Featured Post Today
print this page
Latest Post

SEMINA YA TARUJA YAANZA PANGANI LEO.

SEMINA YA TARUJA YAANZA PANGANI LEO.

MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MAZINGIRA VIJIJI MKOANI  TANGA (TARUJA)GEORGE SEMBONI KUSHOTO AKIBADILISHA MAWAZO NA MBUNGE WA JIMBO LA PANGANI SALEHE PAMBA KABLA YA KUANZA SEMINA YA SIKU TANO AMBAYO ILISHIRIKISHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA TANGA.

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO

Na  Oscar Assenga,Pangani.
Wanahabari wametakiwa kutumia kalamu zao katika kuhakikisha jamii zinazoishi kandokando kuzunguka hifadhi za Taifa zinakuwa na ushirikiano katika maswala mazima ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira ili kuweza kuwa na hifadhi endelevu.

Hayo yalielezwa leo na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi wakati akifungua mafunzo ya siku sita ya uandishi wa habari za hifadhi na utunzaji wa mazingira kwa waandishi wa habari za vijijin na mazingira TARUJA, inayofanyika wilayan Pangani Mkoani Tanga.

Alisema TANAPA inatambua umuhimu wa vyombo vya habari na kwamba shirika limekuwa likitoa mafunzo ya mara kwa mara kwa wanahabari ili kuweza kuhakikisha waandishi wanaandika habari zinazohusu uhifadhi kwa weredi.

‘’Natambua umuhimu wa vyombo vya habari  hivyo ndio maana tunashirikiana navyo kwa ukaribu zaidi wani jamii inapata taarifa kupitia kalamu zenu ,ni vema mkatambua sera na sheria ili muweze ktusaidia hata kutatua migogoro kwa kutumia kalamu zenu”alisema Kijazi.

Alisema ushirikiano ni muhimu ili kuhakikisha hamasa inajengeka katika jamii inaona umuhimu wa kuhifadhi mazingira na maswala ya uhifadhi na kwamba kwa kufanya hivyo nchi itakuwa na hifadhi endelevu kwa kizazi cha sasa na baadae.

Kijazi alizungumzia changamoto zinazoikabili shirika hilo kuwa ni ujangili uliokithiri pamoa na kuvamiwa kwa mapito ya wanyama ambo ambalo linaleta migogoro isiokuwa na tia  baina ya jamii na shirikka.
Kwa upande wake mwenyekiti wa TAJURA George Semboni alisema kufuatia changamoto za kimazingira na uhifadhi katika hifadhi za Taifa  ndizo zilizopelekea wanahabari kuona umuhimu wa kuomba mafunzo ili kutumia taaluma ya uandishi kutoa elimu kwa amii kuhusu maswala ya uhidhi.
‘’Hata sisi waandishi sio wote tunaoelewa faida zitokanazo na uwepo wa mbuga ndio maana mambo yanayorushwa hewani ni malalamiko ya wananchi dhidi ya watendaji wanaofanya kazi katika maeneo ya uhifadhi ambao wanatimiza wajibu wao kisheria’’alisema Sembon.
Mafunzo hayo ya siku sita yanashirikisha waandishi wa habari ,viongozi wa chama na serikali pamoja na wanchi wanaoshi kando ya hifadhi ya taifa ya Saadani yanatariwa kufungwa mwishoni mwa wiki hii.
0 comments

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amwapisha Jaji Francis Mutungi, kama msaji wa vyama vya siasa Tanzania

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amwapisha Jaji Francis Mutungi, kama msaji wa vyama vya siasa Tanzania


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Msajili wa Vyama vya Siasa mpya Jaji Francis Mutungi Ikulu jijini Dar es salaam leo.Picha na Ikulu.
mu4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimmkabidhi vitendea kazi  Msajili wa Vyama vya Siasa mpya Jaji Francis Mutungi Ikulu jijini Dar es salaam leo.
mu7
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na  Msajili wa Vyama vya Siasa mpya Jaji Francis Mutungi na viongozi wa vyama vya siasa Ikulu jijini Dar es salaam leo.
  IMG_1836
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Jaji Francis Mutungi na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Mhe John Tendwabaada ya kumuapisha Jaji Mutungi Ikulu jijini Dar es salaam leo.
0 comments

Hali ilivyokuwa katika kikao cha NEC Mjini Dodoma leo na kuongozwa na mwenyekiti wake Jakaya Mrisho Kikwete

Hali ilivyokuwa katika kikao cha NEC Mjini Dodoma leo na kuongozwa na mwenyekiti wake Jakaya Mrisho Kikwete


 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha NEC, leo Agosti 26, 2013 mjini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa utangulizi kabla ya Mwenyekiti wa CCm Rais Jakaya Kikwete (kushoto) kufungua kikao cha NEC, Agosti 26, 2013.
 Baadhi ya wajumbe wa NEC, ukumbini. Kulia mstari wa mbele ni Mjumbe wa Kamati ya Ushauri ya Viongozi wastaafu wa CCM, John Malecela ambaye ni mwalikwa kwenye kikao hicho.
0 comments

JIACHIE NA PICHA 17 ZA SHOW KABAMBE YA KUKUZA VIPAJI ( SUA ) JIJINI ARUSHA LILILOFANYIKA JANA MAENEO YA KIJENGE JUU WATENGWA RECOD'S!!!

JIACHIE NA PICHA 17 ZA SHOW KABAMBE YA KUKUZA VIPAJI ( SUA ) JIJINI ARUSHA LILILOFANYIKA JANA MAENEO YA KIJENGE JUU WATENGWA RECOD'S!!!

 Jukwaa lilibikiriwa namna hii!!!








Umati wa watu wakifurahia burudani

0 comments

"FOOLISH AGE" YA LULU MICHAEL YARUHUSIWA BAADA YA KUZUIWA.

"FOOLISH AGE" YA LULU MICHAEL YARUHUSIWA BAADA YA KUZUIWA.


Bodi  ya   ukaguzi  wa  filamu  Tanzania  imeridhia  na  kuiruhusu  filamu  ya  Foolish Age  ya  Lulu  Michael  iingie  sokoni  baada  ya  kuizuia  hapo  juzi....

Filam  hiyo  ilizuiliwa   kutokana  na  mavazi  ya  nusu  uchi  yaliyokuwa  yamevaliwa  na  washiriki  wake  na  kumtaka  Lulu  Michael  aifanyie  marekebisho  kwa  kuviondoa  vipande  hivyo  ambavyo  vilikuwa  kinyume  na  maadili  ya  kitanzani....

Filamu hiyo  ambayo yupo Lulu, Diana Kimaro, Jengua na Hashim Kambi itazinduliwa tarehe 30 mwezi huu katika ukumbi wa Mlimani City
0 comments

DILLISH AIBUKA MSHINDI WA BIG BROTHER AFRICA 2013.

DILLISH AIBUKA MSHINDI WA BIG BROTHER AFRICA 2013.

 

 

Fainali za Big Brother zimefikia  tamati  usiku  huu  zikiwa  na  washiriki  watano  ambao  ni  Beverly, Melvin, Cleo, Elikem  na  Dillish.

Mshiriki  wa  kwanza  kutolewa  alikuwa  ni  Beverly  akifuatiwa  na  Melvin  huku  Elikem  akiwa  ni  mshiriki  wa  tatu  kutolewa..

Mchujo  huo  uliwafanya  Cleo  na  Dillish  waingie  katika  masaa  ya  fainali za  mwisho  ambapo  Cleo  alielemewa  na  kutolewa  huku  akimwacha  Dillish  akichekelea  $300,000  za  ushindi  wa  shindano  hilo....

Agalia  jinsi  kura  zilivyopigwa:
 Angola: Dillish
Botswana: Cleo
Ghana: Elikem
Kenya: Dillish
Ethiopia: Beverly
Malawi: Cleo
Namibia: Dillish
Nigeria: Melvin
South Africa: Cleo
Sierra Leone: Elikem
Tanzania: Dillish
Uganda: Dillish
Zambia: Cleo
Zimbabwe: Elikem
Rest of Africa: Melvin
Total: 

Dillish = 5, Cleo = 4, Elikem = 3, Melvin = 2, Beverly = 1.

 

0 comments

MTOTO WA MIAKA 8 AOLEWA NA MWANAUME WA MIAKA 38.

MTOTO WA MIAKA 8 AOLEWA NA MWANAUME WA MIAKA 38.


Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Samson (38), mkazi wa Kijiji cha Mindukeni, Tarafa ya Tarawanda katika Wilaya ya Bagamoyo,
Pwani amefanya maajabu ya milenia baada ya kudaiwa kuoa mtoto mwenye umri wa miaka nane .

Habari za kiuchunguzi zilisema kuwa mwanaume huyo ambaye tayari alishaoa mke wa kwanza, alidaiwa kumtorosha mtoto huyo nyumbani kwao, Iringa.


Ilidaiwa kuwa Samson alifanya tukio hilo kwa kushirikiana na mjomba wa mtoto huyo, wakati akichunga mbuzi mkoani Iringa.

Habari zilieleza kuwa baada ya Samson kumtorosha mtoto huyo kijijini kwao alimpeleka kijijini Mindukeni, Pwani na kumuweka kinyumba akiwa ni mke wake wa pili.


Ilidaiwa kwa kuwa mtoto huyo analingana na watoto wake kwa mke wa kwanza, alimweka chumba kimoja na wanaye.

Kabla ya ishu kubumburuka, Samson alikuwa akiishi na mtoto huyo akiwa ni mke mdogo huku akimtumia kufanya kazi mbalimbali kama kuchunga mbuzi, kuchota maji kisimani na kusaidia kubeba au kulea watoto wa mke mkubwa.
  
Kwa mujibu wa mtoto huyo, hadi sasa hajui alifikaje kijijini hapo na wala hatambui jinsi ya kurudi kwao kwani walimuiba tu.

Alisema baada ya kufikishwa kijijini hapo, alikuwa akilala chumba cha watoto na mwanaume huyo akitaka kumuingilia anaingia chumbani humo na kufanya naye mapenzi kisha kurudi kwa mke mkubwa.
 

“Nilikuwa naumia wakati akiniingilia, alikuwa anakuja chumba tunacholala na watoto wake wengine, ananichukua pembeni na kufanya mapenzi, akimaliza anarudi kwa mke mkubwa,” alisema mtoto huyo na kuongeza:
 

“Kusema kweli mwanzoni nilikuwa nasikia maumivu makali hadi nilipokuja kuona ni kitu cha kawaida.”

Mtoto huyo alisema kuwa kila kulipokucha alikuwa anaona aibu kwani wale watoto wengine wanalingana naye hivyo alikuwa akiumia kufanyiwa kitendo kama hicho cha ukatili na mtu ambaye ni sawa na baba yake.
 

Aliendelea kusema kuwa aliumia kupelekwa katika kijiji hicho na kuishi na mwanaume huyo na tayari ameshakaa miaka minne kama mke wake, akimuingilia mara kwa mara na kumsababishia maumivu.  
“Nimeishi naye muda mrefu kama miaka minne, natamani kurudi kwetu nikasome,” alisema mtoto huyo.
 

Kwa upande wake mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live cha EATV, Joyce Kiria alifika katika kijiji hicho na baadaye alikwenda katika Kituo cha Polisi Bagamoyo kisha kuchukua askari usiku wa manane ambapo Samson alitiwa mbaroni na hadi sasa yupo mahabusu huku mtoto huyo akisubiri kuanza shule.

Habari hii ni ya kusikitisha kwa sababu huu ni zaidi ya ukatili kwa watoto wadogo, ili kujua na kuona mengi zaidi yaliyotokea kupitia runingani, usikose kuangalia Kipindi cha Wanawake Live cha EATV.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio la kuolewa kwa mtoto huyo, serikali ya Rais Jakaya Kikwete kupitia Jeshi la Polisi chini ya IGP Said Mwema wanatakiwa kuchukua hatua kali dhidi ya watu wanaofanya ukatili katika jamii hasa kwa watoto wasio na hatia.

 

0 comments

Marekani:kemikali ilitumika kuuwa Syria

Marekani:kemikali ilitumika kuuwa Syria

 

kerry_0d4b0.jpg
Waziri wa Mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, John Kerry ameshtumu anachokitaja kama hatua ya serikali kutumia silaha za kemikali dhidi ya watu wake kama ukosefu wamaadili wa hali ya juu.
Amesema kanda za video za silaha zinazotuhumiwa kuwa za kemikali karibu na mji wa Damascus ni kweli na zisizoweza kukanushwa.

Kerry aliongezea kwamba Rais Barack Obama anatafakari hatua ya kuchukua.
Haya yanajiri saa chache baada ya wakaguzi wa silaha za kemikali wa Umoja wa Mataifa kushambuliwa karibu na mji mkuu huo.

Wachunguzi wa silaha za Umoja wa mataifa kuwasili katika eneo lililopo viungani mwa mji mkuu Damascus ambapo inashukiwa kuwa wiki iliyopita kulishambuliwa kwa silaha za kemikali .
Wanaharakati wa upinzani nchini Syria wanasema wachunguzi hao wa Umoja wa mataifa wanakutana na waathiriwa wa shambulio linaloshukiwa kuwa ni la gesi ya sumu na madaktari waliowatibu .
Wachunguzi hao watachunguza mabaki na kukusanya sampuli za udongo, damu na tishu kwa ajili ya vipimo vya maabara. .

Awali watu wasiojulikana wenye silaha waliushambulia kwa risasi msafara wa magari waliokuwemo wakaguzi hao walipokuwa wakielekea kwenye eneo la tukio - na kuwalazimisha kurejea nyuma kwa muda .
Vyombo vya habari vya kitaifa nchini viliwashutumu waasi kufanya shambulio hilo.
Rais Assad aliwaruhusu wakaguzi wa silaha baada ya kukabiliwa na shinikizo kubwa la kimataifa, lakini Marekani na Uingereza zimesema ushahidi mwingi huenda uliharibiwa katika muda wa siku tano, tangu kutokea kwa mashambulio.

Wakati huo huo serikali za magharibi zimeikosoa Syria kwa kuchukua muda mrefu kuruhusu timu ya Umoja wa mataifa ya wakaguzi wa silaha kuzuru eneo linalodaiwa kushambuliwa kwa silaha za kemikali na zinaangalia uwezekano kuingilia kati kijeshi nchini humo.

 

0 comments

Mchakato kura ya maoni ya Katiba waanza;


Mchakato kura ya maoni ya Katiba waanza; 

bunge_453b4.jpg

Historia inatarajia kuandikwa katika Mkutano wa 12 wa Bunge la 
 Jamhuri ya Muungano unaoanza leo, mjini Dodoma wakati litakaposafisha njia kwa Watanzania kwa mara ya kwanza, kupiga kura ya maoni ya Katiba.Bunge litajadili Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni 2013, ambao ndiyo utakaotoa njia kwa Watanzania kuamua Katiba Mpya baada ya Bunge la Katiba kumaliza kazi yake.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Tanzania Bara kupiga kura ya
maoni ya aina yoyote ile tangu Uhuru mwaka 1961 na ya pili kwa Zanzibar ambayo ilifanya hivyo kwa mara ya kwanza mwaka 2010 kutoa nafasi ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Kuelekea mchakato huo wa Katiba Mpya, Bunge pia litajadili Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013.

Hatua hiyo inatokana na safari ndefu ya mchakato wa ukusanyaji wa maoni ya wananchi iliyoanza Aprili 13, mwaka jana kwa Rais Jakaya Kikwete kuzindua Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Joseph Warioba.

Juni 3, mwaka huu, Jaji Warioba alizindua Rasimu ya Katiba baada ya mchakato huo na kuruhusu uundwaji wa Mabaraza ya Katiba kwa kutegemea makundi maalumu ambayo mchakato wake unamalizika Agosti 31, mwaka huu.

Baada ya hatua hiyo, Bunge litapelekewa maboresho ya mapendekezo ya rasimu hiyo na kuyajadili ikiwamo kupitisha sheria ya mabadiliko hayo na baadaye kuweka muundo wa sheria na muundo wa kupigiwa kura hatua itakayofuata katika Bunge la Katiba baadaye Novemba, mwaka huu.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Bunge, hoja hizo mbili zimetengewa siku tano kuanzia Septemba 9 hadi 13, mwaka huu na mjadala wa marekebisho hayo unatarajiwa kuchukua nafasi hasa kwa wabunge wa pande mbili, CCM cha Chadema juu ya kutengeneza muundo.

Chadema, kimeshatoa baadhi ya mapendekezo yake katika muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Kura ya Maoni ikiwamo kupinga Rais kuteua wajumbe wa Bunge Maalumu wasiotokana na Bunge na Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

0 comments

MAGAZETI YA LEO AGOSTI 27, 2013.


MAGAZETI YA LEO AGOSTI 27, 2013.



.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger