Featured Post Today
print this page
Latest Post

RC GALLAWA AKABIDHI ZAWADI ZA KRISMAS NA MWAKA MPYA ZILIZOTOKA KWA JK KWA MAKAZI YA WAZEE WASIOJIWEZA MISUFINI MUHEZA.

RC GALLAWA AKABIDHI ZAWADI ZA KRISMAS NA MWAKA MPYA ZILIZOTOKA KWA JK KWA MAKAZI YA WAZEE WASIOJIWEZA MISUFINI MUHEZA.                    

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKISALIMIANA NA WAZEE WASIOJIWEZA WANAOISHI KATIKA KITUO CHA MSUFINI KATA YA NGOMENI WILAYANI MUHEZA LEO WAKATI ALIPOKWENDA KUKABIDHI ZAWADI ZA KRISMAS NA MWAKA MPYA ZILIZO TOKA KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE LEO

MKUU WA WILAYA YA MUHEZA,SUBIRA MGALU AKIZUNGUMZA WAKATI WA MAKABIDHIANO HAYO LEO KABLA YA KUUMKARIBISHA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA.

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIZUNGUMZA NA WAZEE WA KITUO HICHO BAADA YA KUKABIDHI ZAWADI HIZO.

BAADHI YA VITU ALIVYOKABIDHI MKUU WA MKOA WA TANGA.

MKUU WA MKOA WA TANGA KULIA ALIYEINAMA AKIMKABIDHI MWENYEKITI WA KITUO HICHO JUMA BAKARI ZAWADI ZILIZOTOLEWA NA MH.RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA AJILI YA SIKUU YA KRISMAS NA MWAKA MPYA

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KULIA AKISISITIZA JAMBO MARA BAADA YA KUKABIDHI ZAWADI HIZO KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA MUHEZA,SUBIRA MGALU.


ZAWADI ZA MBUZI ZILIZOKABIDHIWA KWENYE KITUO CHA KULELEA WAZEE WASIOJIWEZA CHA MSUFINI KATA YA NGOMENI WILAYANI MUHEZA AMBAZO ZILITOKA KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANI WA TANZANIA,DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE.PICHA ZOTE NA MBARUKU YUSUPH MUHEZA.

 MKUU wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa leo amekabidhi zawadi za sikukuu ya Krismas na mwaka mpya kutoka kwa Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanga Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika eneo la makazi ya wazee wasiojiweza la Misufini kata ya Ngomeni wilayani Muheza

Zawadi zilizokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa Gallawa ni mchele kilo 150,mbuzi watatu(3) na Mafuta ya Chakula lita 40,michezo ya sabuni pamoja na katoni moja y chumivi vyote vikiwa na thamani ya sh.615,000.


Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi hizo, Gallawa ametoa wito kwa kila mwananchi kuweka utaratibu wa kusaidia wale wote ambao hawana uwezo na wenye shinda hasa katika kipindi hiki cha sikukuu ya krismas na mwaka mpya kama alivyofanya Mh.Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Aidha amewataka wananchi kushehereka sikukuu ya krismas na mwaka mpya kwa amani na utulivu kwa kuweka msisitizo kuwa wajiepueshe na vitendo vyovyote vya uvunjifu wa amani.

Mkuu huyo wa mkoa amewataka wananchi kutoa taarifa kwa vyombo vya husika pindi wanapoona katika maeneo yao kuna viashiria vya uvunjifu wa amani ikiwemo kuliweka jiji la Tanga katika hali ya usafi .

Wakati huo huo, Mkuu huyo wa mkoa ameaswa kuacha kuendesha magari mwendo kasi hasa katika kipindi cha sikukuu ya krismas na mwaka mpya kutokana na kuwa wananchi wengi hutumia vyombo vya usafiri kwenda mapumzikoni .
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger