Featured Post Today
print this page
Latest Post

BREAKING NEWS: MJUMBE WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) ATANGAZA KUJIUZULU WASIFA HUO..

BREAKING NEWSSSSSS .... PROF. BAREGU NAYE PIA AJIUZULU CHADEMA....MAJANGA HAYA CHADEMA!!!!Prof Mwesiga Baregu.

Habari zilizotufikia katika chumba chetu cha habari zinaeleza kuwa Mjumbe wa tume ya mabadiliko ya Katiba kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) ametoa kauli ya kujiondoa na kujiuzulu nafasi zake ndani ya Chama hicho kupelekea maamuzi yaliyofanywa na kikao cha kamati kuu ya chama hicho.


Huyu ni Mjumbe wa pili wa kamati kuu ya Chadema kuamua kujiuzulu wadhifa wake katika kipindi kisichozidi masaa 12. CHANZO http://hisiazamapenzi.blogspot.com
0 comments

NEWS ALART: AJALI YAUA WANNE PAPO HAPO RUFIJI 

 (PICHA KUTOKA MAKTABA)

WATU wanne wafanyabiashara wa nguo za mitumba wamekufa papo hapo na wengine nane wapo mahututi baada ya gari walilokuuwa wakisafiria kutoka mikoa ya kusini kwenda jijini Dar esalaam kuacha njia na kupinduka na kusababisha maafa hayo. Tukio hilo limetokea Novemba 22 asubuhi katika kijiji cha Londondo Chumbi Tarafa ya Mohoro katika barabara kuu ya Kilwa Dar esalaam wilayani Rufiji Mkoani Pwani Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama wa wilaya ya Rufiji Nuhudin Babu amethibitisha tukio hilo ambapo amewataja waliokufa ni Fadhili Chaula(55),Ally Mohamed (25),Ally Mnutu (41)pamoja na Selemani Liangavi(45) wote wakazi wa Dar salaam. Babu ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Rufiji amesema katika ajali hiyo watu zaidi ya 10 walijeruhiwa lakini nane kati yao ndiyo hali zao zilikuwa mbaya na hivyo walichukuliwa na kukimbizwa katika hospitali ya Muhimbili Dar salaam kwa ajili ya matibabu zaidi. Mwenyekiti huyo wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani humo ameeleza kuwa ajali hiyo imehusisha gari T 198 ARQ Isuzu Forwad iliyokuwa ikiendeshwa na Ally Mkango kutokea Newala kwenda jijini Dar esalam. Amesema hata hivyo dereva huyo alikimbia mara baada ya kutokea tukio hilo na kwa sasa anaendelea kutafutwa na jeshi la Polisi mkoani humo ili kujibu tuhuma zinazomkabili. Ameongeza kuwa msaidizi wa dereva huyo Haji Khatibu (28) anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo na chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kutozingatia sheria zilizopo barabaran
0 comments

AGE AWASILI KISHUJAA, MAMIA WAMLAKI UWANJA NDEGE, ASEMA YEYE BADO MWENYEKITI SIMBA, HANS POPPE NAYE…

AGE AWASILI KISHUJAA, MAMIA WAMLAKI UWANJA NDEGE, ASEMA YEYE BADO MWENYEKITI SIMBA, HANS POPPE NAYE…

Na Mahmoud Zubeiry, JNIA
MWENYEKITI wa Simba SC, Ahaj Ismail Aden Rage amewasili Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam usiku huu akitokea Sudan na kusema kwamba; “Mimi bado Mwenyekiti wa Simba SC,”.
Rage aliwasili kwa ndege ya shirika la Kenya saa 1:40 usiku na kutokea mlango wa Watu maalum (VIP) ambako alilakiwa na wanachama zaidi ya 200, waliokuwa kwenye mabasi sita aina ya Coaster.
“Umati huu uliokuja hapa ni kielelezo tosha sana kwamba kiasi gani wanachama wa Simba wana imani na Mwenyekiti wao, sasa leo sitasema mengi, nitakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari kesho saa saba mchana makao makuu ya klabu(Msimbazi),”alisema Rage.
Rage akiinua mikono juu kishujaa wakati anatoka Uwanja wa Julius Nyerere, Dar es Salaam usiku wa leo

Alipoulizwa kuhusu kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Jumatatu na kutangaza kumsimamisha, Rage alisema; “Kwa mujibu wa Katiba ya Simba, Kamati ya Utendaji haina uwezo wa kumsimamisha Mwenyekiti, usinimalizie utamu Zubeiry, njoo kesho mchana Msimbazi,”alisema. 
Watu zaidi ya 200 walifika Uwanja wa ndege tangu saa 11 na ushei jioni ya leo kumsubiri Rage wakiimba nyimbo mbalimbali za kumbeza Kaimu Makamu Mwenyekiti, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ na kumpamba Rage huku wakicheza ngoma.
Na alipowasili walimlaki kwa shangwe na kucheza naye. Ilikuwa bonge la picha na waliofika kumlaki Rage walikuwa watu wa rika na jinsia tofauti, hadi wazee.
Rage baada ya kuzungumza kwa kifupi na Waandishi wa Habari alisema anaelekea makao makuu ya klabu, ambako wanachama wengine walikuwa huko wanamsubiri. 
Jumanne wiki hii, Kinesi alisema, Kamati ya Utendaji ilimsimamisha Rage katika kikao chake cha Jumatatu usiku kwa sababu anaendesha klabu kwa kufanya maamuzi yake mwenyewe bila kushirikisha kamati ikiwemo kutoitisha vikao vya kamati ya utendaji kwa mujibu wa Ibara ya 31 (a).











Alisema sababu nyingine ni Rage kuahirisha mkutano Mkuu maalum wa katiba ulioidhinishwa na mkutano mkuu bila kuishirikisha kamati. 
“Rage alisema mkutano usifanyike kwa sababu alikuwa na safari ya nje na kutaka matawi yaendelee kuleta taarifa za katiba, sisi tukaona kikatiba mkutano lazima uendelee kwani alikaidi,”alisema Kinesi.
Aidha, sababu nyingine ni mkataba wa kukiuza kipindi cha Simba Tv bila kuishirikisha kamati hiyo kinyume na ibara ya 30 (b) ya ibara ya katiba ilihali kamati hiyo na Mwenyekiti akiwa na taarifa ilikuwa na mazungumzo na Zuku Tv, kuuza kipindi hicho ambapo maongezi yalikuwa yamefikia Dola za Marekani 300,000 kwa mwaka pamoja na fungu la usajili kila mwaka ambalo lilikuwa bado halijajadiliwa.
Hata hivyo, Baraza la Wadhamini la klabu hiyo, limesema halitambui uamuzi huo wa Kamati ya Utendaji na kumuandikia barua Kinesi aliyeendesha kikao hicho kumtaka awape muhtasari wa kikao na pia aeleze wajumbe waliohudhuria.
Msinipokeel msubirini Rage; Hans Poppe akiwasili JNIA



Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la Simba, Hamisi Kilomoni, alisema ingawa baraza bado halijajulishwa rasmi uamuzi wa kumsimamisha Rage, lakini wamekubaliana kwamba kuna makosa yalifanyika kwenye kikao hicho kulingana na katiba ya Simba, hivyo kutaka muhtasari huo kwa vile wao ndiyo wasimamizi wa masuala ya Simba.
“Kwanza mimi na mwenzangu Ramesh Patel (Mjumbe wa Baraza la Wadhamini) tumekubaliana kuna makosa yalifanyika kwenye kikao chao, hivyo uamuzi wao si sahihi. Tulichokifanya tumemuandikia barua Mwenyekiti aliyesimamia hicho kikao, atupe muhtasari wa kilichotokea na pia tufahamu wajumbe waliohudhuria.
“Sisi hawajatujulisha rasmi, badala yake nasi tumepata taarifa kutokana na vyombo vya habari, na kama unavyojua inawezekana kwenye vyombo vya habari kuna taarifa tofauti na yaliyojitokeza kwenye kikao…
“Hivyo ndiyo sababu tunataka muhtsari wa kikao ili kwanza tupate uhakika wa mambo, tujue walizungumza nini na masuala kama hayo. Ila kama walijadili kama yanavyoelezwa kwenye magazeti, wamefanya makosa. Katiba haisemi hivyo, ” alisema Kilomoni ambaye amepata kuwa kiongozi wa Simba na pia mchezaji wa timu hiyo.
Wakati huo huo: Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe naye amewasili leo ndege moja na Rage, ingawa yeye ametokea, Lubumbashi, DRC alipokwenda kwa shughuli zake za kibiashara.
Hans Poppe, Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) aliwavutia wanachama wa Simba SC alipotokea, lakini akawaomba hataki mapokezi, waendelee kumsubiri Rage.
“Msinipokee tafadhali, nawashukuru, msubirini Rage anakuja huko nyuma, nimemuacha ndani,”alisema. 
Hans Poppe ni kipenzi cha wapenzi na wanachama wa Simba SC kutokana mchango wake mkubwa anautoa kwenye klabu hiyo wa hali na mali.
0 comments

Mtikisiko Chadema: Zitto awekwa benchi, Arfi ang'atuka, lawama zatanda

Mtikisiko Chadema: Zitto awekwa benchi, Arfi ang'atuka, lawama zatanda

Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu Maamuzi ya Kamati Kuu ya Chama hicho ya kuwavua nyazifa Naibu Katibu Mkuu,Zitto Kabwe na  Mjumbe wa Kamati Kuu Kitila Mkumbo Katikati ni Mwanasheria wa chama hicho,Tundu Lissu na Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa. PICHA | FIDELIS FELIX 


Dar es Salaam. 
Mgogoro ndani ya Chadema umezidi kupamba moto baada ya Kamati Kuu kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo, huku Makamu Mwenyekiti Taifa, Said Arfi akiandika barua ya kujiuzulu.
Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa kukisaliti chama.
Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa.
Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge.
Zitto azungumza
 Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Zitto aliliambia gazeti hili, “Sina cha kueleza, kikao kilikwenda vizuri na taarifa rasmi ya chama kuhusu uamuzi wa kikao itatolewa baadaye mchana (jana saa nane mchana), tusubiri Kamanda.”
 
Arfi ajiuzulu
Makamu Mwenyekiti wa Taifa, Said Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, jana aliwasilisha barua ya kujiuzulu nafasi ya uongozi wa chama, akisema; “…kuchoshwa na unafiki unaoendelea ndani ya chama. Napenda ifahamike pia kwangu masilahi ya wapigakura, wakazi na wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya ya Mpanda ni muhimu katika kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari kuchaguliwa marafiki.
 
Katika barua hiyo anasema amechochwa na tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kuwa alimsadia Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita bila ya kupingwa  katika uchaguzi wa ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita.
“Kwa kipindi kirefu zimekuwepo shutuma dhidi yangu na kutiliwa shaka uhusiano wangu na Mhe Pinda Waziri Mkuu. Pamoja na kulijadili katika vikao kadhaa Mpanda na Dar es Salaam bado yapo mashaka kwa nini alipita bila kupingwa. Huo ulikuwa uamuzi wa Wanampanda kwenu imekuwa ni tatizo, lakini hamsemi kwa nini. Majimbo mengine 16 nchini yalipita bila kupingwa mlikuwa wapi na nani alaumiwe? Huu ni unafiki  wa kupindukia.
Vilevile, katika barua hiyo, Arfi anasema amechukizwa na kauli ya mwasisi wa chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Mtei kuwachagulia marafiki.
“Aidha mmechukizwa sana kwa nini nilihoji kauli ya Mwasisi wa chama, Mhe Mtei kutuchagulia viongozi.  Naomba ifahamike wazi kwamba huu ni mtazamo wangu na utabakia hivyo siku zote kwa chama cha demokrasia kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa kukidhi matakwa ya waasisi ambao huvigeuza vyama kuwa mali binafsi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger