Featured Post Today
print this page
Latest Post

STENDI YA MABASI MKOANI DODOMA

STENDI YA MABASI MKOANI DODOMA.



0 comments

PILIKAPILIKA ZA KIBIASHARA NDANI YA STENDI YA MABASI DODOMA.

PILIKAPILIKA ZA KIBIASHARA NDANI YA STENDI YA MABASI DODOMA.


                    DODOMA INAVYOONEKANA ASUBUHI YA LEO.






0 comments

Magazeti ya leo Jumapili December 01 2013

Magazeti ya leo Jumapili December 01 2013

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments

CHADEMA YATOA UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA

CHADEMA YATOA UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA

c1_24e5d.jpg
UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA
Kutokana na kuwepo kwa taarifa ya Ndugu Ali Omari. Chitanda, huku pia waandishi wa habari wakitaka kujua na kupata ukweli kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, tunapenda kutoa ufafanuzi mfupi;
Kwanza suala la maamuzi ya Kamati Kuu ya kuwavua uongozi ndani ya chama, Ndugu Zitto Kabwe na Dkt. Kitila Mkumbo, chama kimeshafunga mjadala kwenye vyombo vya habari kwa kuheshimu na kuzingatia taratibu za kikatiba za ndani ya chama kuendelea.
Pili kuhusu suala la restructuring ya Makao Makuu ya Chama. Chitanda ametoa taarifa akiwataja wakurugenzi wafuatao, kuwa ni wapya;
1.Mkurugenzi wa Oganaizesheni Mhe. Singo Kigaila Benson.
2. Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano ya ndani Mhe. John Mnyika
3. Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji Mhe. Anthony Komu.
4. Mkurugenzi wa Bunge na Halmashuri Mhe. John Mrema.
5. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama Mhe. Wilfred Lwakatale.

Wakurugenzi wote aliowataja si wapya. Mkurugenzi pekee ambaye uteuzi wake ni mpya na umefanyika hivi karibuni na kuthibitishwa ni Mwanasheria Peter Kibatala, atakayesimamia Kurugenzi ya Sheria na Haki za Binadamu.
Kama ni suala la kuangalia mtu anatokea wapi (ambalo halijawahi wala haliwezi kuwa moja ya vigezo), ili kuonesha ukweli na kubainisha uongo wa watu wanaojaribu kufanya kazi ya CCM wakisema wao ni wanaCHADEMA, kwa kutumia propaganda zile zile na kuzifanya kuwa ni kete zao za kisiasa ndani ya chama, tunaweza kutaja maeneo ya wanakotoka au asili yao kama ifuatavyo;(P.T)
Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji, Antony Komu- Kilimanjaro.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama, Wilfred Lwakatare- Kagera.
Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni, Benson Kigaila- Dodoma.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John John Mnyika- Mwanza
Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri, John Mrema- Kilimanjar.o
Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu, Peter Kibatala- Morogoro.
Hadi sasa uteuzi wa kurugenzi za Makao Makuu ya CHADEMA haujakamilika. Bado kuna nafasi zinazotakiwa kujazwa kwa kufuata taratibu za chama.
Hii ni kwa sababu maboresho yanayofanyika ndani ya chama, hadi sasa yanaendelea katika ngazi ya Makao Makuu na kanda, kisha itaendelea kwa ngazi za mikoa, wilaya, majimbo, kata, kijiji na hatimaye kitongoji.
Katika maboresho hayo, kwa nafasi za uteuzi, yanayoendelea sasa ambayo yanakwenda hatua kwa hatua, hadi kuwa na makatibu wa kuajiriwa ngazi ya chini ya chama, chama kinazingatia uwezo, uadilifu na utayari wa mtu katika kutoa utumishi bora kwa wanaCHADEMA na Watanzania wote katika nafasi husika.
Suala la maslahi ya watumishi wa CHADEMA ni utaratibu wa chama ambao unajadiliwa, kufikiwa uamuzi na kisha kuridhiwa kwenye vikao vya chama, kama ilivyofanyika kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichoketi karibuni.
Katika suala hili la maslahi ya watumishi wanaojitolea Makao Makuu ya CHADEMA ambayo si siri, Ndugu Chitanda amesema uongo mkubwa. Kusema kwamba Ofisa Mwandamizi anaweza kulipwa posho kubwa kuliko Mkurugenzi wa kurugenzi husika, ni uongo unaovuka mipaka.
Ndugu huyo anadhihirisha uongo huo yeye mwenyewe kwa kuandika hivi; "800,000/= za awali na sasa itakuwa ni kuanzia Tshs. 1,500,000-2,500,000/= kwa Mkurugenzi na kutoka Tshs.6,800,000/= kwa Afisa Mwandamizi na sasa ni Tshs.1,000,000-1,500,000/=".
Pia si kweli kuwa kila mtumishi anayejitolea Makao Makuu analipwa. Mathalani, wakurugenzi wenye nafasi za ubunge, hawalipwi hata shilingi moja kwa kazi zote wanazokitumikia chama na Watanzania kwa ujumla.
Kwa maelezo hayo ya kutengeneza, ni kwamba hadi sasa Ofisa Mwandamizi anapokea posho kubwa kuliko Mkurugenzi na hata baada ya maboresho atapata posho kulingana na Mkurugenzi. Anapaswa kuwa mkweli. Mtu anayetaka kuonekana muungwana, anapaswa kujiweka mbali na uongo pamoja, maneno ya kutunga pamoja na upotoshaji wa makusudi.
Kama ilivyoelezwa hapo juu, restructuring inaendelea. Ni hatua kwa hatua. Itafika ngazi za chini kama Baraza Kuu lilivyoagiza. Kwa sababu hiyo hadi sasa uteuzi wa Makatibu wa Mikoa na Wilaya haujafanyika.
Hata hivyo ruzuku imekuwa ikipelekwa kila kanda, mkoa, wilaya na jimbo kama ilivyoridhiwa na Kamati Kuu. Na hii ni zaidi ya pikipiki, kompyuta na magari yaliyopelekwa kila kanda. Angelikuwa mkweli, nagelisema na hili pia.
Ndugu Chitanda anajichanganya sana katika taarifa yake yote. Hii ni moja ya sifa ya kukosa hoja hivyo mtu anaamua kuibua viroja au kutunga maneno kwa sababu ya kujaribu kuukana ukweli anaoujua moyoni. Tutatoa mfano mmoja;
Kupitia taarifa yake, anasema alikuwa mtu aliyeaminiwa hadi kuwa katika vikao muhimu, lakini wakati huo huo anasema kuna ubaguzi! Tunapaswa kumhurumia kwa kushindwa kuunganisha hata mawazo yake na kupata mtiririko wa hoja zenye mantiki! Angelikuwa mkweli angesema katika vikao vya sekretarieti na CC, aliingiaje kama kuna ubaguzi wa dini!
Kwa sababu anazozijua yeye, Ndugu Chitanda ameamua kujipachika cheo ambacho hajawahi kuwa nacho. Amejiita kuwa ni Katibu wa Sekretarieti ya Makao Makuu.
Ndani ya CHADEMA pamoja na kwamba nafasi hiyo imetajwa ndani ya Katiba ya Chama, hakuna mtu ambaye ameteuliwa kutumikia nafasi hiyo. Kama anaweza athibitishe kwa kutoa barua ya uteuzi kutoka kwa Katibu Mkuu.
Mahali pengine amejitambulisha kuwa ni Katibu Ofisi ya Katibu Mkuu. Ofisi hiyo ina Katibu Mtendaji mmoja ambaye ni Mzee Victor Kimesera, mmoja wa waasisi wa CHADEMA.
Operesheni ya Chama inayoendelea nchi nzima kwenye majimbo 103, si suala la siri wala lengo bovu kama anavyotaka umma uamini.
Ni mwendelezo wa mpango mkakati wa chama kupitia progamu za Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), unaotekelezwa kwa hatua mbalimbali na kwa mbinu tofauti tofauti pamoja na dhana ya CHADEMA ni msingi.
Operesheni hiyo ambayo ni mwendelezo wa nyingi za namna hiyo zinazokwenda ngazi za chini kabisa za chama, zikilenga kuimarisha taasisi na mifumo, imeanza wiki hii na ilitangazwa mbele ya waandishi wa habari.
Tungependa kumalizia ufafanuzi huu mfupi kwa kutoa tahadhari kwa umma kuwa makini na matamko ya watu wa namna hii. Maana tunajua kwa uhakika yako mengi ya namna hii yataandaliwa na kutolewa kadri ambavyo Watanzania wanakaribia kuona na kuishi matumaini ya mabadiliko ya kiutawala na mfumo ndani ya nchi yao.
Mathalani katika taarifa yake, Ndugu Ali Chitanda amedhihirisha na kuonesha kuwa ni aina ya watu ambao wanaCHADEMA na Watanzania kwa ujumla wanapaswa kuwaangalia kwa macho ya kuhoji na tahadhari ya hali ya juu, anasema hivi;
"Kwa kuwa siamini kwamba kuvuliwa nyadhifa kwa Zitto Kabwe na Dkt Kitila Mkumbo ni kwa sababu ya waraka wa ushindi, bali ninaamini kuvuliwa kwao ni kutokana na hofu ya uchaguzi, ubaguzi wa kikabila na kikanda."
Aya hiyo pekee inayotumia lugha wanayotumia mahasimu wa CHADEMA, wakiongozwa na viongozi waaandamizi wa CCM, wanaohangaika kutokana na Watanzania kuwakataa, wakijiandaa kuwaondoa madarakani kwa sababu sera zao zimeshindwa, inatosha kuonesha uhalisia wa yeye mwenyewe (mtoa taarifa) alivyo.
Ni kauli za namna hii (kuwatisha na kutaka kuwatenganisha Watanzania) ambazo zimekuwa zikitumiwa na watawala kama njia pekee ya kutaka kuzuia upepo wa mabadiliko unaovuma nchi nzima, zimekuwa zikiwaunganisha zaidi Watanzania kuiunga mkono CHADEMA bega kwa bega, ili kupata haki na matumaini ya wanyonge, katika mapambano ya awamu ya pili, kuelekea uhuru wa kweli.
Imetolewa leo Novemba 30, 2013, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari- CHADEMA
0 comments

ARSENAL HAIKAMATIKI, YAWAFUMUA CARDIFF 3-0 BARAZANI KWAO...LUKAKU NI HATARI

ARSENAL HAIKAMATIKI, YAWAFUMUA CARDIFF 3-0 BARAZANI KWAO...LUKAKU NI HATARI

ramsey_4f6c3.jpg
Ramsey hakutaka kushangilia baada ya kuifunga timu yake ya zamani

ARSENAL imezidi kijichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya England, baada ya kuilaza mabao 3-0 Cardiff City, kwenye Uwanja wa Cardiff jioni hii.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Aaron Ramsey dakika ya 29 akimalizia pasi ya Mesut Ozil na 90 pasi ya Theo Walcott na Mathieu Flamini dakika ya 86 pasi ya Ozil tena.
Ushindi huo, unaifanya Arsenal itemize pointi 31 baada ya kucheza mechi 13, ikiizidi Liverpool iliyo katika nafasi ya pili kwa pointi saba.

lukaku_53cf1.jpg
Lukaku akishangilia bao lake leo

Katika mechi nyingine za Ligi Kuu England leo,
Everton imeichapa 4-0 Stoke City Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, mabao ya Gerard Deulofeu dakika ya 45, pasi ya Gareth Barry, Seamus Coleman dakika ya 49 pasi ya Barry tena, Bryan Oviedo dakika ya 58, pasi ya Gerard Deulofeu na Romelu Lukaku dakika ya 79 pasi ya Oviedo.
Bao pekee la Gary Hooper dakika ya 30 limeipa Norwich ushindi wa 1-0 dhidi ya Crystal Palace Uwanja wa Carrow Road, Norwich, Norfolk.

West HamUnited imeifunga 3-0 Fulham Uwanja wa Boleyn Ground, London mabao ya Mohamed Diame dakika ya 47, Carlton Michael Cole Okirie dakika ya 82 na Joe Cole dakika ya 88.
Aston Villa imetoka sare ya bila kufungana na Sunderland Uwanja wa Villa Park na mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu England, Newcastle United imeifunga West Bromwich 2-1.

0 comments

KOCHA WA CAMEROON ASAINI MIAKA MWILI AZAM

KOCHA MCAMEROON ASAINI MIAKA MWILI AZAM

Kocha mpya wa Azam FC. Joseph Marius Omog (katikati) akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kusaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.


KLABU ya Azam inapenda kuufahamisha umma hususan wapenzi wa mpira wa miguu kuwa imeingia mkataba na kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon kwa kipindi cha miaka miwili (2) kuanzia leo.

Kocha Omog ni bingwa kwani anakuja kuifundisha Azam akiwa ametoka kuiongoza klabu ya A.C Leopards ya Jamhuri ya Kongo (Brazaville) kutwaa ubingwa wa ligi ya nchi hiyo kwa misimu miwili mfululizo (2012 na 2013).

Timu hii ilikuwa haijatwaa ubingwa wa ligi kwa zaidi ya miaka 30. Kwa mwaka huu wametwaa ubingwa wakiwaacha wapinzani wao, Diables Noirs kwa pengo la pointi kumi (10) wakikusanya pointi 87 katika ligi yenye timu 18.

Pia ni mwaka jana tu (2012) aliiwezesha A.C Leopards kunyakua ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika kwa kuzipiga kumbo timu ngumu na zenye uzoefu mkubwa kama vile Mas de Fes ya Morocco, Heartlands ya Nigeria na Sfaxien ya Tunisia.

Mafanikio hayo ya kutwaa ubingwa wa Afrika yalifikiwa baada ya miaka 38 tangu klabu ya Jamhuri yas Kongo ifanye hivyo, na kumfanya kocha Omog kuwa moja ya makocha wa kupigiwa mfano barani Afrika.
0 comments

LAAC WAIAGIZA HALMASHAURI HANDENI KUPELEKA ZAIDI YA MILI 105 KWA VIJIJI RUZUKU YA SERIKALI.

LAAC WAIAGIZA HALMASHAURI HANDENI KUPELEKA ZAIDI YA MILI 105 KWA VIJIJI RUZUKU YA SERIKALI.

MWENYEKITI wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajabu Mbaruku imeiagiza Halmashauri ya wilaya ya Handeni kuhakikisha kwamba inapeleka kiasi cha sh.milioni 105,779,260 kwa vijiji vilivyostahili kuzipata ikiwa ni michango ya lazima ya asilimia 20 ya ruzuku ya serikakali kuu kwa ajili ya maendelo vijijini,

Kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo ilitokana na halmashauri hiyo kushindwa kuzipeleka vijijini fedha za ruzuku ya serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo hali ambayo inapelekea kuchangia kudhorotesha kasi yao katika shughuli mbalimbali.
Licha ya kutoa agizo hilo pia aliiagiza halmashauri hiyo kuandaa mchanganuo wa madeni inayodai na kudaiwa kwa kuonyesha majina ya wadai na wadaiwa ikiwemo kuchukua hatua za makusudi za kupatikana kwa fedha zinazodaiwa.

Mwenyekiti huyo alisema katika mchanganuo huo wadai wa halmashauri unaonyesha ni kiasi cha sh.milioni 736,302,302 ambapo katika hilo mchanganuo wa wadaiwa hao haukuonyesha kitendo ambacho kinaleta mashaka hasa katika utendaji wake.
Aidha pia kamati hiyo iliagiza mchanganuo wa matumizi ya mabati 466 yaliyotumika kujengea vyumba 8 vya madarasa katika shule ya sekondari Segera uandaliwe na kupelekwa kwa mkaguzi mkazi kwa ajili ya uhakiki zaidi.
Aliitaka halmashauri hiyo kuzingatia vipimo na vigezo vya ubora katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ambapo agizo hilo lilitokana na kubainika kwa kiwango duni kwa madarasa manne yaliyojengwa kwa sh.milioni 14 katika shule ya sekondari Komnyang’anyo.
Hata hiyo waliitaka halmashauri hiyo kuongeza bidii katika kudai kiasi cha sh.,milioni 133,391,724 ambazo inadai kutoka kwa wadaiwa ambao ni pamoja na MSD sh.milioni 39,310,646,State Business sh.milioni 14,690,000,HADECO sh.milioni 10,200,000, Hazina (15% LAPF) sh.milioni 44,059,300, Hazina(Salaries)sh.milioni 19.806,278 na mfuko wa wanawake ni sh.milioni 5,025,500.
0 comments

Kigoda: Kamanda wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM)

Kigoda: Kamanda wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM)

WAZIRI wa Biashara na Viwanda nchini, Dr.Abdalla Kigoda ameteuliwa kuwa kamanda wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM) katika uteuzi ambao ulifanywa na kamati ya utekelezaji Taifa chini ya Mwenyekiti wao Sadifa Juma.

Akizungumza na Tanga Raha, katika ofisi za Umoja huo mkoani hapa, Mwenyekiti wa Umoja huo, Abdi Makange alisema mchakato huo ulianzia ngazi ya mkoa ambapo wao waliamua kumpendekeza Kigoda na hatimaye kupata baraka kutoka kamati ya utekelezaji na kumuidhinisha kwa kumpitisha.

Makange alisema hatua yao ya kumpendekeza ilitokana na mchango wake mkubwa aliokuwa ukitolewa na kiongozi huo kwa vijana wa mkoa wa Tanga kitendo ambacho kimewapa wigo katika ufanisi wao.

   “Naishukuru sana kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa kuridhia mapendekezo hayo na sasa tunakwenda kufungua ukurasa mpya wa mafaniko ndani yetu “Alisema Makange.

Alisema umoja huo unatarajiwa kuandaa taratibu za kumsimika rasmi kiongozi huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Handeni mkoani Tanga lengo likiwa ni kuhakikisha wanatimiza malengo yao waliojiwekea.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger