Featured Post Today
print this page
Latest Post

Waafrika milioni 200 wanalala na njaa kila siku


Waafrika milioni 200 wanalala na njaa kila siku 

njaa_a179d.jpg

Wataalamu wa kiafrika, wakulima na wadau wamekamilisha siku mbili za majadiliano kuhusu njia za kulisha idadi ya watu wanaoongezeka katika bara hilo na kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Kwa mujibu wa program ya mazingira ya Umoja wa Mataifa-UNEP, waafrika milioni 200 wanalala njaa. Hiyo ni asilimia 23 ya watu. Takwimu za mwaka huu kuhusu usalama wa chakula zinaonesha nchi nane kati ya 10 zenye usalama mbaya sana wa chakula zipo barani Afrika.



Mratibu wa Umoja wa Mataifa katika mabadiliko ya hali ya hewa kwa Afrika, Richard Munang anasema kuna haja ya kuongeza uzalishaji chakula ili kulisha watu bila kuwepo shinikizo juu ya mfumo wa ekolojia katika bara hilo.

Mpatanishi wa kundi moja la Afrika katika mkutano, Emanuel Dlamini, anaeleza kuwa mabadiliko ya hali ya hewa yataendelea kuwepo, lakini serikali za kiafrika na wakulima wanatakiwa kuangalia njia za kukubali hilo.
Nchi nyingi za barani Afrika zinategemea mvua ili kuandaa mashamba yao na kuanza kupanda mazao. Kwa miaka kadhaa iliyopita nchi kadhaa zimekumbwa na ukame na kufanya watu wake kutegemea msaada wa chakula.

Wakulima wa kiafrika wanalalamika kwamba mvua za siku hizi hazitabiriki na ongezeko la joto kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa yanasababisha mazingira ya kuwepo magonjwa ya mazao ambayo yanaathiri uzalishaji.

Mwakilishi wa Nestle Africa, Hans Johr anasema wakulima wanahitaji msaada kutoka makampuni yanayotengeneza vyakula na taasisi zisizo za kiserikali ili kukabiliana na changamoto.

Waandaaji na washiriki wa mkutano huo wanatoa wito wa juhudi za pamoja kutoka jumuiya ya kimataifa, serikali na wakulima kufanya kazi pamoja kuongeza uzalishaji wa chakula na pia kuingilia usalama wa chakula na kilimo endelevu katika sera za bara na za kimataifa.

 

0 comments

Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi....!

Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi....! 

halima_cc4f5.jpg

 Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akitoa hoja yake wakati kamati hiyo ilipokutana na Shirika la Nyumba nchini (NHC) jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mbunge wa viti Maalum (CHADEMA) Suzan Kiwanga. Picha na Rafael Lubava.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge.

Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012.

Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni.

"Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. Tunajua kwamba fedha hizi zilipunguzwa kiasi cha Sh95 bilioni na kupelekwa Wizara ya Uchukuzi, zilibakia Sh252.975bilioni katika kifungu hicho lakini kuna bilioni 100 zimetumika visivyo," alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema).

Alisema katika majumuisho ya Bajeti ya wizara hiyo, Dk Magufuli na Dk Mwakyembe wakati huo akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Lukuvi walitoa maelezo yasiyo ya kweli bungeni kuhusu fedha.
Alikariri maneno yaliyorekodiwa kwenye Hansard ya Bunge yaliyosemwa na viongozi hao watatu.
"Tunaomba fedha Sh252 bilioni kwa ajili ya kuanzia kazi za ujenzi wa barabara," Zitto alisema akikariri maneno ya Dk Magufuli wakati anawasilisha bajeti.

"Fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili," haya yalikuwa maneno ya Dk Mwakyembe wakati akifanya majumuisho.

"Hizi ni fedha kwa ajili ya counterpart fund," alimkariri Lukuvi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.
Zitto alisema CAG alihoji mwaka huu kuhusu matumizi ya fedha hizo na alitoa taarifa akidai kuwa fedha hizo zilikuwa miradi hewa na kasma kivuli.

Zitto alisema kuwa Dk Magufuli na Katibu Mkuu wake walipohojiwa walidai kutumia fedha hizo kulipa madeni.

"Kwa nini mlidanganya Bunge? Mliomba fedha za kuanza miradi maalumu. Hamkuomba fedha za madeni. Kwa nini mliunda kasma kivuli na kuifuta baada ya pesa kulipwa?" Zitto alimhoji Balozi Mrango.
Katika majibu yake, Balozi Mrango alisema kwa nia njema, fedha hizo zilitumika kuwalipa makandarasi waliokuwa wamechachamaa, huku baadhi yao wakisisitiza kusitisha kuendelea na miradi. Hivyo wakalazimika kuomba fedha kwa njia hiyo ili miradi kuendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Zitto hakuridhishwa na majibu hayo akisema hapakuwa na haja ya kutumia fedha hizo kuwalipa makandarasi wakati kulikuwa na kasma yao ya awali. Alisema kama kulikuwa na haja hiyo, wizara isingeita mradi rasmi.
"Jambo hili siyo sahihi hata kidogo kulidanganya Bunge na hadi sasa wewe na waziri wako hamuonyeshi kukubali kosa hili, hata Waziri Lukuvi naye alisisitiza bungeni kwamba fedha hizo zinaombwa ili kutekeleza mradi maalumu lakini sasa imebainika sivyo, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge tutawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ili wahojiwe nao wajieleze kwa kulidanganya," alisema Zitto.

Pia kamati hiyo imeitaka wizara hiyo kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu matumizi ya Sh100 bilioni zilizotumika kinyume na maombi yaliyowasilishwa kwenye Bajeti ya mwaka huo wa fedha.
CAG ameshauri madeni yote ambayo Wizara ya Ujenzi inadaiwa yaorodheshwe ili yawe wazi kuepuka migongano katika matumizi ya fedha.

Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Lukuvi alisema haelewi chochote na kusisitiza kuwa akipata taarifa rasmi za Kamati ya PAC, atatoa ufafanuzi.
Halmashauri zinavyotafuna mabilioni
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAACc), imeeleza namna mamilioni ya fedha za Serikali zinavyoibwa kutoka Hazina kupitia halmashauri za wilaya huku Ilala ikitajwa kuongoza kwa ufisadi huo.

Mwenyekiti wa LAAC, Rajab Mbarouk Mohammed aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba Hazina imekuwa ikipeleka fedha kwenye halmashauri zikiwa zimezidi na kwamba kiasi kinachozidi hakirudishwi badala yake huliwa.

Alisema kamati hiyo imefanya uchunguzi kwenye halmashauri 43 na kubaini kwamba mtindo huo ndiyo unaotumika kuiba fedha za Serikali.

"Mwaka 2011/12 kiasi cha Sh1.5 bilioni zilipelekwa zikiwa zimezidi kwenye halmashauri hizo lakini hazikurudishwa Hazina kama inavyoonyesha kwenye ripoti ya CAG.
Alisema kati ya kiasi hicho, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ilipewa ziada ya Sh213 milioni ikifuatiwa na Geita iliyopewa Sh129 milioni.

"Fedha hizo za mishahara zilipelekwa kwenye halmashauri hizo na Hazina kimakosa zikiwa zimezidi lakini watendaji wa hawakuzirudisha kama wanavyotakiwa kisheria badala yake zikayeyuka," alisema.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa uchunguzi huo pia ulibaini kwamba katika halmashauri hizo 43 kiasi cha Sh693 milioni hulipwa mishahara hewa ambayo wafanyakazi wake walishakufa na wengine kustaafu.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ililipa mishahara hewa yenye thamani ya Sh79.4 milioni ikifuatiwa na Ukerewe iliyolipa Sh57.5 milioni.

Kwa upande wa fedha za miradi ya maendeleo, mwaka 2011/12, Hazina ilipeleka katika Halmashauri ya Mbarali, Mbeya Sh724 milioni kwa ajili ya Mradi wa Maendeleo ya Elimu Sekondari wakati mradi huo ulikuwa ukihitaji Sh70 milioni tu.

"Kiasi cha Sh654 milioni zilipelekwa kimakosa na Hazina lakini badala ya kurudishwa zilitumiwa katika mazingira ya kutatanisha," alisema.

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ilipelekewa ziada ya Sh500 milioni na Mvomero ilipewa Sh85 milioni. "Kuna mtandao mkubwa wa Hazina na halmashauri ambao ukiachwa utaendelea kupoteza fedha nyingi za walipakodi," alisema.
Chanzo:mwananchi.
0 comments

Tamasha la Fiesta kuendelea Agosti 23 Ijumaa hii mkoani Tabora

Tamasha la Fiesta kuendelea Agosti 23 Ijumaa hii mkoani Tabora


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam.
 
TAMASHA la muziki nchini linalojulikana kama Fiesta 2013, linatatarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu mkoani Tabora kwa ajili ya kuwapatia burudani za aina yake.
Linah, mkali wa Bongo Fleva
Khufanyika kwa tamasha hilo ni wiki moja tangu ilipozinduliwa rasmi Jumamosi iliyopita ya Agosti 17 mwaka huu katika Uwanja wa Tanganyika, mkoani Kigoma.
AMkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, pichani.
kizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Kampuni ya Clouds Media Group ambao ndio wandaaji wa Tamasha hilo, Ruge Mutahaba, alisema kuwa wakazi na wananchi wa Tabora wana kila sababu ya kulisubiri tamasha hilo kwa shangwe.


Ahmad Ally 'Madee'
Alisema kuwa hakuna tamasha kubwa linalochanganya wasanii wengi kwa pamoja, hivyo wadau wao wajiandae kupata burudani kabambe kutoka kwao.
“Sisi kama waandaaji tumejipanga imara kuhakikisha kuwa wasanii wote wanafanya mambo makubwa katika jukwaa ili kuwapatia vitu vya aina yake wadau na mashabiki wao.
“Hii ni ziara ndefu inayofanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, ikiwa na wasanii wengi, akiwamo Barnabas, Linah, Chege, Mwana FA, AY, Stamina na wengineo,” alisema.
Baada ya kumaliza ziara zao katika mikoa mbalimbali ya Tanznaia Bara, tamasha hilo litatia nanga katika jiji la Dar es Salaam, ambapo hushirikisha msanii wa Kimataifa.
0 comments

Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN Ametoa vyeti kwa madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda zaidi ya 151 wa Igurusi Wilaya ya Mbarali.

Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN Ametoa vyeti kwa madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda zaidi ya 151 wa Igurusi Wilaya ya Mbarali.

Madereva Bodaboda wakijipanga tayari kwa kwenda kupokea vyeti vyao

Madereva Bodaboda wakiandamana kuelekea kupokea vyeti vyao toka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya


Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN akiongea na madereva Bodaboda kabla ya kuwakabidhi vyeti vyao
Madereva  walikabidhiwa vyeti hivyo baada ya kupatiwa mafunzo ya alama za usalama barabarani kwa msaada wa shirika lisilo la Kiserikali kwa kushirikiana na Kikosi cha usalama Barabarani Mkoani Mbeya.


Picha ya pamoja




Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN Ametoa vyeti kwa madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda zaidi ya 151 wa Igurusi Wilaya ya Mbarali.

Madereva hao walikabidhiwa vyeti hivyo baada ya kupatiwa mafunzo ya alama za usalama barabarani kwa msaada wa shirika lisilo la Kiserikali kwa kushirikiana na Kikosi cha usalama Barabarani Mkoani Mbeya.

Mbali ya kukabidhiwa vyeti pia Madereva hao walipatiwa leseni za udereva ambapo Diwani Athumani aliwataka madereva hao kuwa makini barabarani na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Aidha Kamanda Diwani aliwashukuru madereva wa Bodaboda kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi kwa kufichua vitendo vya uhalifu Mkoani Mbeya ambapo wamekuwa wakitoa taarifa za siri na kupunguza uhalifu mkoani Mbeya.

Hata hivyo Diwani alitumia fursa hiyo kuwataka madereva kuwa makini kwani kwa kipindi cha miezi sita madereva 38 wa bodaboda wamefariki mkoani Mbeya na kusikitishwa na wingi wa ajali hizo za pikipiki kwani wengi wao ni vijana na ni nguvu kazi ya Taifa. 

0 comments

MOURINHO AENDELEA KUTAKATA LIGI KUU ENGLAND...CHELSEA YAIFUMUA ASTON VILLA 2-1

MOURINHO AENDELEA KUTAKATA LIGI KUU ENGLAND...CHELSEA YAIFUMUA ASTON VILLA 2-1 

Three points: Chelsea celebrate after taking a 2-1 lead against Aston Villa through Branislav Ivanovic
Pointi tatu: Chelsea wakishangilia baada ya kushinda 2-1 jana
 
Power: Ivanovic scores the winner with a thumping header
Ivanovic akifunga bo la ushindi
 
Anger: A furious Jose Mourinho screams at Paul Lambert on the touchline
Jose Mourinho akizinguana na kocha mpinzani wake, Paul Lambert 
 
Not happy: The argument stemmed from a challenge made by Ivanovic on Christian Benteke
Hakuna furaha: Ugomzi ulitokana na rafu ya Ivanovic kwa Christian Benteke
 
Heated: The fourth official had to step in to prevent a confrontation
Refa wa akiba akijaribu kuwasuluhisha
 
Not backing down: Lambert gave as good as he got in the argument
Lambert akijibu mapigo
 
Taking a hit: Ivanovic's elbow seemed to catch Christian Benteke but the defender was only booked
Ivanovic akimchezea rafu Christian Benteke, lakini akapewa kadi ya njano tu
 
How are you: Benteke was holding his face as Ivanovic stood over him
Benteke akishika uso wake baada ya rafu ya Ivanovic
 
Ahead: Chelsea had gone ahead when Eden Hazard's shot was turned into his own goal by Antonio Luna
Chelsea ilipata bao la mapema baada ya shutila Eden Hazard kumfanya Antonio Luna ajifunge.

Jinsi Luna alivyojifunga na kuipa Chelsea pointi tatu- gonga kupata zaidi yaliyojiri Stamford Bridge

Antonio Luna
A great leveller: Benteke celebrates scoring the equaliser for Aston Villa in first-half stoppage time
Benteke akishangilia bao lake
 
Get in! Villa boss Lambert jumps into the air after Benteke's goal
Kocha wa Villa, Lambert akiruka kushangilia bao la Benteke
 
Battle: Demba Ba gets up with Jores Okore as they challenge for a ball
Demba Ba akipambana na Jores Okore 
 
Fist pump: Eden Hazard was the architect of Chelsea's first goal
Eden Hazard alitoa mchango mkubwa kwa bao la kwanza la Chelsea
 
Clark spark out: The Villa defender is caught by Demba Ba and had to be substituted
Beki wa Villa, Demba Ba akipambana kabla ya kutolewa
 
Blooded: Ciaran Clark had to come off in the first-half with a head injury
Ciaran Clark akitokwa damu
 
Stretch: Ramires and Fabian Delph fight for possession in the middle of the park
Ramires na Fabian Delph wakipambana

 

0 comments

KUTANA NA BINADAMU MNENE KULIKO WOTE DUNIANI!!

KUTANA NA BINADAMU MNENE KULIKO WOTE DUNIANI!!

Mfalme wa Saudi Arabia, ameingilia kati mpango wa kumsaidia Raia wa nchi hiyo, Khalid bin Mohsen Shaari ambaye ndiye binadamu mnene na mzito zaidi duniani akiwa na uzito wa kilogram 610, katika mchakato wa kumtibu na kumrudisha katika hali nzuri zaidi.

Kutokana na unene, ukubwa na uzito wake, Khalid hawezi kutembea wala kusogea mwenyewe bila msaada wa kifaa maalum cha kumbeba akiwa katika kitanda chake, na cha ajabu zaidi, Ni mshkaji mdogo tu ambaye umri wake ni kati ya miaka 18 na 20.
Kwa mujibu wa rekodi za Guiness, Manuel Uribe kutoka Mexico ndiye aliyekuwa akishikilia rekodi ya mtu mzito na mnene zaidi duniani ambapo alikuwa na uzito wa kilo560, Na baada ya kuonekana na kuingizwa katika matibabu, kwa sasa amepungua na kufikia uzito wa kilo 444.

Mfalme Abdullah tayari ametoa amri kuwa Khalid kuhamishwa huko Riyadh kwaajili ya mchakato wa matibabu yake.

 

0 comments

Wakurugenzi 70 Vinara Mtandao wa Ufisadi

Wakurugenzi 70 Vinara Mtandao wa Ufisadi.

Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda

KAMATI ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imebaini mtandao wa ufisadi unaoshirikisha wakurugenzi 70 wa halmashauri mbalimbali hapa nchini ambao wanashirikiana na baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na Kitengo cha Hazina.

Baadhi ya halmashauri hizo ni pamoja na Wilaya ya Monduli, Arusha, Mwanza, Mbeya na Ilala.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Rajab Mohamed Mbarouk alisema keshokutwa atataja majina ya wakurugenzi hao ili wananchi waweze kuwafahamu.

Mbarouk alisema kuwa Tanzania Bara ina halmashauri 134, kwa hiyo ina maana zaidi ya nusu ya wakurugenzi wanajihusisha na mambo hayo.

“Baadhi ya wakurugenzi hao walihamishwa kwenye vituo vyao vya kazi kutokana na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali, lakini bado wanajihusisha na mambo haya,” alisema Mbarouk.
Alisema kutokana na hali hiyo, kamati hiyo imepanga kukutana kesho na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia ili kuzungumzia suala hilo.

“Kuna zaidi ya wakurugenzi 70 wako kwenye mtandao wa ufisadi kwa kushirikiana na watendaji wa Hazina na Tamisemi, jambo ambalo limesababisha halmashauri zao kupata hati chafu kwa miaka mitano mfululizo,”alisema Mbarouk.

Aliongeza wakurugenzi hao wamekuwa wakishirikiana na wahasibu wao katika kutumia vibaya fedha za Serikali zinazotolewa kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri zao.
Akitolea mfano wa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe ambapo halmashauri yake imefanya vibaya katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), lakini hajachukuliwa hatua na badala yake amekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam.

Alisema mbali na halmashauri hiyo, aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Rhoda Nsemwa ambaye alisimamishwa kazi kutokana na tuhuma za ufisadi, lakini bado anaendelea kupata mshahara na stahiki zake kama mtumishi aliye kazini.

“Tumeshangaa kuona kuwa, aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo bado anaendelea kulipwa mshahara, kodi ya nyumba na marupurupu mengine kama ofisa aliye kazini wakati ana kesi ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali,” alisema.

Alibainisha kamati hiyo pia imebaini kuwa Takukuru inajihusisha moja kwa moja na vitendo vya rushwa, kutokana na kupotosha ukweli wa taarifa za watuhumiwa na kuchelewesha kuwasilisha jalada mahakamani.
“Ukiangalia kesi zilizoko mahakamani ambazo upelelezi wake bado unaendelea utaona wazi kuwa Takukuru ni miongoni mwa watu wanaopokea rushwa, jambo ambalo limesababisha kuchelewesha upelelezi au kupindisha ukweli,” aliwatuhumu.

Akizungumzia tuhuma hizo, Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa alisema, “Hazina kuna taratibu na sheria kuhusu matumizi ya fedha na kama jambo hilo limefanyika kweli ni wazi kuwa litakuwa kinyume na sheria na taratibu zilizopo.”
Alisema licha ya kuwa mpaka sasa hajasikia malalamiko yoyote, aliahidi kufuatilia jambo hilo ili kubaini ukweli na kwamba kama kuna mtu atabainika atachukuliwa hatua stahiki. Alisema, “Ngoja tufuatilie ili kujua ukweli.”

Naye Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Kassim Majaliwa aliomba atafutwe leo kwa maelezo kuwa atakuwa ameshapata maelezo ya kutosha kuhusu tuhuma hizo.
“Sijajua hizo halmashauri ni zipi, pamoja na idara ambazo zipo chini ya wizara hii, ngoja kwanza nizungumze na wahusika ambao pia najua watanieleza kilinachoendelea, nitafute kesho (leo) nitatoa ufafanuzi wa kina,” alisema Majaliwa.

Kamati yawabana Mambo ya Nje

Katika hatua nyingine; Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC), imemwagiza CAG kufanya ukaguzi maalumu wa matumizi ya fedha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa hasa katika uendeshaji wa mikutano ya kimataifa.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Gaudence Kayombo alisema jana alipokutana na viongozi wa wizara hiyo kuwa kuna matumizi makubwa ya fedha katika uendeshaji wa mikutano ya kimataifa.
“Kamati itamwandikia CAG, afanye ukaguzi maalumu ili kubaini utata unaoonekana katika matumizi ya fedha ya wizara hiyo hasa kwenye eneo la mikutano,” alisema Kayombo.

Kayombo alisema kutokana na utata huo, kamati imeona haiwezi kuijadili ripoti hiyo ya fedha ya mwaka 2012/13 hadi CAG atakapofanya ukaguzi maalumu.
Aidha, Kayombo aliwataka viongozi hao wataje gharama za Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliojengwa kwa mkopo na msaada wa Serikali ya China, lakini Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Haule alisema ataitaja baadaye baada kujiridhisha.

“Tunataka kufahamu gharama za ujenzi wa jengo hilo, vifaa vilivyosamehewa kodi ili kamati iweze kujua, kwa sababu hadi sasa haieleweki umegharimu kiasi gani,” alisema Kayombo.
Hata hivyo, alisema asilimia 46 ya gharama za ujenzi wa jengo hilo ni msaada wa Serikali ya China huku asilimia 54 ikiwa ni mkopo.

CHANZO: www.mwananchi.co.tz

 

0 comments

Watendaji Redio za Jamii Nchini Wajengewe Uwezo – Usia Nkhoma

Watendaji Redio za Jamii Nchini Wajengewe Uwezo – Usia Nkhoma

Mwezeshaji kutoka Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mtaifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akionesha baadhi ya machapisho ya Umoja wa Mataifa ambayo yatawasaidia katika kuandika habari zao kiufasaha.

IMG_3248
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akifafanua jinsi waandaaji wa vipindi wanavyoweza kutafuta habari nzuri zenye kuelimisha kwa ajili ya redio za jamii na pia mbinu wanazoweza kutumia ili kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii.

Akizungumza katika warsha ya siku nne inayoshirikisha waandishi na maripota wa redio za jamii inayofanyika Wilayani Sengerema mkoani Mwanza, Bi. Ledama ameongeza kuwa upo umuhimu wa kuwajengea uwezo watendaji katika redio hizo ikiwemo kuwafundisha namna ya kutumia mtandao wa Intaneti kwa ajili ya kuboresha uandishi na utangazaji , haswa katika maeneo muhimu yanayoigusa jamii ikiwemo Elimu, Afya na Kilimo na pia jinsi redio hizo zinavyoweza kuandaa vipindi vitakavyoigusa jamii moja kwa moja. 

Kwa jumla warsha hiyo ya siku nne kwa waandishi wa habari wa redio za jamii imeangalia kwa mapana mambo muhimu ya kijamii, na kuchambua mambo hayo ni yapi ambapo imegusia masuala ya Afya na Kilimo pamoja na mambo mengine na kuangali fursa zinazopatikana, pia changamoto zinazokabili masuala hayo na kutathmini nini kifanyike ili kuboresha utendaji na utoaji huduma katika sekta hizo.

IMG_3079
Mtaalam wa Kilimo kutoka Idara ya Kilimo wilayani Sengerema Bw. Joseph Manota akizungumza katika warsha ya waandishi wa habari wa redio za jamii inayofanyika mkoani Mwanza ambapo fursa zinazopatikana katika sekta ya Kilimo na jinsi ya kuzitumia ili kufanikisha sera ya Serikali ya Kilimo Kwanza na pia amezungumzia changamoto zilizopo katika kutimiza sera hiyo na namna gani maafisa wa Kilimo pamoja na Serikali kwa ujumla wanaweza wakafanya kukabiliana nazo ili kutimiza malengo ya kukuza Kilimo.
IMG_3223
Mshauri wa redio za jamii kutoka Unesco Mama Rose Haji Mwalimu akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
IMG_3191
Pichani juu na chini ni waandishi na maripota wa redio za jamii wanaohurudhuria mafunzo hayo yanayofanyika kwenyen kituo cha Habari na Mawasiliano cha Telecentre Wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
IMG_2996
IMG_3043
Mmoja wa watangazaji wa Redio Kahama FM William Bundala (Kijukuu cha Bibi K) akitoa mrejesho wa mafunzo yaliyopita ambayo yameleta mabadiliko makubwa kwa kituo chao kwa Mshauri wa Redio za Jamii kutoka UNESCO Mama Rose Haji Mwalimu
IMG_3226
Afisa Elimu, Takwimu na Vifaa wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza Pius Lwamimi akizungumza na waandishi wa habari na maripota wa redio za jamii nchini ambapo aligusia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta Elimu wilayani humo na kuwaasa kutumia redio zao katika kutoa taarifa muhimu kwa jamii zitakazopelekea kukua kwa Sekta ya Elimu nchini. Pia amewataka wazazi kuwa mstari wa mbele na kujitokeza kuhudhuria vikao katika shule na kutoa maoni yao kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo mitaala ya elimu na pia kushirikiana na redio za jamii kwa kutoa taarifa muhimu na pia kuwahamasisha watoto wao na jamii nzima kujenga utamaduni wa kusikiliza vipindi vya redio hizo kwa manufaa yao.
IMG_3205
Sehemu ya washiriki wanaohudhuria mafunzo hayo.

 

0 comments

Operesheni Ondoa Wahamiaji Haramu Kuanza Kanda ya Ziwa

Operesheni Ondoa Wahamiaji Haramu Kuanza Kanda ya Ziwa

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu wahamiaji haramu waliorejea kwao baada ya agizo la Rais Jakaya Kiwete alilolitoa Juni 29, mwaka huu katika ziara yake ya Mkoa wa Kagera.

 

 Kamishina Mkuu wa Uhamiaji, Magnus Ulungi wa kwanza kulia mstari wa mbele na Ofisa Uhamiaji Mrakibu Bi. Rosemary Mkandala wakiwa katika mkutano wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu wahamiaji haramu waliorejea kwao baada ya agizo la Rais Jakaya Kiwete alilolitoa Juni 29, mwaka huu katika ziara yake ya mkoa wa Kagera (Picha na Lorietha Laurence –Maelezo)

Na Magreth Kinabo – MAELEZO.

SERIKALI imesema operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu katika Kanda ya Ziwa itaanza kwa kushtukiza, huku ikiendelea kusisitiza watu wanoaishi nchini bila taratibu za kisheria kuondoka kwa hiari na mali zao.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahamiaji haramu waliorejea kwao baada ya agizo la Rais Jakaya Kiwete alilolitoa Juni 29, mwaka huu katika ziara yake mkoani Kagera.

“Nimeshapewa maelekezo rasmi na Rais Jakaya Kikwete ya kuwaondoa wahamiaji haramu nitakapoona inafaa. Operesheni itaanza kwa kushtukiza. Muda muafaka wa kutekeleza vyombo vya dola vitasema.
“Tunatoa wito waondoke wenyewe na mali zao bila kunyang’nywa. Wenye mali nyingi wanatakiwa kutoa taarifa katika vituo vya polisi ili waweze kusindikizwa. Hatutawavumilia wahamiaji haramu,” alisema Waziri Nchimbi.

Aliongeza kuwa wahamiaji hao wanaotaka kuishi nchini kihalali wanatakiwa kurudi nchini kwao kwanza na kufuata taratibu za kisheria kama ambavyo nchi nyingine zinavyofanya mtu akitaka kuishi nchi yoyote anatakiwa kufuata taratibu hizo.

Waziri alitoa onyo kwa viongozi wa vijiji wanaoshirikiana na wahamiaji hao kuwatunza na kusema jambo hilo ni makosa kisheria, hivyo watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumzia kuhusu takwimu za wahamiaji hao waliorejea nchini kwao mpaka sasa ni 10,672 kati ya hao Wanyarwanda ni 6,088, Warundi 4000 na Waganda 269 ambao wametoka Mkoa wa Kagera. Kwa Mkoa wa Kigoma ni Warundi 142, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo nane na katika mkoa wa Geita Wanyarwanda 126 na Warundi 39.

Hata hivyo Waziri Nchimbi alisema kuna wahamiaji 14 wamerejea nchini tena baada ya kurudi makwao na kuwataka wasilione jambo hilo kuwa ni mzaha.

Aidha Waziri Nchimbi alisema Serikali ya Tanzania inashukuru kwa ushirikiano unaotolewa na nchi wanazotoka wahamiaji hao kwa kuwapokea vizuri.

Alifafanua kuwa suala la kuwarudisha wahamiaji hao si la mara ya kwanza, lilishawahi kutokea. Huku akisisitiza kwamba tatizo linatokana na sababu mipaka yetu mikubwa na kuna watu wasio wazalendo ambao wanawapokea na kuwakaribisha kwa kupatiwa zawadi. Hivyo Serikali inalifanyia kazi jambo hilo.

 

 

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger