Featured Post Today
print this page
Latest Post

Mashindano ya Ngalawa yafana Tanga

Mashindano ya Ngalawa yafana Tanga

 

 Ngalawa zikiwa katika mstari kwa ajili ya kuanza mashindano katika pwani ya Kijiji cha Kigombe wilayani Muheza.

Na Mwandishi Wetu, Muheza
Mashindano ya ngalawa yaliyofanyika jana Wilayani Muheza katika Kijiji cha Kigombe yamefana huku Kampuni ya simu ya ZANTEL  ikifanikisha kwa kutoa zawadi .

Kutokana na hali hiyo Mbunge wa Viti Maalum Amina Mwidau (CUF), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mashindano hayo amewataka vijana washiriki katika michezo badala ya kukaa vijiweni.
 
Kauli hiyo aliitoja wakati  akifungua mashindano ya kwanza ya Ngalawa mkoani Tanga yaliyofanyika kwenye Pwani ya Kijiji cha Kigombe wilayani Muheza.

 Mwidau alisema kupitia michezo vijana wataweza kupata fursa nyingi ikiwemo elimu na ujunzi kutoka kwa wenzao ,burudani pamoja na kujenga afya za kimwili na kiakili.

 “Mahindano haya ya Ngalawa hapo awali yalikuwa yanafanyika ngazi ya kijiji lakini kupitia kwa wadhamini Kampuni ya simu ya ZANTEL tumeweza kuyafanya kimkoa kwa lengo la kuibua fursa za ajira kwa vijana na kwashirikisha watu katika michezo, ”alisema Mwidau.

 Nae Meneja mauzo wa  ZANTELTanzania  Salum Ngururu,  alisema kuwa  lengo la kudhamini mashindano hayo ni kurudisha faida wanayopata kwa jamii kutoka na huduma zake na kuendelea kuwatambulisha bidhaa zinazotolewa na kampuni hiyo.

Alisema ZANTEL itakuwa ikiboresha zawadi za mashindano hayo kila mwaka ili yaweze kuvuta washiriki wengi.

Mshindi wa kwanza alijipatia kitita cha Shilingi laki tatu, kikombe cha ushindi pamoja na medali za dhahabu. Katika mashindano hayo mshindi wa kwanza aliibuka ambaye aliweza kujinyakuliwa zawadi hiyo.

Mashindano hayo yalishirikisha jumla ya Ngalawa thelathini zilizokuwa na washiriki watano ambapo washiriki walitoka katika Wilaya za Tanga, Pangani na Muheza huku Wilaya ya Mkinga ikishindwa kushiriki kutokana na kushindwa kufanya maandalizi mazuri.
0 comments

Mvutano juu ya kusudio la kijiji cha Misima, wilayani Handeni mkoani Tanga kuingizwa kwenye Halmashauri ya Mji wa Handeni

Mvutano juu ya kusudio la kijiji cha Misima, wilayani Handeni mkoani Tanga kuingizwa kwenye Halmashauri ya Mji wa Handeni

Mjadala huu umeandikwa na mwananchi wa kijiji cha Misima, Rashid Hassani Kilo, kama alivyouweka katika ukurasa wake wa facebook.

Rashid Hassan Kilo, mchambuzi wa mjadala huu. Umewekwa hapa ili kuwapa fursa wananchi wote kusoma mawazo haya na namna mchakato huo wa Misima kuingizwa kwenye Halmashauri ya Mji wa Handeni, wilayani humo mkoani Tanga. Hata hivyo, serikali kwa kupitia Mkurugenzi wa Mji wa Handeni, Thomas Mzinga, alituthibitishia blog hii kuwa mchakato huo ulifuata sheria zote na ni sehemu ya kimaendeleo ya wilaya nzima.

Habari za mchana huu wana Handeni? Kwa niaba ya watu wa kijiji cha Misima, nauleta kwenu mjadala wa uthibitisho kuwa Kijiji cha Misima hakikushirikishwa kabisa ktk mchakato mzima wa kuwa ndani ya Halmashauri ya mji wa Handeni.

Ni kwamba mnamo 23/04/2009, kupitia TBC-TAIFA, taarifa ya habari ya saa 2 usiku tumesikia tarifa juu ya kijiji chetu kuwa miongoni mwa vijiji vinavyounda mji wa Handeni.

Hatubishi kuwa ni maendeleo ila si mnakaa na kutathmini faida zake na hasara zake ili mizani izidi kwenye faida? Leo huu mkutano uliotoa muhtasari huo umefanyika wapi?

Tar 26/04/2009, majira ya saa 2 usiku tukatafutana watu kama 6 kwenda nyumbani kwa mw/kiti wa kijiji wakati huo mzee ZAKARIA MOHAMMED DOYO, kumuuliza juu ya taarifa hizi, nae alikiri kusikia radioni ila hajui imekuwaje? Lkn akatuahidi kuitisha mkutano 01/05/2009 ili tujadiliane. Tumesubiri hakuna kilichofanyika zaidi ya yy kutorokea kwenye migodi ya madini ya MOHAMMED ADAM HADJI.

Ilipofika tarehe ya ahadi bila mafanikio tukaenda kwa mw/kiti wa ccm kata ya Misima ili amshurutishe baada ya kukutana nae akamwambia ataitisha mkutano huo 06/05/2009, lakini pia hakuitisha. Wakati wote yakifanyika haya hatukuwa na kumbukumbu tukaona sasa tundikane wengi na tifuate taratibu na kuchagua watu wachache watakao fuata ngazi husika, ktk watu waliochaguliwa nilikuwa mmoja wao.

Tarehe hiyo hiyo 6 tukaandika barua kwenda kwa WEO yaani mendaji kata wakati huo Ndg. ISMAIL MROPE ili amshurutishe VEO wakatio huo Bw. MAULID ISMAIL YUSUF amshauri mwenyekiti waitishe mkutano. Kweli WEO aliandika barua yenye Kumb. Na. WEO/MD/VOL-II/08/09 ilikuwa 08/05/2009, yenye anuani YAH: KUITISHA MKUTANO MAALUM WA KUFAFANUA AGENDA YA KIJIJI CHA MISMA KUINGIA KTK MAMLAKA YA MJI HANDENI SIKU YA 13/05/2009 saa 8:00 alasiri.

Angalia jibu la mwenyekiti katka barua yenye KUMB. NA. SER/KIJ/MS/VOL-1/09 na anuani isemayo YAH: KUTOITISHA MKUTANO MAALUM WA KUFAFANUA AGENDA YA KIJIJI CHA MISMA KUINGIA KTK MAMLAKA YA MJI SIKU YA 13/05/2009 saa 8:00 alasiri.
Sababu za kutoitisha mkutano huo ni kwamba sijawahi kutoa ahadi kwa watu eti niwaitishie mkutano wa hadhara kwa ajili ya kuzungumzia agenda ya mji. Kwa kawaida mikutano huandaliwa na serikali si kwa mamlaka ya watu wachache. "Japo ilikuwa inaendelea ila point mmeziona" Mwisho akatia sahihi na kuandika jina lake ZAKARIA MOHAMMED DOYO.

Baadae zikatokea hujuma hali iliyopelekea mtendaji kata kuhamishwa haikuishia hapo mw/kiti wetu alienda hadi kituoni ili tujetukamatwe lakini polisi wanajua kazi yao kwani hakuwa na sababu za msingi wakampuuzia.

Tulipita ngazi hadi mkowani bahati mbaya mkuu wa mkowa kipindi kile Ndg. SAID KALEMBO hatukumkuta na kuacha barua yetu wakati huo wakuu wa mikowa wote waliitwa bungeni.

Hata hivyo baada ya kuipata alikuja mpaka Handeni na kucha maagizo kwa mkuu wa wilaya wakati huo Ndg. SEIF MPEMBENWE nae akafanya nasi mkutano na akaomba mchakato wetu uishie mkowani na kutoa maagizo mkutano uitishwe na akaniomba nimpe barua za madai yetu, nilipiga copy asubuhi yake baada ya mkutano yaani 29/06/2009 nilimpelekea na kumkabidhi ofisini kwake.

Katika mlolongo wote huu hakuna hata siku moja tumekaa mkutano na kulijadili hili. Na hata huo muhtasari wa sisi kuomba ni wa kughushi na sahihi za majina waliitwa wanafunzi wa Misima Sekondari ndio walio saini. Maana muhtasari ulioko huko eti Misima tumeomba wenyewe!

Na sababu ya viongozi kufanya hivyo baada ya wao kuiuza ardhi ya Misima, sasa mnapotawaliwa na sheria ya mji, ardhi si mali ya mkutano mkuu wa kijiji ila ni mali ya kamishna wa ardhi wa mji na si kwa kulima na kufuga ila mipango miji tena. Jamani nina mengi hapa hayatoshi ila siku moja nitakuja unguruma kwenye vyombo husika labda waniuwe mapema kwa kutetea haki ya vizazi vya Misima na uridhi wao pekee ambao ni ardhi tu, uliobaki! Vingine vyote vimeporwa! Mchana mwema.
0 comments

Lembeli: Serikali iondoe VAT vifaa vya mradi

Lembeli: Serikali iondoe VAT vifaa vya mradi 

 

MWENYEKITI  wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya  Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli, ameishauri serikali kuondoa kodi  kwenye vifaa vya  mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu unaoendeshwa na Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), ili kumuwezesha mwananchi wa hali ya chini kuondokana na makazi duni.
Lembeli alitoa kauli hiyo  juzi baada ya  taarifa ya mradi huo iliyosomwa mbele ya kamati hiyo na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa shirika hilo, Benedict  Kilimba na kueleza kuwa kodi za serikali zimesababisha  bei ya nyumba hizo kuwa kubwa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mfumo wa kuwataka  wanunue  vifaa vya ujenzi  kwenye maduka maalumu umeongeza  gharama ya ujenzi huo na kufikia sh milioni 31.3 kwa nyumba  yenye vyumba viwili na sh milioni 35.3 hadi milioni 36.2 kwa nyumba yenye vyumba vitatu bila Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Kilimba alisema mbali na changamoto hizo,  shirika pia linalazimika kuilipa serikali sh milioni 7  hadi 10  kama VAT kutokana  na  manunuzi ya vifaa vya ujenzi wa kila nyumba, jambo lililosababisha kuuzwa sh milioni 40.7  kwa  nyumba ya vyumba viwili na sh milioni 46.3 hadi  milioni 48.2  kwa vyumba vitatu.
Akizungumza baada ya taarifa hiyo, Lembeli alisema ni wajibu sasa kwa serikali kuonyesha moyo wa dhati katika kuwawezesha wananchi kumudu kubadilisha maisha yao ikiwemo la makazi bora ambayo ni haki ya kila mtu.
Aliahidi kubeba jukumu la kuishauri serikali kuondoa VAT  kwenye  vifaa vya ujenzi wa nyumba zinazojengwa na mradi wa shirika hilo, hasa zile zilizolengwa kwa ajili ya  makazi bora kwa watu wa hali ya chini.
0 comments

MADEREVA DALADALA ZA MIKANJUNI TANGA WATOA LA MOYONI KWA HALMASHAURI YA JIJI

MADEREVA DALADALA ZA MIKANJUNI TANGA WATOA LA MOYONI KWA HALMASHAURI YA JIJI


Madereva  wa daladala  ziendazo mikanjuni,Mwahako,Magomeni  na  Tanga Beach  Mkoani hapa   wameushukuru  uongozi  wa Halmashauri  ya Jiji la  kwa kuwa tengenezea  vituo viwili vyakuegeshea magari  katika maeneo ya mabanda ya Papa  pindi wanapo subiri abiria


Mwandishi  wa matukiodaima.com Tanga Bw Dominic Joseph Maro anaripoti  zaidi  kuwa 

Wakizungumza  na kituo hiki  Madereva hao wamesema  vituo hivyo vimewa saidia kupunguza msongamano wa magari, Baiskeli pamoja  na wafanyabiashara  mbali mbali katika maeneo hayo.

Aidha wamesema hapo awali  walikuwa hawana kituo maalum cha kuegeshea  magari hali ambayo ilikuwa ikiwasababishia kazi yao kuwa ngumu kutokana msongamano uliokuwa ukiwapa changamoto kubwa katika kazi yao.


Pamoja na hayo wametoa  ushauri kwa Madereva wenzao ambao wanaendesha vyombo moto kuhakikisha wanavitumia vizuri vituo hivyo  vipya ili  kusaidia kudumu  kwa muda mrefu na itawafanya wafanye kazikwa wepesi pia ni salama kwa  habiria vili ni msada kwa watumiaji wengine.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger