Featured Post Today
print this page
Latest Post

HAPO JANA SHEREHE ILIVYO FANA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIAN HANDENI

HAPO JANA SHEREHE ILIVYO FANA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIAN HANDENI

WANAUME wametakiwa kujenga tabia ya kucheki afya zao badala ya kuwaachia akina mama peke yao, ikiwa ni njia ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi uliozimishwa leo Dunia nzima, huku kiwilaya ya Handeni, yakifanyika katika Kata ya Kwasunga, wilayani Handeni. 
 
 
Kamanda wa Polisi wa Wilaya Handeni, OCD Zuberi Chembera, wa pili kulia mwenye koti jeusi akionyesha ujuzi wa kusakata rhumba katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, ambapo kiwilaya, yalifanyika Kata ya Kwasunga, ambapoi alimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alihudhuria majukumu mengine ya Kitaifa. Picha zote kwa hisani ya Handeni Kwetu Blog.
 
 
Kaimu Mkurugenzi wa Handeni, Mr Mdoe, aliyesimama, akizungumza jambo katika madhimisho ya Ukimwi katika Kata ta Kwasunga, wilayani Handeni mkoani Tanga.
 
 
 Kamanda wa Polisi wa Handeni, OCD Zuberi Chembera, akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi duniani, ambapo kiwilaya yalifanyika katika Kata ya Kwasunga wilayani Handeni mkoani Tanga. Chembera alimuwakilisha DC Muhingo Rweyemamu.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi wa Wilaya Handeni, OCD Zuberi Chembera, akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wilayani hapa.

Akizungumza mbele ya wananchi waliohudhuria katika maadhimisho hayo, OCD Chembera, alisema wanaume wengi hawapendi kupima afya zao, hususan kujua kama wameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi, badala yake wanasubiri matokeo ya wake zao.



 Wanafunzi katika shule ya Sekondari Kwasunga, wakiigiza mbele ya wahudhuriaji katika Maadhimisho ya Ukimwi duniani, katika Kata yao.
 Hapa wanafunzi wakiingia kwa ajili ya kuimba kwaya katika maadhimisho hayo. Hakika yalipendeza kupita kiasi.


OCD Chembera, hapa aliacha kiti na kuwasogelea kwa karibu wananchi kwa ajili ya kuzungumza nao juu ya ugonjwa Ukiwi.

Alisema inapotoke wake zao au wapenzi wao wamepata ujauzito, hugoma kabisa kwenda kupima afya zao, jambo linaloweza kukwamisha harakati za mapambano ya ugonjwa wa Ukimwi ndani nan je ya wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.

"Wanaume tuacheni tabia za kuachia akina mama waende wakapimwe afya zao pale wanapopata ujauzito, maana hiyo si njia nzuri badala yake wote tuwe kitu kimoja na kuyapokea matokeo hayo kwa ajili ya kulinda afya zetu.

"Aidha ni wakati wa kila mmoja wetu kushirikiana kwa dhati katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi ambao unaendelea kuangamiza ndugu zetu, japo kiwilaya maambukizi ya Ukimwi yanaonekana kupungua hadi asilimia 2,” alisema.

Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kwasunga, wananchi wengi walihuudhuria sambamba na kujionea burudani kutoka katika bendi ya Azimio pamoja na magizo kutoka kwa wanafunzi kwenye kata hiyo ya Kwasunga.

Habari hii na picha zote ni kwa hisani ya Handeni Kwetu Blog.
0 comments

PICHA ZA OFISI YA CHADEMA ILIYOPIGWA MOTO HUKO ARUSHA MDA MFUPI ULIOPITA

PICHA ZA OFISI YA CHADEMA ILIYOPIGWA MOTO HUKO ARUSHA MDA MFUPI ULIOPITA

 Hizi  ni picha za Ofisi ya chadema iliyopigwa moto muda mfupi uliopita huko Arusha
0 comments

RAIS KIKWETE AMCHAGUA DR ASHA-ROSE MIGIRO KUWA MBUNGE

RAIS KIKWETE AMCHAGUA DR ASHA-ROSE MIGIRO KUWA MBUNGE

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dr. Asha-Rose Migiro kuwa Mbunge.
Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam leo, Jumanne, Desemba 3, 2013, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dr. Florens Turuka inasema kuwa uteuzi huo umeanza jana, Desemba 2, 2013.
Dr. Asha-Rose Migiro ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa katika Chama cha Mapinduzi.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

3 Desemba, 2013
0 comments

Magazetini leo December 04 2013,

Magazetini leo December 04 2013,

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments

DK SLAA ASITISHA ZIARA YA KIGOMA, NI KUTOKANA NA HALI YA USALAMA KUFUATIA KUVULIWA VYEO MBUNGE WA KIGOMA KASKAZINI.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kushoto na Zitto Kabwe wakimsikiliza Katibu mkuu wa chama hicho Dr Wilbrod Slaa hivi karibuni.


MWANGWI wa uamuzi wa Kamati Kuu ya Chadema wa kumvua madaraka aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto na wenzake, mbali na kutikisa katika kanda sita kati ya kanda nane muhimu za chama hicho nchini, sasa umeanza kukubalika na Sekretarieti ya chama hicho Taifa. 

Jana Kurugenzi ya Habari ya Chadema, ilituma ratiba ya ziara za Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, mikoani iliyoonesha amekubali ushauri wa kusogeza mbele ziara ya kutembelea majimbo nane ya Kigoma.


Awali Dk Slaa alitarajiwa kuanza ziara ya kuimarisha chama mkoani Kigoma kuanzia kesho lakini juzi Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kigoma, Jafari Kasisiko, alisema baada ya kutafakari kwa kina na kwa kutumia hekima na busara, walipendekeza ziara hiyo isogezwe mbele.


Sababu za mapendekezo hayo kwa mujibu wa Kasisiko, ni kutoa nafasi kwa uongozi wa Mkoa, kwenda kuwaelimisha wanachama kutii uamuzi wa Kamati Kuu wa kumvua madaraka Zitto na wenzake, hata kama uamuzi huo umewaudhi, lakini lengo ni kudhibiti vitisho vya kuvuruga amani katika ziara hiyo vilivyokuwa vimetolewa. 


“Mkoa uliomba Taifa liahirishe na kusogeza mbele tarehe ya ziara hiyo muhimu kwa mkoa wetu, ili Mkoa kama ngazi ya chini ya Kanda na Taifa, uende katika majimbo hayo na kuwaelimisha wanachama na wapenzi wetu, kuhusu kuheshimu na kuwa na nidhamu na uamuzi utolewao na ngazi ya juu yetu, hata kama una maumivu. 


“Maoni ya wengi mkoani na kwa viongozi wa Chama ni kuudhiwa na uamuzi wa Kamati Kuu ambao ni dhahiri ulilenga kummaliza Zitto kisiasa. 

Mkoa ulitishika na vitisho baada ya kupokea taarifa kutoka kwa baadhi ya viongozi wa majimbo ya Mkoa, kuwa hali ya usalama si nzuri kwa ujio wa kiongozi wetu Dk Slaa… endapo hali haitokuwa salama Mungu aepushie mbali,” alisema Kasisiko katika taarifa yake. 


Dk Slaa ashaurika Pamoja na Chadema kusisitiza kuwa ziara hiyo itakuwepo, lakini taarifa ya jana ya Kurugenzi ya Habari ya Chadema, ilieleza kuwa badala ya kuanza ziara mkoani Kigoma kama ilivyokuwa awali, sasa ataanza ziara ya siku 20 kuanzia leo lakini mkoani Shinyanga. 


Bila kufafanua atakaa Shinyanga kwa siku ngapi, taarifa hiyo ilifafanua kwamba ziara hiyo itamfikisha Dk Slaa mpaka mkoani Kigoma, ingawa haikueleza lini atakwenda katika mkoa huo anakotoka Zitto na atakaa kwa siku ngapi.


“Siku ya Jumatano Desemba 4 mwaka huu (leo), Katibu Mkuu Dk Slaa atakuwa Wilaya ya Kahama, siku inayofuata Desemba 5, atakuwa Wilaya ya Kakonko, Jimbo la Buyungu na Desemba 6, atakuwa Jimbo la Muhambwe. Ratiba ya siku zinazofuata itaendelea kutolewa kwa vyombo vya habari,” ilieleza taarifa hiyo ya Kurugenzi ya Habari ya Chadema.


Mwenyekiti Singida
Wakati Dk Slaa akianza ziara za kuimarisha chama, vuguvugu la kupinga uamuzi wa kuvuliwa madaraka kwa Zitto, limeendelea kutikisa chama hicho katika kanda zake, ambapo jana katika Kanda ya Kati, Mwenyekiti wa Mkoa wa Singida, Wilfred Kitundu, alijiuzulu. 


Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa tangu 1992, amechukua uamuzi huo kupinga Kamati Kuu kuwavua madaraka akina Zitto, hatua ambayo imeshachukuliwa katika kanda tano za chama hicho nchini. 


“Nimeona ni vema sasa niuthibitishie umma wa Tanzania kuwa kwenye Chadema unaruhusiwa kugombea vyeo na nafasi zote isipokuwa Uenyekiti wa Taifa, ndio maana Zitto tuliyemuunga mkono, leo hii anashambuliwa kwa dhamira yake safi ya kidemokrasia. 


“Tunampa onyo kali Katibu Mkuu Dk Slaa kuwa asithubutu kukanyaga Singida, ikiwa bado hajayafanyia kazi maelekezo yetu hapo juu. Kuzunguka kwake mikoani baada ya kumvua vyeo Zitto ni kwenda kuthibitisha kuwa amefanya makusudi mpango wake huo. 


“Nimejiuzulu Uenyekiti wa Mkoa wa Singida kuanzia leo (jana) tarehe 3.11.2013 na kuahidi kuwa nitapambana mpaka mwisho wa tone la damu ya uhai wangu, kuhakikisha demokrasia ya ndani ya chama hiki inaheshimiwa na kwamba Watanzania hawadanganywi tena,” alisema Kitundu katika taarifa yake ndefu kwa umma. 


Ofisi Arusha
Wakati katika Kanda ya Kati Kitundu akijiuzulu, ofisi za chama hicho za Wilaya ya Arusha, Mkoa na Kanda ya Kaskazini jana zilichomwa moto na watu wasiojulikana. 


Akizungumza na gazeti hili, Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Levolosi, Ephata Nanyaro, alikiri kuchomwa kwa ofisi hizo zilizoko katika jengo moja eneo la Ngarenaro jijini hapa. 


Nanyaro alisema ofisi hizo wana wasiwasi zilichomwa saa moja asubuhi kwa kuwa hali hiyo ilionekana saa mbili asubuhi baada ya ofisi hiyo kufunguliwa na kukuta moto ukiwaka katika baadhi ya maeneo.


“Ofisi imechomwa moto eneo la juu lakini huenda mchomaji alikuja na kutupia moto juu ya paa. Hata hivyo hawajafanikiwa malengo yao maana ni paa tuu na mbao zilizoshika moto,” alisema Nanyaro.


Alisema ana wasiwasi kuwa tukio hilo lilitekelezwa na watu aliowaita wahujumu wa chama chao, ambao ni wale waliofukuzwa hivi karibuni na chama hicho wakiwatumia watu aliowaita kuwa ni wafuasi wao bila kufafanua zaidi. 


Hata hivyo, kiongozi aliyetimuliwa hivi karibuni, Ijumaa iliyopita ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Wilaya ya Monduli, Mchungaji Amani Mollel, ambaye alidaiwa kukiuka kanuni za chama hicho baada ya kuitisha kikao cha kumtetea Zitto.


“Kwa niaba ya Baraza la Uongozi la Mkoa wa Arusha, napenda kuujulisha umma wote kwa ujumla kuwa Mwenyekiti wa Wilaya ya Monduli, Mchungaji Amani Silanga Mollel, amekoma/amesimamishwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Monduli kuanzia tarehe 29 Novemba 2013 kutokana na tuhuma nzito za uvunjifu wa kanuni za maadili ya chama,” alisema Katibu wa Chadema, Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa alipokuwa akitangaza uamuzi huo mwishoni mwa wiki iliyopita.


Kanda zingine
Kanda zingine zilizokwisha kutoa kauli za kupinga Kamati Kuu ni pamoja na Kanda ya Mashariki Dar es Salaam na Pwani, kupitia kwa Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Temeke na mjumbe wa Baraza Kuu, Patrick Joseph, Kanda ya Kusini, Lindi ambako Mwenyekiti wa mkoa huo, Ally Chitanda, alijiuzulu wadhifa wake na kubakia na ujumbe Baraza Kuu Taifa.


Kanda ya Ziwa Magharibi, Mwanza kulitolewa tamko na waliojiita umoja wa matawi 189 ya Chadema Mwanza, yakiongozwa na mwanachama Robert Gwanchele. Kwa sasa Chadema inajiendesha kupitia kanda 10. 


Kanda ya kwanza ni ya Mashariki Dar es Salaam, inayojumuisha mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Kanda ya pili ni Kusini, kwenye mikoa ya Lindi na Mtwara, ikifuatiwa na Kaskazini yenye mikoa ya Tanga, Manyara ,Kilimanjaro na Arusha. 


Pia ipo Kanda ya nne ya Kati inayojumuisha mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida; Kanda ya tano ya Nyanda za Juu Kusini, iliko mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya na Ruvuma. 


Kanda ya sita ya Magharibi inajumuisha mikoa ya Rukwa, Katavi, Tabora na Kigoma; Kanda ya saba ya Ziwa Mashariki yenye mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara na Kanda ya nane ni Ziwa Magharibi, yenye mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera. 


Pia zipo Kanda ya tisa ya Pemba, yenye mikoa ya Pemba Kusini na Pemba Kaskazini na Kanda ya kumi ya Unguja. HABARILEO
0 comments

WAKAZI WA VIJIJI VYA KIDUNDAI, KILUWAI NA VUGA WALILIA BARABARA

WAKAZI WA VIJIJI VYA KIDUNDAI, KILUWAI NA VUGA WALILIA BARABARA

OFISI ya Wakala wa Barabara (Tanroads) mkoani Tanga inaombwa kuangalia uwezekano wa kuiingiza kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha barabara ya Mombo- Bangala chini- Kidundai- Kiluwai- Vuga yenye urefu wa km 9 ili kuwapunguzia kero ya usafiri wananchi wa maeneo hayo.

Wanaomba barabara hiyo ya kiwango cha vumbi kwa kuanzaia angalau itengewe fedha za kuifanyia ukarabati maalum utakaohusisha kazi za kuchonga, kupasua miamba (mawe makubwa) na kunyoosha ili kuwapa fursa wanakivijiji wanaoishi mlimani kusafirisha kwa Mpunga na Mahindi ambayo wanayalima katika mashamba yalioko katika skimu ya umwagiliaji ya Mombo.


Baadhi ya wanakijiji waliozungumza katika mahojiano na mwandishi wa gazeti hili alipotembelea vijiji hivyo mwishoni mwa wiki walisema wanashangazwa na hatua ya Tanroads mkoani Tanga kuamua kuitelekeza barabara yake hiyo kwa miaka mingi sasa bila kuifanyia matengenezo yanayostahili.

Wakulima hao walisema utekelezaji wa hatua hiyo utasaidia sana wavijiji wa Kidundai na Kiluwai vilivyopo kata ya Vuga kupunguza gharama wanayoipata sasa ya kulazimika kusafirisha mazao toka shambani kwa umbali wa zaidi ya km. 30 kwa kupitia barabara ya Mombo- Vuga- hadi Kidundai.


Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Kidundai, Mbwana Rashidi alisema kwa sasa barabara hiyo haipitiki kabisa kwa gari kwasababu inazo kona nyingi zenye mawe makubwa ambazo wananchi wameshindwa kuzinyoosha kwa kutumia sururu na majembe.

“Tunao utaratibu wa kufanya kazi za msaragambo kama wanakijiji ambapo katika barabara mara kadhaa tumelazimika kuchimba kwa mikono ili angalau pikipiki na baiskeli ziweze kupita lakini pamoja na jitihada zetu hizo Tanroads na pia halmashauri yetu hapa wilayani hawajawahi kutusaidia kabisa”,alisema na kuongeza.

“Tunajisikia vibaya na tunadhani serikali yetu imetutenga na Tanroads wametutelekeza kwa hiyo hatuna ila tunahitaji vifaa kama baruti za kuweza kulipulia hayo mawe makubwa njiani ndipo tutaweza kuendelea kuchonga kwa mikono baadhi ya maeneo korofi ili tuweze kupata barabara ya kupitisha magari”,alisema.

Alitaja maeneo hayo korofi yenye mawe makubwa kwamba ni yaliyopo vitongoji vya Madudani ukitokea Bangala chini, Kwemgongo, Kwekiseti, Kwemishwihi na Kiluwai shule na kusema maeneo hayo kwa ujumla yana urefu wa km 4.

Mkulima mmoja aliyejitambulisha kama Mohamed Abdala  alisema kwakuwa Kidundaji iko juu mlimani wanalazimika kushuka uwanda wa chini ambako ni Kata ya Mombo iliyoko wilayani Korogwe ili kulima mazao ya Mpunga na Mahindi kila msimu.

“Kwa hali ilivyo sasa baada ya kuvuna na kupakia mazao kwenye malori tunalazimika kupitia barabara yenye urefu wa km 30 kwa gharama ya sh. 100,000 kwa safari badala ya kutumia sh. 40,000 kwa barabara ya Kidundai yenye urefu wa km 9 kutoka mashambani Mombo ….hii ni kero tunaomba serikali itusaidie”,
0 comments

RC GALLAWA AWAONGOZA WAKAZI WA MKOA WA TANGA MAPOKEZI YA TIMU YA COASTAL UNION BINGWA WA UHAI CUP

RC GALLAWA AWAONGOZA WAKAZI WA MKOA WA TANGA MAPOKEZI YA TIMU YA COASTAL UNION BINGWA WA UHAI CUP



MWENYEKITI WA KLABU YA COASTAL UNION YA TANGA,HEMED AURORA KULIA AKIPOKEA KOMBE LA UHAI CUP TOKA KWA NAHODHA WA TIMU HIYO NZARA NDARO LEO

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU  GALLAWA KUSHOTO AKIPOKEA KOMBE LA UHAI CUP TOKA KWA NAHODHA WA TIMU YA COASTAL UNION NZARA NDARO LEO MARA BAADA YA KUWASILI MKOANI HAPA

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIWAPUNGIA MIKONO MASHABIKI WA SOKA MKOANI TANGA WALIOFURIKA KUWAPOKEA MABINGWA WA KOMBE LA UHAI 2013 COASTAL UNION YA TANGA.

WACHEZAJI WA TIMU YA COASTAL UNION  YA TANGA WAKIWA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI LEO MARA BAADA YA KUWASILI WAKIMSIKILIZA KWA UMAKINI MKUBWA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA LEO

KATIBU MKUU WA COASTAL UNION KASIMU EL SIAGI AKSISITIZA JAMBO NA WACHEZAJI WA TIMU HIYO LEO KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI

MWENYEKITI WA KLABU YA COASTAL UNION YA TANGA,HEMED AURORA "MPIGANAJI ALIYESIMAMA AKIZUNGUMZA KATIKA MAPOKEZI HAYO KULIA KWAKE NI MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA NA KATIBU TAWALA WA MKOA WA TANGA,BENEDICT OLE KUYANI LEO
0 comments

RC TANGA AONGOZA MAPOKEZI YA COASTAL UNION "MABINGWA WA KOMBE LA UHAI"

RC TANGA AONGOZA MAPOKEZI YA COASTAL UNION "MABINGWA WA KOMBE LA UHAI"

Na Oscar Assenga, Tanga.
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa jana aliwaongoza wakazi wa mkoa katika mapokezi ya kuipokea timu ya Vijana ya Coastal Union ambao ni mabingwa wapya wa Mashindano ya Kombe Uhai Cup baada ya kuifunga Yanga kwenye mechi ya Fainali.

Maandalizi ya mapokezi hayo yalianza majira ya saa nane mchana kwa shamrashamra za aina yake huku barabara iliyokua ikielekea kwenye uwanja wa Mkwakwani ilifurika umati mkubwa wa mashabiki wake.

Akizungumza baada ya kupokea kombe hilo, Gallawa ushindi huo ni ishara tosha kuwa historia ya soka mkoa wa Tanga inajirudia kama ilivyokuwa hapo awali hivyo vijana waendelee kujipanga ili kuendelea kupata mafanikio zaidi.

   “Mimi nina furaha kwa sababu mmeijengea heshima Tanga kwa maana ya mkoa mzima na mmenisaidia na kuendelea kufundisha kuwa hakuna kisichowezekana kazi mliyofanya ni mzuri na muendelee kupambana ili muweza kupata mafanikio zaidi “Alisema Gallawa.

Awali akizungumza katika mapokezi hayo, Mwenyekiti wa timu ya Coastal Union, Hemed Aurora aliwapongeza wachezaji hao kwa kufanya vizuri katika mashindano hayo na kueleza ushindi huo umewapa heshima kubwa.
0 comments

AJALI

AJALI

0 027b0
1 96a73
2 3f6b3
Wakazi wa kijiji cha Ndolela Tarafa ya Isimani wilaya Iringa vijijini wakiangalia ajaLi ya Basi la abiria la Urafiki  T 594 ABM lililoanguka kijijini hapo jana likitokea Iringa kuelekea Dodoma. PICHA NA SAID NG'AMILO.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger