Featured Post Today
print this page
Latest Post

HALI YA USALAMA YAZIDI KUZOROTA JAMUHURI YA AFRIKA YA KATI

HALI YA USALAMA YAZIDI KUZOROTA JAMUHURI YA AFRIKA YA KATI

GIGI_3b22b.jpg
Waasi wa kundi la kikristo la Anti Balaka katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wametishia kuwaua mamia ya waislamu wanaojificha katika kanisa moja kama hawataondoka nchini humo katika kipindi cha wiki moja ijayo.

Wanajeshi wa kulinda amani wapatao 30 kutoka Cameroon walilazimika hapo jana kufyatua risasi hewani ili kuwatawanya wapiganaji wa Anti Balaka waliokuwa wamekusanyika nje ya kanisa hilo la Kikatoliki wakipania kuwaua waislamu hao ambao wamekimbilia katika kanisa hilo kuokoa roho zao.

Milio hiyo ya risasi iliwaogofya watoto waliokimbia kujinusuru na vilio vya watu hao waliojawa na uoga vilisikika vikirindima katika kanisa hilo.Wanajeshi hao wa kulinda amani kwa sasa ndiyo tegemeo la pekee kwa waislamu hao wapatao 800 dhidi ya kushambuliwa na magenge yanayotaka kuwaua.


Wapiganaji wa Anti Balaka tayari walionekana wakiwa na mitungi ya lita 40 ya petroli ambayo wametishia kutumia kulichoma kanisa hilo.Kasisi wa kanisa hilo Justin Nary ambaye anatoa hifadhi kwa waislamu hao anajua analengwa na waasi hao.

Waasi walizingira kanisa kuwasaka waislamu
Kasisi Nary amesema wapiganaji hao wa Anti Balaka wamemtishia maisha mara nne kwa kumulekezea mtutu wa bunduki na wamempigia simu kumuonya kuwa punde tu wanajeshi wa kulinda amani wataondoka,watamuua.

Baadhi ya wanaotafuta hifadhi katika kijiji hicho cha Guen wametoroka baada ya kiasi ya waislamu 70 kuuawa katika siku za hivi karibuni.Waislamu na wakristo walikuwa wakiishi kwa amani tangu jadi hadi kundi la waasi la kiislamu kutoka Kaskazini mwa nchi hiyo lilipoipindua serikali na kulitumbukiza taifa hilo katika ghasia.

Kundi hilo la kiislamu la Seleka linashutumiwa kwa mauaji katika vijiji vya wakristo katika taifa hilo.Viongozi waliosaidiwa na Seleka kuingia madarakani walipoondolewa madarakani mwezi Januari,ilichochea mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa kundi lililoibuka la Anti Balaka.

Mauaji yaripotiwa katika miji mingine
Mji mkuuu Bangui ambao ulikuwa ni kitovu cha maasi na ghasia tangu mwezi Desemba kwa sasa hali inaonekana kudhibitiwa kwa kiasi fulani lakini mauaji yanayofanywa kwa misingi ya kidini yanaendelea kuripotiwa katika miji mingine nchini humo.
Majeshi ya Ufaransa na ya umoja wa Afrika yaliyoko nchini humo kudhibiti hali hayatoshi kukidhia mahitaji ya kiusalama na kiulinzi yanayohitajika kwa dharura.

Umoja wa Mataifa umeiomba Jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua kabambe na za dharura kuisaidia Jamhuri ya Afrika ya Kati kujikwamua kutoka kwa mzozo mbaya unaotishia kulisambaratisha taifa hilo.

Bunge la Ufaransa hii leo linatarajiwa kupiga kura kuidhinisha kuendelea kusalia kwa jeshi lake nchini humo hadi mwezi Februari mwaka ujao wakati ambapo Jamhuri ya Afrika ya Kati itafanya chaguzi.

Waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean Yves Le Drian amekiri kuwa itachukua muda mrefu kuliko walivyotarajia kurejesha udhabiti nchini humo kutokana na kiwango cha juu cha uhasama na ghasia.Maelfu ya watu wameuawa tangu Desemba na zaidi ya watu milioni moja wameachwa bila makaazi.
Chanzo, dw.de.com/swahili. R.M
0 comments

OPERESHENI DHIDI YA WAASI WA UGANDA ADF

OPERESHENI DHIDI YA WAASI WA UGANDA ADF

UGANDA_98bb6.jpg
 Waasi wa Uganda ADF.

Operesheni zinaendelea katika wilaya ya Beni, jeshi la serikali limetangaza kuwa, operesheni hizo, zimelipelekea jeshi hilo kuyakomboa maeneo kadhaa, toka mikononi mwa waasi.
Operesheni dhidi ya waasi wa Uganda ADF wanaojihifadhi katika misitu
ya wilaya ya Beni mashariki mwa jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikiwa zinaendelea,huku wanajeshi wakiwa wamepelekwa katika eneo hilo, raia wa mji na wilaya za Beni wameanza kulalamikia usalama wao,kutokana na jinsi wanavyo nyanyaswa na wanajeshi wa serikali. Ili kukomesha vitendo vya unyanyasi wa raia, jeshi la Congo limelivalia njuga suala hilo.
Mwandishi wetu John Kanyunyu na ripoti kamili kutoka Beni. Kusikiliza ripoti hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Chanzo, dw.de.com/swahili. R.M
0 comments

BILIONI 2.4 ZAHITAJIKA UKARABATI WA MIUNDOMBINU SHULE YA SEKONDARI TANGA SCHOOL

BILIONI 2.4 ZAHITAJIKA UKARABATI WA MIUNDOMBINU SHULE YA SEKONDARI TANGA SCHOOL


(Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake)
 
NA OSCAR ASSENGA,TANGA
 
JUMLA ya sh. Bilioni 2.4 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu katika shule ya sekondari ya Tanga School iliyopo mkoani Tanga kutokana na uchakavu ilionao baadhi ya majengo kwenye shule hiyo.

Shule hiyo inahitaji ukarabati wa miundombinu iliyokuwepo tokea mwaka 1967 ikiwemo madarasa,maabara,karakana, maktaba, mabweni,bwalo na zahanati ambazo ukarabati huo utaifanya kuonekana na muonekano mpya.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo amesema maeneo mengine yanayohitajika ukarabati ni viwanja vya michezo,nyumba za walimu ,Jengo la Utawala,Chumba cha Kompyuta na duka na Mgahawa wa shule pamoja na gari la shule.


Gallawa ameongeza kuwa maeneo mengine ni miundombinu ya maji taka,uzio wa shule,uwekaji wa solar power,ufungaji wa security lights,ujenzi wa ofisi ya serikali ya wanafunzi,upakaji rangi wa majengo ya shule na ujezi wa miundombinu ya kuvuna na kuhifadhi maji.
wa kwanza kulia ni Mwandishi wa gazeti la Citizen mkoa wa Tanga,George Sembony ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliosoma kwenye shule ya sekondari ya Tanga School akiwa na walimu wakuu waliopitia shule hiyo na wa sasa.
 Amesema kazi ya kukarabati imepangwa kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itagharimu bilioni 1.4 ambayo itafanya ukarabati wa mabweni ya wasichana na wavulana,samani za madarasa, maktaba, maabara, bwalo,uzio wa shule na nyumba.
Aidha ameongoeza maeneo mengine kuwa ni Jengo la Utawala,Maegesho ya magari,miundombinu ya majitaka,ukarabati wa barabara ikiwemo zahanati kufanyiwa ukarabari katika awamu hii wakati awamu ya pili itagharimu  zaidi ya bilioni 1.
 
Mafundi wakiendelea na ufundi wao kwenye shule hiyo kwenye eneo la karakana.



Akizungumza mkakati wa upatikanaji wa fedha hizo,Mkuu huyo wa mkoa amesema kamati maalumu ya kuratibu zoezi zima imeundwa katika mkoa wa Tanga chini yake ikiwahusisha baadhi ya wakuu wa shule hiyo waliopita na aliyeko madarakani,wataalamu mbalimbali na wajumbe wa bodi kwa kuanzia.
baadhi ya majengo yaliyopo kwenye shule hiyo yanavyoonekana wakati mtandao huu ulipotembelea shuleni hapo
 Kamati hiyo imependekeza mikakati kwa ajili ya kupata fedha hizo ikiwemo kuwakutanisha watu wote walisoma au kufanya kazi shule hiyo pamoja na kutafuta wahisani mbalimbali ndani na nje ya mkoa.
Suala lengine litakalo fanyika ni kuandaa matamasha mbalimbali ikiwemo wazazi za walezi wa wanafunzi waliopo shule hiyo ambapo kamati hiyo itakutana na wadau walisoma shuleni hapo Machi 15 mwaka huu kwenye ukumbi wa bwalo la shule hiyo.

Baada ya mkutano huo makubaliano yataelezwa kwa wadau na mpango wea utekelezaji utaandaliwa

Shule hiyo ilianzishwa mwaka 1895 chini ya utawala wa kijerumani ambapo shule hiyo hapo awali ilijengwa mjini eneo la mkwakwani ambapo hivi sasa kuna shule ya sekondari Old Tanga.
0 comments

Wakulima wilayani Handeni waaswa kulima mazao ya biashara na chakula

Wakulima wilayani Handeni waaswa kulima mazao ya biashara na chakula



Na Mwandishi Wetu, Handeni

WANANCHI wilayani Handeni, mkoani Tanga, wameaswa kulima maza ya biashara na chakula ili kuwaondolea balaa la njaa linalowakumba kila mwaka kutokana na kutegemea kilimo cha aina moja, yakiwamo mahindi.
 
Mkuu wa Wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu, pichani.
 
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Muhingo Rweyemamu katika mahojiano maalum wilaya Handeni mkoani Tanga, ikiwa ni sera na mipango kabambe ya kuweka sawa jambo hilo kwa maendeleo ya wananchi wa Handeni na Tanzania kwa ujumla.


DC Muhingo alisema kuwa wakazi wengi wa Handeni wanategemea kilimo cha mahindi kama zao la biashara na chakula, jaambo linalowafanya kila wakati watu wengi wakabiliwe na njaa na kuwafanya waishi kwa tabu wakati wote.

“Ofisi yangu inajitahidi kuwaelimisha wananchi wengi waone ipo haja sasa ya kulima mazao mengi ya biashara, ukizingatia kuwa sasa wengi wao wanategemea mahindi kama zao la chakula na baadaye huuza kwa mahitaji yao.

“Naamini yapo mazao mengi ambayo endapo yatalimwa kwa wingi, mahindi yatahifadhiwa kwa ajili ya chakula wao na familia zao, maana suala la njaa Handeni linatokea kwasababu kuna mapungufu mengi, hasa ya chakula kuwa haba,” alisema.

Kwa mujibu wa Muhingo, elimu ya ziada kwa wananchi na wakulima wote kwa ujumla inahitajika wilayani humo ili watu wazoee kulima mazao mbalimbali, ukiwamo ufuta, maharage na mengineyo kwa ajili ya biashara na kuweka akiba ya chakula kwa zao la mahindi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger