Featured Post Today
print this page
Latest Post

MELI NDOGO YA MV MERCI 11 YA MIZIGO YAZAMA BAHARI YA HINDI KATIKA GATI LA KILWA MASOKO USIKU WA MANANE.

MELI NDOGO YA MV MERCI 11 YA MIZIGO YAZAMA BAHARI YA HINDI KATIKA GATI LA KILWA MASOKO USIKU WA MANANE.

Meli hiyo ikiwa imezama majini katika gati la Kilwa Masoko safari moja kwa pamoja:
Mtu mmoja aliyefahamika kwa Jina la Nice Mtega fundi mkuu wa Meli ndogo ya mizigo iitwayo MV MERCI II inayomilikiwa na Semuhungu Shingiro anahofiwa kufa maji baada ya kutoweka kwa zaidi ya masaa 36 toka kuzama kwa meli hiyo katika bandari ya Kilwa masoko. 


Akiongea na Globu ya Jamii hii iliyofika katika eneo hilo, meneja wa Bandari ya Kilwa, Bw. Iddi Omary, alieleza kuwa Meli hiyo iliyofunga gati jana jioni ikitokea songosongo na kupakia tani 30 za mchanga na tani 30 za maji ilizama majira ya saa 6 usiku wa kuamkia leo ambapo Nahodha wa Meli hiyo Captain Charles Kalinga na wasaidizi wake 3 walifanikiwa kutoka ila Nice Mtega aliyekuwepo ndani hajaonekana hadi sasa. 



Juhudi za kumtafuta na kuinua meli hiyo zinaendelea. Sababu ya kuzama kwake bado hazijajulikana. Chanzo. Jamii forum
0 comments

BAADA YA SIKU 23 YA KUTOKA GEREZANI, NELSON MANDELA ALIWEKA HISTORIA NYINGINE MBELE YA MWL JULIUS NYERERE NCHINI TANZANIA.


Mwalimu Julius Nyerere akiwa na mgeni wake Nelson Mandela (kushoto) na Winnie Mandela kwenye gari la wazi wakati wakiwasili kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Mandela alifanya ziara nchini mwaka 1990 baada ya kutoka gerezani.Picha na Maktaba.
DAR ES SALAAM. 
SIKU 23 tu baada ya Nelson Mandela kuachiwa huru kutoka gerezani, Februari 11, 1990 aliwasili hapa nchini kwa ziara fupi iliyokuwa na msisimko wa aina yake.


Aliwasili nchini Machi 5, 1990 na kulakiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Dar es Salaam (Sasa Uwanja wa Julius Nyerere) na Mwalimu Nyerere.

Baada ya kuwasili, alikagua gwaride kama ilivyo kawaida, lakini kikubwa ilikuwa ni hamasa ya Watanzania hasa wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake, maelfu kwa maelfu kujipanga barabarani kumlaki kiongozi huyo katika njia zote alizopita kuanzia Uwanja wa Ndege.
Pamoja na mvua za masika zilizokuwa zinanyesha, hakuna aliyejali hali hiyo. Kila mmoja alikuwa na shauku ya kumwona Mandela.
Ilielezwa kuwa Mandela na ujumbe wake angewasili mapema zaidi, saa 4:00 asubuhi, lakini ratiba ilibadilika kuwa angewasili saa 11 jioni, lakini watu hawakupungua barabarani, walijipanga mapema kuanzia Uwanja wa Ndege, Barabara ya Pugu (sasa Nyerere) na maeneo mengine kumlaki mpigania uhuru huyo.

Wakati huo Dar es Salaam ilikuwa na tatizo kubwa la usafiri, lakini hakuna aliyejali. Mara baada ya Mandela kutua, ilinyesha mvua kubwa, watu walikubali kulowa lakini hadi wamwone Mandela.

Mandela alipata mapokezi makubwa na ya aina yake jijini Dar es Salaam. Kikubwa ni kwamba, Mandela alikuwa akizungumzwa sana na vyombo vya habari, kuonwa kwenye magazeti lakini wengi walitaka kumwona Mandela na mkewe Winnie uso kwa uso.

Baada ya shughuli za Uwanja wa Ndege kukamilika na mvua kukatika, Mandela aliyefuatana na mkewe, Winnie walipanda gari ya wazi aina ya Rolls Royce wakiwa na Mwalimu Nyerere kwa pembeni.

Maelfu kwa maelfu ya wakazi wa Dar es Salaam walijipanga kuanzia Uwanja wa Ndege, Barabara ya Pugu, Uhuru, Kariakoo, Stesheni, Luthuli hadi Ikulu na watu wote hao walikuwa na shauku ya kumuona Mandela walitimiza kiu yao. Kila mmoja alifurahi baada ya kumuona Mandela aliyekuwa akipunga mkono muda wote.

“Ndoto yangu imetimia”, “Siamini, nimemwona Mandela?”, “Safi”, “Naweza kufa kwa amani...nimemwona Mandela” zilikuwa kauli za watu mbalimbali waliokuwa wamejipanga barabarani kumlaki Mandela akiwa na Winnie walipokuwa wakipita.

Siku iliyofuata, hali ilikuwa zaidi ya siku ya mapokezi. Watu waliombwa kufika kwenye Uwanja wa Taifa (sasa Uwanja wa Uhuru) na ilikuwa mminyano wa aina yake. Zaidi ya watu 100,000 wanasadikiwa walifurika uwanjani kusikiliza hotuba ya pili ya Mandela tangu atoke gerezani.

Mandela alitoa hotuba ya kwanza akiwa City Hall nchini Afrika Kusini. Aliwahutubia wafuasi wa ANC wapatao 50,000 waliokuwa wakimsubiri kwa hamu kumuona baada ya kifungo cha miaka 27 jela, ambako pamoja na yote alionyesha furaha yake kulakiwa na maelfu ya wapenzi na wafuasi wake hao. MWANANCHI
0 comments

SINTASAHAU HUYU MDADA NIMEMVULIA KOFI

SINTASAHAU HUYU MDADA NIMEMVULIA KOFI

Mambo niaje wakuu..sijui hata nianzie wapi?...hawa wanawake...!! basi tu!!basi bwana nmekua nikimdate dada mmoja mwenyeji wa iringa
.sio siri kwa haraka haraka nlijua huyu ananipenda kwa dhati, mie kiukweli nlimpenda sana.Tumedate kwa almost mwaka na nusu,kwa mda wote huo sharti ilikua ni hakuna kugegendana mpaka tufunge ndoa.Kidume nlijipa moyo nkajikaza kwani mama nilihus namjua sana ni mlokole haswaa mpka watu uwa wananishangaa nlimptaje coz mie cnaga swaga za kilokole,aliku kesha nihakikishia kua yeye ni bikira na ajawai ku do.Kwa mda wote wa mapenzi yetu nmekua nikijaribu kuomba mchezo ila ilishndkana.juzi kati ulizuka ugomvi mkubwa sana kati yangu na yeye kisa kikiwa ni hicho hicho kugegenda,Mimi nkiwanataka yeye ataki,tumekaa bila kuongeleshana kwa almost wiki nzima,jana jumamosi ndo aliamua kuvunja ukimya na kuniita niende kwake ili tusort out ili tatizo.Tuliongea mengi ila dada bado alikua kashikilia msimamo wake ila akaniomba nimpe mda kidogo afikilie jinsi ya kulifanya hilo,nlimkubalia,basi ile kuangana kwa hugs na kisses tukajikuta kitandani bahati nzuri ni kama she was 50/50 kufanya,na mie sikutaka kua ---- nikatoa dudu fasta nikijua leo ndo naifumua zawadi yngu ya chrsmas...mmmh..nlichokikuta huko staki kuamini mpka sa hvi..nahisi mie nlikua mwanaume wa 20 kuzamisha. Hata gori nlishdwa kupiga kwa sababu ya mawazo nlokua nayo,nlivaa surua yangu taratibu. nkimwacha demu analia sana uku akiniomba msamaha daa wanawake siwatamani tena.. 

0 comments

MREMBO ANUSURIKA KUBAKWA BAADA YA KUVAA KIVAZI NUSU UCHI NA KUPITA MTAANI

MREMBO ANUSURIKA KUBAKWA BAADA YA KUVAA KIVAZI NUSU UCHI NA KUPITA MTAANI

Hapo Akisaidiwa na Wasamaria Wema Baada ya Kupewa Khanga
Stori:  Issa Mnally na Richard Bukos
MREMBO wa haja ambaye jina halikupatikana amenusurika kubakwa na wanaume baada ya kuvaa kivazi kilichoacha wazi sehemu kubwa ya maungo yake nyeti.

Tukio hilo lilijiri sehemu yenye mkusanyiko mkubwa, Kariakoo jijini Dar ambapo mrembo huyo alikuwa kwenye ‘shopping’ kwa ajili ya sikukuu ijayo ya Krismasi.

Likiwa linarandaranda maeneo hayo, Ijumaa Wikienda lilinasa laivu tukio hilo ambapo mrembo huyo alivuliwa nguo hadharani na kuacha ‘vitu’ njenje vikishuhudiwa hata na watoto waliokuwa wakimzomea.

Wanaume hao waliokuwa wakiongezeka na kuanza kumshika sehemu nyeti, walisababisha dada huyo kuanza kutoka nduki ambapo alizama kwenye duka moja kisha akasitiriwa kwa khanga na mama mmoja msamaria mwema.

Alipotoka bado wanaume waliendelea kumzingira ambapo ilimlazimu kutoa shilingi elfu hamsini kisha kurukia kwenye ‘kenta’ iliyomuondoa eneo hilo na haikujulikana alikoelekea kwa sababu gari hilo lilichomoka mbio huku akiwa amekoma ubishi wa kutembea nusu utupu.
0 comments

MBUNGE AMSHAURI RAIS KIKWETE KUMG'OA WAZIRI MKUU PINDA ADAI HAWAJIBIKI NI MPOLE MNO

MBUNGE AMSHAURI RAIS KIKWETE KUMG'OA WAZIRI MKUU PINDA ADAI HAWAJIBIKI NI MPOLE MNO

Dodoma. Rais Jakaya Kikwete, ameshauriwa kumng’oa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ikielezwa sababu kuwa ndiye kikwazo katika utendaji wa Serikali na kwamba akiachwa ataipeleka pabaya Serikali na CCM

Kikwete pia ameshauriwa kumfukuza kazi Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia, kwa kushindwa kukabiliana na matatizo ya ubadhirifu katika halmashauri nchini.

“Kama (Rais) unaitakia mema nchi na CCM kuchukua hatua za kuwafukuza kazi Pinda na Waziri Ghasia,” alisema Mbunge wa Mwibara, Khangi Lugola (CCM), juzi alipochangia taarifa za Kamati za Bunge kuhusu hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30 mwaka jana.

“Kwa nini Watanzania wafe kwa kunyimwa misaada na wafadhili kwa sababu ya mtu mmoja tu Pinda, kwa ajili ya Ghasia ameiendesha Tamisemi kama Saccos ama Vikoba?” alihoji.

 “Mchawi wetu ... ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda amekuwa mpole mno hawajibiki,” alisema Mh. Lugola na kuongeza, “Kuanzia jana (juzi) Waziri Mkuu anahudhuria mahafali.”

Wakati Lugola akizungumza mawaziri waliokuwepo bungeni ni wanne, manaibu mawaziri wawiliwawili, wakati  mawaziri wote 53.
0 comments

Kichanga chafariki kwa kukanyagwa na pikipiki

Kichanga chafariki kwa kukanyagwa na pikipiki 

 

MTOTO wa miezi minne, Dora Ramadhani, mkazi wa Kijiji cha Mtumba, Tarafa ya Mlalo, wilayani Lushoto, amefariki dunia baada ya kuanguka kutoka kwenye mbeleko na kukanyagwa na pikipiki.
Mtoto huyo aliyekuwa amebebwa na mama yake, Suzani Francis (32) alidondoka baada ya mbeleko kujisokota kwenye tairi ya nyuma ya pikipiki waliyokuwa wamepanda na kuangukia barabarani.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki, alisema ajali hiyo ilitokea juzi, saa 9:30 jioni na kwamba baada ya mtoto huyo kuanguka alikanyagwa na pikipiki hiyo na kusababisha mauti yake.
Kamanda Ndaki alisema pikipiki hiyo T 395 CCG Fecon ilikuwa ikiendeshwa na Leonard Turo (28), mkazi wa Lukozi, wilayani Lushoto.
Alisema dereva huyo anashikiliwa na polisi na upelelezi wa tukio hilo unaendelea. Mwili wa kichanga hicho umekabidhiwa kwa ndugu zake kwa mazishi.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limetoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri kuwa makini wawapo barabarani, na madereva wanapaswa kuhakikisha abiria wanaowabeba wamekaa kwenye hali ya usalama kabla na wakiwa safarini.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments

UVCCM TANGA KUANZA ZIARA KESHO MKOANI TANGA.

UVCCM TANGA KUANZA ZIARA KESHO MKOANI TANGA.



 JUMUIYA wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga(UVCCM) inatarajia kuanza ziara yake kesho kwa mkoa mzima wa Tanga kukutana na viongozi wa umoja huo ngazi za wilaya pamoja na kufanya mikutano ya hadhara.
Akizungumza leo na Blog hii,Mwenyekiti wa Umoja huo,Abdi Makange amesema ziara hiyo itakuwa na lengo la kukutana na mabaraza ya umoja wa vijana kila wilaya ili  kuwekeana mikakati mbalimbali ya kuufanya umoja huo uzidi kuwa imara pamoja na kuwashukuru wajumbe wa umoja huo.

Amesema  suala lengine watakalolifanya katika ziara hiyo ni kuangalia uhai wa jumuiya hiyo kwenye wilaya hizo utakaoendena sambamba na ufunguzi wa matawi ya umoja huo lengo likiwa ni kuuimarisha

Makange amesema ziara hiyo kwa kila wilaya zitakuwa zikihitimishwa na ufanyikaji wa mikutano ya hadhara ambapo wananchi wa wilaya husika watapata nafasi ya kupata sera makini za umoja huo ambazo zitakuwa zikitolewa na viongozi wake.
0 comments

Magazeti ya leo Jumatatu December 09 201.

Magazeti ya leo Jumatatu December 09 201.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger