Featured Post Today
print this page
Latest Post

KAMATI YAPITIA USAJILI, NGASA KUCHEZEA YANGA

KAMATI YAPITIA USAJILI, NGASA KUCHEZEA YANGA

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea (sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya fedha hizo kwa Simba.
Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa fedha hizo.
Vilevile Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu usajili wa wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka klabu husika ziwe zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).
Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe kucheza hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali vya kufanya kazi nchini (work permits).
Kamati hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili kupata ripoti za pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi Agosti 22 mwaka huu na kutoa uamuzi kwa pande ambazo hazikuafikiana.
UCHAGUZI TFF SASA KUFANYIKA OKTOBA 27
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuzingatia mamlaka iliyonayo katika kifungu cha 10(6) cha Kanuni za Uchaguzi za TFF inasogeza mbele tarehe ya uchaguzi wa TFF kutoka Oktoba 20 mpaka Oktoba 26 na 27 mwaka huu.
Sababu za kusogeza mbele uchaguzi ni kutokana na ukweli kuwa Oktoba 20 mwaka huu uongozi wa TFF utakuwa na shughuli nyingi za maandalizi ya mechi ya Simba na Yanga, na hivyo haitawezekana kusimamia shughuli za Mkutano Mkuu wa Uchaguzi kwa wakati mmoja na mchezo huo.
Siku ya mwisho ya kampeni itakuwa Oktoba 25 mwaka huu. Ukiondoa  mabadiliko hayo ya tarehe ya uchaguzi wa viongozi wa TFF, ratiba ya mchakato wa uchaguzi na itabaki kama ilivyotangazwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF katika mkutano wake na waandishi wa habari Agosti 24 mwaka huu.
Pia Kamati imeamua kuwa uchaguzi wa Bodi ya Ligi utabakia kuwa Oktoba 18 mwaka huu kama ilivyopangwa awali.
Kamati imesema inaamini wahusika wote watapokea vizuri mabadiliko hayo na inasikitika kwa usumbufu utakaosababishwa na mabadiliko hayo.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
0 comments

Mpiganaji Gracemo Bambaza Afariki Dunia



Mpiganaji Gracemo Bambaza (pichani) aliyekuwa mwandishi wa habari za michezo aliyekuwa akikitumia kituo cha Radio cha wapo Radio cha Kurasini jijini Dar es Salaam /Pride Fm ya Mtwara na  kituo cha ABM ya  Dodoma na kufanya Mafunzo ya Habari akiwa katika masomo yake ya Diploma katika kituo cha Channel 10 amefariki Dunia jana Agosti 14, 2013.  
Marehemu alikuwa akisumbuliwa na Saratani ya Koo mpaka mauti yanamkuta katika Hospitali ya Ocean Road. Marehemu alizaliwa Mwaka 1973 Mkoani Kagera na amesafirishwa leo Agosti 15, 2013 kwenda Karagwe mkoani kagera kwa mazishi. Marehemu ameacha Mke na mtoto Mmoja .
Kwa Taarifa zaidi wasiliana na Dada wa Marehemu 
Mary Mihigo 
0713 64 49 41 

0 comments

JESHI LA POLISI MKOA WA TANGA LINAWAKA WATU WAWILI




                          Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga.


 Na  Peter Mtulia.

Watu watatu wamefariki dunia ktk matukio tofauti ya ajali yaliyotokea maeneo tofauti jijini Tanga.

Ktk tukio la kwanza Jeshi la polisi mkoa wa Tanga linamsaka dereva wa gari aina ya fuso kwa kosa la kumgonga na kusababusha kifo cha mwendesha pikipiki aina ya farcon yenye namba za usajili T-196 BLT aliyetambulika kwa jina la Manento Juma mwenye umri wa miaka 20 pamoja na abiria wake Mwajuma Athumani mwenye umri wa miaka 30.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa polisi mkoani hapa Costantino Masawe amesema kuwa ajali hiyo imetokea mnamo siku ya alhamisi katika eneo la mambo leo  majira ya saa mbili usiku ambapo  gari hilo lilikuwa likitokea Muheza kuelekea Segera na kugongana uso kwa uso na pikipiki hiyo na kusababisha  vifo vya watu hao.

Ktk tukio la pili Mwendesha pikipiki aina ya toyo yenye namba za usajili T-445 CJJ aliyejulikana kwa jina la Asnali Saidi mwenye umri wa miaka 20 amefariki dunia  baada ya kugongwa na gari aina ya fuso katika barabara ya pangani  Tanga.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda Masawe amesema kuwa ajali hiyo imetokea mnamo siku ya ijumaa majira ya saa sita usiku katika   maeneo ya Tanga sisi na dereva wa gari hilo ametoroka kusikojulikana

Kamanda Masawe amesema kuwa jitahada za jeshi la polisi mkoa wa Tanga kuwasaka madereva wa magari hayo  zinaendelea ili kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

0 comments

VITA YA NAMBA YAANZA COASTAL UNION.

VITA YA NAMBA YAANZA COASTAL UNION.

(Kocha Mkuu wa Coastal Union,Hemed Morroco juu kulia akizungumza na wachezaji wa timu hiyo jana mara baada ya kumalizika mazoezi yao ambayo yanaendelea uwanja wa Mkwakwani)

NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
KIKOSI cha Coastal Union ya Tanga kimeonekana kuwa tishio sana baada ya kutokea vita ya wachezaji kugombea namba kutokana na kuwepo wachezaji wengi wenye uwezo na hivyo kupelekea ushindani kwenye kugombea nafasi za kucheza kwenye mechi.

Coastal Union ni miongoni mwa timu ambazo msimu huu zimefanya usajili wa kutisha na hivyo kuanza kuonekana makali yake kwenye mechi mbili za majaribio ambapo waliweza kuichapa Simba na URA ya Uganda na mwishoni mwa wiki kutoka suluhu pacha na 3 Pillars ya Nigeria. 


Kocha Mkuu wa timu hiyo,Hemed Morroco aliiambia Tanga Raha kuwa anafarijika na kitendo hicho ambacho msimu uliopita hakikuwepo na kueleza kutokana na hali hiyo anaimani watafanya mambo makubwa kwenye msimu mpya wa ligi kuu.

Morroco alisema ushindani unaonyeshwa kwenye mazoezi unampa faraja kutokana na wachezaji kujituma na kuwa na nidhamu ya hali ya juu na kueleza hali hiyo inampa jeuri ya kuchukua  pointi tatu muhimu kwenye mechi yao ya ufunguzi wa Ligi kuu Tanzania bara dhidi yao na JKT Oljoro itakayochezwa Agosti 24 katika uwanja wa Sheirh Amri Abeid mkoani Arusha.

Morroco alisema mechi za majaribio walizocheza zimempa mwanga mzuri wa kujua kikosi chake kinahitaji kitu gani kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi kuu.

Alisema kutokana na usajili mzuri ambao ulifanywa na timu hiyo matumaini yake ni kuchukua ubingwa wa ligi hiyo ili kuweza kucheza kombe la shirikisho kwani hayo ni malengo yake ya kucheza kombe hilo siku zijazo.
   
Morroco alisema wanatarajia kuondoka mkoani hapa siku moja kabla ya mechi yao na Oljoro JKT na kueleza watakachokwenda kukifanya mkoani Arusha ni kufuata pointi tatu muhimu.
 
;Chanzo, tangaraha.blogspot.com 
0 comments

Simba, Yanga huenda zikavuruga Uchaguzi Mkuu wa TFF

Simba, Yanga huenda zikavuruga Uchaguzi Mkuu wa TFF

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ili kufanya uamuzi wenye manufaa kwa washabiki wa mpira wa miguu baada ya tarehe ya uchaguzi aliyotangaza kuingilia na mechi ya watani wa jadi (Simba na Yanga) ya Ligi Kuu ya Vodacom.
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, pichani
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, aliiambia Handeni Kwetu Blog kuwa, Sekretarieti ya TFF imepokea maoni kutoka kwa wapenzi mbalimbali wa mpira wa miguu wakiomba matukio hayo mawili (Uchaguzi wa TFF na mechi ya Simba na Yanga) yafanyike katika siku tofauti.
Wakati Kamati ya Uchaguzi inatangaza uchaguzi kufanyika Oktoba 20 mwaka huu tayari ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom ilikuwa imeshatoka, na ikionesha kuwa timu ambazo zina historia ya kipekee katika mpira wa miguu zitacheza siku hiyo.

Sekretarieti imelazimika kumwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi kwa vile yeye na kamati yake ndiye wenye mamlaka ya kuitisha Mkutano wa Uchaguzi. Huko nyuma TFF imeshafanya mikutano huku kukiwa na mechi za timu ya Taifa (Taifa Stars), jambo ambalo liliwezekana kutokana na mikutano hiyo kuwa na ajenda moja tu.
Tayari Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Hamidu Mbwezeleni ameitisha kikao cha kamati yake kujadili barua hiyo ya sekretarieti.
0 comments

MAMA AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME PAMOJA NA KIUMBE KINACHOFANANA NA CHURA

BREAKING NEWSSS MAMA AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME PAMOJA NA KIUMBE KINACHOFANANA NA CHURA WILAYANI CHUNYA

Mtoto aliyezaliwa pamoja na kiumbe cha ajabu kinachofanana na chura
Mtoto akiwa na afya tele
Hiki ndicho kiumbe kilchotoka tumboni pamoja na mtoto mchanga kwa mama Matrida picha hii mara baada ya kutenganishwa na mtoto huyo
Kushoto ni Matrida Erick (20) aliyejifungua mtoto pamoja na kiumbe hicho cha ajabu akiwa na mkunga Agripina Sikanyika aliyembeba mtoto wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kujifungua kwa mkunga huyo
Hapa ndipo  kwa mkunga Agripina Sikanyika Matrida alipojifungulia watoto hao
Mkunga huyo akionyesha mkeka unaotumika kuwatandikia wajawazito wanaokuja kujifungulia katika  kliniki yake


Mkunga akionyesha vibali vinavyothibitisha ruhusa aliopewa na Serikali kwa ajili ya kutoa huduma ya kuwazalisha akina mama wajawazito.

Mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la MATRIDA ERICK  mwenye umri  wa miaka ishirini mkazi wa magamba ,wilaya ya chunya ,amejifungua mtoto jinsi ya kiume na wakati huohuo na chura.

Mkunga aliyemzalisha bi AGGRIPINA SIKANYIKA mkazi wa MBUYUNI wilaya ya chunya amesema tukio hilo limetokea majira ya saa tisa alasiri agosti 13 mwaka huu,mara  mwanamke huyo kufikishwa kwa mkunga huyo na mumewe aitwaye BUNDALA JOSEPHAT ISANDU mwenye umri wa miaka thelathini na tano

MATRIDA amesema huo ni uzao wake wanne  na kwamba alishangazwa na kiumbe hicho ingawa wakati anajifungua hakupata tatizo  lolote na pia alifurahia kupata mtoto wa kiume mwenye afya na alisikitishwa kupata hicho kiumbe ambacho kilikuwa na miguu ya mbele yenye vidole vinne na miguu ya nyuma vidole vitano vya binadamu.

Kwa upande wake AGGRIPINA amesema mtoto alikuwa katika kondo lake na chura alikuwa katika kondo lake la nyuma la uzazi wa mwanamke huyo na pia ameeleza kuwa hilo ni tukio la tatu ambapo la kwanza  mwanamke alijifungua kichwa cha ng’ombe mwaka jana na la pili mwaka huu mwezi wa tano ambapo mwanamke alijifungua chura badala ya binadamu kwa hiyo hili ni tukio la tatu  hivyo hakushangazwa na tukio hilo.

Hata hivyo mume wa Matrida amesema katika familia yao hilo ni tukio la kwanza na kwamba limewashangaza.
Baada ya tukio hilo mkunga alimtafuta mwenyekiti wa kijiji cha MBUYUNI bwana CONRAD WAMBOKA ambaye alimtaarifu mtendaji wa kijiji MICHAEL SANZIMWA ambao walishuhudia tukio hilo na walimwamuru mkunga huyo kuondoa kiumbe hicho ‘’CHURA’’ kwenye kondo la uzazi.

Aidha chura hicho kilikufa na ndugu siku moja baadae ambapo ndugu walikabidhiwa na taratibu za mila zilifuatwa.
Baadhi ya ndugu wamehusisha kitendo hicho na imani za kishirikina zilizokithiri huko wilayani chunya.  

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger