Featured Post Today
print this page
Latest Post

NYOSSO ASEMA YANGA WALITOKA KIBAHATI MKWAKWANI

NYOSSO AKIMDHIBITI KAVUMBAGU HIYO JUZI

Beki wa Coastal Union, Juma Said Nyosso amesema Yanga walikuwa na bahati zaidi katika mechi yao jana.


Nyosso amesema walikuwa na nafasi kubwa ya kuifunga Yanga kwa kuwa waliizidi sana.
Lakini akasisitiza katika suala la mpira, ni vigumu kwa kulazimisha kitu ambacho hakiwezekani.

“Tulijitahidi kadiri ya uwezo wetu, tulikuwa katika nafasi nzuri ya kuifunga Yanga ingawa naweza kusema mambo yalikataa tu.

“Sisi ndiyo tulicheza vizuri zaidi siku hiyo, lakini bahati haikuwa yetu,” alisema beki huyo wa zamani wa Simba.
0 comments

LOGARUSIC ATAKA WANAJESHI WASIOKATA TAMAA


Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema anataka kuwa na wachezaji wenye moyo wa ushindani na wasiokubali kushindwa.


Logarusic amesema anaamini kuwa na washindani katika kikosi chake ni jambo la msingi zaidi, na haamini watu wanaokata tamaa mapema.
“Kama unakata tamaa mapema, basi hauwezi kufanya kazi na mimi. Nataka wapambanaji.

“Katika maisha kuna mawimbi, hauwezi kusafiri baharini bila ya kukutana na mawimbi. Ukikata tamaa mapema, hautafika unapokwenda.”
Logarusic anaamini kuwa mmoja wa makocha wakorofi lakini amekuwa akisifika kwa kusimamia suala la nidhamu.

Tokea ametua Simba, inaonekana suala la nidhamu limeimarika zaidi na watukutu wamekuwa na hofu.
0 comments

SERIKALI YATAKIWA KUONDOA KWENYE VIFAA VYA UJENZI WA NYUMBA.

SERIKALI YATAKIWA KUONDOA KWENYE VIFAA VYA UJENZI WA NYUMBA.

MWENYEKITI  wa kamati ya   kudumu ya Bunge ya  Ardhi, Maliasiri na Mazingira James Lambeli


Na Elizabeth Kilindi,Mkinga.

MWENYEKITI  wa kamati ya   kudumu ya Bunge ya  Ardhi, Maliasiri na Mazingira James Lambeli, ameitaka serikali kuondoa kodi  kwenye vifaa vya  mradi wa ujenzi wa nyumba za  gharama  nafuu unaoendeshwa na Shirika la Nyumba Tanzania (NHC)  ili kumuwezesha mwananchi wa hali ya chini kuondokana na makazi duni.

Lembeli aliyasema hayo  baada ya  taarifa ya mradi huo iliyosomwa hapo juzi, mbele ya kamati hiyo na Kaimu Mkurugenzi wa uendeshaji wa shirika hilo, Benedict  Kilimba na kueleza kuwa kodi za serikali zimesababisha  bei ya nyumba hizo kuwa kubwa.


Kwamujibu wa taarifa hiyo  ni kwamba  mfumo  wa kuwataka  wanunue  vifaa vya ujenzi  kwenye maduka maalumu kumeongeza  gharama ya ujenzi huo  na kufikia tsh mil, 31.3 kwa nyumba  yenye vyumba viwili na tsh mil, 35.3 hadi tsh mil, 36.2 kwa vyumba vitatu  bila VAT.

Aidha Kilimba alisema kuwa  mbali na changamoto hizo  shirika pia linalazimika kuilipa serikali kiasi cha tsh mil, 7 mpaka tsh mil, 10  kama kodi  ya ongezeko la thamani VAT   kutokana  na  manunuzi ya vifaa vya ujenzi wa kila nyumba jambo lililosababisha nyumba hizo kuuzwa  tsh mili, 40. 7  kwa  nyumba ya vyumba viwili na tsh million 46. 3 hadi  tsh mil, 48.2  kwa vyumba vitatu.

Hata hivyo  alieleza kuwa  kama shirika litaruhusiwa kutafuta maduka yenye unafuu na  serikali ikaondoa  kodi ya VAT  mauzo ya nyumba hizo yangeweza kufikia tsh mili, 28  bei ambayo mtu wa hali ya chini angeweza kuimudu tofauti na ilivyo  sasa.

Akizungumza baada ya taarifa hiyo, Lembeli alisema ni wajibu sasa kwa serikali kuonyesha moyo wa dhati katika kuwawezesha wananchi kumudu kubadilisha maisha yao ikiwemo hili la makazi bora ambayo ni haki ya kila mtu.

Aliahidi kubeba jukumu la kuishauri serikali kuondoa kodi ya VAT  kwenye  vifaa vya ujenzi wa nyumba zinazojengwa na mradi wa shirika hilo hasa zile zilizolengwa kwa ajili ya  makazi bora kwa watu wa hali ya chini.

“Jamani sisi wanakamati yetu tumetembea katika nchi mbalimbali kama vile nchi ya Singopore, tumejionea na  kujifunza jinsi serikali ya nchi hiyo inavyowawezesha watu wake katika makazi bora……..takriban asilimia 90 ya nyumba zilizojengwa na serikali ya nchi hiyo zimeuzwa kwa wananchi kwa bei nafuu, vipi sisi huku!” alihoji Lembeli.

Hata hivyo alidai kuwa taarifa ya shirika hilo kuhusu mazingira ya ujenzi wa nyumba hizo inaonyesha kwamba mtu wa kawaida hatakuwa na uwezo wa kuzinunua kutokana na ukubwa wa bei jambo alilolieleza kuwa linaondoa maana halisi ya azma iliyokusudiwa na serikali yenyewe ama wananchi walalahoi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger