Featured Post Today
print this page
Latest Post

WAUGUZI NA MADAKTARI WASITISHA KUTOA HUDUMA KWA WAGONJWA NI BAADA YA HOSPITALI KUKUMBWA NA MAFURIKO

WAUGUZI NA MADAKTARI WASITISHA KUTOA HUDUMA KWA WAGONJWA NI BAADA YA HOSPITALI KUKUMBWA NA MAFURIKO


 Huu ni mtaro wa kupitisha maji taka ambao umepita kati kati ya Hospitali ya Palestina amapo ulifumuka na kusababisha kusambaa kwa maji machafu katika kila kona ya Hospitali hiyo
 Mmoja wa wagonjwa akiwa anangojea kupata huduma baada ya mvua hiyo kubwa kwisha
 Haya ni maji machafu ambayo yametapakaa kila sehemu ya hospitali
 Kushoto ni Mgonjwa akiwa amelala juu ya Benchi ambapo pembeni kuna maji na matope ambayo yamechanganyikana na kinyesi kutoka katika vyoo mbalimbali katika makazi ya watu.
 Hii ndio hali halisi ya Chemba hii ambayo ipo ndani ya Hospitali ya  Sinza Palestina
 Hizi ni chemba zaidi ambazo zipo nje na pia zimeungana na zilizopo ndani ya Hospital hiyo
 Wagonjwa zaidi wakingojea waganga kufika pia kumalizia kusafishwa kwa vyumba hivyo ili wapate hudumiwa
 Moja ya Chumba ambacho kilikuwa kimejaa tope kikingojea kusafishwa
 Hapa hata hapapitiki
 Baadhi ya viti vikiwa vimeegeshwa kwa ajili ya kungoja kufanya usafi
 Hakuna mtu katika maeneo haya kutokana na mvua kubwa iliyonyesha
 
 Kila kitu kimekaa hovyo hovyo baada ya mvua kubwa hiyo kunyesha
 Baadhi ya vifaa vya kutibia wagonjwa vikiwa juu ya moja ya kitanda cha kutibia wagonjwa huku watu wakingoja huduma ya matibabu.
 Huu ndio Mtaro wa maji machafu ambapo maji kutoka nje yamepita ndani ya hospitali hiyo na kusababisha maafa baada ya Mtaro huo kuziba.Picha zote Zimeletwa hapa http://kilinyepesi.blogspot.com/ na Dar es salaam yetu
--
Mapema mchana wa leo kumetokea mvua kubwa katika maeneo mbalimbali ya Jijini Dar es salaam kumesababisha usumbufu mkubwa baada ya maeneo mengi kukumbwa na tatizo la maji mengi ambayo yaliziba barabara , nyumba za watu pamoja na maeneo mbalimbali.
 
Mvua hizo kubwa ambazo hata mamlaka ya hali ya hewa wametahadhalisha kwamba zitakuwepo kuanzia Tarehe 5.03.2014 hadi Tarehe 7.03.2014  zimesababisha usumbufu mkubwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Kinondoni Sinza - Palestina kujaa maji kila kona na kupelekea wauguzi kuacha kazi na kupanda juu ya Meza na viti wakikwepa maji hayo. Na wengine kukimbia katika eneo hilo kuhofia maji hayo.
 
Walikwepa maji hayo kutokana na kwamba si ya mvua tuu lakini yalikuwa ni Machafu yaliyochanganyikana na maji kutoka vyooni ambapo kuna chemba moja ya maji machafu imepita hapo.
 
Baada ya mvua hiyo kwisha iliwalazimu wafanya usafi wachukue muda wa zaidi ya dakika 30 kufanya usafi na kutoa matope yaliyokuwa yamejaa kila chumba.
Akiongea kwa Simu Mganga Mkuu wa Hospitalu hiyo amekili kwamba kuna usumbufu mkubwa wa chemba hiyo na mvua hasa katika kipindi hicho ambapo zinanyesha kwa kiasi kikubwa. 
 
Ameongeza kwa kusema kwamba kunajuhudi zinahitajika kufanyika ili kuweza kunusuru tatizo hilo lisiendelee.
 
Nao baadhi ya wagonjwa ambao wengine walikuwa katika hali ambayo si nzuri wamesema  wanaiomba serikali itazame tatizo hilo maana licha ya maji hayo kuwa mengi lakini pia ni hatari kwa afya zao kwa ujumla.
0 comments

CHAUSTA WASHINDWA KUFANYA KAMPENI KALENGA

CHAUSTA WASHINDWA KUFANYA KAMPENI KALENGA



IKIWA zimebaki takribani siku kumi ili kufungwa kampeni za kugombea ubunge katika jimbo la Kalenga, mgombea wa ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Haki na Ustawi (CHAUSTA), Richard Minja anatarajia kuzindua kampeni kesho katika kijiji cha Wasa Kata ya Maboga.
Akizungumza na mtandao huu leo kwa njia ya simu, Katibu Mkuu wa CHAUSTA, Mwaka Mgimwa amesema licha ya kuchelewa kuanza kampeni watafanya kazi kubwa ili kuhakikisha wanapata ushindi katika jimbo hilo.
Mgimwa amesema anatoka kwenye vikao vya Bunge maalum la Katiba linalofanyika mjini Dodoma kwa ajili ya uzinduzi wa Kampeni hizo ambapo baada ya uzinduzi watahakikisha wanatafanya kata kwa kata na kijiji kwa kijiji katika muda huo uliobaki.
Tangu kuanza kwa kampeni Februari 19 mwaka huu, Chama hicho kimekuwa kikishindwa kufanya kampeni kwa sababu zilizoelezwa kuwa Mgombea huyo yupo nje ya mji kwa shughuli za kijamii na kushindwa kufuata ratiba kama ilivyo.
Hata hivyo katika ratiba chama hicho kinaonekana kutokuwa na muda mwingi wa kampeni  kulinganisha na vyama vya CCM na Chadema vinavyoonekana kuwa na muda mwingi wa kufanya kampeni.
Kampeni za jimbo la Kalenga kwa  chama cha CHAUSTA  zilitarajiwa kuzinduliwa rasmi tangu February 22 katika kijiji cha kibaoni kata ya Ifunda jimboni humo ambapo tangu ratiba kuanza chama hicho hakijawahi kuonekana kufanya mkutano hata mmoja.
Mtandao huu ulipomtafuta mgombea huyo kwa njia ya simu ili kupata ufafanuzi zaidi juu ya kukwama kwa kampeni katika chama chake amesema hangeweza kuzungumza chochete kwa kuwa yupo nje ya mji.
“Nipeni muda kwa sasa siwezi kuliongelea hilo suala nitawapeni jibu kesho asubuhi. Kampeni zipo nyingi mimi ninafanya  za kimya kimya sio lazima nifanye kampeni na matarumbeta, magari na mziki ndio mjue nafanya kampeni kwasababu kila mtu anatumia staili yake ya kufanya kampeni” amesema Minja.
Hata hivyo alipododoswa zaidi amesema kuwa kutumia hela nyingi kwenye kampeni ni kuwadanganya wananchi kwasababu wao ndio wanashida nyingi na wanahitaji msaada kutoka kwa viongozi hivyo ni bora pesa zitunzwe ili baada ya ushindi zitumike kuwaletea maendeleo wananchi.
Hata hivyo mgombea huyo ametuma ujumbe mfupi kuwa bado yuko nje ya mji na anatarajia kurudi leo kwa ajili ya kuandaa shughuli za uzinduzi wa kesho katika kijiji cha Wasa Kata ya Maboga.
0 comments

KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amewataka wachezaji wake kutumia vizuri nafasi wanazopata ili washinde katika mechi yao dhidi ya Prisons, mchezo unaotarajiwa kupigwa kesho katika Uwanja wa Sokoine jiji mbeya.

KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amewataka wachezaji wake kutumia vizuri nafasi wanazopata ili washinde katika mechi yao dhidi ya Prisons, mchezo unaotarajiwa kupigwa kesho katika Uwanja wa Sokoine jiji mbeya.




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
 
KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amewataka wachezaji wake kutumia vizuri nafasi wanazopata ili washinde katika mechi yao dhidi ya Prisons, mchezo unaotarajiwa kupigwa kesho katika Uwanja wa Sokoine jiji mbeya.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, Logarusic alisema timu yote inahitaji ushindi katika mechi yao hiyo, hivyo jambo kubwa ni kuona vijana wake wanakuwa makini zaidi uwanjani.

“Tumepoteza pointi muhimu katika mechi iliyopita kwasababu ya wachezaji kutotumia ipasavyo nafasi za wazi wanazozipata, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limetugharimu.

“Naamini wakati huu wachezaji wote wanafahamu jambo gani muhimu wanapaswa kufanya uwanjani kwa ajili ya kuwapatia maatokeo mazuri, maana mpira ni mchezo wa makosa,” alisema.

Alisema kuwa kila mchezaji anaweza kufunga anapokuwa katika nafasi mzuri ya kufunga na kuhakikisha nafasi tatu za wazi wanazozipata moja wapo wanaibuka na ushindi.

Simba itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu za kichapo cha mabao 3-2 dhidi ya JKT Ruvu, uliochezwa Jumapili iliyopita katika uwanja wa Taifa, mechi iliyowasononesha mashabiki wao.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger