Featured Post Today
print this page
Latest Post

HI NDIYO AJALI YA MASHUJA ILIYOWAKA MOTO NA WAHAMIAJI HARAMU WA KIAFRIKA 114 KUFARIKI DUNIA KATIKA KISIWA CHA LAMPEDUSA NCHINI ITALIA.


Shirika la Umoja wa Mataifa la kushugh
ulikia wakimbizi UNHCR, limesema.
 
Miongoni mwa waliofariki yupo mtoto wa miaka 3 na mama mjamzito. 


Na Margreth Itala. 

IDADI YA WAAFRIKA waliofariki imefikia 114 mpaka sasa,150 wameokolewa na wengine 250 hawajulikani walipo, ajali hiyo imetokea jana ambapo boti iliyokuwa imejazwa na wahamiaji kutoka Afrika, kuzama karibu na kisiwa cha Lampedusa nchini Italia.

Kufuatia ajali hiyo, rais wa Italia Giorgio Napolitano ametoa rai ya kuimarisha ulinzi katika pwani za Afrika kaskazini ili kuzuwia wahamiaji kujaribu kuingia barani Ulaya. 


Napolitano ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na Umoja wa Ulaya kushirikiana kukomesha usafirishaji haramu wa binaadamu, na kusisitiza kuwa haikubaliki kwamba Frontex, wakala wa Umoja wa Ulaya anaeshughulikia usalama wa mipakani haupewi vitendea kazi vya kutosha ili kuweza kuingilia kati pasipo kuchelewa. 

karibu abiria 500, wengi wao wakiwa raia wa Eritrea walipanda boti hiyo nchini Libya, na askari wanaolinda pwani wamesema manusura 151 wameokolewa baada ya boti hiyo yenye urefu wa mita 20 kushika moto na kuzama yapatayo kilomita moja kutoka kisiwani Lampedusa.

Taarifa zilizoifikia Fahamutz zinaeleza kuwa idadi kubwa ya waliofariki ni wanawake na watoto, pia chanzo cha habari kimesema kuwa wengi wa wahamiaji hao waliokuwa katika boti hiyo hawajui kuogelea.

Meya wa mji wa Lampedusa Giusi Nicolini ameielezea ajali hiyo kama maafa makubwa, na kuongeza kuwa miongoni mwa waliofariki alikuwepo mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na mama mjamzito. 


Kisiwa cha Lampedusa kiko karibu zaidi na Afrika kuliko Italia bara, kikiwa umbali wa kilomita 113 kutoka pwani ya Tunsia, na ndiyo kimekuwa kituo cha mwisho kwa boti zinazosafirisha watu kwa njia za magendo.

Pichani, mhamiaji haramu mwanamke aliyenusurika katika ajali hiyo akipatiwa huduma katika hospitali mjini Lampedusa.

Meli za ulinzi wa pwani, boti za uvuvi na helikopta zilikuwa zinafanya msako katika bahari hiyo kutafuta manusura.


Chanzo cha ajali
Waziri wa mambo ya ndani wa Italia, Angelino Alfano aliwaambia waandishi wa habari kuwa boti hiyo ilianza kuzama baada ya kuzimika kwa injini yake moja, na abiria hawakuwa na simu kuweza kuomba msaada, na kwa hivyo waliwasha moto mdogo ili kuomba msaada kwa meli zilizokuwa zinapita.

Waziri Alfano ameongeza kuwa kwa kuwa gesi ilikuwa imechanganyika na maji yaliyoingia katika meli hiyo, moto ulisambaa katika meli yenyewe, na kuwalaazimu abiria kukimbilia upande mmoja, hatua iliyosababisha meli hiyo kupinduka na kuwamwaga abiria baharini. Hii ilikuwa ajali ya pili kutokea wiki hii karibu na Italia.


Siku ya Jumatatu wanaume 13 walizama wakati wakijaribu kuufikia mji wa Sicily,pale meli yao ilipopinduka ikiwa imebakiza mita chache kutia nanga. Papa Francis ambaye alitembelea kisiwa cha Lampedusa mwezi Julai katika ziara ya kwanza ya upapa nje ya jiji la Rome, alielezea kusikitishwa kwake na roho nyingi zilizoteketea katika ajali hiyo.
0 comments

PICHA LIVEKIPINDI CHA KWANZA : MECHI KATI YA MBEYA CITY FC NA JKT OLJORO , MBEYA CITY WANAONGOZA KWA GOLI MOJA

PICHA LIVEKIPINDI CHA KWANZA : MECHI KATI YA MBEYA CITY FC NA JKT OLJORO , MBEYA CITY WANAONGOZA KWA GOLI MOJA


 MEZA KUU WAKIWA WANANGOJA KUTAZAMA MPIRA 
 TIMU ZOTE MBILI ZIKIWA ZINAINGIA UWANJANI
 MGENI RASMI  AKIWA ANAKAGUA TIMU ZOTE MBILI
 MA NAHODHA WA TIMU ZOTE MBILI WAKIWA WANACHAGUA WAANZIE KUKAA GOLI LIPI
 KIKOSI CHA JKT OLJORO FC WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
 KIKOSI CHA MBEYA CITY FC WAKIWA WANAOMBA DUA
 KIKOSI CHA MBEYA CITY FC WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
 KOCHA WA TIMU YA MBEYA CITY FC  WA KWANZA AKIWA ANATAZAMA MPIRA KWA MAKINI
 TIMU YA MBEYA CITY FC WAKIWA WANAWASHUKURU MASHABIKI 
 MASHABIKI WA MBEYA CITY FC
 MASHABIKI MBALIMBALI 
 MASHABIKI WA JKT OLJORO NAO HAWAPO NYUMA
 MPIRA UKIWA UMEANZA

ENDELEA KUFUATILIA .
0 comments

"NISAIDIENI, NATESEKA" ALIA MTOTO SELEMANI

"NISAIDIENI, NATESEKA" ALIA MTOTO SELEMANI

HAKIKA ni mateso, tena makubwa. Mtoto Selemani Rajabu mwenye umri wa miaka 17, mkazi wa Ukonga kwa Guta, jijini Dar yuko katika mateso makali baada ya mguu wake mmoja kuvimba mithili ya tairi la gari kiasi kwamba hawezi kufanya jambo lolote zaidi ya kujiburuza tu.
Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwao akiwa na simanzi kubwa, kijana huyo amesema kwamba anakumbuka amezaliwa akiwa na ulemavu kidogo chini ya nyayo za miguu yake ambazo zilikuwa nene kiasi cha kumfanya ashindwe kutembea na badala yake akawa ni mtu wa kutambaa tu.
Alisema wakati huo alikuwa akiishi na wazazi wake wote wawili, lakini baadaye wazazi hao walitengana na kumfanya aishi na mama yake huko Pugu Kajiungeni. Kutokana na uwezo duni wa mama yake, alimpeleka hospitali mara moja tu, licha ya mguu wake kuendelea kuvimba kila siku.


“Nakumbuka mama yangu aliwahi kunipeleka hospitali mara moja tu nilipokuwa mdogo, lakini sikumbuki kama aliwahi kunipeleka tena,” alisema Selemani akiwa na sura ya kukata tamaa.
Alisema tangu wakati huo, mguu wake uliendelea kuvimba siku hadi siku mpaka akashindwa hata kutambaa kama mwanzo na sasa akalazimika kujiburuza licha ya uzito mkubwa wa mguu wake kutokana na kuongezeka kwa uvimbe.
Kutokana na hali hiyo kuzidi kuwa mbaya, alisema mwaka jana mama yake alimpeleka Hospitali ya CCBRT ambako baada ya madaktari kumuangalia walisema mguu wake hauna maji ambayo wangeweza kuyanyonya ili kuyatumia kupata vipimo na kujua tatizo linalomsumbua.
Hata hivyo, kwa bahati mbaya, mama yake mzazi alifariki na kumlazimu baba yake kwenda kumchukua na kumpeleka kwa bibi yake huko Manzese.


Hali ya bibi haikuwa nzuri kiafya, hivyo baba alinichukua tena na kuishi naye kwake nikiwa na mama wa kambo,” alisema Selemani. 
Mtoto huyo analalamika kuwa anatamani hata mguu wake huo ukatwe kutokana na adha anayoipata kwani anakosa raha kama watoto wengine wanaotoka nje wenyewe tofauti na yeye anayetolewa kwa kuburuzwa na watu zaidi ya wawili.
“Siku zote na raha kunapokucha najiona kama sina thamani, natamani hata mguu huu ukatwe, siwezi kufanya kitu chochote, natamani kuwa kama watoto wenzangu,” alisema.
Licha ya adha hiyo, Selemani alisema kingine kinachomuumiza ni kufanya haja zote  sehemu alipokaa na hivyo kutoa wito kwa wasamaria, akiwemo Rais Jakaya Kikwete kumsaidia ili aweze kupata matibabu.
Kwa wenye nia ya kumsaidia mtoto Selamani, kwa matibabu au chakula, wanaombwa kuwasiliana na chumba cha habari kwa simu namba 0713 612 533.
0 comments

Kampuni ya madini ya Canaco yathibitisha wingi wa dhahabu wilayani Handeni, mkoani Tanga

Kampuni ya madini ya Canaco yathibitisha wingi wa dhahabu wilayani Handeni, mkoani Tanga

Na Amina Omari, Handeni
WILAYA ya Handeni ni kati ya maeneo yaliyobarikiwa kuwa na rasilimali nyingi, yakiwamo madini aina ya dhahabu nchini Tanzania, huku kwa kikubwa  yakipatikana katika milima ya Magambazi, Km 30 kutoka Handeni mjini.
Msimamizi Mkuu wa Kampuni ya utafiti wa madini ya Canaco Tanzania Ltd, Bavon Mwaluko akiwaonyesha waandishi wa habari sampuli za udongo zilizofanyiwa utafiti na kampuni yake kwenye mlima wa Magambazi Wilayani Handeni, Mkoani Tanga na matokeo kuonyesha kuwa eneo hilo lina madini aina ya dhahabu yenye ubora mzuri.
Kuwapo kwa rasilimali hiyo kumeweza kuisaidia wilaya hiyo kimapato pamoja na wananchi kwa nia ya kujikimu kimaisha juu ya shughuli za uchimbaji na uuzaji wa madini kwa ujumla.


Sampuli ya udingo uliotumika kufanyia utafiti na Kampuni ya utaifiti ya Canaco Tanzania Ltd wakati wa kazi ya kutafiti madini kwenye mlima wa Magambazi Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga kazi hiyo ilifanyika tangu mwaka 2007 na mwaka jana ikatoka na mtokeo yanayoonesha kuwa eneo hilo lina madini aina ya dhahabu yenye ubora na daraja zuri.



Pia kuwepo kwa madini hayo kunawavutia watu wengi kutoka ndani na nje ya nchi kuja kutafuta madini hayo.
Mfanyakazi wa Kampuni ya utafiti wa madini ya Canaco Tanzania Ltd, akichambua sampuli za udongo uliochimbwa katika mlima wa Magambazi ambao utafiti umeonyesha kuwa yapo madini yenye ubora na daraja zuri katika soko.


Awali eneo hilo lilikuwa linamilikiwa na wachimbaji wadogo waliokuwa wanatumia zana duni za kuchimba pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa teknolojia ya vifaa vya uchimbaji.
Jambo hilo limewafanya wakati wote waonekane ni masikini na wanaopata wasiwasi dhidi ya uharibifu wa mazingira sanjari na kupata mali kidogo tofauti na matarajio ya kazi yao.
Hatua hiyo ilisababisha serikali ya Wilaya ya Handeni kuwakaribisha wawekezaji wageni ambao kwa kutumia teknolojia ya kisasa wataweza kuchimba kwa ufanisi na wakati huo huo kulipa kodi itakayofanikisha kuboresha maisha ya wananchi wote.
Kampuni hiyo si nyingine, ila ni CANACO. Hawa ni moja ya wadau wa madini waliopewa fursa hiyo ya kufanya tafiti tafiti za uwepo wa dhahabu katika eneo hilo.
Meneja Utafiti wa kampuni hiyo, Bavon Mwaluko anasema kuwa waliingia katika eneo hilo mwaka 2007 kwa ajili ya kuendesha shughuli za utafiti wa madini yaliyoko kama hatua za awali kabla ya kuanza kazi ya ujenzi wa mashine kwa ajili ya uchimbaji.

Walipoingia walikubaliana na wenyeji waliokuwa wakimiliki maeneo hayo ambao walikuwa wanaendesha shughuli za uchimbaji mdogo  na walitumia fedha nyingi kuwalipa fidia ili wafanye shughuli hiyo.
Tafiti walizokuwa wanazifanya ni pamoja na kujua aina ya miamba iliyobeba dhahabu kwenye eneo hilo imeelekea upande gani pamoja na tabia za kijiolojia za mimba hiyo bila kusahau thamani ya dhahabu itakayozalishwa.
“Kabla ya kuanza zoezi la uchimbaj ni lazima kufanya tafiti ili kujua tabia za miamba ukizingatia mingine inaweza kuwa na milipuko au ni sehemu ya chanzo cha maji, hivyo shughuli hiyo kuwa na uharibifu wa mazingira,” alisema Mwaluko.
Mwaluko anasema mwaka 2008 waliendeleoa na utafiti pamoja na ukaguzi wa eneo la mradi ili kujua aina ya madini yaliyokuwapo ambapo mwaka 2009 hadi 2010 walianza rasmi uchimbaji katika eneo la magambazi baada ya matokeo ya awali kuonyesha kuwa kulikuwa na madini ya kutosha.
Mwaka 2012 walifanya utafiti wa mwisho ili kujua iwapo uchimbaji utaanza utaweza kudumu kwa miaka mingapi ili katika kazi hiyo kusitokee mkanganyiko wowote.
Anasema kuwa kampuni zinazofanya kazi ya utafiti wa madini nchini
zinapaswa kuweka wazi shughuli zao kwa wananchi ili waondokane na dhana ya kudaiwa kuwa wanahamisha malighafi hiyo na kuipeleka katika nchi zao.

“Si kweli kuwa kampuni za utafiti zimekuwa zikihamisha nje
madini bali kinachofanyika ni kupeleka sampuli ya udongo katika
maabara zilizoko mjini Mwanza na nje ya nchi kwa ajili ya kupata
matokeo.

“Wakati wa  kufanyika utafiti tunapopeleka sampuli ya udongo kwenye
maabara kuna mchakato mrefu  wenye uwazi ambao hupitia na kuchunguzwa na vyombo vya dola kama Mamlaka ya Mapato na Usalama wa Taifa na ikikamilika, lazima irejeshwe kwa utaratibu
ule ule,” Alisema.

Anasema ukweli ni kwamba kampuni zilizojikita hasa katika kutafiti
madini baada ya kupata kibali hulazimika kuwekeza kikamilifu, hivyo si rahisi kufanya hujuma zinazoweza kuhatarisha utendaji
kazi wao ndani na nje ya nchi.

Anasema nchini Tanzania maabara inayofanya kazi ya kutoa majibu ya
sampuli za madini ni moja na ipo jijini Mwanza, huku ikielemewa na wingi wa kazi wanazoepelekewa.
“Hii dhana ni potofu na inatokana na ukweli kuwa nchini hapa taaluma ya utafiti ni ngeni katika mambo mengi hivyo baadhi ya viongozi wanaamini hicho kinachosemwa,” alisema.
Juu ya uhusiano unaowazunguuka, Mwaluko anasema wakati wa shuguli za utafiti waliajiri vijana zaidi ya 300 kutoka katika maeneo yanayaozunguka eneo hili ili kuwanufaisha kiuchumi.
Anasema walishindwa kabisa kuchukuwa watu kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kuwapatia mwangaza wa kimaisha na kuingia katika mfumo mzuri katika mlolongo wao kimaisha.
Mbali na mazuri yote hayo, Mwaluko hakusita kusema kuwa kwa sasa shughuli zao hizo zimesitishwa kwanza na serikali, huku wakiamini kuwa wanatarajia kuwatumia vijana wengi pindia uchimbaji zitakapoanza.
Kipaumbele kwa vijana wa maeneo ya jirani kama vile vijiji vya Nyasa na Madebe ambapo wanatarajia uzalishaji utakapoanza, vijana 1000 watapata ajira ya kudumu kwenye mgodi.
Katika kusaidia miradi ya kijamii wameweza kukarabati  shule ya msingi Nyasa kwa kujenga majengo bora pamoja na kuweka thamani na kununua vitabu vya kiada kwa matumizi ya wanafunzi shuleni hapo pia kuwajengea kisima kwa ajili ya kuuzamaji ili shule iweza kupata fedha kwa matumizi yake madogo madogo.
Nae Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Nyasa Fabian Msofe anasema kuwa  kabla ya kampuni ya CANACO haijafika kwenye eneo hilo shule hiyo ilikuwa kwenye mazingira magumu sana  kwani kulikuwa na madarasa 3 tu ambaya nayo hayakuwa katika hali nzuri na hakukuwa na ofisi ya walimu wala mwalimu Mkuu.
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyasa Shaban Ali, anasema kuwa tangu kampuni hiyo iingine kwenye eneo lao wameweza kuwafanyia mambo mengi ikiwamo ujenzi wa visima virefu viwili pamoja na kutoa nafasi za ajira kwa vijana wa kijiji hicho.
“Kwakweli tulikuwa tumesahaulika kwani huku Nyasa ni mbali kutoka na ubovu wa barabara lakini walipofika hawa wawekezaji wameweza kutusaidia tatizo la maji ila shida ipo kwenye zahanati kwani hakuna kwa sasa,” alisema.
Nae Mwanaid Ali anasema kuwa wanalazimika kwenda umbali wa zaidi ya Km 35 kupata huduma za afya kwenye hospitali ya Wilaya ya Handeni lakini kwa uwepo wa kampuni hii umeaidia kutupa usafiri pindi tunapo hitaji kupeleka mgonja hospitali.
“Kina mama wengi waliweza kupoteza maisha  hapo awali kutoka na ukosefu wa huduma ya afya karibu na kijiji kwani usafiri tuliokuwa tunautegemea ni pikipiki au umgonjwa akokotwe kwenye baiskeli na wanaume likiwa jambo la hatari,” alisema.
Hata hivyo Ali ameongeza kuwa chagamoto inayowakabili kwasasa ni wachimbaji wadogo wamekuwa ni kikwazo kwani kwa sasa eneo hilo linamgogoro na kesi ipo mahakamani ndio wanaokwamisha shuguli zamaendeleo kwenye eneo hilo.
“Tuliahidiwa kujengewa zahanati katika eneo hili ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo karibu na wananchi lakkini imeshindika na kutoka na wacimbaji wachache kuwapeleke wawekezaji hao mahakani kwa ajili ya kudai fidia,” alisema.
Wananchi wachache walikubali kujiunga kwenye kikundi na kuuza eneo kisheria na CANACO waliwalipa Mil200 sasa kuna baadahi walikata kuuza baada ya kuona wenzao wamefanikiwa wanataka  walipwe fidia wakati walikataa kuunga mkono na kuuza maeneo yao,” alliongeza.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger