Featured Post Today
print this page
Latest Post

Diwani aliyewekwa ndani na DC ajiuzulu

Diwani aliyewekwa ndani na DC ajiuzulu 


DIWANI wa Kata ya Mswaha-Darajani, Tarafa ya Mombo, Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga (CCM), Aweso Kipaku (34), amejiuzulu nafasi hiyo akipinga hatua ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Mrisho Gambo, kumuweka ndani.

Akizungumza na mwandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Kipaku alisema Bw. Gambo aliagiza awekwe ndani Januari 24 mwaka huu, saa 11 jioni na kupata dhamana saa nne usiku.
Alisema polisi walimkamata, kumpeleka Kituo cha Korogwe lakini Mbunge wa Korogwe Vijijini, Bw. Stephen Ngonyani, alikwenda kumuwekea dhamana na kufanikiwa kutoka.
Mbali ya Kipaku, wengine waliokamatwa na kuwekwa ndani ni Ofisa Mtendaji Kijiji cha Mswaha-Darajani, Bw. Abbas Siafu na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mswaha-Darajani, Bw. Said Kijiwa.
Chanzo cha kukamatwa kwao ni tuhuma zilizotolewa dhidi yao na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya wakidaiwa kuchochea mgogoro wa wakulima na wafugaji kwenye Kijiji cha Mswaha-Darajani.
"Juzi tuliitwa kwa Mkuu wa Wilaya na viongozi wenzangu, baada ya kumalizika Kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Wilaya (Gambo) alimuamrisha OC-CID anichukue na kuniweka ndani hadi nilipopata dhamana usiku.
"Najiuliza mimi kiongozi wa wananchi nadhalilishwa kwa kufungwa pingu, kukaa chini tena nikisukumwa, je, wananchi wangu wapo salama kiasi gani... nimeamua kujiuzulu nafasi ya udiwani kwa vile nimedhalilishwa sana," alisema.
Kipaku alisema tayari ametoa taarifa ya kujiuzulu kwake kwa Katibu wa CCM mkoani humo, Gustav Muba jana ambapo zaidi ya wanachama 300 wa chama hicho wanaomuunga mkono wamerudisha kadi.
Aliongeza kuwa, sababu iliyomfanya awekwe ndani ni kitendo cha kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Kijiji uliofanyika Januari 21 mwaka huu na kudaiwa anachochea mgogoro wa wakulima na wafugaji.
"Wakulima wanataka wafugaji waondoke wakidai mifugo yao inakula mazao...Gambo aliahidi angekwenda kusimamia kazi ya kuwaondoa wafugaji kwenye eneo husika lakini hakufanya hivyo mara tatu, leo hii anasema sisi viongozi wa kata ndiyo tufanye kazi hiyo kana kwamba tuna Jeshi la Polisi," alisisitiza.
Alisema Januari 22 mwaka huu, watu wasiojulikana walikwenda kuchoma moto mazizi ya wafugaji lakini chanzo si viongozi wa kata ni viongozi wa Wilaya na Mkoa ambao wamechelewa kuchukua hatua za kumaliza mgogoro husika.
Juhudi za Majira kumpata Bw. Gambo kuzungumzia sakata hilo zilishindikana ambapo juzi alipigiwa simu lakini ilipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Alhajj Majid Mwanga akidai wapo Tanga kwenye kikao na kuhoji mnataka kuzungumza na Mkuu wa Wilaya kwa suala lipi.
Jana simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ambapo Katibu wa CCM mkoani humo, Muba alikiri kupokea taarifa ya kujiuzulu diwani huyo lakini hakuwa tayari kuzungumza lolote akidai bado hawajajadili uamuzi wake kama wamkubalie au wamkatalie.
"Nimepewa taarifa hiyo lakini tunasubiri barua rasmi, sisi kama chama lazima tumjadili na turidhike na kile kilichofanya ajiuzulu, kama hakina mashiko tunajadiliana na kumuomba aendelee kuwa diwani," alisema Muba

Chanzo;Majira

0 comments

Serikali kuendeleza viwanda nchini

Serikali kuendeleza viwanda nchini

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda 
SERIKALI imeahidi itaendelea kusaidia sekta ya viwanda, hususani vya ndani kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji, ili kuhakikisha vinasaidia kutoa mchango katika kukuza uchumi na maendeleo ya jamii.
Akizumgumza katika sherehe ya kukabidhiwa nyumba mbili za kisasa zilizotolewa msaada na Kampuni ya Saruji Tanga (TCCL) kwa ajili ya watumishi wa gereza la Maweni, mkoani hapa mwishoni mwa wiki, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda, alisema wizara yake itahakikisha viwanda vya ndani vinapata faida, ili viweze kuchangia maendeleo ya jamii zinazowazunguka.
Alisema serikali inafahamu viwanda vya uzalishaji nchini vinachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya jamii kupitia programu za huduma za kusaidia jamii, na kwamba katika siku za karibuni vimeonyesha matokeo chanya.
“TCCL wamekuwa mstari wa mbele kusaidia na kuchangia jamii kwa madhumuni ya kupunguza umaskini, hasa katika maeneo ya vijijini.
“Tanga Cement wameonyesha mifano ya wazi kabisa kwamba viwanda vya wazawa na wageni wanaokuja kuwekeza nchini wanaweza kuwa na mahusiano mazuri na wenyeji wanaozunguka kiwanda husika,” alisema Dk. Kigoda.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Saruji Tanga (TCCL), Reinhardt Swart, alisema kampuni yao wanaelewa programu ya huduma ya kusaidia jamii ni kurudisha fadhila kwa jamii baada ya kufanya au kuwauzia bidhaa zao.
Alisema mwaka jana kupitia programu za huduma za kusaidia jamii, TCCL wametumia takribani sh milioni 327 kwa kujenga na kukarabati shule, zahanati na kusaidia miradi mbalimbali ya jamii nchini.
Aliongeza kuwa hivi karibuni kampuni hiyo imemalizia ujenzi wa maabara ya sayansi kwa Shule ya Sekondari Pongwe na wanatarajia kukabidhi maabara hiyo kwa uongozi wa shule.
Kamishina Msaidizi Mwandamizi (SACP) wa Jeshi la Magereza, Augustino Mboje, alisema jeshi hilo mkoani Tanga linawashukuru viongozi na wafanyakazi wa kiwanda hicho kwa msaada huo kwa sababu utachochea ufanyaji kazi kwa maofisa wa magereza
 
Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments

Kikwete ataka kilimo kutumia teknolojia mpya

Kikwete ataka kilimo kutumia teknolojia mpya

kikwete1 243ba

Rais Jakaya Kikwete amesema ili kuhakikisha sekta ya kilimo inapiga hatua lazima ugunduzi wa teknolojia mpya zinazogunduliwa zitumike kwa vitendo. 

Rais Kikwete alisema bila kuviwezesha vituo vya utafiti na kuwatumia wataalamu wengi wa kilimo kama mabwana na mabibishamba, sekta hiyo haitapiga hatua.

Alikuwa akifungua mkutano wa wadau wa kilimo na biashara kutoka nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya, jana.
Alisema uhifadhi wa vyakula katika maghala hauridhishi, kutokana na asilimia 30 ya mazao yanayohifadhiwa huharibika jambo ambalo linaweza kuepukika likitafutiwa ufumbuzi.

"Tunatakiwa kutumia ugunduzi wa teknolojia mpya zinazogunduliwa ndani na nje ya nchi kwa vitendo, ili kusaidia kuboresha kilimo nchini jambo ambalo linawezekana tukiamua hasa kwa kushirikiana na wadau wengine," alisema Rais Kikwete.
Alisema wakulima wengi hususan wadogo wanatakiwa kupewa elimu jinsi ya kulima mazao ambayo yanaendana na udongo wa eneo husika, kazi ambayo inatakiwa kufanywa na mabwana na mabibishamba na wadau wa kilimo.

"Pia, rasilimali fedha na watu katika vituo vyetu vya utafiti wa kilimo vinahitaji kuongezewa nguvu, ili kufanya tafiti nyingi na zitakazoweza kusaidia kutatua matatizo," alisema.
yanayowakumba wakulima wengi."

Awali akimkaribisha Rais Kikwete, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza alisema aliwataka washiriki wa mkutano huo kujadili jinsi ambavyo wataweza kuwasaidia wakulima wadogo kuondokana na matatizo yanayowakumba kwa kutumia gunduzi za kisasa zinazovumbuliwa.

 Chanzo: Mwananchi
0 comments

Majalada kesi yasombwa na mafuriko Moro

Majalada kesi yasombwa na mafuriko Moro

janwani1 bb2a6

Wakati Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mwanzo Magole, Fredy Mbogela akisema kesi zote zilizokuwa zikisikilizwa katika mahakama hiyo ambayo imesombwa na maji pamoja na mafaili yote, zitaanza upya, Mkuu wa Wilaya na Mkoa wa Morogoro wanahaha kukusanya takwimu za waathirika wa mafuriko. (HM)
Mafuriko makubwa yalitokea katikati ya wiki iliyopita Kijiji cha Magole, huku yakisababisha uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu. Pia, mafuriko hayo yalisomba majalada ya kesi mbalimbali mahakamani hapo.

Akizungumza, Hakimu Mbogela alisema hivi sasa kesi zote za jinai zilizokuwa zikisikilizwa mahakamani hapo zitafunguliwa na kusomwa na kusikilizwa upya.
"Polisi ndiyo watakaofungua na kuzipeleka kesi hizo katika mahakama hiyo, kwa sababu wao wanazo kumbukumbu za kesi hizo kupitia kwa waendesha mashtaka na wapelelezi," alisema Hakimu Mbogela na kuongeza:
"Hakuna kesi itakayofutwa kutokana kuharibiwa majalada hayo, kama nilivyosema polisi watazileta kesi mahakamani, hata kama kulikuwa na kesi iliyokuwa imekaribia hukumu
itaanza upya." alisema.


Alisema: mahakama itaanza kufanya kazi baada ya kufanyiwa usafi na kuweka samani.
Alisema hatua ya awali ambayo inaendelea kufanywa, ni kusafisha jengo la mahakama hiyo ndani na nje kwa kutoa matope, magogo ya miti na taka nyingine ambazo zilikwama eneo hilo na kwamba, utaratibu wa utendaji unaendelea kufanywa.
Naye Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, Nestory Munjunangoma alisema Idara ya Mahakama kwa kushirikina na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wapo kwenye mchakato wa ukaguzi na tathmini ya uharibifu wa jengo la mahakama hiyo.

Munjunangoma alisema hivi sasa jitihada za kufanya ukaguzi na upembuzi yakinifu zinafanyika kabla ya TBA kutoa ushauri kulingana na uharibifu uliotokea kamajengo hilo linaweza kukarabatiwa ama kujengwa upya.

Alisema hivi sasa shughuli za mahakama hiyo zimesimama, kuruhusu usafi wa mazingira. Chanzo: mwananchi
0 comments

Deni la Taifa linapaa, serikalini ni matanuzi

Deni la Taifa linapaa, serikalini ni matanuzi

bot1 52cbf

Hivi karibuni The Citizen liliandika habari ya kushtua katika ukurasa wa mbele, likielezea wasiwasi wa wataalamu na mabingwa kadhaa wa masuala ya uchumi kuwa, Tanzania inakabiliwa na janga kubwa la mzigo wa madeni iwapo Serikali haitapunguza kasi ya mikopo isiyokuwa na tija katika kuinua uchumi. 

Onyo la wataalamu hao linatukumbusha jinsi janga la Deni la Taifa lilivyoligharimu Taifa kiuchumi katika miaka ya 90, ambapo karibu rasilimali zote ambazo Serikali ingezitumia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na pia kuziwekeza katika huduma muhimu za kijamii zilielekezwa katika kulipa madeni. Ni aibu na ukweli ulio mchungu kwamba ilipofika mwaka 2006, Deni la Taifa lilikuwa asilimia 70 ya Pato la Taifa, ingawa msamaha wa madeni ulipunguza kiwango hicho hadi asilimia 21 mwaka uliofuata.
Hata hivyo, kilichoendelea baada ya pale ni uthibitisho kwamba Serikali haikupata fundisho kutokana na janga hilo, kwani ilizidisha kasi ya kukopa kiasi kwamba
Deni la Taifa hivi sasa linakadiriwa kuwa kati ya asilimia 40 na 50 ya Pato la Taifa, ambalo linakadiriwa kuwa Sh50 trilioni. Ni vigumu kuamini kwamba Deni la Taifa limekua kwa kasi ya kutisha kutoka Sh10 trilioni mwaka 2005 hadi Sh27 trilioni mwishoni mwa mwaka uliopita.


Kama baadhi ya wataalamu wa masuala ya uchumi wanavyohadharisha, suala hapa siyo Serikali kukopa, bali ni kwamba mikopo hiyo inayokadiriwa kuwa Sh2 trilioni kila mwaka inachukuliwa kufanya kitu gani? Takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zinaonyesha kwamba Deni la Taifa lilipaa kwa Tsh5 trilioni kati ya Januari na Oktoba mwaka uliopita.

Mtaalamu mmoja wa uchumi ametukumbusha jinsi miaka ya 70 Serikali ilivyokopa Sh96 bilioni kuanzisha Kiwanda cha Viatu Morogoro, lengo likiwa kuuza viatu nchini Italia. Kutokana na kufilisika kilibinafsishwa miaka ya 90 na hivi sasa majengo yake yamegeuzwa kuwa ghala, huku deni la uanzishwaji wa kiwanda hicho likiwa limelipwa kupitia kodi za wananchi. Mfano mwingine ni bajeti ya Sh122.4 bilioni ya kusambaza pembejeo za ruzuku kwa wakulima kwa mwaka 2011/12, ambapo Tsh89 bilioni zilikuwa ni mkopo kutoka Benki ya Dunia.

Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imefichua uvundo na ufisadi mkubwa katika mfumo mzima wa pembejeo za ruzuku. Kwa hiyo, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) inakutana leo kupokea na kujadili ripoti hiyo. Kwa mfano, katika Kijiji cha Lunyala
, wilayani Nkasi, mkoani Rukwa asilimia 70 ya wananchi walioorodheshwa kupata mbolea walikuwa bandia, huku Benki ya Dunia ikikaririwa ikisema asilimia 60 ya Bajeti ya pembejeo za ruzuku ililiwa na mafisadi.


Kinachosikitisha ni kwamba Deni la Taifa litalipwa na wananchi wote ingawa waliofaidika nalo ni mafisadi na viongozi wachache walio serikalini na mashirika ya umma. Lakini kinachosikitisha zaidi ni tabia ya Serikali kuendelea kukopa kwa lengo la kuendeleza matanuzi na matumizi makubwa yasiyo ya lazima.

Mfano mzuri ni ziara fupi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mkoani Mtwara mwishoni mwa wiki, ambapo aliongozana na ujumbe mkubwa kupita kiasi na magari ya kifahari ya Serikali yasiyopungua 30. Sisi tunadhani unahitajika mjadala mpana wa kitaifa kuhusu Deni la Taifa.

Chanzo: mwananachi
0 comments

MKWAKWANI KUKARABATIWA TENA BAADA YA KUMALIZIKA MZUNGUKO WA PILI WA LIGI KUU

MKWAKWANI KUKARABATIWA TENA BAADA YA KUMALIZIKA MZUNGUKO WA PILI WA LIGI KUU


Na Oscar Assenga, Tanga.
UONGOZI wa Uwanja wa Mkwakwani umesema awamu ya pili ya ukarabati wa uwanja huo unatarajiwa kufanyika mara baada ya kumalizika mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara mwaka huu lengo lao likiwa ufikie kwenye viwango vya kitaifa na kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga,
  Gustav Mubba wakati akizungumza na waandishi wa habari uwanjani hapo ambapo alisema suala la ukarabati wa uwanja huo ni mkakati wao waliojiwekea kila mwaka.


Mubba alisema mara baada ya uwanja huo kumalizika mashabiki wa soka
  mkoani hapa wanapaswa kuwa na nidhamu kwa kuacha kuingia uwanjani wakati mchezo ukiwa umalizika kwani kufanya hivyo kunaweza kusababisha uharibifu wa vitu vilivyopo uwanjani hapo.    “Napenda kuwaomba mashabiki wa soka baada ya kumalizika mpira wawe na nidhamu waache kuingia uwanjani baada ya kumalizika mechi kwani baadhi yao wanachana nyavu za magoli kitendo ambacho kinaleta usumbufu mkubwa sana “Alisema Mubba.

Aliwataka mashabiki wa soka wajifunze nidhamu ya matumizi ya uwanja
  hasa kwenye mechi ya Yanga na Coastal Union wa wale wanaotokea Dar es Salaam na mikoa mengine kuja kushuhudia mechi hizo wawe wastaharabu na kuacha kuleta vurugu.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger