Featured Post Today
print this page
Latest Post

Wanamgambo wa Nigeria wauwa watu 33

Wanamgambo wa Nigeria wauwa watu 33

Mabaki ya chuo cha serikali ambapo wanafunzi 60 walichomwa moto hadi kufa Februari 25, 2014
Mabaki ya chuo cha serikali ambapo wanafunzi 60 walichomwa moto hadi kufa Februari 25, 2014
 
Shambulizi hilo la Alhamis karibu na mpaka wa Cameroon lilifanyika siku moja baada ya mashahidi kuripoti kuwa takribanu wanafunzi 60 waliuwawa katika chuo cha serikali.
 
Mashahidi na maafisa wa ndani kaskazini mashariki mwa Nigeria wanasema kundi linalotuhumiwa la  wanamgambo wa Boko Haram limeuwa watu 33 na kushambulia kwa bomu chuo cha kidini katika jimbo la Adamawa.

Jeshi ambalo mara nyingi haliamini taarifa za idadi ya vifo kutoka kwa mashahidi limesema washambuliaji sita waliuwawa katika tukio hilo pamoja na mwanajeshi mmoja  na raia watatu .

Shambulizi  hilo la Alhamis  karibu na mpaka wa Cameroon lilifanyika siku moja baada ya mashahidi kuripoti kuwa karibu wanafunzi 60 waliuwawa katika chuo cha serikali karibu na jimbo  hilo la Adamawa.
0 comments

Ufaransa yataka kuepusha kugawika kwa taifa la CAR

Ufaransa yataka kuepusha kugawika kwa taifa la CAR

Rais wa Ufaransa Francois Hollande
Rais wa Ufaransa Francois Hollande

 Rais wa Ufaransa ameiambia Jamhuri ya Afrika ya Kati, wanajeshi wa Ufaransa walioko huko watafanyakazi kuiepusha nchi hiyo isigawike, na kuwapokonya silaha wanamgambo na makundi ya wahalifu wanaowapiga vita Waislamu. 

Akiwasili mjini Bangui kutoka Nigeria, alikohudhuria sherehe ya miaka 100 ya muungano wa nchi hiyo, Rais Hollande alikutana na rais wa mpito wa Jamhuri ya Afrika ya kati Catherine Samba-Panza na pia kuwahutubia wanajeshi wa Ufaransa. Hii ni ziara ya pili ya Francois Hollande tangu mwezi Desemba mwaka jana na inakuja wakati kukiwa na ongezeko la wanajeshi wa kulinda amani katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Siku ya Jumanne bunge la Ufaransa lilipiga kura kurefusha muda wa wanajeshi wa Ufaransa nchini humo, licha ya Wafaransa wenyewe kutounga mkono ushirikishwaji wa wanajeshi wao katika koloni lake hilo la zamani.

Baadhi ya wanajeshi walioko Jamhuri ya Afrika ya Kati
Wakati huo huo Umoja wa Mataifa umesema watu milioni moja wameikimbia nchi hiyo tangu kuanza kwa ghasia za kimadhehebu mwaka uliopita na kwamba watu wapatao milioni 1.3 wanahitaji msaada wa haraka wa chakula katika nchi hiyo ya Afrika.

Miezi minne iliopita, Ufaransa ilituma wanajeshi wake ambao kwa sasa wamefikia takriban 2000 katika nchi hiyo ilio na idadi kubwa ya Wakristo, na waasi wa Kiislamu wa kundi la Seleka walichukua madaraka baada ya mapinduzi waliyofanya mwezi Machi mwaka Jana, na wamekuwa wakisukumwa nyuma na wanamgambo wa kundi la "anti-balaka."

Kando na kuwepo kwa wanajeshi wa Ufaransa, Wanajeshi 6000 wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika (MISCA) pia wapo nchini humo huku takriban wanajeshi 1000 wa Umoja wa Ulaya wakiwa bado wanatarajiwa kuwasili Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Samba Panza atoa wito wa kuundwa kikosi cha kulinda amani cha U.N

Hata hivyo akizungumza mjini Geneva, baada ya miezi miwili ya kusimamia shirika la Umoja wa Mataifa la ulinzi wa Raia mjini Bangui, Philippe Leclerc, amesema bado nchi hiyo haina wanajeshi wa kutosha wa kulinda amani.
0 comments

Mataifa ya magharibi kuisusia Urusi kisiasa

Mataifa ya magharibi kuisusia Urusi kisiasa

Turtschinow / Jazenjuk / Ukraine Viongozi nchini Ukraine

 Balozi wa Ukraine katika Umoja wa Mataifa ameomba kikao cha dharura cha Baraza la Usalama ili kufanya kila linalowezekana kuzuwia uvamizi wa Urusi, wakati vikosi vya jeshi la nchi hiyo vikidhibiti jimbo la Crimea. 

Lakini hatua hazionekani kuwa zinaweza kuchukuliwa na chombo hicho chenye nguvu cha Umoja wa Mataifa. Kama mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama, Urusi ina nguvu za karata ya turufu na inaweza kuzuwia baraza hilo kuidhinisha azimio lolote litakalokosoa ama kuiadhibu nchi hiyo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amemtaka Rais Vladimir Putin katika mazungumzo kwa njia ya simu "kuanza mazungumzo ya ana kwa ana na maafisa wa serikali mjini Kiev."
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon

Hali ni ya hatari Ukraine.

Akiita hali nchini Ukraine kuwa "ya hatari na inayodhoofisha amani", balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Samantha Power, ameliambia Baraza hilo kuwa "umefika wakati kwa uvamizi wa jeshi la Urusi nchini Ukraine kusitishwa."

Power na wajumbe wengine wa Baraza hilo wametoa wito wa kutumwa kwa wakaguzi wa kimataifa nchini Ukraine haraka iwezekanavyo kuangalia hali nchini humo, na Power ameonya kuwa "hatua za uchokozi za Urusi zinaweza kirahisi kuipeleka hali hiyo kupindukia hali ya kuporomoka kabisa." Pia ametaja kuhusu kazi za ujumbe wa upatanishi wa kimataifa kutumwa nchini Ukraine.
0 comments

AUA KIKONGWE ,NAYE AUAWA


AUA KIKONGWE ,NAYE AUAWA 

 

Kilindi. Kijana mmoja mkazi wa Kijiji cha Mabalanga wilayani Kilindi, Hassani Said (28) amemuua kwa kumkata na jembe kichwani bibi yake, lakini baadaye akauawa na wananchi wa eneo hilo.
Akizungumza na gazeti hili, mkazi mmoja wa kijiji hicho Omari Waziri alisema kuwa Februari 25 mwaka huu kijana huyo alikuwa akitoka shamba na bibi yake aliyefahamika kwa jina la Mwajuma Waziri (62), lakini ghafla alinyanyua jembe alilobeba na kumkata kichwani bibi yake na kufariki dunia.
Alisema kuwa baada ya kufanya mauaji hayo, Hassan alijificha kwenye nyumba iliyo jirani na wananchi walipopata taarifa akiwemo babu yake, Mkomwa Mkombozi (72) walikwenda kwa lengo la kumkamata.
Katika jitihada za kumkamata, mtuhumiwa alitoa panga na kumjeruhi vibaya Mkombozi ambaye anaendelea kupata matibabu kwenye Hospitali ya Handeni.
Baada ya kumtia mikononi, wananchi walimshambulia kwa zana mbalimbali hadi kumuua.
Hata hivyo, taarifa zilizopatikana baadaye zilidai kuwa, mtuhumiwa alikuwa na matatizo ya akili.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe alipotafutwa na kuhusu tukio hilo, alis


0 comments

SARUMAGAO WAJIANDAA KUANDAMANA

SARUMAGAO WAJIANDAA KUANDAMANA


Mgogoro wa wakazi wa Sarumagaoni Halmashauri ya Jiji la Tanga, wanaodai kutokana na kuhamishwa katika eneo hilo umeingia katika sura mpya baada wakazi hao kutishia kuandamana hadi ofisi za mkuu wa mkoa.
Eneo la Sarumagaoni limekuwa katika mgogoro wa muda mrefu pamoja na juhudi kutoka viongozi wa Serikali kujaribu kuutatua.
Mgogoro huo ulipamba moto baada ya kuwepo na taarifa za kuanza ujenzi wa barabara na reli kwenda Bandari Mpya ya Mwambani. Wakizungumza katika mkutano wa wananchi jana, wakazi hao walisema kwamba wamechoshwa na ukimwa wa Serikali hivyo dhamira iliyo mbele yao kwa sasa ni kufanya maandamano kwenda kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa.
Weshangazwa na ukimwa wa serikali, kwani mpaka sasa hakuna tathmini yoyote iliyofanywa jambo ambalo wananchi wanaona kama vile ni maandalizi ya kunyimwa haki yao.
“Tumeshasema na leo tunafanya hivyo tena, hatuondoki mpaka haki zetu tuzipate. Hatutaki tathmini ya kutumia darubini,” walisema zaidi.
“Baada ya kumalizika mkutano huu, tutaunda kamati ya maandalizi ya maandamano ya amani mpaka kwa Gallawa, tuna imani polisi wataturuhusu.”
0 comments

DC DENDEGO AMKABIDHI ZAWADI MFANYAKAZI BORA MWEZI WA KWANZA HOTEL YA TANGA BEACH

DC DENDEGO AMKABIDHI ZAWADI MFANYAKAZI BORA MWEZI WA KWANZA HOTEL YA TANGA BEACH

Kushoto ni Mfanyakazi bora wa mwezi wa kwanza katika hotel ya Tanga Beach Resort jijini Tanga kutoka kitengo cha Upishi akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego kwenye halfa ya kuwapongeza wafanyakazi bora iliyofanyika kwenye ukumbi wa La Crande La Casachika mwishoni mwa wiki
0 comments

WABUNGE WAWALIPUA BONGO MOVIES WASEMA NI OMBA OMBA BALAA

WABUNGE WAWALIPUA BONGO MOVIES WASEMA NI OMBA OMBA BALAA 

 

 

 


SKENDO nzito ya Bongo Muvi imeibuliwa na baadhi ya wabunge waliopo mjini Dodoma kufuatia kuwalipua wasanii wake kuwa, ni ombaomba balaa, Risasi Jumamosi lina mkanda mzima.

Kwa mujibu wa wabunge hao ambao walitaka majina yao yasitiriwe kwa sasa, baadhi ya wasanii hao ambao wengi ni mastaa wamekuwa wakiwazukia na kuwapiga mizinga jambo linalowashangaza hasa wakizingatia kuwa, wapiga mizinga hao wana majina makubwa na huonekana wakitembelea magari ya kifahari.

“Hivi nyie mapaparazi, mnashindwa kabisa kukomesha hii tabia ya mastaa wa Bongo Muvi? Hawa jamaa ni ombaomba sana.

“Wamekuwa wakitupiga mizinga sana. Tunawashangaa maana wengine wana majina makubwa, wanatembelea magari ya kifahari lakini bado wanaomba pesa ndogo,” alisema mbunge mmoja ambaye anatoka kwenye moja ya majimbo ya Mkoa wa Dar es Salaam.

KINACHOWASHANGAZA WABUNGE
Kwa mujibu wa wabunge hao, linalowashangaza zaidi ni kwamba wasanii hao ambao  ni wake kwa waume, wamekuwa wakipiga mizinga ya pesa ndogo badala ya kuomba pesa za kufanyia mambo makubwa yenye mikakati mizito.

“Mtu anakuja, anasema anasumbuliwa na kodi ya nyumba au anasema hajala. Hivi kweli mastaa wakubwa kama akina…(anataja jina) ni wa kuomba vijisenti kama vya kodi ya nyumba jamani?” alihoji mbunge mwingine kati ya watano waliokuwa wakizungumza na gazeti hili.

Waheshimiwa hao waliendelea kuwaanika mastaa hao kwa kudai kwamba, walichogundua ni kuwa inapotokea wakapewa hitaji lao la fedha, huishia kukaa baa hadi usiku wa manane na asubuhi wakiamka wako vilevile kama hawakupewa.

MWAKIFWAMBA ABANWA NA RISASI
Ili kuweka sawa madai hayo mazito na yenye aibu kubwa kwa tasnia hiyo maarufu nchini, Risasi Jumamosi lilimtafuta Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba ambaye alikiri kuwepo kwa malalamiko hayo ya wasanii wake kuwa ombaomba!

HUYU HAPA MWAKIFWAMBA
“Ni kweli kabisa. Mimi mwenyewe nimewahi kusikia malalamiko hayo, lakini unajua tena ni mambo binafsi, mtu anapiga mizinga kwa mambo binafsi si rahisi kumwingilia,” alisema rais huyo.
Aliendelea kusema kuwa, katika vikao mbalimbali vya kisanii, amewahi kuweka wazi msimamo wa taasisi kwamba kila msanii aishi maisha yenye heshima huku akiwa mbali na mazingira yenye kusababisha aibu katika jamii.

KUMBE HATA JK ALIWAHI KUMLALAMIKIA
Katika kuonesha hasira zake juu ya tuhuma hizo zenye dharau katika gemu la filamu, Mwakifwamba alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, katika moja ya mazungumzo yake na Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete ‘JK’ aliwahi kumlalamikia kwamba, wapo mastaa ambao kazi yao ni kupiga mizinga isiyo na tija.

“Rais mwenyewe aliwahi kuniambia kuna wasanii wakiwasiliana na yeye wanamwambia mambo ya pesa za kula.

“Kuna msanii aliwahi kumtumia meseji JK akimwambia, ‘mjukuu wako leo hali mbaya’,” alisema Mwakifwamba.
Akaendelea: “Sasa we’ unakutana na rais badala ya kumweleza mikakati mikubwa na nini cha kusaidiwa kuifanya tasnia iweze kuendelea, unapiga mizinga hujala, ni aibu sana.”

WALISHAMPIGA ‘MIZINGA’ HADI ‘MTOTO WA MKULIMA’
Mwakifwamba hakukubali kufumba midomo yake bila kupasua yote ambapo alizidi kudai kuwa, hawashangai sana wasanii wake hao kwani waliwahi kumpiga mizinga hadi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda ‘Mtoto wa Mkulima’. 
“Niliwahi kukutana na Waziri Mkuu Pinda, nikamwomba mambo ya kuisaidia tasnia ya filamu Tanzania, akasema afadhali mimi nimeongea vitu vya maana, kuna wenzangu alikutana nao ‘wakambomu’ fedha za matumizi binafsi, nilishangaa sana,” alisema Mwakifwamba. 

RISASI LAWASAKA MASTAA, WAPATIKANA HAWA:
Jacqueline Wolper, ni staa wa filamu za Kibongo. Filamu yake ya kwanza ni Ama Zao Ama Zangu. Yeye alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema:
“Ni kweli, sikatai kwamba hiyo tabia ipo tena sana tu. Lakini wanaoongoza ni mastaa wa kiume, hao ndiyo wanaotutia aibu ya kuonekana sisi ni o
mbaomba.”

STEVE NYERERE
Yeye ndiye Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity. Alisema anavyojua kuna kuonana kirafiki na waheshimiwa na kuonana kiajenda.
“Tabia ya kuomba fedha kwa waheshimiwa ipo. Lakini linapokuja suala la tasnia yetu kupeleka hoja kwao, tunaanza hoja baada ya hapo kuna waheshimiwa wengi wana urafiki na wasanii, tunaitana pembeni na kupiga kirungu.
“Siwezi kukaa na waheshimiwa kama Rostam Aziz, William Ngeleja, Mheshimiwa Abood na Nimrod Mkono halafu nikawaacha hivihivi, kisa eti mimi ni Mwenyekiti wa Bongo Muvi,” alisema Steve akionesha kumshangaa mwandishi aliyempigia simu kutaka usawa wa mizani ya habari hiyo. 
ODAMA YEYE
Jennifer Kyaka ‘Odama’ yeye alipata umaarufu mkubwa kupitia Tamthiliya ya Odama iliyokuwa ikirushwa na Televisheni ya Taifa (wakati huo TVT). Alipopigiwa simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa licha ya kurudiwa mara kadhaa.
AUNT EZEKIEL
Risasi pia lilimtafuta  nyota mwingine aliye mahiri kwenye sinema za Bongo, Aunt Ezekiel ambaye filamu iliyompaisha sana inaitwa Miss Tanzania. Yeye simu yake ya mkononi ilionesha kutokuwa hata na laini kwa wakati huo.

RAY AFUNGUKA
Staa mkongwe katika gemu tangu enzi za Kaole Sanaa Group, Vincent Kigosi ‘Ray’ aliposakwa na kuulizwa kuhusu madai hayo ya wasanii kuwa ombaomba alisema:
“Wasanii wengi wanawaza maisha ya hapa na si baadaye. Badala ya mtu kuweka shida zake kwenye mfuko wa karatasi, anaweka kwenye rambo ambao unapiga kelele.
“Mwisho wa siku anaomba shilingi milioni tatu akagombolee gari au asaidiwe kodi ya nyumba, anasahau kuwa kapata nafasi ya kuonana na mheshimiwa azungumzie tasnia tunavyonyonywa hadi kuuza hati miliki,” alisem Ray.
Credits:Global Publishers

0 comments

UKATILI:MTOTO ABURUZWA NYUMA YA PIKIPIKI NA BABA YAKE KISA HAJAENDA SHULE

UKATILI:MTOTO ABURUZWA NYUMA YA PIKIPIKI NA BABA YAKE KISA HAJAENDA SHULE 

 

Mtoto Anastazia Jumanne (12) ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi katika wilaya na mkoa wa Geita amefanyiwa ukatili wa kutisha baada kufungwa mpira kwenye pikipiki na baba yake mzazi na kisha kuanza kumburuza mtaani.

Tukio hilo la kusikitisha limetokea jana majira ya sa tatu asubuhi katika moja ya mitaa ya mjini humo ambapo inadaiwa kuwa binti huyo anayesoma darasa la nne katika shule hiyo alikataa kwenda shule kitendo ambacho kilimkasirisha baba yake aitwaye Jumanne Nkoyogi ambaye pia ni mfanyabiashara wa samaki mjini Geita.

 mashuhuda wa tukio hilo baada ya kuona asubuhi hiyo mtoto huyo akiburuzwa huku amefungwa kwenye pikipiki walianza kupiga makelele na kukusanyana kwa lengo la kumkamata baba huyo aliyekuwa anafanya unyama huo.

  Baada ya kumkamata na kumtia kumtia mikononi mwao walimpeleka kwenye ofisi ya sungusungu iliyopo Ihayabuyaga kata ya Kalangalala na kufungiwa humo kwa usalama wake.
Akizungumzia tukio hilo katibu wa sungusungu kata ya Kalangalala aliyempokea mtuhumiwa huyo Abel Richard amesema tukio hilo liliwafanya wananchi kujaa jazba dhidi ya mzazi huyo na kutaka kumpiga.

Amesema mzazi huyo kwa sasa anashikiliwa na jeshi la polisi wilayani Geita baada ya katibu huyo kuwasiliana na uongozi wa jeshi hilo na kuwatuma askari kwake kumchukua haraka kwa usalama wake.

Afisa upelelezi wa mkoa wa Geita Simon Pasua amekiri kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi hadi sasa kwa upelelezi zaidi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger