba rasilimali za umma.

Sambamba na hayo aliweza kuongelea umuhimu wa serikali tatu ambapo alisema kuwa itapunguzia ghalama za uendeshaji wa serikali kwa kuokoa fedha nyingi kwani asilimia ya wabunge na mawaziri itapungua kwa kiasi kikubwa.

Pia aliwata watanzania  kuacha woga katika kudai haki kwani kufanya hivyo ni kutojitendea haki na hata mungu anakataza.

Naye mjumbe wa kamati kuu wa chama cha demokrasia na maendeleo{chadema} Mabere Marando alisema kuwa watahakikisha kwa kila njia kuwafikiwa watanzania na kuwaelewesha rasimu ya katiba mpya na msimamo wa chama hicho.

Hata hivyo alisema kuwa chama hicho kitawafikia wananchi katika maeneo yao kuwaelewesha na kupata maoni na vyema kusema nini wanataka kiwepo katika  katiba hiyo mpya.

0 comments

AFANDE MAPEMBE YUPO HAI TANGA.

MCHEKESHAJI MAARUFU HAPA NCHINI KUTOKA KUNDI LA VITUKO SHOW HALI TETE KWA GONJWA LISILOTAMBULIKA !.

 ''Afande Mapembe'' (Baba Kundambanda).
 
KWA wadau wa vichekesho hapa nchini nadhani walio wengi wanamfahamu msanii huyu kutokana na umaah
iri wake wa uchekeshaji kwa swaga za kimakonde, Wengi mnamtambua kwa jina ''Mapembe'' almaarufu ''Baba kundambanda'', Hususani wale mnaofatilia kipindi cha ''VITUKO SHOW'' kinachorushwa na runinga ya ''CHANNEL TEN'' Kila siku ya alhamisi saa mbili na
nusu usiku au wale mnaofatilia filamu za vichekesho zinazoandaliwa na kampuni ya Al-Riyamy Production chini ya mkurugenzi wa kampuni hiyo ''Alphan ''Nassoro Abdala''. 


Baba kundambanda yuko hoi bin taaban kupitia ugonjwa ambao haujatambulika mpaka sasa.

Akiwa kambini Jijini Tanga huko wasanii wa kundi hilo walikoweka kambi ya takribani miaka miwili sasa,.
 
Wasanii hao wa kundi la ''VITUKO SHOW'' wakiwa katika maandalizi ya kipindi na filamu za vichekesho, ndipo mwenao alipoanza kuumwa gafla na kuzidiwa !.  mpaka sasa hali yake ni utata ila anaendelea kufatilia vipimo mwenyezi mungu atamjalia atapona na kuendelea na kazi kama kawaida hivyo wadau na wasomaji wetu muoombeeni m/mungu amsaidie msanii wetu arudi katika hali yake ya kawaida ili azidi kuwavunja mbavu kama ilivyo ada. chanzo www.masainyotambofu.com
0 comments

CHELSEA YAUA 2-0

CHELSEA YAUA 2-0 

chelsea1 d853f
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesherehekea kurejea kwake Stamford Bridge kwa kuanza na ushindi wa mabao 2-0 katika Ligi Kuu ya England dhidi ya timu iliyopanda daraja msimu huu, Hull.
 
Kiasi cha miaka sita tangu aachane The Blues, kocha huyo maarufu kama Special One alifurahia mapokenzi mazuri na mchezo mzuri wa timu yake akirejea nyumbani.

Haikuwa kazi rahisi kwa Chelsea kushinda, baada ya mkwaju wa penalti wa Frank Lampard dakika ya sita kuokolewa na Allan McGregor na sheria ya teknolojia kwenye mstari wa goli ikachukua nafasi yake wakati kipa huyo wa Scotland alipookoa mpira wa kichwa wa Branislav Ivanovic na kudhaniwa ni bao dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza, ikisahihisha si bao.

Pamoja na hayo, Chelsea ilipata mabao yake yote kipindi cha kwanza kupitia kwa Oscar dakika ya 13 na Lampard dakika ya 25.
Kikosi cha Chelsea leo kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Lampard, Ramires, De Bruyne/Schurrle dk67, Oscar/van Ginkel dk85, Hazard, Torres na Lukaku dk75.

Hull City: McGregor, Elmohamady, Chester, Davies, Figueroa, Brady, Meyler/Huddlestone dk59, Koren, Sagbo, Graham/Livermore dk59 na Aluko/Boyd dk79.

 

0 comments

Kurasa za magazetini leo August 19 2013


Kurasa za mwanzo na mwisho magazetini leo August 19 2013.


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments

UJUMBE WA RAY C KWENDA KWA WANAOTUMIA MADAWA ZA KULEVYA!!



Haya ndiyo maneno ya Ray C mwenyewe ambayo yana ujumbe mzuri ndani yake,
 “Wote hawa tuliokaa hapa(picha hapo chini) tuliathirika na dawa za kulevya na tumepona
kwa kunywa dawa moja tu inayoitwa Methadone.
Inapatikana Muhimbili na Mwananyamala pekee na ni bure kabisa.
Tunamshukuru sana Mh Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutuletea dawa hii.Ningependa kuwashauri walioathirika wa dawa za kulevya iwe wewe,ndugu yako,rafiki,kaka,dada,mjomba,jirani au yoyote aliye karibu na wewe.Usiogope amua tu kwamba unataka kupona na nenda kanywe hii dawa utapona kabisa.”

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger