Featured Post Today
print this page
Latest Post

HII NDIYO SHERIA YA MAGAZETI YA MWAKA 1976 INAYOMKERA MHE ZITO KABWA NA KUDHAMILIA KUWASILISHA MUSWADA BINAFSI ILI SHERIA HIYO IVUTWE PALE BUNGENI.

MUSWADA BINAFSI KUFUTA SHERIA YA MAGAZETI YA 1976

 
NAPENDA kuujulisha umma kwamba Ijumaa tarehe 4 Oktoba, 2013 nimewasilisha kwa Katibu wa Bunge muswada binafsi Bungeni kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.

Changamoto iliyopo ni Sheria mbadala ya vyombo vya habari baada ya Sheria ya sasa kufutwa. Hata hivyo wad

au wa habari kama Baraza la Habari Tanzania wameshafanyia kazi suala hili kwa muda mrefu sana na wana mawazo kuhusu sheria mbadala. 

Nimejulishwa kuwa muswada wa sheria mpya ya habari tayari upo. Kwa hiyo katika mchakato wa kujadili muswada binafsi wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 mabadiliko yanaweza kufanywa ili kutunga sheria mpya. 

Hatua ya kwanza ni kuifuta sheria hii kandamizi ambayo kiukweli tumechukua muda mrefu sana na baada ya madhara makubwa kufikia hatua ya muswada wa kuifuta.

Nimeamua kutumia njia za kawaida za kuwasilisha muswada na kuepuka njia ya dharura ili kujenga mazingira ya wadau wa habari kushiriki vya kutosha katika mabadiliko yanayotakiwa. Njia ya dharura ni ya haraka lakini huziba fursa za kupata maoni ya wadau ambao kimsingi ndio wenye sheria yenyewe haswa. 


Hivyo nimepeleka muswada ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali (GN) kwa mujibu wa kanuni za Bunge, kisha usomwe kwa mara ya kwanza, uende kwa wadau kwa mjadala na marekebisho na kisha kusomwa kwa mara ya pili na kupitishwa na Bunge.

Ikumbukwe kuwa juhudi za kufuta sheria hii ni juhudi za wadau wa tasnia ya habari na ni juhudi walizofanya kwa muda mrefu sana. Mimi kama Mbunge ninawasilisha tu kwa sababu taratibu zetu za kuandika sheria zinataka ama Serikali, Kamati ya Bunge au Mbunge kuwasilisha muswada. 


Kwa muda mrefu tumewaangusha wana habari kwa kutosukuma vya kutosha mabadiliko waliyokuwa wanayapigania. Hata hivyo, kuna msemo wa kihindi 'asubuhi huanza pale unapoamka'. Sasa tuchukue hatua za kufuta sheria hii kandamizi.
 

Zitto Kabwe,Mb
Kigoma Kaskazini
0 comments

SHILOLE AONGEA "KUWAPANDISHA JUKWAANI WANAUME NA KUNISHIKA KINAWAFURAHISHA WENGI"

SHILOLE AONGEA "KUWAPANDISHA JUKWAANI WANAUME NA KUNISHIKA KINAWAFURAHISHA WENGI"

Baada ya watu kuongea sana kuhusu jinsi Shilole anavyo fanya show zake na staili ya kuwapandisha wanaume jukwaani na kucheza nao kwa staili ya nisheke popote ...Amejitokeza na kuongea na chombo kimoja cha habari na kusema yeye hajivunjii heshima kama watu wanavyosema bali anakizi mahitaji ya mashabiki wake..."watu wanapenda sana jinsi navyofanya ...ni njia moja wapo ya kuchangamsha show jukwaani kwahiyo sioni tatizo hapo ...wanaosema najivunjia heshima niwashamba..mimi ni msanii lazima nitafute njia ya kuwapa burudani mashabiki wangu....
0 comments

AFRIKA KUSINI YAGUSWA KUFUNGIWA KWA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

AFRIKA KUSINI YAGUSWA KUFUNGIWA KWA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

HATUA ya Serikali ya Tanzania kuyafungia magazeti mawili ya kila siku, Mtanzania (kwa siku 90) na Mwananchi (siku 14), imesababisha mjadala wa hali ya juu katika maeneo mbalimbali barani Afrika. Gazeti la Mail&Guardian la Afrika Kusini, liliandika kuwa hatua hiyo ni kusambaratisha uhuru wa vyombo vya habari na kuwanyima wananchi haki ya kupata habari. 

Gazeti hilo liliendelea kudai kuwa hatua ya kufungia vyombo vya habari ni kuvunja maana ya upashanaji habari, ambayo inatakiwa kuwafikia wananchi. 

Chombo hicho cha habari kimeifananisha adhabu hiyo ya kuyafungia magazeti hayo mawili kama ile iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda, mwanzoni mwa mwaka huu ya kulifungia gazeti jingine la NMG, la Daily Monitor, kwa madai lilichapisha habari ya uchochezi.

Tangazo la Serikali ya Tanzania kupitia Gazeti la Serikali namba 333 Septemba 27 mwaka huu lilitangaza magazeti ya Mwananchi na Mtanzania yamefungiwa.

Katika hatua nyingine, gazeti la Mail&Guardian lilimkariri Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akisema kuwa “Kufungia magazeti hakutazuia haki ya wananchi kutoa maoni yao na kupambana mpaka kupatikana utawala bora. 

“Kwanza kufungiwa kwa magazeti hayo kutawaimarisha waandishi kwa kiwango cha juu. Unalifungia gazeti kwa kutoa taarifa za mishahara? Tatizo liko wapi, je, watu hawatakiwi kujua mishahara ya watumishi wa umma?”

Ikitumia Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976, Serikali kupitia kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene, iliyafungia magazeti hayo kwa madai ya kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani. Serikali ilitangaza kulifungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90, kuaNzia Septemba 27, mwaka huu. 


Uamuzi huo ulichukuliwa na serikali kwa madai kwamba, magazeti hayo yaliandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola. Uamuzi huo, ambao ulikuwa ghafla, ulipokewa kwa mshituko mkubwa na wadau mbalimbali, huku wengi wakihoji mwelekeo wa demokrasia nchini. Wadau hao wa kada mbalimbali, wakiwamo wanasheria, wanataaluma, wanahabari, wanaharakati, wanasiasa na watetezi wa haki za binadamu, wote wamekuwa na kauli moja ya kufanana.

Source:Mtanzania
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger