Featured Post Today
print this page
Latest Post

SUMATRA TANGA YATOA ONYO KALI KWA WAMILIKI WA VYOMBO VYA USAFIRI MAJINI

SUMATRA TANGA YATOA ONYO KALI KWA WAMILIKI WA VYOMBO VYA USAFIRI MAJINI

  Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Tanga,Walukani Luhamba wa kwanza kulia aliyevaa kofia akisisitiza jambo kwa abiria wanaotumia usafiri wa kutoka Korogwe mjini kwenda Bungu juu ya umuhimu wa kutoa taarifa kwenye vyombo vinavyosimamia sheria pindi wanapobaini magari yanaendeshwa mwendokasi au kuzidishiwa nauli,
Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Tanga,Walukani Luhamba wa kwanza kulia aliyevaa kofia akiwasikiliza abiria wanaotumia magari yanayofanya safari zao kati ya Korogwe mjini hadi Bungu kero wanazokabiliana nazo wakati alipofanya ziara ya kutembelea wilaya ya korogwe kupanga nauli mpya za kutoka mjini kwenye Vijijini,Picha na Oscar Assenga,Korogwe.

Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Tanga,Walukani Luhamba akitangaza viwango vipya kutoka Korogwe mjini kwenda maeneo mbalimbali jana kwenye kikao chake ni wadau wa usafirishaji wilaya ya
Korogwe,kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mrisho Gambo.
MAMLAKA ya Udhibiti na Usimamizi wa Usafiri wa nchi kavu na Majini (Sumatra)Mkoani Tanga umewapa muda wa wiki mbili wamiliki wa vyombo vya usafiri wa majini mkoani hapa kuhakikisha vyombo hivyo vinakaguliwa na kuwa salama kabla ya kuanza kazi zao ili kuweza kupunguza ajali zisizo za lazima.

Wito huo ulitolewa na Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Tanga,
Walukani Luhamba wakati akizungumza na Mtandao huu ambapo alisema kuwa kwa atakayekaidi agizo hilo atachukulia hatua kali ikiwemo kufutiwa leseni.

Alisema dhamira yao kubwa ya kuhakikisha vyombo hivyo vinakaguliwa ni kupambana na wimbi la ajali za mara kwa mara ambazo zimekuwa zikigharimu maisha ya wananchi ambao hawana hatia kutokana na uchakavu wa baadhi ya vyombo hivyo.

Sambamba na hilo,Afisa huyo alisema kuwa watafanya ukaguzi wa vyombo vidogo vidogo  na vikubwa vinavyotoa huduma za usafiri ndani na nje ya mkoa wa Tanga kwa kuvitaka vijisalimishe vyenyewe kabla ya hatua kali hazijachukuliwa dhidi yao.

Hata hivyo alisema kuwa halmashauri mbalimbali mkoani hapa kwa
kushirikiana na wakurugenzi wao hawana budi kuweka utaratibu wa kubandika viwango vya nauli kwenye mabango yaliyopo kwenye stendi za mabasi ili kuweza kuwapunguzia usumbufu wasafiri wao.

    “Hii nadhani ndio njia sahihi ya kuepusha ulanguzi kwa abiria kwa sababu wapo baadhi ya vyombo vya usafiri vyenye kutaka kutoza viwango vikubwa vya nauli kuliko viwango vilivyowekwa na mamlaka husika“Alisema Luhamba.

Akizungumzia suala la baadhi ya mabasi yanayofanya safari zake mkoani hapa kushindwa kutoa tiketi kwa wasafiri, Afisa huyo alisema kuwa kutokutoa tiketi ni kosa hivyo kwa atakayebainika atatozwa faini ya kuanzia shilingi laki moja.
0 comments

HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA YAOMBWA KUTENGA BAJETI KWA AJILI YA KUNUNULIA VIFAA VYA WATU WENYE ULEMAVU.

HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA YAOMBWA KUTENGA BAJETI KWA AJILI YA KUNUNULIA VIFAA VYA WATU WENYE ULEMAVU.

SHIRIKISHO la Vyama watu wenye Ulemavu mkoani Tanga (Shivyawata) limeiomba Halmashauri ya Jiji la Tanga kuangalia uwezekano kuwatengea bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa visaidizi kwa jamii hiyo.

Vifaa hivyo ni pamoja na fimbo nyeupe, kiti mwendo (wheelchair) Shime Sikio,(hearing aid) na Mashine ya kuchapia ambapo bila kutegemea msaada kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo na Halmashauri hawawezi kuvipata.

Ombi hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Zuhura Mussa wakati alipokuwa akizungumza na Mtandao huu ambapo alisema kuwa jamii hiyo imekuwa ikikumbana na changamoto hiyo kutokana na kuwa vifaa hivyo ni ghali hivyo familia nyingi hushindwa kumudu gharama
zake.

Alisema licha ya kuwepo kwa changamoto hiyo lakini wanaiomba
Halmashauri hiyo kuhakikisha miundombinu iliyopo chini yake inakuwa rafiki kwa jamii hiyo pamoja na kuwapa kipaumbele kwenye masuala ya afya katika vituo vya afya na zahanati.

   “Changamoto zinazoikabili jamii ya watu wenye ulemavu ni nyingi lakini hili la vifaa kwetu ni kubwa hivyo tunaiomba Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo mkoani hapa kuangalia uwezekano wa kutusaidia “Alisema Zuhura.

Alisema kuwa changamoto nyengine ambazo wanakumbana nazo ni kutokuwepo kwa wataalamu wa kutosha katika mashule kwa ajili ya kusaidia na kufundisha watoto wenye ulemavu au kugundua ulemavu wao mapema.

Hata hivyo aliongeza kuwa ufinyu wa bajeti ya kuendesha shughuli zao za kila siku huwalazimu viongozi kufanya kazi za kujitolea na wakati mwengine kushindwa kufikia malengo yao kutokana na uhitaji wa fedha jambo ambalo linachangiwa kwa asilimia kubwa na kukosekana kwa wafadhili na fungu maalumu kutoka halmashauri
.
0 comments

WAWILI WAUAWA TANGA MSIMU WA SIKU KUU

WAWILI WAUAWA TANGA MSIMU WA SIKU KUU



·       TANGA.
 
J JESHI la Polisi Mkoani  Tanga linatoa shukrani kwa wananchi kwa kutoa ushirikiano  mzuri  wa kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu kipindi hiki cha Krismas  na hivyo  kuwezesha wananchi kusherehekea  kwa amani na utulivu . 
Akitoa taarifa ya hali ya uhalifu kwa waandishi wa habari akiwa ofisini kwake kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Frasser Kashai amesema wanawaomba wananchi kuendeleza ushikiano huo ili kuweza kuvuka salama mwaka 2014 kwa amani.
Aidha Kamanda Kashai amesema kutokana hali ya uvunjivu wa amani kuendelea kuijtokeza katika maeneo mbalimbali mkoani hapa kumekuwa matukio yaliyojitokeza baadhi ya Wilaya za mikoa .
Amesema  watu wawili wamefariki katika matukio mawili taofauti ,ambapo amesema mnamo tarehe 26 majira ya saa moja kamili asubuhi huko maeneo ya Ndekai Kata ya Baga   Tarafa ya Mgwashi Kando ya barabara ya Baga –Kwemakame Wilaya Lushoto ,Mtu aliyefahamika kwa jina la Rshidi Kilua  mwenye umri wa miaka mkazi wa Ndekai ,aligundua mwili wa Mpwa wake aitwe Hashimu  Rajabu  ukiwa na majereha kichwani .
Hata kamanda amesema mwili marehemu umefanyiwa uchunguzi na madaktari na kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.
Amesema chanzo cha mauaji hayo kinasakiwa kuwa ni Migogoro ya ardhi  ,ambapo mpaka sasa watu wawili ambao ni Waziri Salimu umri wa miaka 35 mkazi wa Ndekai Baga  wapili ni Ramadhani Ayub umri wa miaka 40 mkazi wa Mwangoi  Baga wamekamatwa kufauati mauaji hayo kwa ajili ya mahojiano .
Katika tukio njingine kama hilo Mtun mmoja aliye fahamika kwa jina la Husein Muamed amefariki Dunia wakati alipokuawa anapata matibabu katika Hospitali ya Bombo mara baada ya kokolewa wakati alipokuwa akishambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kwa tuhuma za uwizi baada ya kuvunja nyumba na kuingia ndani kwa nia ya kuiba .Kamanda Kashai amesema upelelezi unaendelea kufuatia tukio hilo ili kuwabaini  waliojichukulia sheria mkonani.
Katika hatua nyingine jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia  watu wapatao sita ambao ni ni Raia wa Ethiopia kwa kosa la kuingia Nchini bila kibali .
Kamanda Kashai amewataja watuhumiwa hao kuwani Gesamu Abato mwenye umri wa miaka 30,Hash Negash Grinanu umri wa miaka 20,Tsegaye Aliso umri wa miaka  21 ,Jamal Godso umri wa miaka 25 ,Alemayo Ataro umri wa miaka 22 na Erigudo Elitiro umri wa miaka 25 .
Kamanda Kashai amesema Watuhumiwa hao watafishwa mahakamani baada ya upelelezi wa awali kukamilika .
0 comments

MAHAKAMA YADAIWA KUITESA FAMILIA YA WATU 18 MOROGORO

MAHAKAMA YADAIWA KUITESA FAMILIA YA WATU 18 MOROGORO

 
 
 
MOROGORO.

 FAMILIA ya watu 18 wakiwemo watoto 10 na akina mama Nane mtaa wa Juma 50 kata ya Mwembesongo eneo la Mafisa Msamvu Kilabu cha Makondeko Manspaa ya Morogoro wako hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko na uambukizo baada ya kutupiwa vitu vyao nje ya nyumba kwa madai ya amri ya mahakama.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi nyumbani  hapo, baadhi ya wanafamila hao Magreth Kainyingi  na Adistela Kainyingi walisema tukio hilo walichofanyiwa Desemba 23 limelenga kuwadhalilisha,kuwafedhehesha na kuwadhoofisha kimaendeleo kwakua hapo ni kwao kihalali.
Walisema chimbuko la mgogoro huo ni deni wasilolitambua la shilingi 800,000 walilokopeshana kati ya baba yao na mtu waliemtaja Josia Masini aliebadili dhana ya mkopo nakuwa malipo ya ununuzi wa nyumba hiyo.
Katika ufafanuzi huo Magreth alisema mbali na vielelezo vya hati miliki walivyonavyo katika eneo hilo Ploti namba 35 kitalu ‘A’Msamvu,na kuthibitishwa na vyombo vya usimamizi ikiwemo Manspaa bado Mahakama imekuwa ikipinga uhalali wake na kumpatia haki Masini.
Wakizungumzia kutupwa nje kwa mizigo yao walisema Desemba 23 walivamiwa na watu wasiowajua waliojitambulisha kuwa wafilisi wa mahakama kisha kuanza kubeba mizigo na kuitoa nje huku wakiwataka kulipa shilingi 900,000 kama usumbufu.
Kwa nyakati tofauti imefikia Masini akishirikiana na uongozi wa mtaa amekuwa akiwakamata kuwafikisha polisi na mahakamani na tayari alishawahi kuwafunga jela mwaka mmoja na kazi ngumu wakiwa na watoto wadogo.




0 comments

Azam FC itaanza kampeni za kusaka kombe la mapinduzi



Leo tarehe 2 January 2015, Azam FC itaanza kampeni za kusaka kombe la mapinduzi hapa mjini Zanzibar kwa kupambana na KCCA ya Uganda ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hili. Mechi itaanza saa 11 jioni na itaonyeshwa moja kwa moja na kituo bora cha televisheni cha Azam TV. Mungu ibariki Azam FC
CHANZO:AZAM FC
0 comments

RAIS KIKWETE ASHEREHEKEA MWAKA MPYA KIJIJINI MSOGA

RAIS KIKWETE ASHEREHEKEA MWAKA MPYA KIJIJINI MSOGA

unnamed
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiomba dua pamoja na Mashekhe wa
Bagamoyo na wananchi wakati wa hafla ya kumuombea dua katika mkesha
wa mwaka mpya kijijini Msoga, Chalinze, Mkoa wa Pwani (PICHA NA IKULU)


unnamed1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa neno la shukurani kwa Mashekhe
wa Bagamoyo na wananchi kwa kumuandalia hafla ya kumuombea dua
katika mkesha wa mwaka mpya kijijini Msoga, Chalinze, Mkoa wa Pwani


unnamed4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na viongozi wa jamii ya
wamasai wanaoishi mkoa wa Pwani. Kiongozi mkuu wa jamii hiyo, Laiboni
Tikwa Moreto (wa pili kushoto), Majaliwa Lihalei na Zuberi Tangono
katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya kijijini Msoga, Chalinze,

                                                                                  
0 comments

Viongozi wa African Sport ya Tanga

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger