Featured Post Today
print this page
Latest Post

MAKAMBA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO VYENYE THAMANI YA SH.MILIONI 2,JIMBONI KWAKE.

MAKAMBA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO VYENYE THAMANI YA SH.MILIONI 2,JIMBONI KWAKE.                    

Na Rais Said,Lushoto.

 
NAIBU Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Technologia,Januari Makamba amemwaga vifaa vya michezo jimboni kwake vyenye thamani ya sh.milioni 2 lengo likiwa ni kuhamasisha vijana kupenda mchezo wa mpira wa miguu.
 
Vifaa vilivyotolewa na Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ni mipira 50 kwa vijana ikiwa ni harakati za kuhamasisha kuinua sekta ya michezo jimboni humo na kupata timu ambayo baadae itakuja kuwa tishio kwenye medani ya soka mkoani hapa.

 
Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya mbunge,Katibu wa Mbunge huyo ,Hozza Mandia alisema vifaa vilivyotolewa ni katika kutekeleza ahadi zake alizozitoa kwa vijana jimboni humo kuwa atainua michezo kwa kutoa misaada kwa timu mbalimbali hasa za vijana.
 
 
Katibu huyo ambaye ni diwani wa kata ya Milingano alisema jitihada zinazofanywa na Makamba zinapaswa kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa soka jimboni humo lengo likiwa kuwapa fuksa vijana kushiriki kwenye michezo.
 
   “Kama unavyojua michezo ni ajira ambayo inaweza kuwainua vijana na ni fursa ya kipekee kwao hivyo tunamshukuru Mh,Naibu Waziri kwa msaada huu kwani utaweza kuwaondoa vijana kukaa vijiweni ambapo muda mwingi hufikiria kufanya vitendo viovu badala yake watakuwa wakishiriki michezo kutokana na kuwa na vifaa vya kuchezea “Alisema Hozza.
 
Aidha katibu huyo alitoa wito kwa vilabu vya Mgambo Shooting na Coastal Union kuweka utaratibu wa kutembelea Jimboni humo ili kuweza kuangalia wachezaji wenye viwango vya hali ya juu ambao wanapatikana wilayani kuliko kuchukua wachezaji nje ya mkoa ambao wakati mwingine wanashindwa kuipa mafanikio timu hizo.
0 comments

PPF YAELEZA MAFANIKIO YALIYOPATIKANA TOKEA KUANZISHWA KWAKE.

PPF YAELEZA MAFANIKIO YALIYOPATIKANA TOKEA KUANZISHWA KWAKE.

Na Raisa Said,Handeni.
 Mfuko wa Pensheni wa PPF,umeeleza mafanikio yaliyopatikana kuanzishwa kwake kuwa ni pamoja na kuwalipia ada za masomo ya juu watoto yatima walioachwa na wazazi wao ambao ni wanachama wa mfuko huo kutokana na kufanya vizuri kwenye shule mbalimbali nchini. 
Meneja wa Kanda wa PPF, Zahra Kayugwa, alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa tamasha la Handeni Kwetu lililofanyika mjini hapa na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.


"Tangu tulipoanzisha fao la elimu kwa wanachama waliokufa kwa watoto wao, limeonesha mafanikio makubwa kiasi cha kupelekea wengi wao kuendelea kusomeshwa na PPF hadi elimu ya juu"alisema Kayugwa.
Mfuko huo kwa mujibu wa takwimu alizozitoa jijini Tanga mwezi Septemba 2013, kwenye maonesho ya Kimataifa ya biashara, ambayo PPF ilishiriki kwa mara ya kwanza, zinaonyesha kwamba hadi kufikia Desemba mwaka jana, ulikuwa umetumia kiasi cha shilingi milioni 682.9 kusomesha wanafunzi wapatao 1,333 kote nchini.

Zahra akielezea changamoto zinazoukabili mfuko huo, ni suala la uwekezaji wa nyumba ambapo wanapotaka kujenga nyumba za gharama nafuu, mamlaka zinazohusika katika miji huwa zinawauzia bei kubwa kuliko uwezo wa mfuko hatua ambayo, wanashindwa kuendelea na kasi ya ujenzi wa nyumb

a hizo.
"Kwa kweli mfuko umekuwa na nia njema kabisa ya kuendelea kujenga nyumba za gharama nafuu kwa wanachama wake, lakini tatizo kubwa tunakatishwa tamaa na mamlaka za miji hapa nchini, tunapotaka ardhi kwa ajili ya kujenga nyumba hizo bei yake inakuwa kubwa kuliko maelezo," alisema Zahra ambaye anashuhghulika na mikoa ya Kinondoni, Pwani na Tanga.

Hata hivyo, alisema pamoja na hali hiyo bado mfuko huo, unajipanga kuhakikisha unajenga nyumba hizo na kwamba kwa sasa wanajenga katika mikoa ya Mwanza, Pwani, Mtwara, Iringa, na Dar es salaam ambapo pia wamekuwa wakifungua ofisi za mikoa kwa lengo la kuwahudumia wateja wao.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger