Featured Post Today
print this page
Latest Post

WAWILI WAPANDISHWA KUZIMBANI KWA KUTAKA KUMPA RUSHWA DC KILINDI.

WAWILI WAPANDISHWA KUZIMBANI KWA KUTAKA KUMPA RUSHWA DC KILINDI.

 


Na Oscar Assenga, Kilindi.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoa wa Tanga (Takukuru) imewafikisha mahakama ya wilaya ya Handeni wakazi wawili wa wilaya ya Kilindi kwa tuhuma za kutaka kutoa rushwa ya sh.1,100,000kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Suleima Liwowa ili atamke eneo la Elerai liwe kijiji halali na kimeundwa baada ya kupitia taratibu zote za kisheria jambo ambalo halikuwa la kweli.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga,Edson Makala alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 12 mwaka huu mara baada ya taasisi hiyo kuweka mtego ambao uliwekwa na ofisi ya mkuu huyo wa wilaya na kufanikiwa kuwakamata wahusika hao.

Makala alisema watuhumiwa hao  walitenda kosa la kujihusisha na vitendo vya kushawishi na kutoa hongo ya kiasi cha sh.milioni moja na laki moja kwa mkuu wa wilaya hiyo ili kulifanya jambo la eneo hilo lifanikiwe kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.

Kamanda Makalo aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Sharrif Lemanda Lemteka mkazi wa Lesoit Kiteto na Emanuel Ole Kileli mkazi wa Elerai kata ya Kibirashi  wilayani Kilindi na kufunguliwa kesi  ya jinai Na CC 228/2013 ambapo washtakiwa wanadaiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa kinyume na kifungu  cha 15(b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na 11/2007.

Alisema washtakiwa wote wawili walisomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa George Magoti mbele ya hakimu wa wilaya ya Handeni Patrick Maligana ambapo washtakiwa wote wawili walipata dhamana baada ya kutimiza masharti yaliyotolewa na mahakama wakati kesi hiyo ikipangwa kutajwa tena mahakamani hapo Novemba 28 mwaka huu.

Aliongeza kwa kutoa wito kwa wananchi kuzingatia maadili na kutojikujihusisha na vitendo vya rushwa kwani kufanya hivyo watakuwa wameingia matatani.
0 comments

KUTOKA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 18.11.2013

0 comments

KUTOKA KWENYE MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

0 comments

BARABARA KUTOKA KITUO KIKUU CHA MABASI JIJINI MBEYA HADI META SASA MAMBO SHWARI

0 comments

MOURINHO: RONALDO NDIYE MCHEZAJI BORA KULIKO WOTE niLIOWAHI KUWAFUNDISHA'

MOURINHO: RONALDO NDIYE MCHEZAJI BORA KULIKO WOTE niLIOWAHI KUWAFUNDISHA'

mourinho-ronaldo-22-nov 1200x6751 27b8b
Jose Mourinho amesema kwamba kumfundisha Cristiano Ronaldo walipokuwa Real Madrid kinabakia kuwa kitu muhimu na kizuri katika maisha yake. (HM)

Wawili hao walikaa pamoja kwa miaka mitatu ndani ya Santiago Bernabeu, huku Ronaldo akifunga jumla ya mabao 168 katika mechi 164 wakati Mourinho akiwa katika benchi la Bernabeu.
Na japokuwa imewahi kuripotiwa kwamba hawakuwa wakielewana walipokuwa Madrid, lakini kocha wa sasa wa Chelsea amemsifia sana mshambuliaji huyo mwenye miaka 28.
"Kumfundisha Ronaldo kilikuwa kitu kikubwa sana kwenye maisha yangu ya ufundishaji," Mourinho aliiambia France Football.
"Ndio mchezaji mweledi zaidi ambaye nimewahai kumuona.
"Kocha na mchezaji wanaweza kuwa na tofauti zao kwa muda fulani, lakini inashiia pale pale, sina tatizo nae.
"Kuwa na Ronaldo katika klabu moja ni kitu bora kabisa kilichowahi kunitokea kwenye soka. "
Ronaldo mpaka sasa ameshafunga mabao 24 katika mechi 17 alizocheza msimu huu katika mashindano yote, na jana usiku aliingiza mguu mmoja timu ya Ureno katika mashindano ya kombe la dunia baada ya kuifunga Sweden 1-0 katika mechi ya kufuzu kucheza World Cup 2014. Chanzo: shaffihdauda
0 comments

Mandela sasa hawezi kuzungumza

Mandela sasa hawezi kuzungumza

mandela_43632.jpg
Mke wa zamani wa Nelson Mandela, amesema rais huyo wa zamani hawezi kuzungumza, lakini anatumia uso kuwasiliana na watu.
Winnie Madikizela-Mandela alieleza kuwa Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 95, ni mgonjwa kweli lakini alikanusha tetesi kuwa mashini ndio inamsaidia kupumua.
Mwezi wa Septemba Bwana Mandela alirudi nyumbani baada ya kulazwa hospitali mjini Pretoria kwa karibu miezi mitatu akitibiwa ugonjwa wa mapafu.
Serikali ya Afrika Kusini imesema hali yake bado ni ya kutia wasi-wasi na wakati mwengine hubadilika.(P.T)
0 comments

HUYU MCHEZAJI KUSAJILIWA YANGA KWA MASHART

HUYU MCHEZAJI KUSAJILIWA YANGA KWA MASHART


YANGA na Azam kama zinamtaka straika wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi ni fedha yao tu, lakini kuna sharti lazima walifanye.


Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) limetoa masharti na muongozo wa klabu zinazomtamani mchezaji huyo aliyesitisha mkataba na Etoile du Sahel ya Tunisia.

Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Saad Kawemba aliiambia Mwanaspoti kuwa: “Hakuna kinachoizuia klabu kutaka kumsajili Okwi, cha muhimu wanatakiwa kuongea na Etoile du Sahel ya Tunisia, wakimalizana nao basi watamchukua, hivyo ni ruksa cha muhimu ni kufuata sheria na haki.”

Okwi ameidhinishwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuichezea SC Villa ya Uganda kwa muda wa miezi sita huku sakata lake la Etoile likifanyiwa ufumbuzi.

Mchezaji huyo anaidai Etoile malimbikizo ya mishahara pamoja na dau lake la usajili huku Simba iliyomuuza kwa Waarabu hao nayo ikidai dau lake Sh 480 milioni.

Suala hilo lipo Fifa na Kawemba amewahakikishia Simba kwamba wasiwe na wasiwasi watapata haki yao.


credit:Mwanaspoti.
0 comments

AFANDE SELE KAJIUNGA RASMI CHADEMA SOMA HAPA!!

AFANDE SELE KAJIUNGA RASMI CHADEMA SOMA HAPA!!

akuna kusanda,hakuna kumbwanda,mbele kwa mbele makamanda,vua gamba vaa
0 comments

PICHA: UKATILI! MWANAMKE AKATWA MGUU NA MUMEWE

 



Hali ya wanawake inazidi kuwa mbaya ndani ya nchi yao TANZANIA inayosifiwa kuwa ni Kisiwa cha Amani (Amani kwa wanaume) Tukio hili lilitokea mapema mwezi wa nane mwaka huu Kijiji cha Nyantira Tarime Mara. Katika mazungumzo yake huyu binti alisema kwamba anatamani sana kurudi nyumbani kwa wazazi wake, tatizo ni kwamba kwa kuwa alilipiwa MAHARI na mume wake (aliyemkata panga mguu na kuutoa) hawezi kurudi kwao , wala mama yake hawezi kumkubalia arudi kwao ni mpaka baba yake aje atoe ruhusa ya yeye kurudi nyumbani au abaki kwa mume muuaji avumilie-MFUMO DUME UMEKAMATA MIZIZI (mbayaaaaa, sanaaaa. anajisemeaga Mch Rwakatare)




Samahani kwa picha mbaya, lakini hatuna budi kuonyesha unyama uliopita kipimo ambao wanawake wanaupitia. Na huu ni mfano halisi kwa mwanamke huyu wa Tarime Musoma. picha ya juu ni kipande cha mguu wa huyo binti ambao mume alipitisha panga mithili anakata muwa, picha inaonyesha mguu uliobaki na mguu wa kushoto pia ulikatwa lakini haukutoka, pamoja na mkono wake wa kushoto ulikatwa lakini haukutoka. ( Kumbuka tupo kwenye maandalizi mazito ya kuandimisha siku 16 za kupinga ukatili dhili ya Wanawake)



Mama mzazi wa binti aliyekatwa mguu na mkwe wake akilia kwa uchungu mkubwa alipokuwa anaelezea kisa kilichomkumba binti yake. Ni huzuni kubwa sana ukivaa viatu vya familia hii. Mama anasema kwa utamaduni wao baba wa mtoto aliyekatwa yaani mume wake ndiye mwenye dhamana ya kuamua mtoto arudi nyumbani au aendelee kubaki kwa mume fedhuli aliyemgeuza mwenzake ni pingili la muwa au kitoweo Bucher.


Juu ni mama na chini ni binti akiwa na mawazo juu ya kupoteza mguu wake kwa sababu tu mume kaamua kuukata. Huyu binti ameathirika sana kisaikolojia kutokana na tatizo hilo la kukatwa mguu wake na mume wake. hivyo anaomba asaidiwe arudi nyumbani kwa wazazi wake, au popote pa kuishi ilimradi aondolewe kwenye mazingira yale aliyopatia mkasa huo. Mbaya zaidi baba mkwe wake anamwambia "wewe unaona raha kulala kitandani wakati mtoto wangu analala chini jela) kwa kauli hiyo huyu binti yupo hatarini zaidi. wanaweza kumuua wapoteze ushaidi. hata hivyo binti aligusia sababu ya kufanyiwa unyama huo ni mwanaume kuwa na mwanamke mwingine na kwamba alishahamishia mapenzi huko, na kumuona yeye kama dudu mtu. (Wakati tunaendelea na maadhalizi ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya Wanawake, bado hali ni tete)

Hawa ndio Washika dau wetu wakubwa serikalini. wanasimamia Wizara ya Jinsia Maendeleo ya Jamii na Watoto. jamani waheshimiwa sana mko wapi? huku wanawake twafaaa, mnatusaidia vipi? viti vya bunge vinakalika vipi kwa hali hii? ni lini wanawake tutapaza sauti zetu ili dunia ijue unyama huu unaoendelea dhidi ya wanawake wa Tanzania? Wanawake Hatuna AMANI kabisa ndani ya nchi yetu. Wizara na Taasis mbalimbali, Wadau wa kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake, kuna jinsi ya kumsaidia huyu mama kwa kumuondoa pale kwenye ile nyumba alimofanyiwa UNYAMA huu na akapewa makao salama? Usikose kufuatilia Joyce Kiria Wanawakelive EATV na hapa kwenye ukurasa wetu, ili upate mkasa huu wakati tunajipanga kuendelea na mapambano ya Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake. 
-Credit Wanawake Live
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger