Featured Post Today
print this page
Latest Post

MWALIMU MKUU ANASWA NA MAGUNIA 6 YA BANGI.

MWALIMU MKUU ANASWA NA MAGUNIA 6 YA BANGI.

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Mukubu, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Silidion Kaiza (43), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na bangi gunia sita.

  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 17, mwaka huu, shuleni hapo katika kata na kijiji cha Muganza majira ya saa tano asubuhi.
  
Alisema kuwa raia wema walitoa taarifa kituo cha polisi Rulenge kwamba kuna mwalimu anajihusisha na biashara ya kuuza dawa za kulevya, jambo walilohofia kuwa huenda akawaathiri wanafunzi wa shule hiyo kwani anazihifadhi shuleni.
  
Kalangi alifafanua kuwa baada ya polisi kupata taarifa hiyo walifika shuleni hapo na kumhoji mwalimu Kaiza, na alikiri kufanya biashara hiyo kisha akawapeleka katika moja ya darasa ambalo alikuwa akitunza bangi hiyo.
  
Kamanda alisema kuwa baada ya polisi kukamata bangi hiyo, waliifikisha kituoni na kwamba mwalimu huyo anaendelea kuhojiwa kisha atafikishwa mahakamani wakati wowote ili kujibu tuhuma hizo.
  
Aliwataka wananchi kuendelea kuwafichua wahalifu wanaojihusisha na vitendo vya uuzaji wa dawa za kulevya ambavyo vimekuwa tishio kwa taifa.
0 comments

KWELI KUTONGOZA KIBOKO ..HAKUNA CHA BOSS WALA BAUNSA WOTE MATONYA KWA PENZI

KWELI KUTONGOZA KIBOKO ..HAKUNA CHA BOSS WALA BAUNSA WOTE MATONYA KWA PENZI

Usicheze na mapenzi, katika kutongoza watu huonyesha unyenyekevu utafikiri kuomba kazi. Wengine hata hufikia ku kneel na hata kulia. Kuna wengine hufikia hata kunywa sumu kisa kukataliwa. Mtongozaji ni zaidi ya matonya. Cha ajabu sasa mtu huyohuyo ukimkuta ofisini kwake mfano kama ni baunsa anasukuma watu hovyo, kama ni bosi ni mkali balaa kwa surbordinates. Ule unyenyekevu, upole, hauonekani tena! 

Kwa maana nyingine kila mtu anaweza kuwa mnyenyekevu, kuwa na adabu, kuwa na heshima wakati wote kama vile anatongoza.
0 comments

PETE YA NDOA IMENIPONZA....NDOA IPO HATARINI

PETE YA NDOA IMENIPONZA....NDOA IPO HATARINI

Wadau nipo njia panda naombeni ushauri wenu, nimefanya kosa kubwa na nalijutia
Tafadhali naomba ushauri badala ya kunituhumu

Mwezi nilikuta na demu mmoja tulisoma naye chuo kitambo alikuwa demu wangu for time being, so baada ya miaka kadhaa tukaja kukuta sehemu, shetani akanipitia nikavunja amri ya sita naye

Baada ya kurudi home nikagundua sina pete, nikajaribu kukumbuka nilipoiweka sikupata majibu
Baada ya siku kadhaa yule demu akzidi kunisumbua na kutaka niwe karibu naye sana lakini nikaona si vyema maana anaweza kusababisha mtafaruku kwa ndoa yangu

Baada ya kuona nampotezea akaniambia sasa unajifanya mjanja pete yako ni nayo na nahitaji sh 500,000 cash ama sivyo naharibu kwa mkeo kwamba pete ninayo na ulinikopa.

Kibaya zaidi wife aliniuliza pete umepeleka wapi nikadanganya nimeisahau ofisini nilikuwa nafungua printer sasa pete ikawa inani disturb nikaivua , nilipoenda jumatatu nikamwambia nahisi wahudumu wa usafi wameiiba maana siiona pale nimeiweka naendelea na uchunguzi.

Mwanzo nilimpuuzia lakini mshenzi yule kapeleleza hadi wife anapofanya kazi na kapata simu yake, juzi kampigia kamwambia "naomba mkumbushie mumeo deni langu mimi xxxxx nampigia simpati" halafu akakata simu.
Niliporudi wife kanibana nikamwambia ni mambo ya kazi tu akataka kujua no yake kaipataje, nikazuga zuga na ubabe wa kiume yakaisha

Nikipiga akili nimuendee Polisi naona kama kitanuka na wife atajua
Nikifikiria kumlipa akili hainipi kabisa....kilo tano?
Sijui nimueleze wife ukweli?

Nimejaribu kumpiia simu na kumbembeleza kagoma anachohitaji ni kilo tano au aniharibie kwa wife
Tafadhali ushauri wakuu lawama na madongo hayatanisaidia
0 comments

DAKTARI FEKI AKAMATWA AKIHUDUMIA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI

DAKTARI FEKI AKAMATWA AKIHUDUMIA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI

DAKTARI anayedaiwa kuwa bandia amekamatwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akiwa na vitambulisho bandia vya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) akisomea Shahada ya Pili.
  
‘Daktari’ huyo ambaye amekuwa akitafutwa na uongozi wa chuo kwa zaidi ya mwaka alikamatwa jana asubuhi akiwa hospitalini hapo karibu na jengo kilimo kitengo cha meno.
Katika kitambulisho chake cha kupigia kura anatambulishwa kwa jina la Dismas John Macha aliyezaliwa mwaka 1979 Kilimanjaro na anaishi maeneo ya Upanga Magharibi, Dar es Salaam.

Gazeti hili, lilimshuhudia mtuhumiwa huyo akiwa katika kituo cha usalama cha Muhas na kupekuliwa na askari Polisi wa Muhimbili, Anthony Mwamatepela na kukutwa akiwa na vifaa vya udaktari .

Baadhi ya vifaa alivyokutwa navyo ni pamoja na koti jeupe la udaktari na stetoskopu ambacho ni kifaa cha kusikilizia mapafu yanavyofanya kazi na mapigo ya moyo.

Pia alikuwa na begi jeusi lenye aina mbalimbali za dawa, vitambulisho na karatasi nyingi, lakini alipoulizwa alidai kuwa hizo ni dawa zake.

Macha alikutwa pia na vitambulisho vitatu tofauti, kimoja kikimtambulisha kuwa mwanafunzi wa Muhas wa Shahada ya Pili ya Udaktari (Masters of Medicine ) yenye jina la Macha Dismas kikionesha kusajiliwa kwa namba 60520/2011 na kumaliza muda wake Septemba 30 mwakani. Kitambulisho kingine kilimtambulisha kwa jina la Macha Rogers anayesoma Shahada hiyo hiyo ikionesha kuwa anamaliza masomo yake mwakani.

Alikutwa pia na kitambulisho kinachomwonesha kuwa mwanafunzi wa Shahada ya Kwanza na kadi ya anuani yenye jina la Amos Nnko ambaye ni Ofisa Rasilimaliwatu wa Chuo hicho.

Akizungumzia alivyomkamata askari wa chuo hicho, Fulgence Semfukwe alisema walimkamata baada ya kupata taarifa za yeye kuwa maeneo hayo na kupanga mbinu za kumkamata.

Alisema saa 4.45 asubuhi jana alimkuta kwenye jengo la meno na kumwomba kwa nafasi yake ya udaktari amsaidie tatizo lake na hivyo waongee pembeni, naye bila wasiwasi akakubali. Alimwuliza anatibu magonjwa gani naye kumjibu anatibu maradhi ya aina nyingi na kumwomba kitambulisho na yeye kumpa cha kwake.

Baada ya hapo alishituka na kudai kuwa ni daktari wa Mwananyamala na amekuja hapo kwa ajili ya kuona wagonjwa wake wa dharura ndipo alipokamatwa na kupelekwa kituo cha Polisi.

Alisema amekuwa akiwachenga kwa muda mrefu kutokana na kuwa kila walipopewa taarifa yuko wodi au sehemu Fulani hawakumkuta kwani walipishana naye baada ya kuvua koti na kuweka kwenye begi lake jeusi.

Akizungumza na gazeti hili, Macha limweleza mwandishi wa habari hizi kuwa yeye ni mwanafunzi ambaye anaelewa masuala yote ya matibabu, lakini alifeli chuoni hapo mwaka jana.

Alidai kuwa dawa alizokutwa nazo ni zake kwani ana matatizo katika njia ya mkojo na kifua huku akiamua kufanya hivyo kutokana na ugumu wa maisha.

“Uwezo wa kutibu ninao na nimesoma katika chuo hiki, lakini mwaka jana nilifeli ndiyo maana nikaamua kuwa hivi,” alisema.

Ofisa Uhusiano wa Muhas, Hellen Mtui alisema kutokana na kukamatwa na nyaraka akijitambulisha kuwa mwanafunzi wa ‘Masters of Medicine’, ambaye anaweza kutibu watu hawana uhakika na idadi ya watu ambao ameshatapeli hospitalini hapo.

Kuhusu kusoma Muhimbili, Mtui alikana akisema baada ya kupekua nyaraka za chuo hawakubaini jina la mwanafunzi wa aina hiyo na katika vyeti vyake bandia vinaonesha kusainiwa na Mkuu wa Chuo aliyekuwapo kabla chuo hakijapanda hadhi na kuwa chuo kikuu.

Mtui alisema baada ya kumkamata na kumpiga picha akiwa na mavazi ya udaktari, kumpekua na kumhoji walimpeleka katika kituo cha Polisi cha Selander Bridge kwa mahojiano na uchunguzi zaidi.

0 comments

BAADA YA KUUMIA KWENYE MECHI YA KWANZA TANGU ARUDI KUTOKA MADRID - KAKA AOMBA AC MILAN ISIMLIPE MSHAHARA MPAKA ATAKAPOPONA

BAADA YA KUUMIA KWENYE MECHI YA KWANZA TANGU ARUDI KUTOKA MADRID - KAKA AOMBA AC MILAN ISIMLIPE MSHAHARA MPAKA ATAKAPOPONA


Mchezaji wa kiungo cha kati wa AC Milan Kaka ameitaka klabu yake kutomlipa mshahara wake huku akiendelea kupona kutokana na jereha lake la paja ambalo alilipata wakati wa mchezo wake wa kwanza tangu kujiunga na kilabu hiyo.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa timu ya Brazil aliondolewa uwanjani na jeraha hilo katika dakika ya 70 ya mechi waliyokwenda sare ya mabao mawili na timu ya Rossoneri.

Alirejea Milan bila malipo yoyote mapema mwezi huu baada ya kuhamia Madrid mwaka 2009 kwa kima cha pauni milioni 56.

"Sitaki chochote kutoka kwa Milan, kwa sababu ya mapenzi yangu ya mchezo huu hadi nitakapopata afueni,'' alisema Kaka

''Na kwa sababu hii, nimeamua kutopokea mshahara wangu kwa kipindi hiki. Kile ambacho ningeomba tu ni kusaidiwa ili niweze kupona vyema.''

"Ni wakati mgumu kwangu lakini nimeanza kufanya kila niwezalo kupona, ninatumai nitapona haraka. ''

Kaka alisema kuwa alikuwa ameshauriana na makamu wa rais wa kilabu hiyo Adriano Galliani na madaktari wa kilabu hiyo kabla ya kuitaka klabu kutomlipa.

Haijulikani ikiwa Milan imekubali ombi la mchezaji huyo.

Kaka, ambaye alishinda tuzo la mchezaji bora zaidi duniani mwaka 2007 alichezea Milan katika mechi 268 na kufunga mabao 95 kati ya mwaka 2003 na 2009. Alisaidia klabu hiyo kushinda ligi ya Serie A mwaka 2004 na 2007 kwenye michuano ya mabingwa wa Ulaya.

Mnamo mwaka 2010, mlinzi wa Milan Oguchi Onyewu alikubali kutia saini mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo bila malipo baada ya kutochezeshwa kwa mwaka mmoja mfululizo.
0 comments

MBEYA CITY FC NA SIMBA UWANJA WA TAIFA, SIMBA 2 MBEYA CITY FC 2

MBEYA CITY FC NA SIMBA UWANJA WA TAIFA, SIMBA 2 MBEYA CITY FC 2

 Ikiwa kipindi cha kwanza kinakaribia kuanza sasa Mashabiki wa Mbeya City wakiwa wanashangilia kwa Nguvu zote
 Simba Bila Mbeya City Fc Bila

 Mashabiki wa Pande zote wakingoja mpira kwa hamu kubwa 
 Timu ya Simba na Mbeya City Fc wakiwa wanaingia uwanjani 
 Wachezaji wa Mbeya City Fc wakiwa wanasalimiana na Wachezaji wa Simba kabla ya Mechi kuanza
 
Wachezaji wa Timu zote Mbili wakiomba Dua
 Mpira ukiwa umeanza kwa kasui 

 Hivi ndivyo Walivyo fanya mashambulizi ya kufunga goli la kwanza
 Baada ya Simba kufunga Goli
Mashabiki wa Simba wakishangilia goli la kwanza

 Mashabiki wa Simba wakishangilia Goli la Pili
 Mbeya City Fc wakishangilia Goli lao la kwanza
Wachezaji wakiwa wanatoka kwa ajili ya Mapumziko 
0 comments

January Makamba apinga kuhusisha siasa na mgogoro wa kiwanda cha chai Bumbuli

January Makamba apinga kuhusisha siasa na mgogoro wa kiwanda cha chai Bumbuli



Ray Said, Bumbuli
 
Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi na  Teknolojia  January  Makamba  amewataka  baadhi  ya watu  kuondokana  na dhana  ya  kusema  mgogoro  wa  kiwanda cha  chai  cha  Mponde   ni siasa badala  yake amewataka  kuiacha  serikali  indelee na taratibu zake  za  kulitafutia  ufumbuzi  swala hilo. 
 
Mbunge wa Bumbuli, January Makamba, pichani.
 
Makamba  ambaye pia ni Mbunge  wa  jimbo  la Bumbuli, alisema lazima ashirikiane na wananchi wake na si kikundi cha watu wachache licha ya kutukanwa kwa kwasababu ya kuwaunga mkono wananchi.
Naibu  waziri huyo alieleza kusikitishwa kwake na baadhi ya watu kuliingiza suala hilo kwenye kisiasa na kwamba lina maslahi binafsi  huku mambo hayo yakiachwa tangu mwaka 2010  baada ya kumalizika uchaguzi, hivyo kwa sasa ni wakati wa kuleta maendeleo.
“Siamini   kama  kuwaunga  mkono  wananchi  walionichagua yanatokana na tofauti za kisiasa kwani eneo hili linamilikiwa na Chama kimoja ambacho ni Chama cha Mapinduzi na wala sina  maslahi binafsi katika suala hilo,” alisema Makamba nakuongeza kuwa  yeye anawasimamia  wakulima wa zao la chai.

Kiwanda cha Mponde  kimefungwa  takribani  miezi  mitano  sasa kufuatia wakulima kususa kupeleka majani mabichi ya chai kwa madai ya kutaka uongozi wa Chama cha Wakulima wa Chai Usambara (UTEGA) uitishe Mkutano Mkuu kwa ajili ya kuwasomea mapato na matumizi.
Hivi karibuni Makamba, alimwaga machozi hadharani katika kijiji cha Mponde Kweminyasa kutokana na taarifa za watu watano kujeruhiwa kwa risasi za moto kutokana na vurugu zilizotokea kati ya wakulima wa zao la chai na Jeshi la polisi.
Vurugu hiyo ilitokea kutokana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kuamuru kiwanda cha chai cha Mponde kilichokuwa kimefungwa kwa mwezi mmoja na nusu wakati  huo kifunguliwe kwa nguvu chini ya usimamizi wa Polisi jambo  ambalo zilisababisha vurugu kubwa mpaka watu kujeruhiwa  kwa  risasi za  moto.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger