Featured Post Today
print this page
Latest Post

PINDA KUFUNGUA KONGAMANO LA UWEKEZAJI TANGA ALHAMISI

PINDA KUFUNGUA KONGAMANO LA UWEKEZAJI TANGA ALHAMISI

NA AMINA OMARI,TANGA.
WAZIRI Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la uwekezaji la kanda ya Kaskazini linalotarajiwa kufanyika Septemba 26 hadi 27 mwaka huu Mkoani Tanga.
Akiongea na waandishi wa habari hapo leo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Gallawa alisema kuwa waziri Mkuu anatarajiwa kuwasili Mkoani humo kesho majira ya saa kumi na Moja kwa ajili ya kushiriki kwenye kongamano hilo.
Alisema kuwa kongamano hilo lenye lengo la kutangaza fursa za uwekezaji na kimaendeleo zilizoko kwenye mikoa ya Tanga,Kilimanjaro,Manyara na Arusha zinatarajiwa kuhudhuriwa na wageni 450 kutoka nje ya Tanzania.
“Tayari tumepata wageni wenye nia ya kushiriki ili kujionea fursa zilizopo takribani 450 wamethibitisha ushiriki wao kutoka nje ya Tanzania achiambali  wale wadau kutoka kwenye Halimashauri zetu mbalimbali zilizoko kwenye ukanda wa kaskazini”alisema RC Gallawa.
Aidha alieleza kuwa kongamano hilo litakuwa na midahalo ,maonyesho ya raslimali zilizopo ,maeneo ya uwekezaji pamoja na fursa zinazopatikananaili kumvutia mwekezaji  kwa lengo la kuleta mabadiliko ya kuichumi kwenye mikoa hiyo.
Pia aliwataka wakazi wa jiji la Tanga kuhakikisha wanaituma fema fursa ya uwekezaji hasa kwa wafanyabiashara wa mnumba za kulala wageni na waendesha biashara za chakula kutoa huduma bora kwa wageni watakao fika kwa wingi kwenye kongamano hil
0 comments

Handeni sasa kujipanga na maabara shule za sekondari

Handeni sasa kujipanga na maabara shule za sekondari


Na Kambi Mbwana, Handeni

MKURUGENZI Mtendaji wilaya Handeni, mkoani Tanga, Khalfany Haule, amesema wanakabiriwa na changamoto ya ukosefu wa maabara kwa shule za sekondari, hivyo wanajipanga kushirikiana na wadau ili kufanyia kazi na kuinusuru elimu wilayani humo.



Mkurugenzi Mtendaji wilayani Handeni, Dr Khalfany Haule, pichani, akiwa ofisini kwake.
Akizungumza mjini hapa, Haule alisema maabara hizo ni kwa shule zote za sekondari zilizopo wilayani humo, jambo ambalo linaweza kuchangia kufanya vibaya kwa wanafunzi kwenye mitihani ya Taifa.
Alisema anajipanga na watendaji wengine wilayani humo, ikiwa ni sambamba naa kubuni wazo la kuwashirikisha watu wenye moyo na uwezo wao kulitatua suala hilo kwa kiasi kikubwa.
"Hapa kuna shule za sekondari ambazo kwa hakika zinafanya vibaya kwasababu ya ukosefu wa maabara za kuwapa wanafunzi mwanga wa kuendelea vyema katika masomo yao.


"Lengo ni kuanza kujenga maabara hizo, hivyo tutapenda kushirikiana na wadau wote wenye malengo ya kuinusuru elimu ya Tanzania kwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanaandaliwa vyema,” alisema Haule.
Wilaya ya Handeni ipo chini ya Mkuu wa wilaya wake, Muhingo Rweyemamu, huku ikifanikiwa na kuwa na mbunge Abdallah Kigoda ambaye pia ni Waziri wa Viwanda na Biashara.
0 comments

SIMBA SC NA OKWI SASA KITAELEWEKA NDANI YA WIKI MOJA TU...KUSUKA AU KUNYOA ITAJULIKANA

SIMBA SC NA OKWI SASA KITAELEWEKA NDANI YA WIKI MOJA TU...KUSUKA AU KUNYOA ITAJULIKANA

Na Mahmoud Zubeiry,
SIMBA SC itaamua hatima ya msambuliaji wake wa zamani, Emmanuel Okwi mwishoni mwa mwezi huu kama itamrejesha au la, baada ya kufika kwa tarehe ya mwisho ya klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia iliyomnunua Januari mwaka huu ya kulipa fedha za manunuzi yake, dola za Kimarekani 300,000 zaidi ya Sh Milioni 480. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameiambia BIN ZUBEIRY juzi kwamba, Septemba 30 ndio wataamua wafanye nini baada ya kufika tarehe ya mwisho ya kulipwa fedha zao.
Tarehe 30; Fedha za Okwi zitawasilishwa Septemba 30?

Kwa sasa, tayari Okwi, mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda yupo Dar es Salaam akiwa amesusa kurejea Tunisia kutokana na madai ya klabu hiyo kushindwa kumlipa mishahara kwa miezi mitatu.
Okwi amekaririwa akisema kwamba tayari kesi yake ameifikisha Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), wakati Etoile nayo imekaririwa kudai imemshitaki mchezaji huyo FIFA pia kwa kushindwa kuripoti kazini kwa muda mrefu sasa, baada ya ruhusa ya kwenda kujiunga na timu yake ya taifa miezi miwili iliyopita. 
Baada ya kumnunua mchezaji huyo Januari mwaka huu, Etoile iliahidi kutuma fedha za manunuzi yake mjini Dar es Salaam, lakini siku zilikatika hadi katikati ya mwaka, uongozi wa Simba ulipolazimika kwenda Tunisi kufuatilia fedha hizo.
Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Hans Poppe aliongozana na Katibu wa klabu, Mwanasheria, Evodius Mtawala hadi Tunis na wakiwa huko, klabu hiyo iliahidi kulipa fedha hizo ifikapo Septemba 30. 
Kapteni ndani ya Tunis; Hans Poppe akiwa Tunis kufuatilia fedha za Okwi. Ahadi ya Septemba 30 itatimizwa? 

Katikati ya ahadi hiyo, Okwi naye akasusa kwa madai ya kutolipwa mishahara- jambo ambalo linazidi kuiweka pagumu biashara hiyo, ingawa kwa mujibu wa sheria, Etoile wanatakiwa kuilipa Simba SC fedha zake kisha kuendelea na kesi yao na mchezaji huyo.
Tayari Simba SC imepata hasara ya kumkosa mchezaji huyo katika mzunguko wote wa pili wa Ligi Kuu msimu uliopita na mzunguko wote wa kwanza msimu huu- na haijulikani hata ikimrejesha watasaini Mkataba mpya na kumlipa fedha tena au itakuwaje.
Mkataba ambao Simba SC ilisaini na Etoile kuhusu Okwi, mbali na kulipwa dola 300,000 pia una kipengele cha atakapouzwa timu yoyote, Wekundu wa Msimbazi wapewe sehemu ya fedha. Hii ni kesi ngumu.   
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger