Featured Post Today
print this page
Latest Post

Leo hii rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amehudhuria msiba wa Balozi Abrahamu Sepetu (Baba mzazi wa Wema Sepetu) uliotokea hapo juzi jijini Dar es Salaam.

Leo hii rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amehudhuria msiba wa Balozi Abrahamu Sepetu (Baba mzazi wa Wema Sepetu) uliotokea hapo juzi jijini Dar es Salaam.









Mheshimiwa kiwete amefika msibani akiongozana na mkewe hapo kutoa pole kwa familia hiyo kwa  kuondokewa na Balozi Sepetu ambaye hapo alishawahi kushika nyadhifa mbalimbali kwenye serikali nchini ikiwemo ya kuwa waziri wa mambo ya nje kwenye miaka ya sabini (70) kabla  ya kuwa balozi wa urusi kwenye kipindi cha miaka ya 80. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
0 comments

TIMU YA AZAM FC YAILAMBISHA SIMBA KONI KATIKA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM

TIMU YA AZAM FC YAILAMBISHA SIMBA KONI KATIKA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM

Mshambuliaji wa Azam FC Kipre Tchetche akipambana na Issa Rashidi"Baba Ubaya" wa Simba FC.

Timu ya Azam imeichapa  timu ya Simba kwa mabao 2-1 leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwenye muendelezo wa mechi za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.Bao la Simba lilifungwa na Ramadhani Singano na mabao ya ushindi ya Azam yalifungwa na mshambuliaji wao hatari kutoka Ivory Coast Kipre Tchetche.Kwa ushindi huo Azam inaongoza ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.
0 comments

UWEZI AMINI TANZANIA IMETEGWA TENA KATIKA MKUTANO WA EAC


UWEZI AMINI TANZANIA IMETEGWA TENA KATIKA MKUTANO WA EAC

NCHI za Tanzania na Burundi, kwa mara nyingine zimetengwa na wenzao wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya marais wa Kenya, Uganda na Rwanda kukutana mjini Kigali jana. Marais hao walitarajia kujadili namna ya kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia uimarishwaji wa miundombinu, uchumi, biashara pamoja na kuweka mikakati ya shirikisho la kisiasa.

Kitendo cha kuziacha Tanzania na Burundi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kinazidi kutia shaka mtangamano wa jumuiya hiyo.

Nchi hizo mbili zimeshaeleza kusikitishwa na muungano wa nchi hizo tatu, ambao zimesema unakwenda kinyume cha makubaliano na mkataba wa EAC.

Katika mkutano huo, marais hao, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda na Uhuru Kenyatta wa Kenya, pamoja na mambo mengine, walitarajia kusaini makubaliano ya kuanzisha kituo kimoja cha kukusanya ushuru kinachotarajia kurahisisha uchukuzi wa bidhaa kutoka Mombasa nchini Kenya, Uganda hadi Rwanda.

Aidha Sudan Kusini ilialikwa ikiidhinishwa kama mshirika katika kikao hicho.

Mkutano huo unakuja baada ya ule uliofanyika mjini Kampala, Uganda, Juni mwaka huu na mwingine uliofanyika Mombasa, Agosti, ambako viongozi hao watatu walipendekeza kupanuliwa kwa Bandari ya Mombasa, ili kuwezesha uharaka wa bidhaa kupitishwa katika kuhudumia kanda nzima.

Mkutano mwingine wa marais wa nchi 15 za Afrika, ikiwamo Tanzania, utafanyika leo nchini hapa, katika kongamano la siku nne ambalo linatarajiwa kuweka kipaumbele kwa uimarishwaji wa huduma za internet katika mataifa hayo.


Kwa mujibu ya waandaaji, zaidi ya wajumbe 1,500 watahudhuria mkutano huo, chini ya uenyeji wa Rais Paul Kagame na Dk. Hamadoun I. Toure, Katibu Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ya Kiteknolojia (ITU).
-Mtanzania
0 comments

COASTAL UNION WAISHIKISHA ADABU MTIBWA SUGAR,WAICHAPA 3-0

COASTAL UNION WAISHIKISHA ADABU MTIBWA SUGAR,WAICHAPA 3-0


KIKOSI CHA COASTAL UNION KIILICHOICHAPA MTIBWA SUGAR BAO 3-0 LEO KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI. TANGA


WACHEZAJI WA MTIBWA SUGAR NA COASTAL UNION WAKISALIMIANA KABLA YA KUANZA MPAMBANO HUO

WACHEZAJI WAKIINGIA UWANJANI LEO .
Na Oscar Assenga,Tanga.
TIMU ya Coastal Union ya Tanga leo wakiwa chini ya Kocha Joseph Lazaro wamefanikiwa kuibamiza Mtibwa Sugar mabao 3-0,katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa uwanja w a Mkwakwani mjini hapa.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkubwa ambapo Coastal Union waliweza kuandika bao lao la kwanza kwenye dakika ya 20 kupitia Crispian Odulla aliyemalizia kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Moshi “Boban’
Baada ya kuingia bao hilo,Coastal Union waliweza kuendeleza wimbi la mashambulizi langoni mwa Mtibwa Sugar na kufanikiwa kuongeza bao la pili lililofungwa dakika ya 38 kupitia Jerry Santo kwa njia ya penati iliyotokana na Keneth Masumbuko wa Coastal Union kuangushwa katika eneo la hatari na Yusuph Nguya wa Mtibwa Sugar na mwamuzi wa mchezo huo Hashim Abdallah kuamuru ipigwe penati.
Mpaka timu zote zinakwenda mapumziko Coastal Union walikuwa wakiongoza kwa bao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa kila timu kuingia uwanjani hapo zikiwa na hari mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Wakionekana kujipanga baada ya kufanya mabadiliko kwa kuwatoa baadhi ya wachezaji wake wakiwemo Dickson Mbeikya na kumuingiza Jamal Mnyate hali ambaye iliweza kukiongezea nguvu kikosi hicho.
Kutokana na mabadiliko hayo,Mtibwa Sugar waliweza kujipanga na kupeleka mashambulizi langoni mwa Coastal Union lakini Mlinda mlango wake,Shabani Kado aliweza kuwa shujaa kwa kupangua mashuti makali ambayo yalikuwa yakiekezwa langoni lake.
Kwa kuonyesha wao wanacheza kwa umakini mkubwa,Coastal Union waliweza kubadilisha aina ya mchezo ambao walikuwa wakioncheza hapo awali na kufanikiwa kulishambulia lango la Mtibwa Sugar kwa dakika kadhaa na hatimaye Coastal Union kuweza kuhitimisha karamu ya mabao langoni mwa Mtibwa kupitia Daniel Lyanga baada ya kutokea piga ni kupige langoni mwa timu hiyo.
Mwisho.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger