Featured Post Today
print this page
Latest Post

WAFANYABIASHARA WA SOKO LA TANGAMANO WALILIA HUDUMA YA CHOO.



WAFANYABIASHARA WA SOKO LA TANGAMANO WALILIA HUDUMA YA CHOO.



Sanura Nyangasa /Veronica Julius

Wafanyabiashara wa gulioni maarufu la tangamano wameiomba halimashauri ya jiji la tanga  kuwapatia huduma ya choo kwani imekuwa ni tatizo kubwa  kwa wanaohitaji huduma ya choo katika eneo hilo.

Hayo  yamesemwa na RAJABU SAIDI ambaye nimfanyabiashara wa nguo katika soko hilo katika mahojiano na kituo hiki ambapo   amesema kuwa ukosefu wa choo katika gulio hilo imetokana na choo kilichopo kwa sasa kutumiwa na viongozi tu na kupelekea wafanyabiashara kulazimika kutoka nje ya eneo hilo kufuata huduma hiyo muhimu.

Naye HUSENI AWADHI ambaye pia ni mfanyabiashara  katika  soko hilo amesema viongozi wa jiji la Tanga hawawathamini wafanyabiashara  wadogowadogo (wamachinga) na badala yake kuwajali wafanyabiashara wakubwa.

Sambamba na hayo mama SHEILA ambaye pia ni mfanyabiashara wa soko hilo hakusita kutoa ushauri kwa kusema  wanaomba kujengewa choo katika eneo hilo kwani imekuwa usumbufu kwa upande wao kutokana kulazimika kutoka mbali na biashara zao kufata huduma hiyo muhimu.
0 comments

SEREKALI YAOMBWA KUWASAIDIA VIJANA KUPATA AJIRA



SEREKALI YAOMBWA KUWASAIDIA VIJANA KUPATA AJIRA

Na Rose Sempeho

Kutokana na Vijana wengi kukosa Ajira Serikali imeombwa kutoa fursa za Ajira kwa Vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi na kimaendeleo hali itakayopelekea vijana hao kutopotea kimaadili.

Rai hiyo imetolewa na Wafanyakazi wa Kampuni ya Amboni Plantation,Deo Peter Mungia na Gauwa Nyumbwe katika mahojiano na Redio Huruma jijini Tanga ambapo wamesema serikali itoe fursa kwa vijana ili waweze kujikwamua na Umasikini na kujitenga na makundi hatarishi kamavile Wizi Ujambazi na mengineyo ambayo hayaruhusiwai katika Jamii.

Aidha wamesema Vijana wawe mastari wa mbele katika kufanya shughuli za halali ambazo zitawasaidia wao wenyewe kupata kipato chao kwa njia ya halali kama matakwa ya Mungu yanavyosema.

Naye Bi Suzana Sinza ambaye ni mfanyakazi wa Halmashauri ya jiji la Tanga kitengo cha Afya na kinga amasema  ni wajibu wa kila kijana kujua umihimu wake katika jamii kwa kufanya shughuli za kujitolea , kujitunza na kujithamini katika kazi zao kwa kutambua wao ni nani katika jamii.

Sambamba na hayo amewataka vijana kutochagua kazi bali kufanya kazi yoyote ile halali kwani wao ni wategemewa wakubwa katika Taifa la kesho.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger