Featured Post Today
print this page
Latest Post

PINDA AKUTANA NA 'NGUVU YA UMMA' MLOGANZILA

Pinda Mloganzila-aug17-2013 a3a09
Mamia wazuia msafara wake, apokewa kwa mabango
Iilikuwa mfano wa nguvu ya umma iliyoelekezwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipofanya ziara katika eneo la Mloganzila–Kwembe, jijini Dar es Salaam jana.
P.T

Umati wa watu walijitokeza wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe tofauti, wakasimama barabarani kuukwamisha msafara wa Pinda, wakilalamikia kupunjwa fidia, dhuluma na unyanyasaji waliofanyiwa baada ya serikali kutwaa ardhi yao.
Mloganzila iliyoko nje kidogo ya Dar es Salaam, imetwaliwa na serikali ili kujenga Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi za Tiba, pamoja na hospitali kubwa ya kisasa. Hatua hiyo inakusudia kukifanya chuo hicho kikuu cha Muhimbili kujitegemea na kuondoka kwenye majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Eneo hilo ambalo ni mali ya kampuni ya kusindika nyama ya Tanganyika Packers, iliyofilisika miaka ya 1980, lilibaki pori na wananchi kuliendeleza kabla ya serikali kulitangaza kuwa kijiji cha Ujamaa na watu kumilikishwa ardhi. Eneo linakaliwa na wanakijini wapatao 2,000.
'PICHA' ILIVYOANZA
Katika tukio la jana asubuhi, wanaume, wanawake na watoto waliokadiriwa kufikia 300, walikusanyika eneo la Kabimita wakiwa na mabango ya kulalamika, kulaani na kuitaka serikali iwape haki yao.
Kisha, walisimama barabarani kuuzuia msafara wa Pinda, tukio lililodumu kwa takribani dakika tano, hali iliyomlazimu (Pinda) kushuka kutoka ndani ya gari ili kuzungumza nao.
Pinda, aliwaambia wakazi hao kuwa analifahamu tatizo lao na kwamba ziara yake, ililenga a kuwasikiliza na kuwaeleza jinsi walivyojipanga kuwafidia. Alisema, hapakuwa na sababu ya kumzuia, bali walipaswa kufika katika mkutano ili wasikilizane.
"Najua kudai fidia ni haki na wajibu wenu, maelezo ya matatizo yenu ninayo, njooni niwape maelezo jambo lenu linajulikana njooni mnisikilize," alisema. Taarifa za ndani zilidai kuwa wakazi hao walipanga kuususia mkutano wa Pinda, lakini kwa kauli yake (Pinda) walikwenda kumsikiliza.
Endelea kusoma habari hii kwa kubofya hapa chini
UJUMBE WA MABANGO
Miongoni mwa mabango yaliandikwa hivi;
"Tunachotaka ni haki ya ardhi, Mheshimiwa Pinda usidanganywe fidia ya ardhi hatujalipwa, tumeishi hapa kwa zaidi ya miaka 50."
"Nyerere na Kawawa fufukeni muone udhalimu huu." Baada ya Waziri Mkuu kutoa kauli za kuwaalika mkutano, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza, aliwaambia wananchi waweke mabango vizuri ili Pinda ayasome. "Mengine nitamkusanyia aondoke nayo ili akayasome..." alisema Mahiza.
SABABU ZA KUZUIA MSAFARA
Wananchi hao walidai walilazimika kumzuia ili kumshinikiza awasikilize na kutoa hatma ya madai yao, kwani walihofu asingekutana nao kwa vile taarifa za ziara yake eneo hilo hazikutangazwa kwa uwazi.
Awali, walipanga kulala chini ili wamzuie baada ya kuambiwa kuwa angefika Mloganzila kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo.
Pia alitarajiwa kuzindua barabara inayojengwa kuanzia Kibamba CCM hadi Kisopwa sehemu iliyotwaliwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali na Chuo Kikuu kipya cha Muhimbili.
Hata hivyo, wakazi hao walimzuia Pinda kwenda kwenye hema ambalo liliandaliwa kwa ajili ya kuhutubia, likiwa limewekwa kwenye ofisi za Kabimita na kufanya askari kudhibiti ghasia hizo.
ULINZI WAIMARISHWA
Kutokana na tukio hilo na kuwapo dalili za kutokea vurugu zaidi, polisi na walinzi wake walilazimika kulizingira gari la Pinda ili kumuepusha na kadhia hiyo. Hata hivyo polisi hawakutumia silaha wala vitisho kuwatawanya watu, badala yake diplomasia na ushawishi ulitumiwa zaidi kuwasihi wananchi.
Kabla ya kuzuia msafara huo walimkwamisha Mkuu wa Kituo cha Polisi Kimara , aliyefahamika kwa jina la CD Papalika, aliyefuatana na maofisa wengine wa jeshi hilo. Walizuiwa kwenda kwenye hema na jukwaa lililoandaliwa kwa ajili ya mkutano wa Pinda.
Pia wakazi hao walizuia lori namba T 972 BYG lililokuwa limebeba chimbuo (excavator) na katapila kwa ajili kusawazisha eneo la hema ambalo mkutano huo uliandaliwa. Kadhalika walizuia magari ya kikosi cha mbwa na maofisa wa polisi waliokuwa na mbwa hao wakitishia kuwa endapo watawashusha wangewaua.
Licha ya magari hayo kuzuiliwa hata msafara wa Waziri Mkuu uliokuwa na magari zaidi ya 26 likiwamo la Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Shukuru Kawambwa, Naibu Waziri wa Afya, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza nayo pia yalikwamishwa.
FIDIA KUANGALIWA UPYA
Akizungumza na wananchi hao, Pinda, alisema serikali imeamua kuwalipa fidia ya maendelezo ambayo ni gharama walizotumia kuendeleza sehemu zao, ikiwa ni pamoja na mazao na majengo , lakini hawatafidiwa ardhi kwa kuwa ilikuwa mali ya serikali.
Alisema kutokana na watu kumsihi kuwa fidia ni ndogo, iliyoanzia Sh 6,000 hadi 100,000, suala hilo litatazamwa upya na kuona kama serikali inaweza kuwasaidia.
CHANZO: NIPASHE
0 comments

Ghasia nchini Misri Udugu wa Kiislamu waitisha maandamano zaidi


Ghasia nchini Misri Udugu wa Kiislamu waitisha maandamano zaidi

Mji mkuu wa Misri Cairo ulitumbukia katika ghasia Ijumaa(16.08.2013) wakati watu waliokuwa wakilinda doria katika vizuwizi vilivyowekwa katika vitongoji vya mji huo walipopambana na waandamanaji. 

Waandamanaji wa Udugu wa Kiislamu wanapinga kuondolewa madarakani kwa Mohammed Mursi na ukandamizaji uliosababisha umwagikaji mkubwa wa damu.

Mapigano makali kabisa ya mitaani ambayo hayajawahi kuonekana mjini Cairo katika muda wa zaidi ya miaka miwili ya ghasia yamesababisha kiasi watu 82 kuuawa, ikiwa ni pamoja na maafisa wa polisi.

Mapambano ya silaha.

Wakaazi wamekuwa wakifyatuliana risasi na kuashiria mwelekeo mbaya katika mzozo huo, wakati raia ambao walikuwa na bastola na bunduki walipopambana na waandamanaji waliokuwa wakishiriki kile ambacho kundi la Udugu wa Kiislamu ilikiita "siku ya hasira" , iliyozushwa na hasira dhidi ya majeshi ya usalama kuwaondoa kwa nguvu waandamanaji waliokuwa wamekita kambi katika maeneo mawili mjini Cairo siku ya Jumatano na kuzusha mapambano ya nchi nzima ambapo watu zaidi ya 600 walipoteza maisha.

A member of the Muslim Brotherhood and supporter of ousted Egyptian President Mohamed Mursi shouts slogans in Cairo August 16, 2013. Thousands of supporters of Mursi took to the streets on Friday, urging a Day of Rage to denounce this week's assault by security forces on Muslim Brotherhood protesters that killed hundreds. The army deployed dozens of armoured vehicles on major roads in Cairo, and the Interior Ministry has said police will use live ammunition against anyone threatening state installations. REUTERS/Louafi Larbi (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)  
 
Kundi la Udugu wa Kiislamu linaendeleza upinzani dhidi ya jeshi
 
Helikopta za jeshi zilizunguka hewani wakati wakaazi wakiwa na hasira dhidi ya maandamano ya Udugu wa Kiislamu wakiwatupia mawe na chupa waandamanaji. Pande hizo mbili pia zilifyatuliana risasi, na kuzusha mapambano katika mitaa katika maeneo yanayokaliwa na watu katika vitongoji vya mji huo.
Maandamano zaidi

Udugu wa Kiislamu wakionyesha ukaidi wameitisha wiki ya maandamano nchini Misri kuanzia leo Jumamosi.Majeshi ya usalama na raia kadhaa waliuzingira msikiti wa al-Fateh katikati ya jiji la Cairo katika eneo la Ramses ambako waandamanaji wa kundi la Udugu wa Kiislamu walikimbilia kujisalimisha wakati wa mapambano hayo siku moja kabla.

Supporters of ousted Egyptian President Mohamed Mursi run away from tear gas during clashes in Cairo August 16, 2013. Thousands of supporters of Mursi took to the streets on Friday, urging a Day of Rage to denounce this week's assault by security forces on Muslim Brotherhood protesters that killed hundreds. The army deployed dozens of armoured vehicles on major roads in Cairo, and the Interior Ministry has said police will use live ammunition against anyone threatening state installations. REUTERS/Louafi Larbi (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)  
 
Waandamanaji wakifyatuliwa mabomu ya kutoa machozi
 
Polisi ya Misri imewakamata watu 1004 wanaosadikiwa kuwa ni waungaji mkono wa kundi la Udugu wa Kiislamu katika siku nzima ya mapambano ya nchi nzima jana , imesema wizara ya mambo ya ndani katika taarifa mapema leo Jumamosi(17.08.2013).
Idadi ya waliokamatwa ikiwa ni wafuasi wa kundi la Udugu wa Kiislamu imefikia 1004, taarifa hiyo imesema , mjini Cairo pekee wakiwa wamekamatwa watu 558. Mapambano hayo yamesababisha zaidi ya watu 80 kupoteza maisha, kwa mujibu wa maafisa na watu waliokuwa wakishuhudia katika eneo lililowekwa la muda la kuhifadhi maiti.
Umoja wa Ulaya kujadili ghasia Misri
Viongozi wa Umoja wa Ulaya wamezungumza jana Ijumaa (16.08.2013) juu ya haja ya jibu la pamoja la ghasia nchini Misri na kukubaliana kuitisha mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni wa Umoja huo wiki ijayo.

ATTENTION EDITORS - VISUAL COVERAGE OF SCENES OF INJURY OR DEATH
A man sprays air freshener over the bodies of dead supporters of ousted Egyptian President Mohamed Mursi at El Eyman mosque in Cairo August 15, 2013. Egypt is in turmoil after security forces moved in to clear the protest camps of thousands of supporters of deposed Islamist president Mohamed Mursi on Wednesday, and violence spread around the country. Protesters clashed with police and troops who used bulldozers, teargas and live ammunition to clear two Cairo sit-ins. Egypt's health ministry says 623 people were killed and thousands wounded in the worst day of civil violence in the modern history of the most populous Arab state. Muslim Brotherhood supporters say the death toll is far higher, with hundreds of bodies as yet uncounted by the authorities. Picture taken August 15, 2013. REUTERS/Amr Abdallah Dalsh (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST TPX IMAGES OF THE DAY) TEMPLATE OUT.
ATTENTION EDITORS: PICTURE 24 OF 29 FOR PACKAGE '48 HOURS IN CAIRO'. SEARCH '48HOURS' FOR ALL PICTURES  
 
Maiti zikiwa zimepangwa msikitini
 
Rais wa Ufaransa Francois Hollande na kansela wa Ujerumani Angela Merkel wametoa wito wa kumalizwa kwa ghasia na kuanza kwa majadiliano nchini Misri.
Taarifa ya serikali ya Ujerumani imesema kuwa Merkel amemwambia rais wa Ufaransa Hollande kuwa Ujerumani, moja kati ya mshirika mkubwa wa kibiashara na Misri , itaangalia upya uhusiano wake na Misri kuhusiana na umwagaji damu uliotokea wiki hii.
0 comments

POLISI FEKI AJITETEA.ADAI KUWA NJAA NDO ILIMFANYA AJIFANYE TRAFFIC.

HUYU NDIYE TRAFIKI FEKI ALIYEDAKWA AKIPIGA MZIGO KAMA KAWA


MKANDA mzima wa askari bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani (trafiki), James Juma Hussein (45)  aliyekamatwa saa 1:30 asubuhi ya Agosti, 14, 2013 maeneo ya Tabata Kinyerezi Mnara wa Voda, jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya sare zake za kazi, umepatikana....

  
Kwa nini James alikamatwa? Asubuhi hiyo, afisa mmoja wa trafiki mwenye cheo cha ukaguzi alikuwa akipita eneo hilo kwenda kazini, alipomwona James alisimamisha gari, akashuka kwenda kumsalimia. 


Lakini alishangaa kuviona vifungo vya shati lake ni vya kawaida (vya polisi vinatakiwa kuandikwa police force yaani ‘jeshi la polisi’), akamtilia shaka. 
 
Afisa huyo Alimkamata ‘askari feki’ huyo  mkazi wa Kimara Matangini, Dar na kumfikisha kwenye Kituo cha Polisi Stakishari, wilayani Ilala, Dar akafunguliwa jalada namba STK/RB/15305/2013 KUJIFANYA ASKARI ili taratibu za kisheria zichukuliwe juu yake.

Ndani ya kituo cha polisi, James alihojiwa haya: Askari:Wewe mtu wa wapi?
James: Mnyamwezi wa Tabora.
Askari: Una muda gani ukijifanya trafiki?
 James: Wiki moja sasa.
Askari: Hii kofia ya polisi uliipata wapi?
James: Nguo nyeupe juu ya kofia niliitengeneza kienyeji, krauni, tepe za usajenti na mkanda ni za shemeji yangu alikuwa polisi Tabora, ni marehemu, alikuwa akiitwa Shaban.

James aliwaambia polisi kuwa suruali nyeupe ya kitrafiki aliishona mtaani lakini kamba ya filimbi na kizibao cha kung’ara vilikuwa vya polisi.

Askari: Uliwahi kuwa polisi?
James: Niliwahi kupata mafunzo ya upolisi katika Chuo cha Polisi Moshi (CCP) mwaka 1990-91 lakini nilifukuzwa kazi kwa sababu nilikwenda muziki. Nilirudi Tabora nikawa mkulima na mke wangu na mtoto mmoja ambao wote sasa ni marehemu.

Ndani ya nguo za kitrafiki alizokuwa amevaa James, alikutwa na suruali ya bluu na fulana ya kijani.
 
James alisema njaa ndiyo iliyomfanya ajifanye trafiki na ‘kuwapiga mikono’ madereva, hasa wa daladala ili anapowakuta na makosa kwenye magari yao ajipatie chochote.


 Kamishina wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova amethibitisha kukamatwa kwa polisi huyo feki.
 
:Chanzo d'jaroarungu.blogspot.com

0 comments

WAZIRI WA UCHUKUZI ASHINDWA KUWATAJA VIGOGO WANAOHUSIKA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA NCHINI.

Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe.
 
WAZIRI wa Uchukuzi Dk. Harisson Mwakyembe jana alishindwa kuwataja vigogo wanaohusika na biashara ya dawa za kulevya nchini na badala yake akawataja watu waliofanikisha kupita kwa bidhaa hiyo haramu iliyokamatwa hivi karibuni nchini Afrika Kusini.
 
Waziri huyo pia alisimulia bidhaa hiyo ilivyopitishwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa waJulius Nyerere (JNIA), uliopo jijini Dar es Salaam na kukamatwa Afrika Kusini ikidaiwa kusafirishwa na wasanii wa hapa nchini.
 
Wengi wa watu waliotajwa kuwasaidia wauza ‘unga’ na wasafirishaji ambao hadi sasa hawajulikani, ni wafanyakazi wa uwanja huo katika idara mbalimbali.
 
Wafanyakazi wa uwanja huo waliotajwa kusaidia usafirishaji wa dawa walizokamatwa nazo Watanzania wawili Agnes Gerald “Masogange” na Melisa Edward nchini Afrika Kusini ni Koplo Ernest wa Jeshi la Polisi Tanzania, Zahoro Mohamed Seleman ambaye ni mbeba mizigo uwanjani hapo, Yusuph Daniel Issa, Jackson Manyonyi, Juliana Thadei na Mohamed Kalungwa ambao ni maofisa wa usalama wa uwanja huo.
 
Hatua ya Dk. Mwakyembe kutangaza kuwataja hadharani vigogo wa dawa za kulevya ilisubiriwa kwa kiasi kikubwa na wananchi ambapo jana waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali waliingia katika Wizara ya Uchukuzi kuanzia saa 7:30 mchana hadi saa 8:40 wakati waziri huyo alipoingia na kutoa taarifa yake kwa umma.

Dk. Mwakyembe alisema baada ya serikali kupata taarifa ya kukamatwa kwa Watanzania Julai 5 mwaka huu katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo nchini Afrika Kusini na kubaini wahusika walianzia safari jijini Dar es Salaam, waliamua kupitia mfumo mzima wa kamera za uwanja wa ndege wa JNIA (CCTV) na kubaini matukio yaliyohusika moja kwa moja na usafirishaji wa dawa hizo.
 
Alisema waliangalia mfumo wa kamera kuanzia saa 9:25 hadi 10:30 alfajiri ya Julai 5 na kubaini namna mkakati huo ulivyofanikishwa.
 
“Saa 9:28 alfajiri kamera zinamuonyesha kijana mbeba mizigo kwa jina la Zahoro akiwa anazunguka zunguka eneo la kuingia abiria mithili ya mtu mwenye miadi fulani, na kisha eneo jingine alionekana Issa akitoka nje ya jengo na kuingia tena huku akiongea na simu na hili haliruhusiwi,” alisema Mwakyembe.
 
Aliongeza kuwa wakati kamera zikimuonyesha Issa, pia alionekana Koplo Ernest akiranda randa eneo la uhakiki wa hati za kusafiria akiwa na dalili za kusubiri kitu na ilipofika saa 10:15 alfajiri waliingia watu watatu.
 
Aliwataja watu hao ni Agnes Masogange, Melisa Edward na Nasoro Mangunga wakiwa na mabegi tisa ambapo katika eneo hilo anaonekana tena Koplo Ernest akiwasaidia abiria kupanga mizigo na wakati huo huo mbeba mizigo Zahoro akisaidia kuweka vizuri mizigo ya kina Masogange na wenzake kabla ya kuizungushia karatasi za nailoni.
 
“Huu mtandao ni mkubwa na unahitaji uadilifu kwani baada ya shughuli hiyo tulimuona Yusuph akimuondoa mfanyakazi mwenzake yule Manyonyi na kukalia kiti cha mkaguzi wa mizigo na hili lilifanyika kwa dakika sita. Baada ya kufanikisha kazi hiyo akamwachia mwenzake jukumu alilokuwa nalo,” aliongeza Dk. Mwakyembe.
 
Alisema jambo jingine walilobaini ni kucheleweshwa kwa mbwa wa ukaguzi wakati mizigo hiyo ikipitishwa na kwamba ukaguzi wa kutumia mbwa ulifanyika wakati mabegi yenye dawa hizo yalipoingizwa katika sanduku la chuma na mbwa kunusa sanduku badala ya mabegi.
 
Aliongeza kuwa mkakati mwingine uliofanikisha hatua hiyo ni kwa Mangunga kuruhusiwa kusafiri siku hiyo hiyo licha ya kutokuwa na tiketi, na kwamba alilipa dola 60 kufanikisha safari yake ya dharura.
 
Uamuzi wa wizara
Kutokana na hali hiyo Dk. Mwakyembe alisema serikali imeiagiza Mamlaka ya Uwanja wa Ndege (TAA) kuwapiga picha watu wote watakaokamatwa na dawa za kulevya na kusambazwa katika vyombo vya habari, kampuni iliyomuajiri Nasoro imfukuze kazi mtumishi wake huyo na asikanyage uwanja wa ndege wa JNIA.
 
Waziri huyo pia alilitaka Jeshi la Polisi limkamate Zahoro na kumuunganisha na wenzake kujibu mashitaka ya jinai chini ya sheria ya kuzuia dawa za kulevya sura ya 95 ya mwaka 1996.
 
Dk. Mwakyembe aliitaka TAA kuwafukuza kazi wafanyakazi wake wanne ambao ni maofisa wa ulinzi uwanjani hapo na kisha wakamatwe na kufunguliwa mashitaka, huku Jeshi la Polisi likitakiwa kumchukulia hatua za kinidhamu Koplo Ernest.
 
Mbali na hatua hizo, pia Dk. Mwakyembe alisema serikali inaiagiza Idara ya Usalama wa Taifa kuendesha uchunguzi wa kina kwa maofisa wake waliokuwa zamu Julai 5 mwaka huu, kwa kuchelewa kuwafikisha mbwa wa kubaini dawa hizo katika muda muafaka wa kukagua mizigo.
 
Wakati Dk. Mwakyembe akielezea hali hiyo kwa Tanzania, taarifa zilizopatikana na gazeti hili zinabainisha kuwa nchini Afrika Kusini mtandao huo ulijipanga kufanikisha upitishaji wa dawa hizo aina ya Cyrsatl Methamphetamine au “TIK” pasipo kubughudhiwa.
 
Taarifa zinaeleza baada ya Masogange na wenzake kufanikiwa kupita katika maeneo ya ukaguzi ya uwanja wa Oliver Tambo, Mangunga alifanikiwa kuondoka uwanjani hapo na mabegi matatu yenye jumla ya kilo 60 bila kujulikana.
 
“Masogange kilichomponza ni pale alivyokuwa anajiremba baada ya kuruhusiwa kupita katika vizuizi vyote. Kiuhakika hakukamatwa katika mashine bali ilikuwa ni ukaguzi usio rasmi uliofanywa na polisi. 
 
Nadhani huyu askari aliyewashika hakujua mpango huo,” kilisema chanzo chetu ndani ya Jeshi la Polisi.
;Chanzo, jumamtanda.blogspot.com
0 comments

HELIKOPTA ILIYOMBEBA KATIBU MKUU WA CHADEMA, DK WILLBROAD SLAA YAPOTEA NJIA ANGANI.

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Willbroad Slaa, jana alilazimika kutua kwa dharura na helikopta aliyokuwa akisafiria, baada ya kupotea akiwa angani kwa muda wa robo saa.

Rubani aliyekuwa akiendesha helikopta hiyo, alilazimika kutua kwa dharura baada ya kupotea eneo alilotakiwa kutua.

Tukio hilo lilitokea jana jioni wakati Dk. Slaa akitokea wilayani Korogwe akielekea Lushoto kwenye mkutano wa kuhamasisha kuunga mkono mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya ambayo yanaungwa mkono na chama chake.

Dk. Slaa ambaye alikuwa atue Lushoto mjini, alipotea na kwenda kutua mji wa Mlalo katika wilaya hiyo ya Lushoto. Kutokana na tukio hilo, mkutano wake uliopangwa kufanyika katika wilaya ya Muheza ulichelewa kuanza.

Akihamasisha kuugwa mkono uwapo wa serikali tatu ambayo ni Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, alisema kuwa mfumo huo hauna gharama ikilinganishwa na serikali mbili za sasa.

Aliyasema hayo jana jioni katika uwanja wa Mavi, wilayani Muheza, alipohutubia maelfu ya wananchi wa Muheza.

Alisema kuwa serikali ya sasa ina gharama kubwa kwani ina wabunge wengi zaidi ya 438, wakiwamo wa Zanzibar na Tanzania bara na kulipwa mshahara mkubwa wa Sh. milioni 11 kwa mwezi.

Alisema zikiwapo serikali tatu, wabunge watapungua idadi na kubaki 314 kwani wabunge 124 watakuwa hawapo.

Alisisitiza Rais apunguziwe madaraka na pale anapokuwa madarani au akimaliza muda wake, kisha ikabainika kuwa ametumia vibaya mamlaka yake akiwa Ikulu ashitakiwe.
Katika mkutano huo, Dk. Slaa aliongozana na mratibu wa ziara, Mwita Waitara na mjumbe wa kamati kuu Chadema Taifa, Mabere Marando. chanzo:nipashe
0 comments

YANGA SC IKIIFUNGA AZAM FC LEO ITAWEKA REKODI NA KUIPOTEZELEA MBALI SIMBA SC


Saturday, August 17, 2013

YANGA SC IKIIFUNGA AZAM FC LEO ITAWEKA REKODI NA KUIPOTEZELEA MBALI SIMBA SC

 
Watavunja rekodi? Yanga SC wakitwaa Ngao leo watakuwa timu ambayo imetwaa mara nyingi taji hilo
 
Na Mahmoud Zubeiry,
IMEWEKWA AGOSTI 17, 2013 SAA 3:00 ASUBUHI
YANGA SC itaweka rekodi ya kuwa timu iliyotwaa mara nyingi zaidi Ngao ya Jamii, iwapo itaifunga Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam- hivyo kuwapiku wapinzani wao wa jadi, Simba SC.
Hadi sasa, vigogo hao wa soka nchini, kila mmoja ametwaa Ngao mara mbili, wakati timu nyingine zaidi ya hizo iliyowahi kutwaa ubao huo ni Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Yanga SC ndio washindi wa kwanza wa Ngao mwaka 2001 walipoifunga mabao 2-1 Simba SC, enzi hizo Ligi Kuu inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager. 
Watavunja rekodi? Yanga SC wakitwaa Ngao leo watakuwa timu ambayo imetwaa mara nyingi taji hilo

Baada ya hapo, haikuchezwa tena mechi ya Ngao hadi mwaka 2009 wakati Mtibwa Sugar ilipoilaza 1-0 Yanga SC.
Mwaka 2010 Yanga walirejesha Ngao kwenye himaya yao, baada ya kuwachapa tena wapinzani wa jadi, Simba kwa penalti 3-1 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90.
Simba SC walitwaa mara mbili mfululizo Ngao na kufikia rekodi ya watani, kwanza 2011 walipoifunga 2-0 Yanga na mwaka jana walipotoka nyuma kwa 2-0 na kuilaza Azam 3-2.
Katika mchezo wa leo, Kocha Mholanzi, Ernie Brandts atamkosa mshambuliaji wake Mrisho Khalfan Ngassa ambaye amefungiwa mechi sita na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Kamati hiyo baada ya kupitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom jana, ilimuidhinisha Ngassa kuchezea Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini kuwa Ngassa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea (sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya fedha hizo kwa Simba.
Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa fedha hizo.
Wako tayari kwa Ngao ya kwanza? Azam FC iliikosa Ngao mwaka jana baada ya kufungwa na Simba SC 3-2 licha ya kuongoza 2-0 hadi mapumziko

Kwa sababu hiyo, Simon Msuva anaweza kurejea uwanjani leo katika nafasi ya Ngassa, huku wachezaji wapya wanaotarajiwa kucheza leo Yanga sana ni Hussein Javu.
Kocha Muingereza wa Azam, Stewart John Hall atatakiwa kutorudia makosa mawili makuu aliyoyafanya msimu uliopita hata yakachangia kumkosesha ubingwa.
Alifungwa na Yanga SC 1-0 katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu kwa sababu siku hiyo alimjaribu kiungo Kipre Michael Balou katika beki ya kulia, badala ya kupanga beki halisi.
Akafungwa na Simba SC katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu pia msimu uliopita kwa kosa la kujaribu mfumo ambao wachezaji hawakuwa wamuelewa vyema na hizo ndizo pointi sita zilizowapa Yanga ubingwa.
Burudani inatarajiwa kuwa nzuri katika mchezo leo, kutokana na ukweli kwamba pande zote zina mafundi na wataonyeshana kazi uwanjani.
Upande wa Azam, langoni anaweza kusimama Aishi Manula badala ya Mwadini Ally, kulia Erasto Nyoni, kushoto Waziri Salum na katikati Aggrey Morris na Joackins Atudo. Himid Mao anaweza kuanza katika kiungo cha chini badala ya Balou na juu yake bila shaka atacheza Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Kulia anaweza kucheza Kipre Tchetche, kushoto Khamis Mcha ‘Vialli’ na John Bocco ‘Adebayor’ akaanza katika ushambuliaji na Ibrahim Mwaipopo.
Gaudence Mwaikimba ni mchezaji anayetarajiwa sana kutokea benchi leo kipindi cha pili kuja kujaribu kuisulubu timu yake ya zamani, Yanga SC.
Yanga SC hapana shaka Ally Mustafa ‘Barthez’ ataendelea kusimama langoni, Juma Abdul atacheza kulia badala ya Mbuyu Twite, kushoto David Luhende badala ya Oscar Joshua, katikati kama kawaida Kevin Yondan na Nadir Haroub ‘Cannavaro’- Athumani Iddi ‘Chuji’ ataanza badala ya majeruhi Frank Domayo na juu yake anaweza kucheza Haruna Niyonzima.
Kwa kuwa washambuliai ni wengi kwa sasa Yanga, kiungo kulia na kushoto wanaweza kuenea wao tu. Kulia anaweza kucheza Simon Msuva na kushoto Hamisi Kiiza, wakati washambuliaji wanaweza kuanza Didier Kavumbangu na Jerry Tegete, Javu akianzia benchi. 

MABINGWA WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:
Mwaka Mshindi            Matokeo     
2001: Yanga SC 2-1 Simba
2009: Mtibwa Sugar 1-0 Yanga SC
2010: Yanga SC 0-0 Simba (3-1penalti)
2011: Simba SC   2-0 Yanga
2012: Simba SC 3-2 Azam FC
 
;Chanzo, Binzuberyblogspot.com
0 comments

MKUTANO WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA TANGA ULIOFANYIKA LEO

 MWENYEKITI WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA TANGA HASSAN HASHIMU AKITOA MAELEZO KWA WAJUMBE HAWAPO PICHANI, KTK KIKAO CHA WANACHAMA WA CHAMA HICHO.



        MUSA LABANI AKIFUATILIA KIKAO CHA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI






 MWENYEKITI WA TANGA PRESS CLUB HASSAN HASHIMU AKITOA MAELEZO


BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI WAKIFUATILIA MAELEZO KUTOKA KWA MWENYEKITI WA TANGA PRESS CLUB HAYUPO PICHANI


0 comments

KATIBU MKUU WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) DK SLAA AKIHUTUBIA JANA JIJINI TANGA





0 comments

PICHA MBALIMBALI ZA MKUTANO WA CHADEMA ULIOFANYIKA JANA MKOANI TANGA

                                            
                KATIBU MKUU WA CHADEMA DK WILBROD SLAA AKIHUTUBIA JANA KWENYE
                 WA TANGAMANO JIJINI TANGA.


               DK SLAA AKIWASHA MOTO JANA KTK UWANJA WA TANGAMANO JIJINI TANGA


0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger