Featured Post Today
print this page
Latest Post

MWILI WA WAZIRI WA FEDHA DK WILLIAM MGIMWA WAWASILI TANZANIA UKITOKEA AFRIKA YA KUSINI.

 
Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk.William Mgimwa umewasili nchi hii leo kwa ndege ya shirika la Kenya (KQ) na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue opamoja na Mawaziri mbalimbali na Wabunge. http://mrokim.blogspot.com
0 comments

YAW BERKO KUANZA KESHO MAPINDUZI



 Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema kesho atatoa nafasi kwa kipa Yaw Berko rais wa Ghana kuanza katika kikosi cha kwanza.


Logarusic raia wa Croatia amesema itakuwa nafasi nzuri kwa Berko kuanza ili aweze kumuona.
Simba kesho inashuka dimbani kuivaa KMKM katika mechi yake ya pili ya Kombe la Mapinduzi.

Akizungumza akiwa katika kambi ya Simba mjini Zanzibar, Logarusic alisema Berko na wachezaji wengine ambao hawakupata nafasi ya kucheza wataipata.

“Pia Humud, nitataka kumuona na ndiyo maana naitumia michuano hii kwa ajili ya kutengeneza timu.

“Hivyo nitajitahidi kuendelea kutoa nafasi kwa karibu kila mmoja ambaye ninaamini anastahili,” alisema.
0 comments

IVO ASEMA ANAFURAHIA MAISHA SIMBA SC…NI KAMA ALIKUWEPO KITAMBO SANA

IVO ASEMA ANAFURAHIA MAISHA SIMBA SC…NI KAMA ALIKUWEPO KITAMBO SANA

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
KIPA namba moja wa Simba SC, Ivo Mapunda amesema kwamba anafurahia maisha katika klabu hiyo na anatamani kuisaidia ishinde mataji zaidi, baada ya mwishoni mwa mwaka kuipa taji la kwanza, Nani Jembe.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY mjini hapa, Ivo alisema kwamba anafurahi namna anavyokubalika na kuheshimika kuanzia na benchi la Ufundi, wachezaji wenzake, viongozi na hata wapenzi wa Simba SC.
Anafurahia maisha Msimbazi; Ivo Mapunda amesema anajisikia kama alikuwepo miaka kadhaa Msimbazi

“Huu ni mwanzo mzuri kwangu, najisikia vizuri na ninafurahia kuwa hapa, lakini pia hii ni changamoto kwangu kuweza kuisaidia zaidi klabu hii, ili ishinde mataji zaidi. Kwa ushirikiano wa pamoja na wachezaji wenzangu, naamini tunaweza,”alisema Ivo. 
Kipa huyo wa zamani wa mahasimu, Yanga SC amesema anajisikia kama alikuwepo katika klabu hiyo miaka kadhaa iliyopita, kutokana na namna ambavyo amezoea maisha mapya haraka Msimbazi.
Amesema kwamba ana matumaini makubwa watabeba Kombe la Mapinduzi, michuano inayoendelea visiwani humo hadi Januari 13, mwaka huu.
“Tunahitaji hata sare dhidi ya KMKM ili kufuzu Robo Fainali, hilo tunaweza tena kwa kuwafunga kabisa. Tukifika Robo naamini kwa uzoefu wetu tunaweza kucheza hadi fainali. Na tukifanikiwa kufika fainali tutapigana tushinde turejee na Kombe Dar es Salaam,”alisema.
Ivo ameidakia mechi zote mbili za michuano hiyo Simba SC dhidi ya AFC Leopard ya Kenya na KCC ya Uganda ikivuna pointi nne, bila nyavu zake kuguswa hata kwa bao la kuotea. Baada ya Simba SC kuifunga Leopard 1-0 na sare ya 0-0 na KCC, itashuka tena dimbani kesho Uwanja wa Amaan, kumenyana na KMKM Saa 2:00 Usiku katika mchezo wa mwisho wa Kundi B.
Tayari Ivo amekwishaidakia Simba SC mechi tatu tangu ajiunge nayo mwezi uliopita akitokea Gor Mahia ya Kenya, ikiwemo ya Nani Mtani Jembe Desemba 21, mwaka jana dhidi ya mahasimu, Yanga ambayo Wekundu wa Msimbazi walishinda 3-1.
0 comments

RC ataka waandishi kuitangaza Tanga

 RC ataka waandishi kuitangaza Tanga





Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa amewataka waandishi wa habari mkoani Tanga kuutangaza mkoa wao kiutalii,  pamoja na vivutio vyake na kuacha kuandika habari ambazo hazina faida kwa jamii na Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi wakati akielezea maendeleo ya Mkoa wa Tanga mwaka 2013/14, Gallawa aliwataka waandishi wa mkoa huo kuitumia vyema kalamu yao kwa kuvitangaza vivutio vilivyoko mkoani humo.
Alisema Mkoa wa Tanga una vivutio vingi vya utalii, lakini vimekuwa havitambuliki ndani na nje ya nchi kutokana na kutotangazwa katika vyombo vya habari  na hivyo kuwa chanzo cha maendeleo kudidimia na Serikali kukosa mapato.
“Nashangazwa kuona Tanga ina vivutio vingi vya kiutali zikiwemo fukwe, mapango pamoja na mbuga ya wanyama, lakini sioni watalii wa ndani wala wa nje wanaokuja---tuweni wazalendo tupate maendeleo” alisema na kuongeza:
“Nadhani mko waandishi wa vyombo vyote hapa nchini na natambua kuwa mko mahiri katika kuandika na msomaji kuvutika kwa kile mnachokiandika,sasa kwanini hamuutangazi mkoa wenu kiutalii au mmeghafirika,nawakumbusha” alisema Gallawa
Gallawa alisema Mkoa wa Tanga umejaliwa kuwa na vivutio  vingi vikiwemo mbuga ya wanyama ya Saadan, Mapango ya watu wa kale yalioko Amboni pamoja na fukwe nzuri za bahari za Pangani.
Alisema endapo waandishi wa habari wataweza kuzitumia vyema kalamu zao kwa kuutangaza mkoa huo kiutalii maisha ya watu yataweza kubadilika ikiwa ni pamoja na biashara kuchangamka na Serikali kuweza kupata mapato kutoka kwa wageni.
Akizungumzia matajiri  kuzichangamkia fursa zilizoko mkoani humo, Gallawa aliwataka kuwa wabunifu na kuweza kuweka vitega uchumi na kuacha wageni kuwa waanzilishi na kuja kujutia baadae.
Alisema kuna fursa nyingi ambazo wenyeji wanaweza kubuni na kuweza kupata vipaumbele katika sekta nzima ya uwekezaji ikiwemo kujenga mahoteli pembezoni mwa bahari  na  usafirishaji wa watalii kwa njia ya anga mbugani.
Aliwataka watu hao wenye uwezo kuwa wabunifu wa miradi mbalimbali kwani jambo ambalo litaweza kuisaidia Serikali katika suala zima la maendeleo na kiuchumi

0 comments

Kijiji cha Msomela wilayani Handeni mkoani Tanga chapewa cheti cha ardhi yao

Kijiji cha Msomela wilayani Handeni mkoani Tanga chapewa cheti cha ardhi yao

Mkuu wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga, Muhingo Rweyemamu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Msomela jana baada ya kukabidhi cheti cha ardhi pamoja na ramani ya kijiji hicho, ikiwa ni hatua ya kuwapa umiliki halali wa eneo hilo. Picha na Rajabu Athumani, Handeni
0 comments

MATUKIO KATIKA PICHA YA FAINALI YA MASHINDANO YA KOMBE LA MWIDAU CUP

MATUKIO KATIKA PICHA YA FAINALI YA MASHINDANO YA KOMBE LA MWIDAU CUP

Mbunge Amina Mwidau, akimkabidhi kikombe cha ushindi Nahodha wa timu ya APL Mwera Shabani Athuman, baada ya timu hiyo kutawazwa kuwa mabingwa wa ligi ya Mwidau CUP, mjini Pangani jana

            Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga, Amina Mwidau (CUF), akihutubia kabla ya kuchezwa kwa fainali kati ya timu ya APL Mwera na Torino (kulia) ni Katibu wa Chama cha Soka Wilaya ya Pangani, Salehe Swazi.

 
        Mgeni rasmi katika Mashindano ya Mwidau CUP, Amina Mwidau akijadiliana na viongozi wenzake wakati wa mchezo wa fainali ya Mwidau CUP kati ya APL Mwera dhidi ya Torino leo mjini hapa.
0 comments

PATO LA MKOA WA TANGA LAONGEZEKA TOKA TRILIONI 1.78 HADI TRILIONI 2.009

PATO LA MKOA WA TANGA LAONGEZEKA TOKA TRILIONI 1.78 HADI TRILIONI 2.009

Na Oscar Assenga
Pato la Mkoa wa Tanga limeongezeka kutoka trilioni 1.78 hadi kufikia trilioni 2.099 kwa mwaka 2012 ambapo ongezeko hilo ni sawa na asilimia 17.8.
Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni Mstaafu Chiku Gallawa wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Mkoani hapa desemba 30 mwaka huu kuhusiana na mafanikio ya Mkoa wa Tanga ya mwaka 2012 hadi 2013.
Gallawa amesema katika ongezeko hilo Mkoa umechangia wastani wa asilimia 4.69 ya pato la Taifa ambalo ni Trilioni 44.7  kwa mwaka 2012 kulinganisha na 37.5 Trilioni kwa mwaka 2011.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema pia pato la mtu mmoja mmoja limeongezeka kutoka wastani wa shilingi laki 8,86,343 mwaka 2011 hadi shilingi 1,26,432 kwa mwaka 2012 ambapo wastani wa kitaifa ni shilingi 1,025,038 kiasi ambacho Mkoa wa Tanga unashika nafasi ya nane kati ya mikoa 25 ya Tanzania bara tangu mwaka 2010.
Aidha katika utekelezaji wa malengo ya kukuza uchumi Mkoa wa Tanga umeandaa mkakati wa kutekeleza miradi kwa kutumia mfumo wa tekeleza sasa kwa matokeo makubwa kwa miaka 2013 hadi 2015.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa   ameainisha vipaumbele katika maeneo ya kukuza mapato kwa mtu mmoja mmoja kufikia wastani 1.5, kuendeleza huduma za jamii za  elimu kwa kuongeza ufaulu kutoka asilimia 32 hadi 60 msingi na sekondari na maji kufikia asilimia 50 ifikapo 2015 kwa kutoa huduma za maji kwa umbali usiozidi mita 400 kutoka eneo la makazi.
0 comments

MADIWANI BUMBULI WAPEWA SOMO.

MADIWANI BUMBULI WAPEWA SOMO.



       (Katibu wa January Makamba(Hoza Mandia ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Milingano)
 
Na Raisa Said, Bumbuli
MADIWANI  wa Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto wametakiwa kusimamia ipasavyo maazimio na mikakati wanayopitisha katika vikao vyao  ili kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo.
Ushauri huo umetolewa na Mbunge wa Jimbo la Uchaguzi la Bumbuli, January Makamba akizungumza katika mahojiano na waandishi wa Habari hivi karibuni kufuatia kikao maalumu cha wajumbe wa Kamati ya Madiwani wa CCM kilichoitishwa kwa niaba yake na Katibu wake Hoza Mandia.
Mbunge huyo amesisitiza kuwa madiwani wanapaswa kusimamia maazimio waaliyoyapitisha katika kikao hicho ili kuiharakisha maendeleo kwa wananchi wa eneo hilo ambalo limebahatika kuwa Halmashauri kamili.
Katika maazimio hayo madiwani walimshauri Mbunge ajipangie utaratibu wa kuwasIliana kwa simu na madiwani angalau kila baada ya wiki au kadri atakavyoona inafaa zaidi ili kupata taarifa na kujua changamoto gani zilizopo katika jimbo hilo.
Pia waliazimia kuwa kero zote za wananchi zinazohusui miradi ya maendeleo ziwasiklishwe kwa kupitia vikao husijka na madwani wahusike kumuona mkurugenzi ili kupata majibu ya ufumbuzi wa kero hizo
Kikao hicho pia kiliazimia kuwa kila diwani awe amekamilisha na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwenye vikao husika  ndani ya mwezi mmoja na nakala ya taarifa hiyo iliyopitishwa iwasilishwe kwa katibu wa CCM wilaya na kwa mbunge.
Mbunge huyo alisisitiza kuwa hayo yote yaliyoazimiwa yasimamiwe kwa faida ya wananchi na Chama cha mapinduzi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger