Featured Post Today
print this page
Latest Post

BREAKING NEWS !!!! MAITI YAKAMATWA NA KETE ZA MADAWA YA KULEVYA MOROGORO.


Maiti ikiwa ndani ya gari aina ya SPACIAL yenye namba ya usajili T 887 BSW eneo la nje ya chumba cha kuhifadhia maiti cha hospotali kuu ya mkoa wa Morogoro, baada ya gari hilo kukamatwa majira ya saa 7 usiku eneo la Mikumi,likiwa na watu watatu na maiti ya binadamu inayodaiwa kupoteza maisha baada ya kumeza kete hizo za zinazodaiwa kuwa ni madawa ya kulevya na kufariki dunia, ikisafirishwa kutoka Tunduma mkoani Mbeya kwenda Jijijini Dar es Salaam. PHOTO/MTANDA BLOG.

Polisi wakiendelea kupekua gari hilo.
HIZI ndizo kete zinazodaiwa kuwa ni madawa ya kulevya yaliyopatikana katika gari baada ya kupekuliwa kituo kikuu cha polisi.
0 comments

BREAKING NEWS: JAMES KISAKA AFARIKI DUNIA

 
KISAKA (KULIA) WAKATI AKIWA KAZINI SIMBA MSIMU ULIOPITA, WANAOMFUATIA NI NICO NYAGAWA, JULIO NA ABDALLAH KIBADENI
Kipa wa zamani na kocha wa zamani wa makipa wa Simba, James Kisaka amefariki dunia.

 
..WAKATI AKIWA MGONJWA NYUMBANI KWAKE MSASANI.
Kisaka amefariki dunia leo alfajiri na taarifa zinasema mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar.
Kisaka alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kupooza upande mmoja kwa zaidi ya miezi miwili.
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger