Featured Post Today
print this page
Latest Post

DK.KIGWANGALLA HATARINI KUVULIWA UANACHAMA CCM

DK.KIGWANGALLA HATARINI KUVULIWA UANACHAMA CCM

Dar es Salaam. Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis Kigwangalla yuko hatarini kuvuliwa uanachama wa chama hicho, hatua ambayo endapo itachukuliwa itasababisha apoteze nafasi yake ya ubunge.

Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Nzega mkoani Tabora tayari umemjadili Dk Kigwangalla katika vikao vyake vya Kamati za Usalama na Maadili na Kamati ya Siasa, kuhusu kile kinachodaiwa kuwa ni utovu wa nidhamu wa mbunge huyo.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana jioni zinasema baada ya vikao hivyo vilivyofanyika Januari 11 mwaka huu, imeazimiwa kuwa suala la Dk Kigwangalla pamoja na madiwani watano wilayani humo lipelekwe katika ngazi ya CCM mkoa na baadaye taifa.

Dk Kigwangalla jana alipotafutwa kuzungumzia suala hilo alisema: “Hata mimi nimesikia taarifa hizo, isipokuwa sijapewa taarifa rasmi. Ila nafahamu kwamba vikao vya chama vilikuwepo na mimi niliitwa ila kama ambavyo nimeshasema siwezi kuhudhuria”.

Gazeti hili lilimtafuta Mbunge huyo machachari kutokana na taarifa yake aliyoitoa kwenye mitandao ya Facebook na Tweeter akieleza kuhusu taarifa za kuwapo mpango wa kumfukuza uanachama.

Kupitia mitandao hiyo Dk Kigangwalla aliandika: “Nimepokea taarifa kuwa madiwani walioungana na wananchi wa Nzega pamoja na mimi kupinga uamuzi wa Baraza la Madiwani kuzigawa pesa kwenye Kata wameadhibiwa na Kamati ya Siasa ya Chama Wilaya ya Nzega, bila kusikilizwa na ilhali miongoni mwa ‘mahakimu’ hawa ni watu waliokuwa wakilalamikiwa na madiwani na wananchi. “

Mbunge huyo aliongeza: “Nimepewa taarifa kuwa mapendekezo ya adhabu dhidi yangu kutoka wilayani kwenda vikao vya juu, ...tena bila kusikilizwa maana nilitoa udhuru, ni kuwa ninyang’anywe kadi ya uanachama wa CCM. Nimeshangazwa sana na kusikitishwa na jinsi chama kinavyoendeshwa Nzega.”

Mbunge huyo alisema anaamini viongozi wakuu wa CCM wanafuatilia kwa karibu suala hilo na watachukua hatua stahiki, huku akisema hatahudhuria tena kikao chochote cha CCM wilayani humo.

“Kama chama hiki kimefika huku, kwamba kuna watu wana nguvu kuliko chama, kwamba wachache wanaweza kuwaonea wengine kwa kuwa wana vyeo na mamlaka ya kufanya hivyo na hakuna wa kuingilia kati na kusema ‘no’, basi sina haja ya kuendelea kupambana,” aliongeza.

Aliendelea: “Nimechoka, sintokata rufaa wala sintolalamika tena. Watekeleze hukumu hiyo. Sintojitetea na sintohudhuria kikao chochote kile kuanzia sasa, nimechoka kupambana na watu wenye nguvu, nimechoka. Ni bora kuwa mnyonge, lakini ukabaki na uhai, uzima, heshima na furaha yako”.

Kauli ya CCM Nzega

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nzega, Amos Kanuda alikiri Dk Kigwangwalla kujadiliwa katika vikao vya chama vya wilaya, ikiwamo Kamati ya Siasa.
0 comments

WABUNGE WAFUATILIA MIRADI YA WANAWAKE TANGA

WABUNGE WAFUATILIA MIRADI YA WANAWAKE TANGA



Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Said Mtanga akitambulisha wajumbe wa Kamati yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bibi Chiku Ngalawa wakati wa ufuatiliaji wa fedha ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake katika mkoa wa Tanga, tarehe 21/1/2014. Picha na Erasto ching’oro WMJJW. IMG_2334 
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Said Mtanga akisaini kitabu cha wageni cha Kikundi cha Maendeleo ya wanawake Vumilia kinacholima zao la mwani katika kijiji cha Saadani  kata ya Tongoni jijini Tanga tarehe 21/1/2014. Picha na Erasto ching’oro WMJJW. IMG_2352 
Mwenekiti wa Kikundi cha Maendeleo ya Wanake Bibi Hadija Saida akionesha zao la mwani linalolimwa baharini wakati alipotembelewa na Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii na baadhi ya viongozi wa juu wa Harimashauri ya jiji la Tanga tarehe 21/01/2014. Picha na Erasto ching’oro WMJJW. IMG_2394 
Mwenyekiti wa kikundi cha Sanaa Endelevu ‘Arts and Culture’ Bibi Mariam Makoko cha barabara ya 5 jijini Tanga (aliyeko katikati mlangoni) akitoa maelezo kwa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii kuhusu matumizi ya fedha ya Mfuko wa Maendeleo ya wanawake katika kujiletea maendeleo. Picha na Erasto ching’oro WMJJW.
0 comments

CHANETA YAWANOA WALIMU TANGA

CHANETA YAWANOA WALIMU TANGA


CHAMA cha Netiboli (CHANETA) Mkoa wa Tanga, kimeanza kutoa semina ya walimu wa michezo kutoka wilaya zote, lengo likiwa ni kuwaandaa kwa ajili ya kufundisha kwenye michezo ya Umitashumta na Umisseta mkoani Tanga.
 
Akizungumza jijini hapa juzi, Katibu wa chama hicho, Julieth Mndeme, alisema semina hiyo ina lengo la kuwajengea uwezo washiriki na kuhamasisha mchezo huo ambao unaendeshwa na mkufunzi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA), Anna Kibira.
 
Mndeme alisema semina hiyo itaendeshwa kwa siku 11 na ilianza Januari 16 na itafikia tamati Januari 27 ikishirikisha wanawake na wanaume kwenye viwanja vya Bandari.
 
Katibu huyo alisema mikakati waliyokuwa nayo katika kuuendeleza mchezo huo ni kuanzisha ligi za vijana wadogo na kuweka msukumo kwenye mashindano mbalimbali yakiwemo ya wilaya na mkoa.
 
Mndeme alisema ni matumaini yake mafunzo hayo yatakapomalizika watapatikana walimu wazuri ambao watakuwa ni chachu ya kukuza maendeleo ya netiboli kwenye wilaya wanazotoka na mkoa kwa ujumla.

0 comments

BREAKING NEEEWZZZZ!!!!! NDEGE YA ZAN AIR YAANGUKA PEMBA

BREAKING NEEEWZZZZ!!!!! NDEGE YA ZAN AIR YAANGUKA PEMBA

Ndege ya shirika la Zan Air imeanguka Pemba jioni hii ikiwa imebeba jumla ya abiria 19, miongoni mwa abiria hao pia alikuwamo Waziri wa Habari na Katiba wa Zanzibar mhe. Abubakar Kahamis, abiria wote wametoka salama.
 
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger