Featured Post Today
print this page
Latest Post

MAONYESHO YA KIMATAIFA YA BIASHARA JIJI LA TANGA

MAONYESHO YA KIMATAIFA YA BIASHARA JIJI LA TANGA



 Na Peter Mtulia, Tanga.



Halmashauri ya jiji la Tanga imetoa wito  kwa  wakazi  wake kupitia maonesho ya biashara ya kimataifa yanayoendelea  kwenye viwanja vya Tangamano mkoani hapa kuwa wananchi wapate kutembelea banda lao ili waweze kupata taarifa sahihi kuhusu mji wa Pongwe pamoja na mambo ya usafi wa Mazingira .

     Hayo yamesemwa na mwoenyeshaji wa maonesho haya kwa niaba yah alma shauri Juma Mkombozi wakati akizungumza na redio huruma  viwanjani hapo kuhusu utoaji wa huduma yao kwenye maonyesho hayo ya kimataifa .

  Aidha amesema kuwa lengo la wao kushiriki kwenye maonesho ni kueleza kazi   zao   na shughuli zote za halamashauri kwa wananchi ili wapate ufafanuzi    juu ya mambo ambayo hawayafahamu .

Akielezea shughuli za halmshauri amesema kuwa ni pamoja na  fursa  na maeneo ya uwekezeji yliyopo ktika jiji la Tanga  na kutolea ufafanuzi   wa  shughuli  za wadau wa maendeleo ya jiji.

Sanjari na hayo amesema wakazi wa jiji la hawana budi kutambua kuwa halmshauri  inendelea kufanya jitihada zake kufanikisha kuwa Tanga Televisheni  itaanza  kutumika baada ya muda mfupi  hivyo  wananchi wameombwa kuwa na subira.
 
0 comments

WAZEE MKOA WA TANGA WALIA NA USAWA

WAZEE MKOA WA TANGA WALIA NA USAWA




Na Peter Mtulia, Tanga.
 
BARAZA la wazee mkoani tanga limeiomba serikali kutunga sheria  ambayo itasaidia kuleta hali ya usawa, ulinzi  na usalama kwa wazee ili kuwaondolea changamoto  mbalimbali wanazokumbana nazo katika jamii.

Rai hiyo imetolewa na katibu  wa umoja huo [TARINGO] mkoani hapa ferdolin mbunda wakati akizungumza na redio huruma ofisini kwake amesema kutokana na wazee wengi kutotendewa haki katika jamii serikali haina budi kuingilia kati suala hili kwa kuweka sheria za kuwajali wazee.

Aidha amesema serikali  itoe elimu kwa jamii ili iweze kujua umuhimu wa  wazee kwa kuwajali zaidi ki afya kwa kuweka vituo maalum ambayo yatasaidia  upatikanaji  wa matibabu kwa urahisi ili waweze kuepukana na foleni pale wanapofika mahospitalini.

Wazee hao wameiomba serikali iweke pensheni ya jamii na pensheni ya kawaida ambayo itasaidia wazee kupata huduma za matibabu kupitia maafao ya huduma hizo ili waweze kukidhi mahitaji yao.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger