Featured Post Today
print this page
Latest Post

SHOMARI KAPOMBE ANUKIA YANGA, WAKALA WAKE AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA

KAPOMBE AKIWA AS CANNES NA GALLAS
Baada ya chenga za hapa na pale, kila kitu sasa kimewekwa hadharani kwamba beki wa zamani wa Simba, Shomari Kapombe, ametaka mkataba wake na AS Cannes ya Ufaransa uvunjwe na imeelezwa anataka kubaki nchini na kujiunga na Yanga.


Habari za uhakika kutoka ndani ya AS Cannes nchini Ufaransa na kuthibitishwa na wakala wake anayeishi nchini Uholanzi, zimeeleza Kapombe amefanya mazungumzo na Yanga ambao wamemshawishi kubaki nchini.

Mmoja wa viongozi wa AS Cannes ameliambia Championi Jumatatu kwamba: “Shomari amesusa kuja na anataka mkataba wake uvunjwe, lakini bado hatujaelewa hasa tatizo ni nini, ila tunajua amefanya mazungumzo na timu ambayo ni mabingwa wa Tanzania (Yanga), kitu ambacho si sahihi.

“Amesema anataka kubaki Tanzania, kidogo inatushangaza kwa kuwa kesi yake moja kuhusiana na kutaka kulipwa fedha imefika Fifa, lakini ajabu kabisa hatukuwahi kukataa kumlipa, badala yake tulisimamisha malipo kutokana na kuchelewa kwake. Huo ndiyo ukweli, ila sipendi jina langu liandikwe gazetini.”

Blogu hii ilikuwa ya kwanza kuandika kuwa Kapombe amekwama nchini na yuko mkoani Morogoro licha ya kuripotiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwamba alishaondoka kwenda Ufaransa.

Juhudi za kumpata wakala wake, Dennis Kadito akiwa nchini Uholanzi anakoishi zilizaa matunda jana na akasema ana taarifa za Yanga pamoja na Azam FC kufanya naye mazungumzo.

“Kweli kuna hizo taarifa, si nzuri kwa kuwa ni kukiuka utaratibu. Tayari Kapombe amesema anataka mkataba uvunjwe, kama umesikia hivyo ni sahihi. Nawashauri Yanga au Azam kama wanamtaka waje nizungumze nao tukae na AS Cannes, basi tumalizane.

“Mkataba wake ni wa miaka miwili, hivyo wasitumie njia ya mkato kwa kuwa mambo yako wazi na mimi au AS Cannes hakuna mwenye shida,” alisema.

Kapombe alitokea Simba na kujiunga AS Cannes bure, Simba ikitegemea kupata fedha kama atauzwa katika timu nyingine za Ulaya, lakini mgogoro ulianza baada ya kutolipwa mshahara wake kutokana na kutokuwa na akaunti ya benki za kule Ufaransa lakini baadaye alilipwa baada ya kumaliza utata huo.
“Kweli kuna fedha anadai, utaona katika miezi minne aliyokuwa Ufaransa hajalipwa mwezi mmoja. Hii inatokana na ile ishu ya kuchelewa alipokuwa katika timu ya taifa. Halafu, awali alichelewa kulipwa kutokana na suala kutokuwa na kibali cha kazi kilichochelewesha ashindwe kufungua akaunti ya benki.

“Ila AS Cannes ambao walikasirishwa na Kapombe kuchelewa Tanzania walitaka TFF ndiyo wamlipe mshahara kwa kuwa ndiyo walimchelewesha, sasa kesi yake iko Fifa. Ninaamini atashinda na mimi niko upande wake maana ndiyo wakala wake.

“Lakini bado nasisitiza kuwa lazima Yanga wafuate utaratibu maana taarifa za kuzungumza naye ninazo na ni za uhakika,” alisema wakala wake huyo.

Kiongozi wa AS Cannes alisema wametumia mamilioni ya fedha kumtibu Kapombe, lakini wanashangazwa na mambo yanavyokwenda.

“Suala lake tutalishughulikia baadaye, tulikuwa na mechi muhimu na ngumu za FA. Tumeitoa St Etienne inayoshiriki ligi kuu, sasa tutarudi kushughulikia suala lake ingawa tunaweza kulifanyia kazi zaidi baada ya Fifa kutoa hukumu.”

Yanga wamekuwa wakikataa katakata kulizungumia suala la Kapombe kwa hofu ya kuingia kwenye adhabu ya kuzungumza na mchezaji mwenye mkataba.

“Najua sasa Yanga hawawezi kukubali, ila wanawasiliana naye na walishakaa wakamalizana kwa mazungumzo ya awali na sasa kuna mambo kadhaa wanamsaidia,” alisema rafiki yake aliyetoa siri kwa mara ya kwanza kuwa yuko Morogoro.

Taarifa zinaeleza Yanga wamelenga kumjumlisha kwenye dirisha la Caf kama watasonga mbele au mwanzoni mwa msimu mpya, mara tu baada ya dirisha kufunguliwa.

Kabla ya kuondoka nchini na kujiunga na AS Cannes inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Ufaransa, Kapombe alikuwa nahodha msaidizi wa Simba.
0 comments

MAMIA YA WAMZIKA DEUSDEDIT MTAMBALIKE

MAMIA YA WAMZIKA DEUSDEDIT MTAMBALIKE

 
Jaji Mstaafu Mark Bomani,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye  na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Mh.Stephen Wassira ni miongoni mwa viongozi mbali mbali walioshiriki mazishi ya kada maarufu ambaye pia alishawahi kuwa Mkuu wa Wilaya katika Wilaya mbalimbali nchini.
Mama Anna Mkapa,Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka na Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini Elizabeth Minde wakiwa miongoni mwa mamia ya Watanzania waliojitokeza kumzika kada wa siku nyingi Deusdedit Mtambalike.
Waombolezaji wakiwa kwenye nyuso za huzuni wakati wa mazishi ya mpendwa wao Deusdedit Mtambalike.
Sala ya kumuombea Marehemu Deusdedit Mtambalike aliyefariki tarehe 15 Januari 2014 nchini Afrika ya Kusini ilisomwa nyumbani kwake kabla ya Mazishi.

Wanandugu wa Marehemu Deusdedit Mtambalike wakiwa wamebeba mashada ya maua .
Mwanasiasa wa siku nyingi na ambaye alishawahi kushika nyazfa mbalimbali za serikali Balozi Paul Rupia akitoa salaam za pole kwa familia ya marehemu Deusdedit Mtambalike na kumuelezea marehemu kama mtu aliyemwema na asiyechoka kushauri kwenye jambo lolote alotakiwa kushauri.
Jaji Mstaafu Mark Bomani akimuelezea marehemu Deusdedit kama mtu ambaye hakusita wala kuwa na woga katika kuzungumzia jambo lenye manufaa kwa jamii.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa salaam za rambirambi kwa niaba ya CCM Makao Makuu wakati wa mazishi wa aliyekuwa Kada wa Chama Cha Mapinduzi Marehemu Deusdedit Mtambalike.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Mahusiano na Uratibu) Mheshimiwa Stephen Wassira akitoa salaam za pole kwa niaba ya Serikali kwenye mazishi ya Ndugu Deusdedit Mtambalike yaliofanyika nyumbani kwa marehemu Kimara Bonyokwa.
Watoto wa Marehemu Deusdedit Mtambalike wakiwa wenye nyuso za simanzi na huzuni pamoja na Mama yao na Ndugu wa karibu wakati wa sala ya mwisho kabla ya mazishi ya Baba yao mpendwa.
Sehemu ya watu waliojitokeza kwenye mazishi ya Deusdedit  Mtambalike
Profesa Mahalu akiweka mchanga kama ishara ya kumzika rafiki yake Marehemu Deusdedit Mtambalike
Mke wa Marehemu Deusdedit Mtambalike akiweka shada la maua juu ya kaburi .
Watoto wa marehemu wakiweka shada la Maua kwenye kaburi la baba ya mpendwa Marehemu Deusdedit Mtambalike aliyefariki dunia tarehe 15 Januari 2014 nchini Afrika ya Kusini.
0 comments

Ajali ya Lori na NOAH yaua 13 Singida

Ajali ya Lori na NOAH yaua 13 Singida

 



  Imetokea ajali mbaya huko Singida ambapo gari aina ya NOAH na Lori la mizigo yamegongana uso kwa uso na kisha gari hiyo aina ya NOAH kuingia chini ya uvungu wa Lori na kusababisha vifo vya watu hao 13 ambao wote walifia katika eneo la ajali.

Taarifa inasema gari aina ya NOAH ilikuwa imebeba abiria kutoka Itigi wakielekea Singida Mjini.

Dereva na utingo wa Lori walikimbia baada ya ajali hiyo kutokea.

 CHANZO: ITV breaking News.


0 comments

BREAKING NEWS, AJALI MBAYA YATOKEA MBALIZI MAGARI ZAIDI YA MATANO YAGONGWA.

BREAKING NEWS, AJALI MBAYA YATOKEA MBALIZI MAGARI ZAIDI YA MATANO YAGONGWA.



 Magari yakiwa yamegongwa Mbalizi Mbeya

Watu mbalimbali wakiwa wanashangaa ajali hiyo iliyosababisha Gari moja kugonga magari mengine zaidi ya matano
Mashuhuda wakiwa wanashuhudia ajali hiyo


Watu wakiwa wanaongezeka kushuhudia ajali hiyo





PICHA NA MBEYA YETU BLOG
0 comments

UVCCM TANGA YAWATANGAZIA KIAMA MADIWANI,WENYEVITI MIZIGO.

UVCCM TANGA YAWATANGAZIA KIAMA MADIWANI,WENYEVITI MIZIGO.

Na Oscar Assenga, Kilindi.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga(UVCCM)Abdi Makange amewataka madiwani na wenyeviti wa serikali za vijiji na vitongoji wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo kwa wananchi kuacha kuchukua fomu za kugombea nafasi hizo katika uchaguzi mkuu ujao 2015.

Makange alitoa kauli hiyo hivi karibuni katika mkutano wa hadhara uliofanyika
katika kijiji cha cha Makasia Kata ya Kwediboma wilayani hapa ambapo alisema viongozi wengi baada ya kupata nafasi za uongozi wamejisahau na kushindwa kutatua kero zinazo wakabili wananchi wao waliowachangua kitendo ambacho kinapelekea wananchi kuichukia serikali.


Alisema katika maeneo mbalimbali mkoani hapa viongozi hao wamekuwa
wakichangia kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi wao ikiwemo kusababisha migogoro baina ya wakulima na wafungaji kwa kugawa maeneo kwa wageni na kuwaacha wazawa wakiwa hawana ardhi kutokana na maslahi binafasi.     “Wenyeviti ambao wanachangia migogoro kwenye maeneo yao kiama chenu kinakuja nawaambiane  hatutafumbiwa macho ni lazima waondoke wapishe wengine wenye uwezo wa kuwafanya wananchi kuishi kwa amani na kutatua kero zao “Alisema Makange.

Mwenyekiti huyo alienda mbali sana kwa kusema kuwa viongozi wa aina
  hiyo hawafai kuwaongoza wananchi hivyo kuwataka wakamatwe na kuwekwa ndani kisha wafukuzwe katika maeneo yao.

Akizungumzia suala la mikopo asilimia 10 ya vijana na wakina mama
  inayotoka serikali kuu kwa ajili ya maendeleo yao inayokana na makusanyo ya Halmashauri alisema suala hilo sio ombi bali ni lazima hivyo maafisa wanahusika wahakikishe wanalipa msukumu mkubwa ili ipatikane kwa wakati.

Aliwataka vijana na wakina mama kuunda vikundi katika maeneo yao na
  kufuata taratibu zote zinazopaswa ili waweze kupata mikopo hiyo ambayo itaweza kuwakwamua kimaendeleo na kuchangia ongozeko la pato lao.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger