Featured Post Today
print this page
Latest Post

NAIBU WAZIRI MAKAMBA ATAKA WANAWAKE KUJIUNGA NA VIKUNDI

            
Raisa Said, Bumbuli.
 MBUNGE wa Jimbo la Bumbuli, January  Makamba amewataka wanawake na vijana wa Jimbo hilo kuanzisha vikundi vya ujasiriamali ili waweze kupata mikopo kutoka taasisi mbalimbali likiwemo shirika la Maendeleo la Bumbuli.
 
Akizungumza kwa niaba  ya  Makamba,Makamu Mwenyekiti  wa Halmashauri  hiyo Bakari Kavumo wakati  wa  uzinduzi  wa kikundi  cha  Tumaini (VIKOBA)  kilichopo  kata   ya Soni alihimiza uanzishwaji wa vikundi na kwamba kufanya hivyo kutawarahisishia upatikanaji mikopo na misaada kwa wahisani.

Pia Mbunge  huyo  alichangia  shilingi 3. milioni  kama  mtaji  wa  kuendesha  kikundi hicho  ambacho kimezinduliwa  katika  jimbo  lake lengo  kubwa  kuwakomboa  wanawake  na umaskini. 

 
Alisema ni vema wananchi hao wakaanzisha  vikundi  maalumu ambavyo vitafahamika kisheria na hivyo kuwa njia mbadala ya kujinasua na umasikini badala ya kutegemea shughuli za mtu mmoja mmoja.
 
Makamba ambae  pia ni  Naibu  Waziri wa  Mawasiliano  Sayansi  na  Teknolojia  aliahidi kusimamia vikundi hivyo na kuhakikisha kuwa akinamama na vijana waliyojiunga wanapata mikopo kutoka Shirika hilo la Maendeleo ya Jimbo la Bumbuli (BDC).

Alisema atatekeleza hayo ikiwa ni miongoni mwa ahadi zake alizozitoa wakati wa kuomba ridhaa ya ubunge kwa wakazi wa Jimbo hilo na kwamba licha ya mikopo hiyo atahakikisha kuwa sekta zote muhimu zinapata mabadiliko huku akiwa na  nia  kuwakwamua  wana  bumbuli  kiuchumi.


Shirika la Maendeleo la Bumbuli lilianzishwa rasmi mwaka juzi na  Mbunge wa Jimbo hilo, January Makamba kwa ajili kuratibu na kuharakisha maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.

Taasisi ya Utoaji Mikopo ya shirika hilo, BDC-MFI imeanzishwa kama chombo cha kuziba pengo lililopo la ukosefu wa mitaji na vyombo vya utoaji mikopo kwa ajili ya wajasiriamali wa kawaida.
                        MWISHO
0 comments

MWANAHARAKATI ATAKA SERIKALI KUSITISHA MCHAKATO WA KATIBA

MWANAHARAKATI ATAKA SERIKALI KUSITISHA MCHAKATO WA KATIBA 

 

 


Raisa  Said, Tanga
 
Katika hatua inayotishia mchakato wa upatikanaji katiba mpya, mwanaharakati mmoja wa Tanga amefungua shauri linaloitaka serikali kusitisha mchakato  hadi hapo itakapofanyia marekebisho ya masuala ambayo amedai kuwa yanakiuka katiba ya sasa, utawala bora, uwazi, demokrasia na haki ya kijamii.

Mwanaharakati huyo, Dr. Muzamil Kalokola, ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Kuhifadhi Mawazo ya Mwalimu Nyerere alifungua shauri hilo juzi katika Mahakama Kuu jijini Tanga dhidi ya  Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba Kama mdaiwa wa Kwanza, Tume ya Mabadiliko ya Katiba, kama mdaiwa wa Pili na Mwanasheria wa Serikali kama mdaiwa wa tatu.

Mdai huyo anataka Mahakama itoe  amri kumzuia Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba kutoendelea na mchakato huo hadi hapo shauri hilo litakaposikilizwa.

Pia ameitaka mahakama kutoa amri na  kutamka kwamba Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekiuka katiba ya sasa kwa kutoa uwezo ambao juu ya uwezo wao wa kikatiba hususan masuala ambayo yanayohusiana na orodha iliyoko katika Nyongeza ya pili ya Katiba hiyo.

Dr. Kalokola pia ameiomba Mahakama kutamka kwamba uteuzi wa wabubnge wa Bunge la Katiba haukufuata misingi mikuu ya demokrasia kitu ambacho kimeathiri uhalali wa Bunge hilo.

Mwanaharakati huyo ameiomba mahakama kutupilia mbali uteuzi wa wajumbe wa Bunge hilo kwa kutofuata misingi ya demokrasia na uwakilishi.

Katika shauri hilo ameitaka mahaka kuliazimisha Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutumia uwezo na wajibu wake kusahihisha udhaifu katika masuala yote ambayo yanakikuka katiba katika muda ambao utatolewa na Mahakama hiyo.

Mwanaharakati huyo pia amezungumzia posho za wabunge hao na kuitaka mahakama kuzikataa kwa sababu zitakua mzigo kwa kiuchumi kwa taifa.

MWISHO
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger