Featured Post Today
print this page
Latest Post

MKWASA AWATEMA MWADINI, BANDA NA TSHABALALA STARS KILA MMOJA NA SABABU ZAKE, WENGINE WAGONJWA

MKWASA AWATEMA MWADINI, BANDA NA TSHABALALA STARS KILA MMOJA NA SABABU ZAKE, WENGINE WAGONJWA


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari leo mchana ofisi za TFF, Uwanja wa Karume                                                                                 
Wachezaji Said Ndemla (kulia) na Simon Msuva (kushoto) wakiwa kwenye basi lao tayari kwa safari ya Uwanja wa Ndege      

 
 KOCHA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa amewaengua wachezaji watano katika kikosi chake kinachoondoka leo jioni kwenda Kampala kumenyana na wenyeji, Uganda mwishoni mwa wiki. 
Stars itakuwa mgeni wa Korongo wa Uganda Jumamosi Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza kuwania tiketi ya kucheza michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2016 Rwanda.
Na Mkwasa amewaengua beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na kiungo Abdi Banda wote wa Simba SC kwa sababu ni majeruhi, wakati Samuel Kamuntu wa JKT Ruvu na Andrew Vincent wa Mtibwa Sugar wameachwa kwa sababu za kiufundi na Mwadini Ally wa Azam FC ni mgonjwa.
 
Mkwasa ameteua wachezaji 20 wanaoondoka jioni ya leo kwenda Kampala, ambao ni makipa; Mudathir Khamis (KMKM) na Ally Mustafa ‘Barthez’ (Yanga), mabeki ni Juma Abdul (Yanga), Shomary Kapombe (Azam), Michael Aidan (Ruvu Shooting), Mwinyi Hajji Mngwali (KMKM), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga SC), Kevin Yondan (Yanga SC) na Hassan Isihaka (Simba SC).
Viungo ni Mudathir Yahya (Azam FC), Salum Telelea (Yanga SC), Frank Domayo (Azam FC), Simon Msuva (Yanga SC), Said Ndemla (Simba SC), Ramadhani Singano ‘Messi’ (Simba SC) na Deus Kaseke (Mbeya City).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam FC), Atupele Green (Kagera Sugar), Rashid Mandawa (Kagera Sugar) na Ame Ali (Mtibwa Sugar).
Mara baada ya kuteuliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kurithi mikoba ya Mholanzi, Mart Nooij aliyefukuzwa mwishoni mwa wiki kufuatia kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Uganda katika mchezo wa kwanza na Uganda, Mkwasa alitaja kikosi wachezaji 26 na kuwa nacho kambini kwa wiki moja hoteli ya Kiromo, Bagamoyo huku mazoezi akifanya uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam.
Mbali na wachezaji hao, benchi la Ufundi litaongozwa na Mkwasa, Mshauri wake wa Ufundi, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’, Msaidizi wake Hemed Morocco, kocha wa makipa, Manyika Peter, Mtunza Vifaa Hussein Swedi ‘Gaga’, Meneja Omar Kapilima pamoja na Mratibu Msafiri Mgoyi. Stars inatakiwa kushinda 4-0 Jumamosi ili kusonga mbele CHAN
0 comments

JK ASHUHUDIA KUSIMIKWA CHIFU KINGALU WA 15 KIJIJINI KINOLE.

JK ASHUHUDIA KUSIMIKWA CHIFU KINGALU WA 15 KIJIJINI KINOLE.


01

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia kusimikwa kwa Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 katika kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 3, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki jana Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa leo kijijini hapo.

02

Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 akitolewa nje baada ya kusimikwa rasmi kuwa kiongozi wa kabla hilo kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 3, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki jana Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa leo kijijini hapo.

03

Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 akichomeka fimbo yake ya Uchifu kabla ya kuketi  meza Kuu na Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kusimikwa rasmi kuwa kiongozi wa kabla hilo kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 3, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki jana Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa leo kijijini hapo.
PICHA NA IKULU
0 comments

MBUNGE WA JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI-CHADEMA JOSHUA NASSARI AMALIZA MIKUTANO YA KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA KWA KUTUMIA CHOPA

Rubani wa Helkopta akimfunga mkanda Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassar kabla ya kuanza safari ya kuelekea katika mikutano ya hadhara ya kuhasisha wananchi kujitokeza kujinadikisha katika daftarai la kudumu la wapiga kura.
Wananchi katika kata ya King'ori wakimpokea Mbunge Nassari wakati alipowasili katika mkutano wa hadhara wa uhamasishaji zoezi la uandikishaji .
Kada wa Chadema ,Samwel Nnko akizunumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya King'ori .
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari ,akiwa na mtoto aliyevalia fulana iliyoandikwa Dogo Janja jina ambalo Nassari alipewa mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi uliompatia Ubunge,
Mbunge Nassari akiwahutubia wananchi katika kata ya King'ori jimbo la Arumeru Mashariki akihamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Ng'arenanyuki waliofika katika mkutano wa hadhara wa uhamasishaji juu ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la kupiga kura .
0 comments

WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUUNDA KITENGO MAALUMU

WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUUNDA KITENGO MAALUMU


Na Peter Mtulia
Msimamizi wa masuala ya ushiriki wa watanzania wa wizara ya nishati na madini Neema Apson akizungumzia jinsi wizara ya nishati na madini inavyoshiriki katika kuhakikisha taarifa zinawafikia wananchi kwa usahihi kuhusiana na mafuta na gesi katika ukumbi wa mikutano wa British Cancil jijinin Dar es Salaam leo. pia wizara hiyo itaunda kitengo maalumu kwaajili ya kusimamia masuala ya gesi na mafuta na kuwajulisha wananchi kushiriki vyema katika nishati zitolewazo hapa nchini.

Mkuu wa Biashara wa British Concil Hugh Penrhyn Jones akizungumza katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa British Cancil jijinin Dar es Salaam leo.

 Mratibu wa kitengo cha uwajibikaji wa makampuni na mazingira-kituo cha sheria na haki za binadamu,Wakili Flaviana Charsles akiuliza swali katika mkutano wa kujadili masuala ya mafuta na gesi pamoja na changamoto zake kwa jamii katika mkutano uliofanyika ukumbi wa mikutano wa British Cancil jijinin Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya wadau wa maendeleo ya mafuta na gesi wakimsikiliza mtoa maada katika ukumbi wa mikutano wa British Cancil jijinin Dar es Salaam leo.(Picha na Avila Kakingo)
1 comments

WIZARA YA UCHUKZI WAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA CHINA

WIZARA YA UCHUKZI WAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA CHINA


Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Uchukuzi Tanzania, Bw. Gabriel Migire (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa uongozi wa Wizara na ujumbe kutoka Kiwanja cha ndege cha Guang Dong kutoka nchini China, wakati ulipotembelea Wizara ya Uchukuzi, leo asubuhi. Ujumbe umeonyesha nia kuwekeza katika Viwanja vya Ndege vya Tanzania. (Habari Picha Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi).                                                                               

 Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Uchukuzi Tanzania, Bw. Gabriel Migire (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanja cha Guang Dong cha nchini China, Bw. Wen Wenxing wakati ujumbe huo ulipokutana na uongozi wa Wizara ya Uchukuzi, leo asubuhi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanja cha Ndege cha Guang Dong cha nchini China, Bw. Wen Wenxing (kushoto), akimpatia zawadi Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Uchukuzi Tanzania, Bw. Gabriel Migire, leo asubuhi baada ya ugeni huo kukutana na uongozi wa Wizara ya Uchukuzi leo asubuhi.
0 comments

Coastal Union yajiandaa na mechi ya Ligi kuu dhidi ya Polisi Morogoro itakayochezwa Jumatano wiki ijayo

Coastal Union yajiandaa na mechi ya Ligi kuu dhidi ya Polisi Morogoro itakayochezwa Jumatano wiki ijayo

unnamed
Kocha Mkuu wa Coastal Union,Jamhuri Kihwelu “Julio”  (kulia) akisisitiza jambo kwa wachezaji wa timu hiyo mara baada ya
kumalizika mazoezi yao juzi kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao ya Ligi kuu dhidi ya Polisi Morogoro itakayochezwa Jumatano wiki ijayo kwenye uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.
Picha kwa Hisani ya Coastal Union.
0 comments

Rais Zuma awatembelea waathirika wa ghasia

Rais Zuma awatembelea waathirika wa ghasia

Südafrika Präsident Jacob Zuma
Rais Jacob Zuma wa Afrika kusini

Rais Jacob Zuma wa Afrika kusini amewaomba raia wa kigeni kubakia nchini humo wakati wakati akikatisha ziara yake ya kiserikali nchini Indonesia kushughulikia wimbi hilo la chuki dhidi ya wageni. 

Wiki tatu za ghasia zinazoongezeka dhidi ya wageni nchini Afrika kusini zimesababisha kiasi watu sita kuuwawa na kuwalazimisha wahamiaji 5,000 kutafuta hifadhi katika makambi ya muda.
Machafuko hayo , ambayo yameanzia katika mji wa mashariki wa bandari wa Durban kabla ya kusambaa katika maeneo mengine ya nchi hiyo, yanabeba ghasia za hisia za chuki dhidi ya wageni ambazo ziliikumba Afrika kusini mwaka 2008 wakati watu 62 walipouawa.
Xenophobie in Südafrika Raia wa Afrika kusini akishikilia bango linalosema "tupinge chuki dhidi ya wageni".
Katika tukio la hivi karibuni kabisa, polisi jana Jumamosi(18.04.2015) wamesema wageni waliouwawa wamefariki kutokana na kuchomwa visu mjini Alexandra , mji ulioko kaskazini mwa Johannesburg. Eneo hilo linaloishi watu masikini limekuwa lengo ya ghasia nyingi katika siku hiyo, ambapo maafisa wa polisi walifyatua risasi za mipira kuwatawanya watu waliokuwa wakifanya uporaji.
Zaidi ya watu 30 wamekamatwa usiku ya Jumamosi kuzunguka mji wa Johannesburg pekee. Akiwa chini ya mbinyo kuzuwia kurudiwa mauaji yaliyotokea mwaka 2008, Zuma alisafiri kwenda Durban kutembelea kambi wanayohifadhiwa wageni waliokimbia makaazi yao kutokana na ghasia hizo, lakini alikabiliana na mapokezi yasiyokuwa mazuri kutoka kwa kundi lililomsubiri, ambalo lilipaaza sauti, "rudi nyumbani, rudi nyumbani" na umechelewa , umechelewa".
"Kama serikali , hatuwaambii nendeni zenu". Sio kila raia wa Afrika kusini anasema , nendeni zenu". Ni idadi ndogo sana ya watu ambao wanasema hivyo," Zuma amesema katika kambi ya Chatsworth, ambako alikabidhi hundi ya dola 4,100 kuwasaidia wahanga wa ghasia za chuki dhidi ya wageni.
Ameahidi kumaliza ghasia hizo na alilihakikishia kundi hilo la watu kwamba kuna nafasi kwa wageni nchini Afrika kusini. "Hata kama kuna wale wanaotaka kurejea nyumbani, wafahamu kwamba wakati tutakapositisha ghasia wanakaribishwa kurejea, " Zuma amesema.
Gewalt gegen Ausländer in Südafrika geht weiter Mkaazi wa Afrika kusini akiwa na gongo na ngao tayari kwa mapambano na wageni
Zuma afuta ziara
Kiongozi huyo wa Afrika kusini alitarajiwa kusafiri kwenda Indonesia jana Jumamosi, lakini alitangaza kufuta ziara hiyo "kushughulikia suala hilo nyumbani linalohusiana na mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni."
Uamuzi huo umekuja wakati hali ya tahadhari inaongezeka nchini Afrika kusini---na kutoka Umoja wa Mataifa pamoja na miji mingine mikubwa-- kuhusiana na mashambulio hayo.
Nchi jirani za Zimbabwe , Malawi na Msumbiji zimetangaza mipango ya kuwaondoa raia wake. Ikiakisi wasi wasi wa kimataifa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi UNHCR limesema wahanga wengi walioshambuliwa, "ni wakimbizi na wanaohitaji hifadhi ya kisiasa ambao wamelazimika kukimbia nchi zao kutokana na vita pamoja na kukamatwa."
Kinachoelekezewa kidole cha lawama kwa kiasi kikubwa kutokana na ghasia hizo ni hotuba mwezi uliopita iliyotolewa na mfalme Goodwill Zwelithini, kiongozi wa kabila la Wazulu, ambapo amewalaumu wageni kutokana na kiwango cha juu cha uhalifu nchini Afrika kusini na kusema ni lazima"wafunge virago na kuondoka".
Südafrika Fremdenfeindliche Ausschreitungen Mhamiaji akikimbia wakati polisi akijaribu kuzuwia ghasia hizo
Mfalme huyo amekuwa akisema maneno yake yametafsiriwa vibaya.
Wakati mzozo huo ukiendelea, Zuma ameyataka makanisa yote kufanya sala maalum kwa ajili ya amani na urafiki leo Jumapili.
"Tunafahamu kwamba wengi wa watu wetu wanaamini kuhusu haki za binadamu na amani na kwamba wanaheshimu utu wa kila mtu anayeishi katika nchi hii," amesema katika taarifa iliyotolewa jana Jumamosi.
"Wanafahamu kwamba mahali palipo na hali ya wasi wasi na tofauti, haya yanaweza kutatuliwa kwa njia ya Afrika kusini, kupitia majadiliano, na sio kupitia ghasia na ukandamizaji."
Hasira miongoni mwa mataifa jirani na Afrika kusini
Ghasia hizo zimezusha hasira katika mataifa mengine ya Afrika.
Nchini Msumbiji kundi la watu wapatao 200 siku ya Ijumaa lilizuwia kivuko cha kusini kati ya nchi hizo cha Lebombo, wakirusha mawe dhidi ya magari ya Afrika kusini.
Südafrika Fremdenfeindliche Ausschreitungen Kundi la raia wa kigeni likijaribu kujilinda
Nchini Zambia , redio inayomilikiwa na mtu binafsi ilisitisha kupiga muziki wa Afrika kusini katika hatua ya kupinga mashambulizi hayo dhidi ya wageni. Na katika mji mkuu wa Zimbabwe Harare, waandamanaji walifika katika ubalozi wa Afrika kusini kulaani kile walichokiita "mauaji ya kiwendawazimu na ya kikatili" dhidi ya Waafrika wenzao.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe pia amelaani ghasia hizo siku ya Jumamosi, akielezea "hali ya kushitushwa na kuchukizwa".
0 comments

Ghala lenye dawa zilizopigwa marufuku na zilizokwisha muda limekamatwa Mwanza.

Ghala lenye dawa zilizopigwa marufuku na zilizokwisha muda limekamatwa Mwanza.


Maofisa zaidi ya 30 kutoka mamlaka ya chakula na dawa na baraza la Famasi Tanzania wamekamata ghala lenye dawa za serikali,zilizopigwa marufuku na zilizokwisha muda wake wa matumizi zenye thamani ya shilingi milioni 97 zikiwa zinamilikiwa na mfanyabiashara wa jijini mwanza CHARLES MBUSIRO kinyume cha sheria.
Ghala hilo lililopo eneo la ilemela jijini mwanza limekutwa likiwa limesheheni zaidi ya 120 za dawa ambazo ni sawa na tani 42 zikiwemo dawa za serikali za Kenya na Uganda, dawa za misaada, dawa zilizopigwa marufuku nchini kama vile klorokwini ya sindano, amodiaquine na gripe water -dawa nyingine zilizokutwa ndani ya ghala hilo na kwenye duka lake la dawa lililopo Natta barabara ya nyerere ni pamoja na ambazo hazijasajiliwa na TFDA na azisizoruhusiwa kuuzwa kwenye maduka ya dawa.
Meneja wa usalama wa dawa wa TFDA Kissa Mwamwitwa ndiye aliyeongoza zoezi hilo liliendeshwa chini ya usimamizi mkali wa askari polisi wenye silaha za moto.
Baadhi ya maofisa wanaotekeleza operesheni hiyo, wakiwemo wanasheria kutoka TFDA na baraza la famasi tanzania pamoja na meneja wa mamlaka hiyo kanda ya kati Florent Kyombo wakizungumzia tukio hilo wamesema taratibu za kisheria zinafanyika ili kumfikisha mahakamani mtuhumiwa.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kahasa ilemela Richard Peter alikuwa shuhuda wakati maofisa hao wa TFDA, baraza la famasi tanzania na askari polisi walipokuwa wakitekeleza zoezi hilo kwenye ghala la dawa ambalo linasemekana bado halijasajiliwa na TFDA huku mmliki wake charles mbusiro akitoroka kwa kuruka ukuta na kutokomea kusikojulikana.(KILONGE)
0 comments

KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO CHAFANYA SHERERE

KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO CHAFANYA SHERERE

Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za kumaliza msimu uliopita na kukaribisha msimu mwingine pamoja na kutoa zawadi kwa wafanyakazi waliotumikia kampuni hizo kwa muda mrefu pamoja na wafanyakazi bora zilizofanyika Kiwandani hapo.Katika Hotuba yake Mkurugenzi Huyo alisema Makampuni hayoyamesaidia Mkoa wa Morogoro kuanza kuinuka kiuchumi kutokana na kutoa ajira za msimu takribani 3000 kila mwaka na kusaidia kupunguza matatizo ya uhalifu yaliyokuwa yakifanywa na vijana wasio kuwa na shughuli  za kujiingizia kipato. 
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akikabidhi zawadi kwa wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu Ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya Miaka 15 Mfululizo.
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akiwapakulia Chakula waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa tafrija hiyo
(kilonge)
Mkurugenzi wa Ufundi wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) Henry Lembert Akiwahudumia wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa Sherehe ya Kufunga Msimu.
 
Mkurugenzi mkuu w David Crowhorst akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda hicho
 Picha ya Pamoja ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda cha Tumbaku  cha Mkoani Morogoro
0 comments

Afariki kwa kugongwa na treni Morogoro

Afariki kwa kugongwa na treni Morogoro


Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kugongwa vibaya na treni wakati akivuka reli na kisha viungo vyake kusambaa katika mtaa wa ujenzi manispaa ya morogoro .
Wakizungumza na ITV mashuhuda wa tukio hilo wamesema marehemu alijulikana kwa jina moja la mangi ambapo wameeleza kusikitishwa na ajali kwakua hii ni mara ya tatu watu kugongwa na treni katika maeneo hayo na kueleza kuwa amarehemu alikua anavuka Reli.
Naye mwenyekiti wa mtaa wa ujenzi Christopha Chales ameelezea tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha tabia ya kupita kwenye njia ya Reli kwani wataendelea kusababisha ajali zisizo za lazima ambazo zingeweza kuepukika.
Askari wajeshi la polisi wamefika katika eneo la tukio na kuchukua mwili wa marehemu ambapo umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro .(KILONGE)
0 comments

HARUSI YA MTOTO WA MIZENGO PINDA ILIVYOMTOA MACHOZI LULU KATIKA HARUSI YAKE JANA

Ikumbukwe kwamba Chrispine Mizengo Pinda na Adeline Ngugi wote wamehitimu pamoja katika chuo cha kimataifa cha Diplomasia kilichopo kurasini jijini Dar es Salaam amabapo walisoma Post Graduate in Management of Foreign Relations.
Bwana Harusi Chrispine Mizengo Pinda akiingia ukumbini wakati wa Sherehe ya ndoa yake na Bi.Adeline iliyofanyaka katika ukumbi wa JK Hall viwanja vya Saba saba Jijini Da r es Salaam Jana.
Marafiki wa karibu wa Chrispine na Adeline waliowakilisha wanafunzi wa chuo cha Diplomasia katika Hrusi hiyo wakifurahi Pamoja walipokuwa katika sherehe hiyo wakiongozwa na Khadija,Hassan ,Zitta,Lulu,Diana,Kennedy,Ngamanya,Mwanakatwe na Glady
Hassan Abbas kutoka ofisi ya Rais Ikulu ambaye ni mkuu wa mawasiliano wa BRN Tanzania akifurahia Jambo na Kennedy Ndosi  katika Harusi Hiyo
Binti huyu mwenye gauni la bluu Lulu Rodgers (katikati) ndiye aliyedaiwa kumwaga chozi kwa furaha baada ya kuona wawili hao ambao ni marafiki zake wakifunga ndoa takatifu jana kwani anasema walikuwa wakitaniana sana kiasi kwamba anaamini ndoa yao itakuwa ya furaha na amani sana..
0 comments

BALOZI WA CHINA TANZANIA ATEMBELEA WIZARA YA ARDHI.

BALOZI WA CHINA TANZANIA ATEMBELEA WIZARA YA ARDHI.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimkaribisha Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing alipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar es salaam na kufanya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China katika masuala ya uendelezaji wa Ardhi na Mipango miji.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (kulia) akimweleza Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing (kushoto) namna Wizara yake inavyoendelea kuimarisha shughuli za Mipango Miji ,Usimamizi na Matumizi endelevu ya Ardhi katika maeneo mbalimbali nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Alphayo Kidata (kushoto) akifurahia jambo wakati akizungumza na ugeni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania ulioitembelea Wizara hiyo leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kuendeleza ushirikiano kati ya China na Tanzania katika Matumizi endelevu ya Ardhi.
Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing akitoa ufafanuzi kuhusu uendelezaji wa ushirikiano kati ya China na Tanzania katika katika sekta ya ardhi hususan utoaji wa mafunzo kwa watalaam wa Ardhi, Matumizi endelevu ya Ardhi na Mipango miji nchini.
0 comments

AJALI NYINGINE YATOKEA JIJINI MBEYA LEO, 10 WADAIWA KUPOTEZA MAISHA

AJALI NYINGINE YATOKEA JIJINI MBEYA LEO, 10 WADAIWA KUPOTEZA MAISHA

Pichani ni Baadhi ya wakazi wa maeneo ya jirani na ilipotokea ajali hiyo wakiiangalia basi hiyo ikiwa kando kando ya mto Kiwira.
Wananchi wa Mji wa Kiwira wakienda kuangalia ajali hiyo.
Sehemu ya wananchi wa Mji wa Kiwira wakiangalia Baadhi ya Miili ya Watu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo.
Taarifa iliyoifikia Globu ya Jamii hivi punde toka Wilayani Rungwe, Jijini Mbeya inaeleza kuwa Basi dogo aina ya Toyota Hiace imetumbukuia kwenye Mto Kiwira mapema leo na inadaiwa kuwa zaid ya watu 10 waliokuwepo kwenye basi hilo wamepoteza Maisha.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa, amesema kwamba ajali hii imetokea wakati Mabasi yafanyayo safari zake kati ya Mbeya na Kyela (maarufu kama Coaster) kugoma kutoa huduma ya kusafirisha abiria katika maeneo hayo, hivyo baadhi ya hiace za mjini kuamua kubeba abiria, hali iliyopelekea hiace hizo kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo wake.
Inaelezwa kuwa gari hiyo ilipoteza muelekea na kuingia mtoni, baada ya dereva wake kushindwa maarifa kutokana na mwendo aliokuwa nao.
Mungu aziweke pema roho za marehemu hao,Amin.(Muro)
0 comments

Matumaini ya amani Ukraine kwa mkutano wa Minsk

Matumaini ya amani Ukraine kwa mkutano wa Minsk


 Mapigano yamepamba moto mashariki mwa Ukraine, kuelekea mkutano wa Belarus, unaowaleta pamoja viongozi wa Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Ukraine. Rais Barack Obama alizungumza na Vladimir Putin kuelekea mkutano huo. 


Kansela Angela Merkel, marais Francois Hollande, Vladimir Putin na Petro Poroshenko wanatarajiwa mjini Minsk baadae siku ya Jumatano, kwa mazunugumzo muhimu juu ya mgogoro nchini Ukraine. Ikiwa mazungumzo hayo yatashindwa kuleta muafaka, vikwazo zaidi vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi vinatarajiwa. Marekani pia inatafakari kulipatia silaha jeshi la Ukraine ikiwa hakutakuwa na hatua zozote katika mazungumzo.
Kabla ya mkutano huo ikulu za White House na Kremlin ziliripoti juu ya mazungumzo kwa njia ya simu kati ya marais Obama na Putin. Kwa mujibu wa Whote House, Obama alisisitiza umuhimu kwa rais Putin kutumia fursa ya mazungumzo ya Minsk kufikia suluhu ya amani. Kremlin ilisema viongozi hao wawili wlikubaliana juu ya haja ya kuwa na suluhu ya kisiasa kwa mgogoro wa ndani wa Ukraine.
Pushilin (kulia) alisema aliwasilisha mapendekezo kwa wawakilishi wa serikali ya Kiev. Pushilin (kulia) alisema aliwasilisha mapendekezo kwa wawakilishi wa serikali ya Kiev.
Ni mapema mno kwa usitishaji mapigano
Wajumbe wa upatanishi kutoka Ukraine, waasi wanaowania kujitenga, Urusi na shirika la usalama na ushirikiano barani Ulaya OSCE, waliweka msingi wa mazungumzo ya leo katika majadiliano ya karibu masaa mawili mjini Minsk jana. Licha ya taarifa za usitishaji mapiagano, ilibainika baadae ni hatua kidogo sana zilizopigwa.
"Ni mapema mno kuzungumzia usitishaji mapigano,"alisema Denis Pushilin, mjumbe wa ujumbe wa wanaotaka kujitenga. Aliongeza kuwa waasi wamewasilisha pendekezo juu ya namna ya kusonga mbele na kwamba walikuwa wanasubiri majibu, bila kubainisha undani wa mapendekezo hayo.
Na taarifa zinazotoka Ukraine zinasema mashambulizi ya waasi yamewauwa wanajeshi 19 wa Ukraine na kuwajeruhi wengine 78 katika mji wa Dibalseve. Mapigano mengine makali jana Jumanne yaliripotiwa kuuwa zaidi ya raia 10 na wanajeshi katika mji wa Kramatasorsk. Wakati mapigano yakiendelea, waziri wa mambo ya nje ya Ujerumani Frank-Walter Steinmeier aliwatolewa mwito wanaohusika kujizuwia wakati wanadiplomasia wakifanya kazi.
"Ukweli kwamba mkutano huo unafanyika siyo uthibitisho wa mafanikio. Ndiyo maana nazisihi, na nazitaraji Moscow na Kiev kuyachukulia kwa uzito, na kutumia nafasi hii, kwa kuzingatia kitisho kilichoko mbele yetu cha mgogoro wa kijeshi," alisema waziri Steinmeier.
Kansela Angela Merkel, rais Francois Hollande walipozungumza na rais Vladimir Putin mjini Moscow. Kansela Angela Merkel, rais Francois Hollande walipozungumza na rais Vladimir Putin mjini Moscow.
Mpasuko barani Ulaya
Mgogoro huo umesababisha mpasuko miongoni mwa mataifa ya Ulaya, na kuitikisa dhana ya mshikamano usiyoyumbishwa wa mataifa ya Atlantic. Ufaransa na Ujerumani zimeweka chini matarajio ya juhudi zao mpya za amani. Rais wa Ufaransa Francois Hollande alisema viongozi hao walikuwa wanaongoza mazungumzo hayo kwa dhamira ya kufanikiwa, lakini bila ya kuwa na uhakika wa iwapo wataweza kutimiza lengo hilo.
Vita hivyo na miaka kadhaa ya rushwa iliyokithiri vimeipeleka nchi hiyo kwenye kingo za kufilisika, ambapo sarafu yake iliporomoka wiki iliyopita. Ukraine inajadiliana mkopo wa uokozi na shirika la fedha la kimataifa IMF, na duru zilisema mkopo huo huenda ukapanuliwa kwa kiasi kikubwa na kuipatia nchi hiyo kiasi cha dola bilioni 40 za msaada.
Mwandishi: Iddi Ssessanga/dpae, rtre,DW
Mhariri: Elizabeth Shoo
0 comments

RAIS KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA JAJI AUGUSTINO RAMADHANI, DAR ES SALAAM

RAIS KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA JAJI AUGUSTINO RAMADHANI, DAR ES SALAAM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitoa heshima za
mwisho kwa mwili wa Marehemu Bibi Bridget Ramadhani, Mama Mzazi wa
Jaji Augustino Ramadhani,  wakati wa mazishi Ijumaa February 6, 2015
huko Kimara King’ongo jijini Dar es salaam. jky2 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakijumuika na
waomboilezaji wengine  katika mazishi ya Marehemu Bibi Bridget
Ramadhani, mama Mzazi wa Jaji Augustino Ramadhani,  wakati wa mazishi
Ijumaa February 6, 2015 huko Kimara King’ongo jijini Dar es salaam.
jky3 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiweka udongo
kwenye kaburi la  Marehemu Bibi Bridget Ramadhani, mama Mzazi wa Jaji
Augustino Ramadhani,  wakati wa mazishi Ijumaa February 6, 2015 huko
Kimara King’ongo jijini Dar es salaam. jky4 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiweka shada
kwenye kaburi la  Marehemu Bibi Bridget Ramadhani, mama Mzazi wa Jaji
Augustino Ramadhani,  wakati wa mazishi Ijumaa February 6, 2015 huko
Kimara King’ongo jijini Dar es salaam.

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger