Featured Post Today
print this page
Latest Post

Jeshi la Polisi wilayani Handeni lashukuru msaada wa sare za Ulinzi Shirikishi

Jeshi la Polisi wilayani Handeni lashukuru msaada wa sare za Ulinzi Shirikishi

Na Kambi Mbwana, Aliyekuwa Handeni
MKUU wa Jeshi la Polisi wilayani Handeni, mkoani Tanga, OCD Zuberi Chembera, amewashukuru wadau waliojitokeza kusaidiana na jeshi lao kuhakikisha kuwa kunaanzishwa Polisi jamii.
OCD Handeni, Zuberi Chembera, akionyesha sare za Ulinzi Shirikishi kwa baadhi ya vikundi vilivyoanzishwa wilayani humo.
Katika kuanzishwa huko, wafanyabiashara Adolf Lyakundi na Kareem Abdulsalim, walijitolea kununua jezi zinazotumiwa na vijana hao wa ulinzi shirikishi.
Akizungumza na Handeni Kwetu Blog, OCD Chembera, alisema kuwa jeshi haliwezi kufanikiwa kuleta amani kama hakuna ushirikiano wa wadau na wananchi kwa ujumla.

Alisema kwa kujitokeza wadau hao na wengine watakaokuja mbele ya safari, kila kitu kitakuwa kizuri na kuwafanya wananchi waishi kwa amani na utulivu wa aina yake.
“Hawa wenzetu wamejitokeza kununua sare zinazotumiwa na polisi jamii kwa ajili ya kushirikiana nao kulinda usalama katika mitaa mbalimbali, huku tukiamini kuwa ni mwanzo mzuri.
“Kwa pamoja wamenunua pea 25, hivyo sisi kama jeshi la Polisi tunawashukuru wenzetu hawa na hakika kitendo hiki kitaleta faida kubwa katika jamii yote, hususan wakazi na wananchi wa Handeni,” alisema.
Sera ya ulinzi shirikishi ina matunda makubwa katika sehemu mbalimbali za Tanzania, huku ikiungwa mkono na jeshi la Polisi na viongozi mbalimbali
0 comments

TANZANIA NAYO YAJITOSA KUMSAIDIA RUTO HUKO ICC..!!

TANZANIA NAYO YAJITOSA KUMSAIDIA RUTO HUKO ICC..!!

Serikali ya Tanzania, imeiomba Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuruhusu Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto kutohudhuria baadhi ya mashauri ya kesi yake ili kuweza kutimiza majukumu mengine ya kiserikali.

Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Jaji Fredrick Mwita aliandika barua kwenda ICC Jumatatu wiki hii akitetea hoja ya Ruto kutaka asihudhurie baadhi ya vikao vya kesi hiyo.
Katika barua yake, Jaji Werema alisema kuruhusu Ruto kutohudhuria baadhi ya vikao vya kesi kutaimarisha ushirikiano baina ya ICC na washirika.

 
Hata hivyo, maombi hayo yanayotaka Ruto kuruhusiwa kutohudhuria kesi hiyo binafsi yamesimamishwa baada ya mwendesha mashtaka wa ICC, Fatou Bensouda kuyawekea pingamizi na sasa yanasubiri uamuzi wa majaji.
Hii ni mara ya pili kwa Tanzania, kuwasiliana na ICC kwani iliwahi kuwasilisha ombi la kutaka kesi hiyo ya kina Ruto isikilizwe Tanzania au Kenya.
Hata hivyo, mpango huo ulikwama baada ya majaji kuupinga kwa kura za hapana.

 
Mwandishi Sang ajitetea

 
Mwandishi wa habari wa kituo cha KASS FM Joshua Arap Sang, amekamilisha ungwe ya kwanza ya utetezi wake kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) na kueleza kuwa hakuhusika kwa namna yoyote kuchochea machafuko yaliyojiri baada ya uchaguzi nchini Kenya.

 
Sang aliwasilisha utetezi wake katika hali ya kujiamini huku akionyesha sura yenye matumaini na kuiambia mahakama kuwa, kesi inayomkabili imetengenezwa ili kukatiza ndoto yake ya kuwa mtangazaji bora duniani .

 
Mwandishi huyo ambaye anatetewa na mawakili wanaoongozwa na Wakili Katwa Kigen, alipangua hoja zilizowasilisha na upande wa mashtaka kwa kutumia historia ya maisha yake aliyoyaelezea kuwa ni ya kumcha Mungu na uadilifu.

 
Kama ilivyo kwa washtakiwa wengine, Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto, Sang anadaiwa kuratibu na kupanga mashambulizi na kusababisha zaidi ya watu elfu moja kupoteza maisha.

 
Pia anadaiwa kuendesha kampeni ya uchochezi kupitia vipindi mbalimbali vya redio baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2007.

0 comments

MSANII MWINGINE WA BONGO MOVIE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA HUKO NCHINI BRAZIL

MSANII MWINGINE WA BONGO MOVIE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA HUKO NCHINI BRAZIL

Msanii wa Bongo muvi ambaye pia aliwah kuwa mke wa mfanyabiashara maarufu nchini marehemu Mohamed Mpakanjia bibie Aisha Bui anadaiwa kukamatwa na madawa ya kulevya 
nchini Brazil.. Mtandao huu bado unafatilia kwa ukaribu ishu hii na utawaletea habari kamili muda mchache ujao.
0 comments

WANAUME VIJANA 20'S-30 MNABOA SANA...HAMTUFIKISHI MNATUPAKA VUMBI TU

WANAUME VIJANA 20'S-30 MNABOA SANA...HAMTUFIKISHI MNATUPAKA VUMBI TU

Utakuta umempenda kijana mwenzako aaa kwa mapenzi kabisa unampa gemu kwa kujua atakushusha mlima kitonga mwisho wa siku unaambulia kubakizwa na vumba tu!!!
 
Jamani inakera sana vijana fanyeni mazoezi,mle vyakula vizuri chips yai na mikate asubuhi zinawaharibu mbona wakubwa miaka 40's na kuendelea wanatufikisha?Nimefanya resercha yangu wababa 3 vijana 3 ila kwa kweli wababa wanajua jamani tuwape hongera sasa nyie vijana sijui tatizo ni nini?sijui vyakula,sijui haraka,sijui stress za maisha hamko stable.

 
Huku mjini kuna wamama wanauza mihogo mibichi na matango muwe mnanunua kidogo zinasaida pia mule korodani za jogoo.
Itakuwa mnatuoa nyie ila starehe tunazipata kwa wababa.

0 comments

CCM yajisalimisha kwa Tundu Lissu baada ya kuiomba mahakama ifute Rufaa ya kupinga ubunge wake.


CCM yajisalimisha kwa Tundu Lissu baada ya kuiomba mahakama ifute Rufaa ya kupinga ubunge wake.
 
WAKATI rufaa ya kupinga ubunge wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) ikitarajiwa kuanza kusikilizwa katika Mahakama ya Rufaa Dodoma, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Wakili wake, Godfrey Wasonga, kimeiomba mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.


Kwa mujibu wa wakili huyo, sababu ya kuomba kufutwa kwa kesi hiyo ni kutokana na walalamikaji wote kujitoa na kuapa mahakamani kuwa hawapo tayari kuendelea na kesi hiyo.

Hata hivyo wakazi wawili wa Kijiji cha Makiungu mkoani Singida, Shabani Selema na Paskali Hallu, ambao walifungua kesi ya msingi kupinga ubunge wa Lissu, tayari walikwisha kuweka bayana kukubaliana na hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma Aprili, mwaka huu.

Mara kadhaa wananchi hao wamenukuliwa wakimlalamikia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kuwa anawashinikiza kuendelea na rufaa hiyo licha ya kwamba walikwisha kujitoa.

Wasonga ambaye alikuwa akiwatetea wanachama hao katika kesi hiyo, alisema kuwa baada ya kuwasiliana na wateja wake walimwambia hawapo tayari kuendelea na kesi hiyo.

“Ni kweli walalamikaji wote wamejitoa na mimi kama wakili sioni haja ya kuendelea, nitakuwa namwakilisha nani? Nimeongea nao jana, hakuna mwenye nia ya kuendelea na kesi,” alisema.

Wasonga alipoulizwa kama bado anadai malipo kutoka kwa walalamikaji hao, alisema japokuwa wateja wake ni wanakijiji wasio na uwezo mkubwa wa fedha walijitahidi kulipa madai yote.

Selema na Paskali wakiwa Muyanji kijijini, walisema kuwa: “Sisi tulishatoa msimamo tangu mapema hatuna mpango wa kuendelea na kesi.

“Tuliapa mahakamani lakini tulishangaa kuona kesi hiyo inapangiwa majaji, sisi pia tumepata taarifa kuwa huyo wakili aliyekata rufaa bila ridhaa yetu amepeleka ombi mahakamani ili kesi iondolewe, hayo ni matakwa yake binafsi kama yeye alikuwa anafuata maneno ya Kinana,” walidai.

Naye Lissu amesema kuwa tayari anao wito wa mahakama kesho kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo.

Alisema kuwa jana jioni alipata barua kutoka kwa wakili wa walalakaji kwenda Mahakama ya Rufaa, wakiomba kuifuta rufaa hiyo.

“Nimepokea samansi niende kusikiliza kesi hiyo siku ya Ijumaa na tayari nilishaweka pingamizi kupinga rufaa hiyo. 
  
Hii taarifa ya kuondolewa au kufutwa kesi wakati tayari nimeshaweka pingamizi nitatoa msimamo siku hiyo palepale mahakamani kwa kutumia vigezo vya kisheria,” alisema.
Rufaa hiyo imepangiwa kusikilizwa katika Mahakama ya Rufaa na jopo la majaji watatu, Salumu Massati, Engela Kileo na Natalia Kimaro.
  
Kabla ya kuanza kusikilizwa kwa rufaa hiyo, mahakama ilitarajiwa kusikiliza pingamizi zilizotolewa na upande wa walalamikiwa, ambao ni Lissu na Jamhuri za kupinga rufaa hiyo na jopo hilo la majaji litatoa uamuzi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Lissu alitoa hoja saba za kupinga rufaa hiyo, muda mfupi kabla hajapokea maombi hayo ya kuiondoa kesi hiyo.

Lissu alisema hoja hizo ni mkata rufaa Selema ambaye ndiye mlalamikaji namba moja kupinga kwamba hajakata rufaa kwa hati ya kiapo ya Mei 24, mwaka huu.

Alisema hoja nyingine ni notisi ya kiapo kutopelekwa kwa mjibu rufaa, ambaye ni yeye, kinyume cha masharti ya kanuni ya 84 (1) ya Kanuni za Adhabu za Mahakama ya Rufaa Tanzania za mwaka 2009.

“Vilevile nakala zote rekodi ya rufaa hazijathibitishwa usahihi wao, na wakata au wakili kinyume cha masharti ya Kanuni ya 96 (5) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa Tanzania za mwaka 2009.

“Rufaa hii pia imepitwa na muda wake, kwa sababu hati ya ucheleweshaji iliyotolewa na Msajili wa Mahakama Kuu haijasainiwa, haina tarehe wala muhuri, kinyume cha Kanuni ya 90 (1) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa ya Tanzania za mwaka 2009,” alisema.

Lissu aliongeza kuwa walalamikaji walitakiwa kukata rufaa siku sitini baada ya notisi ya rufaa kutolewa na kwamba tarehe ya mwisho ya kukata rufaa ilikuwa Julai 3, mwaka jana, lakini rufaa hiyo ilikatwa Mei 7 mwaka huu.

“Hoja nyingine ni kwamba rufaa hiyo si halali kwa kuwa imeacha nyaraka muhimu, ikiwamo maombi ya mwenendo wa shauri wa kusamehewa gharama za dhamana,” alisema.

Lissu alisema pia katika rufaa hiyo, amri iliyomshindisha kesi si halali, kwa kuwa haionyeshi tarehe ambayo amri hiyo ilitolewa, kinyume cha kanuni ya 9 ya Kanuni za Masijala za Mahakama Kuu za mwaka 2005.

Alisema pia wakata rufaa wamesindwa kuwasilisha mahakamani hoja za maandishi za kuunga mkono hoja za rufaa yao ndani ya siku 60 au kuomba muda wa kuziwasilisha.

Pia hoja nyingine ni kushindwa kuwasilisha hoja hizo za maandishi kinyume cha Kanuni ya 106 (1), (2) na (9) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa ya Tanzania za mwaka 2009.

Kesi ya kupinga ubunge wa Lissu ilianza kusikilizwa Machi 12, 2012 na Jaji wa Mahakama Kuu, Moses Mzuna, aliyetoa hukumu Aprili 27, mwaka huu na kumtangaza Lissu kuwa mbunge halali wa Singida Mashariki, kwa kigezo kuwa hoja zote zilizotolewa na wanachama hao wa CCM hazitoshi kutengua au kubatilisha ubunge wake.

Kufuatia hukumu hiyo, wanachama hao wa CCM waliridhia hukumu ya Mahakama Kuu, hivyo kuandika barua kwa Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Kati kuomba wapewe fedha walizokuwa wameweka kama dhamana yao sh milioni 15.
Lakini Ofisi ya Msajili wa Mahakama Kuu imekuwa ikisuasua kutoa majibu kurejesha fedha hizo kwa Selema na Halu.

Tanzania Daima
0 comments

MWANAMKE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AKIWA AMEYAFICHA KWENYE MIMBA BANDIA.


MWANAMKE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AKIWA AMEYAFICHA KWENYE MIMBA BANDIA.
 
Kila kukicha vita dhidi ya biashara haramu ya dawa za kulevya inazidi kupamba moto, wakati mataifa mbalimbali yakizidi kuimarisha udhibiti wa biashara hiyo, na wafanyabiashara wanazidi kuja na mbinu mpya za kusafirisha dawa hizo.


Huko Colombia mwanamke mmoja raia wa Canada amekamatwa uwanja wa ndege akiwa na tumbo la ujauzito wa bandia ambalo ndani yake alificha kilo mbili za dawa za kulevya aina ya Cocaine.


Polisi wa uwanja wa ndege wa Bogota Colombia alimshtukia mwanamke huyo Tabitha Leah Ritchie aliyeonekana kuwa na tumbo lisilo la kawaida ndipo baada ya kumkagua wakakutana na dawa hizo.

Bongo 5
0 comments

JK katika mtihani wa Katiba Mpya;

JK katika mtihani wa Katiba Mpya;

bisimba_c7e67.jpg

Wakati Rais Jakaya Kikwete akisubiriwa asaini Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa 2013 ili kuwa sheria kamili, wasomi, wanasiasa na wanaharakati wamemshauri asifanye hivyo, wakisema itapatikana Katiba Mpya isiyo na tija.

Wananchi hao kutoka Tanzania Bara na Zanzibar walisema kwa nyakati tofauti kuwa, Rais Kikwete anatakiwa kutumia busara ya kushauriana na kupata maoni ya watu wa kada mbalimbali ili kujua nini kifanyike, kabla ya kuamua kusaini muswada huo.

Mjadala wa muswada huo uliopitishwa Ijumaa iliyopita na wabunge wengi wakiwa wa CCM, ulizua tafrani bungeni iliyosababisha Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) kutolewa nje na askari. Katika tafrani hiyo, baadhi ya wabunge wa upinzani walirushiana makonde na maofisa usalama, huku wabunge wote wa upinzani, isipokuwa Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema, wakiususia.
Wapinzani walisema Serikali iliubadili kwa nguvu muswada huo kwa kuondoa maoni muhimu ya wadau, pia walilalamikia kitendo cha wajumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ya Bunge kutokwenda Zanzibar kuchukua maoni ya upande huo wa muungano.

Wasomi
Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Gaudence Mpangala alisema mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya ulikuwa ukienda vizuri... "Lakini umebadilika vibaya, tena katika kipindi muhimu. Kupitishwa kwa muswada na kusubiri saini ya Rais kunaweza kuleta Katiba Mpya, ikawa siyo ile ambayo Watanzania wanaitarajia." Alishauri busara itumike kabla ya kusainiwa kuwa sheria kamili.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tunguu Zanzibar, Ali Uki alisema hakuna haja ya muswada kukimbiliwa kusainiwa kwani katiba ni mali ya wananchi na kuupitisha ili uwe sheria bila kuyashirikisha makundi mengine, kutaendeleza malalamiko na kurudisha nyuma malengo ya kupatikana kwake. Uki alisema upo wasiwasi kwamba Katiba Mpya itatokana na utashi wa kisiasa badala ya matakwa ya wananchi, jambo ambalo alisema linaweza kuathiri malengo ya kuandikwa kwake.

"Utashi wa vyama umeanza kujitokeza, huku chama kimoja kikiwa na uwakilishi mkubwa kwenye Bunge hilo, chama kimoja kina uwakilishi wa asilimia 72 katika Bunge la Katiba," alisema Uki.
Alikosoa Kifungu cha 8 na Kifungu kidogo cha 4 na 5 cha muswada huo kwamba vina kasoro kwa kuruhusu wabunge wa Bunge la Katiba kufanya uamuzi kwa wingi wa kura badala ya kutumika utaratibu wa theluthi mbili kutoka Zanzibar na Tanzania Bara.
Profesa mwingine wa UDSM, Chris Peter Maina alisema ikiwa kuna nia njema ya kupata Katiba bora, lazima suala la uwiano wa idadi ya wabunge katika Bunge la Katiba litazamwe upya.
"Rasimu ya pili ikishatolewa na kukabidhiwa kwa Bunge la Katiba, kazi ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ndiyo itakuwa imekwisha. Sasa inakuwaje Bunge linajadili Rasimu ya Katiba huku waliyoiandaa hawapo, hiki kitu kinashangaza," alisema Profesa Maina.

Mhadhiri Mwandamizi wa chuo hicho, Dk Frank Tilly alisema hakuna umuhimu wa kukimbiza muswada kutiwa saini wakati kuna mambo mengi ya msingi ambayo hayajapatiwa ufumbuzi... "Watanzania hawajakubaliana kwa pamoja, ili jambo liwe zuri ni lazima pande mbili au zaidi zenye masilahi na kitu husika zikubaliane, sasa hilo halijafanyika tunakimbilia wapi?" alihoji.
Mhadhiri wa UDSM, Bashiru Ally alisema mchakato mzima wa Katiba umeshaingia doa kwa kupitishwa muswada unaolalamikiwa na kwamba manung'uniko ya wananchi hayajajibiwa.
Alisema busara zisipotumika, itapatikana Katiba isiyokuwa na uhalali wa kisiasa... "Nasema hivi kwa sababu wanasiasa hawajakubaliana katika kupitisha sheria itakayounda Bunge la Katiba".

Vyama vya kiraia
Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar, Hassan Nassor Moyo alisema Rais anapaswa kutafakari kwa umakini kabla ya kusaini muswada huo na kuwa sheria mpya kwa kuwa bado kuna manung'uniko.
"Hakuna mantiki ya kuupitisha muswada ukawe sheria wakati kuna manung'uniko. Wakati umefika misimamo ya vyama kuwekwa kando ili malengo yenye manufaa na tija yaweze kufikiwa kutokana na mahitaji ya wananchi."
Moyo alisema ushirikishwaji wa Wazanzibari ulikuwa finyu kwani waliopata fursa ya kutoa maoni yao walikuwa ni viongozi wa Serikali pekee.
"Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umetokana na washirika wawili, Zanzibar si mtoto wa kambo, ni mshirika na mdau mkuu katika kupata Muungano uliopo," alisema Mzee Moyo.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema kitendo cha kupitishwa muswada wenye kasoro ni wazi kuwa kitazalisha Katiba isiyo na tija kwa taifa.

"Muswada umepitishwa na wabunge wa CCM kwa asilimia 80, sidhani kama hii ni sawa katika hatua muhimu kama hii na haitoi picha kamili ya mwelekeo chanya wa kupata katiba stahiki," alisema Dk Bisimba.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba alisema: "Ukipitisha sheria kinyemela maana yake ni kwamba unataka ifanye kazi kinyume na matakwa ya watu wengi, jambo ambalo ni hatari kiuchumi na kielimu."

Alisema Rais Kikwete anatakiwa kutumia busara katika suala hilo, kwa maelezo kuwa, amebakiza muda mfupi kumaliza kipindi chake cha utawala, hivyo aache Katiba yenye tija kwa Watanzania.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus Mgaya alisema: "Ikiwezekana muswada uliopitishwa usisainiwe na urejeshwe bungeni na kupitiwa upya ikiwa ni pamoja na pande zote mbili za Muungano kutoa maoni sambamba na kurekebishwa kwa kasoro zilizopo."

Alisema watu wataondoka lakini Tanzania itaendelea kuwapo, hivyo ni jambo la busara kama ikipatikana Katiba itakayokuwa na masilahi kwa wakati huu na ujao.

Wanasiasa

Katibu Mkuu wa TADEA, Juma Ali Khatib alisema muundo wa Bunge la Katiba ndio unaozua malalamiko kutokana na wanasiasa kupewa nafasi kubwa, jambo ambalo alisema linaweza kutanguliza dhima ya kisiasa na kuweka kando masilahi ya kitaifa na utaifa.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kitendo cha Zanzibar kutoshirikishwa ni kosa kwani Katiba hiyo ni ya Jamhuri ya Muungano... "Namshauri Rais asisaini muswada huu kwani utakuwa ni majanga. Namshauri akutane na watu walioonyesha wasiwasi na sheria hiyo ili kusikiliza mawazo yao, huenda wakamshauri jambo la msingi la kufanya na iwapo atasaini bila kufanya hivyo mchakato mzima hautakuwa wa taifa, bali wa CCM."

Chanzo:Mwananchi
0 comments

Taasisi ya WAMA yakabidhi Gari la Wagonjwa Hospitali ya Sokoine Mkoa wa Lindi

Taasisi ya WAMA yakabidhi Gari la Wagonjwa Hospitali ya Sokoine Mkoa wa Lindi

Picha-no--1_d872a.png

Mke wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) Mama Salma Kikwete akitoa risala fupi wakati wa halfa ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa lililotolewa na Taasisi hiyo kwa hospitali ya Sokoine Mkoa wa Lindi,kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo Ludovick Mwananzila na kulia ni Kaimu katibu tawala wa hospitali hiyo Tawani Selemani.

picha-no-3_a81d7.png

Mke wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) Mama Salma Kikwete akimuonyesha gari la kubebea wagonjwa Mkuu wa Mkoa wa lindi Ludovick Mwananzila lililotolewa na Taasisi hiyo wakati wa alipolikabidhi kwenye hospitali ya Sokoine mkoani hapo.

Picha-no-4_f6564.png

Mke wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Hospitali ya Sokoine Mkoa wa Lindi baada ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika hospitali hiyo.

Picha-no-5_18404.png

Picha no 5 Mke wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya 
Wanawake na Maendeleo(WAMA) Mama Salma Kikwete akikabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa kwa Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Sokoine Dk.Abdallah Chome kulia ni Mkuu wa Mkoa wa lindi Ludovick Mwananzila gari hilo limetolewa na Taasisi hiyo kwa ajili ya kusaidia wagonjwa.

(Picha na Lorietha Laurence-Maelezo)
0 comments

Magazeti ya leo September 13 Udaku, Michezo na Hardnews


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments

Urusi yasema amani yawezekana Syria

Urusi yasema amani yawezekana Syria

Sergei Lavrov na John Kerry wanakutana Geneva Uswisi kujadiliana kwa kina kuhusu mpango uliopendekezwa na Urusi katika kuzishughulikia silaha za sumu za utawala wa Assad 

Mawaziri wa nje wa Urusi na Marekani Sergei Lavrov na John Kerry Mawaziri wa nje wa Urusi na Marekani Sergei Lavrov na John Kerry

Urusi inapendekeza mpango wa hatua nne kwa marekani kutekeleza azma yake ya kutaka kuziharibu silaha za sumu za Syria.Taarifa hizo zimechapishwa na gazeti moja la mjini Moscow katika wakati ambapo waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov anatazamiwa kukutana leo na mwenzake wa Marekani John Kerry mjini Geneva.Suala hilo litajadiliwa kwa kina katika mkutano huo.

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amenukuliwa akisema bado kuna nafasi ya kupatikana amani nchini Syria na ulimwengu haupaswi kuiacha nafasi hiyo ipite bila kuitumia.Lavrov ametowa kauli hiyo mbele ya wanafunzi huko Kazakhstan kabla ya kuelekea mjini Geneva baadae kwa ajili ya mazungumzo na mwenzake wa Marekani John Kerry kuhusu pendekezo la nchi yake ambalo limemfanya hata rais Obama kulitaka Bunge la nchi yake kuakhirisha zoezi la kura ya kutowa ridhaa ya kushambuliwa Syria.

Lavrov ameridhsishwa na hatua ya Syria ya kuridhia mpango wake wa kuitaka nchi hiyo izisabilie silaha zake za sumu chini ya uangalizi wa Kimataifa.Aidha ameonya kuhusu kuchukuliwa hatua za kijeshi dhidi ya Syria akisema ni jambo litakalozidisha mafuta katika moto ambao tayari unawaka na kulitekeleza eneo zima.

Mawaziri wa nje wa Ufaransa na Marekani Laurant Fabius na John Kerry  
Mawaziri wa nje wa Ufaransa na Marekani Laurant Fabius na John Kerry
Pingamizi la waasi

Hata hivyo kutoka Syria kwenyewe waasi wamelipinga pendekezo la Urusi kuhusu kuzisalimisha silaha za sumu za utawala wa Assad wakisema utawala huo unabidi kufikishwa mbele ya mahakama ya Kimataifa kuhusiana na shambulio la mwezi uliopita lililofanywa karibu na mji wa Damascus ambako silaha za sumu zilitumika na mamia ya watu waliuwawa.

Jenerali Salim Idrsi ambaye ni kamanda wa ngazi ya juu wa jeshi la waasi nchini humo amesema silaha za sumu zilikuwa chombo cha uhalifu katika shambulio hilo la Agosti 21 katika mji wa Ghouta.Tamko hilo la waasi linakuja saa chache kabla Kerry kuwasili Geneva kwa ajili mkutano wake na Lavrov.Pamoja na hayo Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa Lareunt Fabius amebaini kwamba ripoti ya wachunguzi wa Umoja wa Mataifa katika suala la kutumiwa silaha za sumu nchini Syria huenda ikatolewa siku ya Jumatatu.

Akizungumza na redio moja ya kifaransa waziri huyo ameweka wazi kwamba ripoti hiyo itaeleza kwamba yamefanyika mauaji ya halaiki kwa kutumika silaha za sumu na kwamba ripoti hiyo itabaini chanzo cha shambulio hilo.Wachunguzi hao waliondoka Syria Agosti 31 baada ya kukusanya sampuli za ushahidi utakaowasaidia katika uchunguzi wao kuhusu shambulio la Ghouta.

Msimamo wa Marekani

Lavrov asema njia ya amani inawezekana katika mzozo wa Syria  
 
Lavrov asema njia ya amani inawezekana katika mzozo wa Syria
Marekani na washirika wake ambao ni pamoja na Ufaransa wanasema ni utawala wa rais Bashar al Assad uliofanya shambulio hilo lakini serikali hiyo ya mjini Damascus na mshirika wake Urussi wanalitwika mzigo jeshi la waasi.Wajumbe kutoka nchi tano wanachama wa kudumu katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa walikuwa na kikao katika Umoja wa Mataifa juu ya Syria ambacho hakikufikia mwafaka hapo jana.
Mazungumzo ya Geneva kwahivyo yanategemewa kuchukuwa siku mbili au tatu na pia yatajadili juu ya kuzitia msukumo juhudi za kuitishwa mkutano wa amani unaonuiwa kumaliza vita vya Syria.Lavrov na Kerry watakutana pia na Lakhdar Brahimi mjumbe wa Kimataifa kujadiliana kuhusu mapngo wa kuwakutanisha waasi na utawala wa Assad katika meza ya mazungumzo.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger