Featured Post Today
print this page
Latest Post

MKURUGENZI WA VIJANA TAIFA ATOA SEMINA KWA VIJANA MKOA WA TANGA.


Mgeni rasmi Bw. Ramadhani  Kaswa, Mkuu wa kitengo cha Mipango  katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa akifungua semina hiyo. Bw. Kaswa amemwakilisha Katibu Tawala Mkoa.


Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Tanga Bi Digna Tesha akiteta jambo wakati wa semina


Profesa Elisante Ole Gabriel akitoa neno katika semina hiyo.



Profesa Elisante Ole Gabriel,kushoto,kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Taifa akiwa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Chiku Gallawa mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ajili ya semina ya vijana.


Baadhi ya vijana waliohudhuria semina.  Ni Maafisa vijana na vijana wa wenye umri wa miaka 15 hadi 35 kutoka Halmashauri zote mkoani Tanga.


Baadhi ya vijana waliohudhuria semina.  Ni Maafisa vijana na vijana wa wenye umri wa miaka 15 hadi 35 kutoka Halmashauri zote mkoani Tanga.


Baadhi ya vijana waliohudhuria semina.  Ni Maafisa vijana na vijana wa wenye umri wa miaka 15 hadi 35 kutoka Halmashauri zote mkoani Tanga.


Baadhi ya vijana waliohudhuria semina.  Ni Maafisa vijana na vijana wa wenye umri wa miaka 15 hadi 35 kutoka Halmashauri zote mkoani Tanga.
Habari na picha kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa “www.mkoatanga.blogspot.com”
0 comments

Ukimya mjini Cairo, idadi ya vifo yaongezeka

Mji mkuu wa Misri Cairo unaripotiwa kuwa na utulivu asubuhi ya leo, baada ya operesheni ya kijeshi hapo jana, ambayo iliuwa watu zaidi ya 525. Udugu wa kiislamu umepanga maandamano zaidi mchana wa leo.
Asubuhi ya leo mitaa ya Cairo ambayo kwa kawaida huwa na msongamano mkubwa wa magari ilikuwa mitupu, baada ya tangazo la hali ya hatari lililoanza kutekelezwa usiku wa kuamkia leo. Vyombo vya habari nchini Misri vimesema kuwa


Ukimya mjini Cairo, idadi ya vifo yaongezeka

benki, soko la hisa na posta vitafunga milango leo, kwa hofu kuwa ghasia zaidi zaweza kutokea.
Ulinzi wa kijeshi umeimarishwa kando kando ya barabara muhimu na ofisi za serikali, na jeshi limesema halitakuwa na mzaha katika kuhakikisha kuwa sheria ya hali ya hatari inaheshimiwa, hilo likiwa onyo la wazi kwa wafuasi wa kundi la udugu wa kiislamu ambao wanaweza kujaribu kuonyesha ukaidi.

Idadi ya vifo yazidi kuongezeka

Idadi ya waliokufa inazidi kuongezeka  

 
Tangazo la hivi karibuni kutoka maafisa wa wizara ya afya limesema kuwa watu 525 waliuawa katika operesheni ya jana, iliyoendeshwa na jeshi kuwafurusha waandamanaji wanaotaka Mohamed Mursi arejeshwe madarakani. Tangazo hilo lilisema kuwa watu 137 waliuawa katika kambi ya Rabaa al-Adawiya, 57 walipoteza maisha katika uwanja wa al-Nahda, na 227 waliuawa katika maeneo mengine ya nchi. Udugu wa kiislamu umesema takribani watu 2,600 waliuawa jana.
Umwagaji damu huo umelaaniwa kutoka pande mbali mbali za dunia. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani John Kerry alisema mauaji hayo hayakubaliki, na yanapaswa kulaaniwa vikali. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Guido Westerwelle aliitaka serikali ya Misri siyo tu kutoa uhuru wa maandamano ya amani, bali pia kuhakikisha usalama wa waandamanaji. Rais wa Ufaransa Francois Hollande amemuita balozi wa Misri nchini humo, kumtaka atoe maelezo kuhusu umwagaji damu huo wa jana.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Guido Westerwelle ametaka usalama wa waandamanaji uhakikishwe  
 
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Guido Westerwelle ametaka usalama wa waandamanaji uhakikishwe
Denmark imetangaza kuwa imesimamisha msaada wake wa Maendeleo kwa Misri, kudhihirisha kukerwa kwake na umwagaji damu uliotokana na operesheni ya jana mjini Cairo.
Wakristo walengwa kwa kisasi
Huku hayo yakiarifiwa, makanisa kadhaa ya madhehebu ya kikoptiki yamechomwa moto na wafuasi wa udugu wa kiislamu, kama kisasi kwa mkuu wa madhehebu hayo Papa Tawodros, ambaye aliunga mkono mapinduzi ya kijeshi yaliyomuangusha rais Mohamed Mursi. Shirika la habari la Misri MENA, limesema kuwa wakristo katika miji ya Minya,
Sohag na Assiut walilazimika kukimbia kupitia mapaa ya kanisa, baada ya kuvamiwa na umati wa watu wenye hasira.
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa serikali ya Misri imekifunga kivuko kati ya nchi hiyo na ukanda wa Gaza, kwa kile ilichokieleza kuwa sababu za kiusalama.
0 comments

MKUU WA MKOA WA TANGA AMSWEKA LUPANGO MKAGUZI WA HALMASHAURI YA PANGANI.




https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhn1GAbCNujks4KgD4Nw8Nt77ejOQ_fNJGIer5_MgkUEG0vdp_xEPaccj6b2g9sG0EYBLaU8uXv-qd6a9DBOVB6QdR7knXcHjTMYsw3izoMA_PreIbQ5p36YVfMZJgY5Fvn6UBzx6651erI/s1600/P1020398.JPGMKUU wa mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa, amemuweka rumande Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, Najim Mpate, kwa madai ya kumdharau wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Tukio hilo lilitokea jana wakati Mpate alipokuwa anatoa maelezo kufuatia hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Halmashauri ya Pangani ambapo ilionek
ana kuna hoja ambazo hazijapatiwa majibu tangu mwaka wa fedha 2008/2009.

Hoja kuu inayoongelewa ni ile inayohusu mkandarasi mmoja aliyelipwa fedha zaidi ya mkataba ulivyokuwa unaonyesha hivyo Mkuu wa Mkoa alikuwa anataka maelezo kwa nini hoja hiyo ya karibu miaka mitano iliyopita inaendelea kujirudia na kwanini mkandarasi husika hajarudisha fedha hizo ili kufuta hoja hiyo.

Mara baada ya kujieleza Mkaguzi huyo alilipiga chini kabrasha alilokuwa amelishinda, kitendo ambacho kiliwashtua madiwani kwani kilionekana kuwa ni dharau ya wazi kwa Mkuu wa Mkoa.

Bada ya tukio hilo, hilo Mheshimiwa Gallawa alisikika akisema, “Hivi huyu ni nani mbona amekaa kijeuri. Kwanza unajibu maswali kijeuri, lakini mimi ni mtu wa kunitupia faili chini” Hii ni halmashauri yako? OCD mchukue huyu mtu ukampumzishe.”

Akieleza baada ya kuisha kikao, Mheshimiwa Gallawa alisema yeye ndiye anawajibika HAlmashauri zinapokuwa na hoja zilizokosa majibu na hivyo hatakubali wazembe wachahce kwenye halmashauri wamharibie dhamana aliyopewa ya kuwatumikia wananchi.”
 
Chanzo Juma Mtanda.blogspo.com
0 comments

ENKI YA CRDB YATANGAZA NEEMA YA MIKOPO YA NYUMBA

Benki ya CRDB yatangaza neema ya mkopo wa nyumba kwa wateja wao

Mkugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei, akizungumza na wadau mbalimbali katika akizindua Mikopo ya nyumba ijulikanayo kwa jina la Jijenge itakayotolewa na benki hiyo, Dar es Salaam jana.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WATEJA wa benki ya CRDB na Watanzania kwa ujumla, sasa wanaweza kupata nyumba kwa urahisi, endapo wataamua kujiunga na huduma mpya ya Jijenge iliyozinduliwa jana jijini Dar es Salaam.
Katika huduma hiyo mpya, mteja wa CRDB anaweza kukopa fedha za kujenga nyumba ya kisasa, kukarabati au kununua na kutakiwa kulipa katika kipindi cha miaka 20.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dk Charles Kimei, alisema wameamua kuanzisha huduma hiyo ili kuwakomboa Watanzania katika kipindi cha ukosefu wa nyumba bora za kuishi.
Alisema kuwa Watanzania wengi wamekuwa na changamoto za kukosa makazi bora ya kuishi, hivyo yoyote anaweza kuchukua mkopo wa kununua nyumba, kujenga au kukarabati na kutakiwa alipe katika kipindi cha miaka 20.
“Hii ni hatua ya CRDB kuboresha makazi ya Watanzania wote, ukizingatia kuwa kumiliki nyumba kwa Dunia ya leo ni mtihani mkubwa kutokana na ugumu wa maisha.
“Kinachotakiwa ni kufika kwa tawi lolote la CRDB na kuonyesha kiwango cha mshahara wako, huku mtu kuanzia mwenye mshahara kuanzia 200,000 akiwa na sifa ya kupata mkopo,” alisema.
Aidha, Kimei alisema sio waajiriwa tu, ila hata wajasiriamali nao wanaweza kupata mkopo huo ambao umeanzishwa kwa ajili ya kuboresha makazi ya Watanzania wote.
 
chanzo Handeni kwetu;
0 comments

JAMAA AMDUNDA MKEWE NA KUSABABISHA KIFO

UKATILI:! JAMAA MMOJA MKAAZI WA NAMTUMBO MKOANI RUVUMA AMUUA MKEWE! SOMA KISA HAPA


       
Huu ni moja ya ukatili kwa kina mama(Picha na maktaba)
 
Na Steven Augustino wa Demashonews Namtumbo,
 
 Mfugaji wa Jamii ya Kisukuma anayeishi katika Kijiji cha Mtelamwahi Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma aliyefahamika kwa jina la Maiko Sajini(24) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumpiga na kumuua Mkewake kutokana na kilicho daiwa kuwa chanzo cha ugomvi huo ni wivu wa kimapenzi.
Shuhuda wa tukio hilo Anna Yohana ambaye ni mjomba wa Marehemu alisema kuwa Marehemu Dagwanedi Jogi (22) alikubwa na makasa huo baada ya mumewe huyo kumtuhumu kuwa amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mmoja Kijijini hapo hali ambayo ilizusha mtafaruku huo kati ya wanandoa
hao. Alisema siku ya tukio mumewe huyo alisafiri kwenda kijiji jirani nakwa kawaida yake huwa anarudi usiku wa manane kama alivyo fanya siku hiyo,lakini kila anapo rudi humkuta mkewe akiwa amelala lakini cha kushangaza wakati akikaribia nyumbani hapo alikutana na kijana huyo njiani ambaye kila mara alidai kuwa amekuwa akimhisi kumuiingilia katika ndoa yake na hata alipofika nyumbani kwake alimkuta mkewe akiwa hajalala hali ambayo ilimfanya amhoji juu ya hali hiyo. 
Alisema wakiwa katika mahojiano hayo ilitokea kuto elewana kati yao ambapo mwanaume huyo aliomba amkague mkewe huyo katika sehemu zake za  siri ili kujiridhisha juu ya mashaka yake hayo lakini marehemu
alikataa kata kata hali ambayo ilimfanya mtuhumiwa huyo kutumia nguvu katika ukaguzi huo ambapo baada ya kuangalia aligundua kuwa mkewe huyo alikuwa ametoka kufanya tendo hilo alilo lihisi. 

Akizungumzia tukio hilo mtendaji wa kata ya Ligera Alli Manoni alisema kuwa baada ya kupokea taarifa hizo yeye kwa kushirikiana na uongozi wa Kijiji cha Mtelemwahi walienda eneo la tukio na kushuhudia unyama huo lakini kwavile mtuhumiwa alikuwa amekimbia walitoa taarifa Polisi  ambao walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa anaelekea katika Kijiji cha Suruti Wilaya ni humo. 
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusidedith Nsimeki amedhibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kueleza kuwa mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma za mauaji hayo baada ya kukamilika kwa taratibu za kipolisi. 
Aidha Kamanda Nsimeki aliendelea kufafanua kuwa pamoja na mambo mengine Polisi wanaendelea kumsaka mtu ambaye alidai kuwa chanzo cha ugomvi huo ambao ulisababisha mauaji hayo ambayo hadi sasa jina lake halijafahamika.
 


0 comments

TRAFIKI FEKI ALIVYONASWA JIJINI DAR ES SALAAM

TRAFIK FEKI ANASWA JIJINI DAR ES SALAAM MAENEO YA KINYEREZI.KILA MOJA ANA NJIA YAKE YA KUTAFUTA HELA BHANA!!

 Askari Bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliyekamatwa jana mchana maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya sare zake mara baara ya kukamatwa.Askari huyu feki amefikishwa kwenye Kituo cha Polisi Stakishari ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa juu yake.
Afande huyo akiwa chini ya ulinzi wa Polisi mara baada ya kukamatwa mchana wa jana akila vichwa maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es Salaam.
Afande huyo akiwa Kituo cha Polisi Stakishari.
0 comments

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA MAJI TAKA MKOA WA TANGA YAPANIA KUBORESHA HUDUMA ZAKE



·       



 BWAWA LA MAJI MABAYANI AMBALO NDILO LINALOTEGEMEWA NA    WAKAZI WA JIJI LA TANGA.

Mamlaka ya maji safi na maji taka mkoa wa Tanga, Tanga UWASA inatarajia kuongeza mitandao ya usambazaji wa maji ktk baadhi ya maeneo ya jiji la Tanga, kwa lengo la kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo ya pembezoni mwa jiji la Tanga.
Hayo yamebainishwa hivi karibuni kwenye hafla ya kusimika bodi mpya ya mamlaka hiyo iliyofanyika hivi karibuni mkoani hapa na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na Serekali.
Maeneo yatakayonufaika kutokana na kuboreshwa kwa mitandao hiyo ya maji safi ni pamoja na Kange masiwani, Kange Mkurumuzi, Mwakidila C na baadhi ya maeneo ya mji wa Pongwe.
Kwa upande wa maji taka mamlaka imekwisha tenga fedha kwa ajili ya upanuzi ambao hadi sasa bomba la maji taka la barabara ya tano upo ktk hatua ya mwisho na pia ulazaji wa mabomba maeneo ya barabara ya Mnyanjani Lumumba kwa barabara ya 13 utafanyika mwaka huu wa fedha.
Mbali na maboresho hayo mamlaka hiyo pia inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji kupitia mpango wa maendeleo ya sekta ya maji ktk maeneo ya pembezoni mwa mji ambapo inatarajiwa ifikapo mwaka 2015, wakazi wote wa pembezoni mwa jiji la Tanga watakuwa wanapata maji safi na salama.
0 comments

meza ya magazeti leo alhamisi

DSC 0189 1e8c9
DSC 0190 a41aa
DSC 0191 99c6d
DSC 0191 aeca4
DSC 0192 71002
0 comments

Makunga, Kibanda wana kesi ya kujibu


kibandaa 5a158
Meneja Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Theophil Makunga (katikati) akizungumza na Mwanasheria wa Kampuni hiyo, Doris Marealle nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana baada ya kuahirishwa kwa kesi inayomkabili pamoja na aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda (kushoto).
hdg

Meneja Uendelezaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Theophil Makunga na wenzake wawili, wamepatikana na kesi ya kujibu katika kesi ya makala ya uchochezi inayowakabili.
Makunga na wenzake Absalom Kibanda na Samson Mwigamba wanakabiliwa na kesi ya uchochezi dhidi ya askari wa majeshi ya ulinzi kwa kuchapisha makala kwenye Gazeti la Tanzania Daima yenye maneno yaliyolenga kuwashawishi wasiwatii viongozi wao.
Makala hayo ya Novemba 30, 2012 yaliyokuwa na kichwa cha habari 'Waraka maalumu kwa askari wote' yaliandikwa na mshtakiwa wa kwanza, Mwigamba ambaye ni mwandishi wa makala katika safu yake ya 'Kalamu ya Mwigamba' katika gazeti hilo.
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Warialwande Lema jana aliwaamuru washtakiwa hao kujiandaa kupanda kizimbani kujitetea baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wake.
Wakili wa Serikali Beatha Kitau, alisema upande wa mashtaka haukuwa na shahidi mwingine zaidi hivyo kuiomba mahakama kufunga ushahidi wao. Kabla ya kufunga ushahidi wake, upande wa Jamhuri uliwaita mashahidi watatu kutoa ushahidi.
Mashahidi hao ni pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Usajili wa Magazeti, Raphael, Hokororo, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza (ACP) kutoka Kitengo cha Sheria cha jeshi hilo, George Mwambashi na Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SSP), David Hizza.
Baada ya Jamhuri kufunga ushahidi wake, mawakili wa utetezi wakiongozwa na Isaya Matambo waliiomba mahakama iwapatie mwenendo wa kesi hiyo kwa ajili ya kuandaa hoja kama washtakiwa wana kesi ya kujibu au la.
Mbali na Matambo, mawakili wengine wa utetezi ni Nyaronyo Kicheere na John Mhozya ambao wote watatu wanawatetea Mwigamba na Kibanda na Imam Daffa kwa niaba ya Makunga.
Hata hivyo, Hakimu Lema aliwakatalia akisema kuwa hawezi kutoa nafasi ya kufanya majumuisho ya hoja kama washtakiwa wana kesi au la.
Hata hivyo, Hakimu Lema hakufafanua sababu ya kukataa ombi hilo, badala yake alitoa uamuzi papo hapo kuwa washtakiwa wote wana kesi ya kujibu.
"Baada ya prosecution (upande wa mashtaka) kufunga ushahidi wake na kwa kuzingatia ushahidi ulioko mahakamani, Mahakama hii imeona kuwa washtakiwa wote wana kesi ya kujibu na wanatakiwa wajiandae kwa utetezi," alisema.
Kutokana na uamuzi huo, Hakimu Lema aliamuru washtakiwa waanze kujitetea Septemba 3, mwaka huu.Wakati uamuzi huo ukitolewa, mshtakiwa wa kwanza, Mwigamba hakuwepo mahakamani, badala yake aliwakilishwa na mdhamini wake Rose Moshi ambaye alisema mshtakiwa huyo hakuweza kufika mahakamani kwa kuwa ni mgonjwa na amelazwa Hospitali ya St. Thomas Arusha.
Makunga ambaye ni mshtakiwa wa tatu aliunganishwa katika kesi hiyo kutokana na gazeti hilo kuchapisha makala hayo katika mitambo ya uchapaji ya Kampuni ya MCL, wakati alipokuwa akikaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji.
Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda alidai kuwa Novemba 30, 2011, Makunga akikaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwananchi Communications ilichapisha waraka wenye kichwa cha habari "Waraka Maalum kwa askari wote".
Kibanda ambaye ni mshtakiwa wa pili, anakabiliwa na mashtaka ya kuruhusu makala hayo kuchapishwa katika gazeti hilo, wakati huo akiwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima.
Upande wa mashtaka unadai kuwa makala hayo yaliyotoka katika gazeti la Tanzania Daima Toleo Na. 2552 ni kinyume na kifungu cha 32 (1) (c) na 31 (1) (a) cha Sheria ya Magazeti, Sura ya 229, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Unadai kuwa makala hayo yalilenga kuwashawishi askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Polisi, Magereza na Mgambo kutokutii amri za viongozi wa majeshi hayo na Serikali kwa jumla.
:CHANZO MWANANCHI
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger