Featured Post Today
print this page
Latest Post

Mapigano yazuka tena Kongo

Mapigano yazuka tena Kongo

Mapigano yazuka tena Kongo

Mapigano yanayoendelea baina ya waasi wa M23 na wanajeshi wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo katika eneo la Kibati karibu na mji wa Goma, yanatajwa kuwa yamewaathiri raia katika eneo la mapigano. 

Mji wa Goma ulipigwa na mshituko jioni jana, pâle mabomu yalipokuwa yanavurumishwa katika mji huo. Ni kata za Katindo ya kushoto pamoja na Murara ndizo ziliathirika na mabomu hayo. Katika kata la Murara, duru toka machifu wa kata hizo zadokeza, kuwa watu watano ndio walijeruhiwa mukiwemo watoto watatu ambao hali yao ni mahututi.

Ili kuwakinga raia, mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo, Martin Kobler, aliwaamuru wanajeshi wa Umoja wa Mataifa kuhakikisha kuwa wanawalinda raia hao, huku msemaji wa Tume ya Umoja wa Mataifa katika Kongo hasa katika miji ya Beni na Butembo, Moussa Demba Dialo, akipewa muda wa masaa 44 kuondoka eneo hilo. Ilani hiyo imetolewa na mashirika ya kiraia.
Vita vya maneno vimezuka baina ya serikali za Rwanda na DRC. Rwanda kupitia msemaji wa jeshi lake Joseph Nzabamwita imesema kuwa Kongo kwa maksudi ilivurumisha roketi katika ardhi yake, jambo alilolitaja kuwa ni uchokozi mtupu.

Jeshi la UN kwenye tahadhari

Wanajeshi wa Monusco wakilinda amani Kongo  
                Wanajeshi wa Monusco wakilinda amani Kongo
 
Kwa upande wake msemaji wa serikali ya Kongo Lambert Mende Omalanga, ametangaza kuwa, mabomu yaliyoanguka Goma nakusababisha mahafa katika mji huo, yalitokea katika nchi jirani ya Rwanda. Navyo vita vikiwa bado vinaendelea baina ya jeshi la serikali ya DRC na waasi wa M23 katika kijiji cha Kibati, na ilikuwazuia waasi wa M23 kuuteka mji wa Goma pamoja na kuwakinga raia, muwakilishi maalumu wa katibu mkuu wa UN katika DRC Martin Kobler, aliamuru majeshi ya UN kufanya hima ilikuwakinga raia.

Kauli hiyo inatokea, baada ya vituo vya Monusco pamoja na makaazi ya raia kulengwa na mashambulizi. Msemaji wa jeshi la UN katika DRC luteni kanali Félix Basse, akizungumza na redio ya UN Okapi alisema, kuwa tayari jeshi la UN liko kwenyi tahadhari, na kuwa liko tayari kukabiliana na waasi wa M23 ikiwa watasubutu kuusogelea mji wa Goma. "Kwa kweli tumezidisha mipango yetu ya ukingo na tumekuwa tukipiga doria katika viunga vya mji wa Goma na upande wa Sake, na huko Munigi tumeongeza idadi ya wanajeshi wetu, na Tuko tayari kukabiliana na waasi wa M23 ikiwa watasubutu kuelekea katika mji wa Goma," alisema Basse.

Wakati huo huo mashirika ya kiraia katika mji na wilaya ya Beni, yamempatia muda wa ma saa arubaini na nane, msemaji wa Monusco katika DRC hasa katika miji ya Beni na Butembo Bwana Moussa Demba Dialo. Mashirika ya kiraia katika mji na wilaya ya Beni, yamemupatia ma saa arubaini na nane kuondoka eneo hili. Na ikiwa hatatii amri ya mashirika ya kiraia, kwa madhara yatakayotokea atajijuwa mwenyewe.
Msemaji wa Monusco katika miji ya Beni na Butembo, anashukiwa na mashirika ya kiraia kuwatusi na kuita hatua yao yakutaka magari ya UN kutozunguka katika mitaa ya Beni kuwa ya utoto, na kuwa haikuathiri tume ya UN katika kazi zake.

 

0 comments

Washauri wa rais Obama wakutana kuijadili Syria

Washauri wa rais Obama wakutana kuijadili Syria

Washauri wa rais Obama wakutana kuijadili Syria

Washauri wa rais Barack Obama watakutana katika ikulu ya Marekani ya White House mwishoni mwa wiki hii kujadili nafasi mbali mbali za nchi hiyo, ikiwa ni pamoja na hatua za kijeshi, dhidi ya serikali ya Syria.
Washauri wa rais Barack Obama watakutana katika ikulu ya Marekani ya White House mwishoni mwa wiki hii kujadili nafasi mbali mbali za nchi hiyo , ikiwa ni pamoja na hatua za kijeshi , dhidi ya serikali ya Syria.
Mjadala huo utahusu iwapo serikali ya Syria ilitumia silaha za kemikali katika shambulio mapema wiki hii.

U.S. President Barack Obama makes a statement about the violence in Egypt while at his rental vacation home on the Massachusetts island of Martha's Vineyard in Chilmark August 15, 2013. REUTERS/Larry Downing (UNITED STATES - Tags: POLITICS)  
                   Rais Barack Obama 
 
Maafisa wa Marekani wamesema jana Ijumaa(23.08.2013) kwamba iwapo rais Obama atashiriki katika mkutano huo , hali inayoonekana kuwa kuna uwezekano , itakuwa kikao chake cha kwanza kamili akiwa na wasaidizi wake wa ngazi ya juu wa sera za mambo ya kigeni tangu shambulio la gesi ya sumu siku ya Jumatano katika kitongoji kimoja mjini Damascus.
Uamuzi bado
Lakini afisa huyo ambaye amezungumza kwa masharti ya kutotajwa jina, ametahadharisha dhidi ya matarajio kuwa uamuzi wowote wa mwisho huenda unaweza kutolewa katika duru hii ijayo ya majadiliano.
Wakati huo huo wizara ya ulinzi inayaweka tayari majeshi yake iwapo rais Barack Obama ataamua kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Syria, amesema waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel siku ya Ijumaa.

WASHINGTON, DC - APRIL 17: Defense Secretary Chuck Hagel testifies during a Senate Armed Services Committee hearing on Capitol Hill, April 17, 2013 in Washington, DC. The committee is hearing testimony from Secretary Hagel on the Defense Departments budget request for FY2014 and beyond. (Photo by Mark Wilson/Getty Images)  
                 Waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel
 
Huku kukiwa na miito kadha ya kujingilia kati kijeshi baada ya utawala wa Syria kutumia kile kinachodaiwa kuwa ni silaha za kemikali wiki hii, makamanda wa jeshi la Marekani wamenajitayarisha kwa uwezekano mbali mbali kwa rais Obama iwapo ataamua kuanzisha mashambulio dhidi ya utawala wa Syria, Hagel amewaambia waandishi habari akiwa katika ndege yake iliyokuwa ikielekea nchini Malaysia.
Lakini amekataa kutoa taarifa zaidi kuhusiana na wapi majeshi ya Marekani yatawekwa pamoja na vifaa huku kukiwa na hali ya kuongezeka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
"Wizara ya ulinzi inawajibu wa kumpa rais uwezekano kwa kila aina ya hali," Amesema Hagel.
epa03363568 USS Blue Ridge, the command ship of the U.S. 7th Fleet, enters a naval base in South Korea's largest port city of Busan amid a welcome by the South Korean Navy, 17 August 2012. The ship arrived in South Korea to join the Ulchi Freedom Guardian (UFG), an annual military exercise between the two nations, set for 20-31 August 2012. EPA/STRINGER SOUTH KOREA OUT +++(c) dpa - Bildfunk+++
 
                        Manowari ya jeshi la Marekani
 
Meli zawekwa katika tahadhari

Amesema wakati afisa wa wizara ya ulinzi akisema kuwa jeshi la majini litapanua uwapo wake katika bahari ya Mediterranean kwa kuweka meli ya nne ikiwa na uwezo wa kubeba makombora.

Kikosi cha sita cha jeshi la Marekani , kikiwa na wajibika katika bahari ya Mediterranean , kimeamua kuibakisha manowari ya USS Mahan katika eneo hilo badala ya kuiruhusu kurejea nyumbani katika bandari ya Norfolk , jimboni Virginia.

Manowari nyingine tatu hivi sasa zimewekwa katika eneo hilo, USS Gravely , USS Barry na USS Ramage. Meli zote nne za kivita zina makombora kadha ya Tomahawk.
Meli hizo za ziada zinairuhusu wizara ya ulinzi kuchukua hatua za haraka iwapo Obama ataamuru shambulio la kijeshi.

"Rais ameitaka wizara ya ulinzi kutoa mapendekezo mbali mbali. Pamoja na hayo , wizara ya ulinzi iko tayari na imekuwa tayari kutoa uwezekano wa aina yoyote kwa rais wa Marekani ," Hagel amesema.
FILE -This undated photo provided by Northrop Grumman Corp., shows a pre-production model of the F-35 Joint Strike Fighter. The Pentagon on Friday grounded its fleet of F-35 fighter jets after discovering a cracked engine blade in one plane. The problem was discovered during what the Pentagon called a routine inspection at Edwards Air Force Base, California, of an F-35A, the Air Force version of the sleek new plane. The Navy and the Marine Corps are buying other versions of the F-35, which is intended to replace older fighters like the Air Force F-16 and the Navy F/A-18. All versions , a total of 51 planes , were grounded Friday, Feb. 22, 2013 pending a more in-depth evaluation of the problem discovered at Edwards. None of the planes have been fielded for combat operations; all are undergoing testing.AP Photo/Northrop Grumman, File) no sales  
                      Ndege ya kivita ya jeshi la marekani F-35 
 
Mkuu hiyo wa wizara ya ulinzi pamoja na maafisa wengine wa wizara ya ulinzi katika utawala wa rais Obama wameweka wazi kuwa hakuna uamuzi ulikwisha chukuliwa iwapo kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya utawala wa rais Bashar al-Assad.

Magazeti ya Marekani yamekuwa yakieleza kuwa kuna hali ya kutokubaliana ndani ya utawala wa Marekani kuhusiana na hatari ya kujiingiza katika vita vingine katika mashariki ya kati.

 

0 comments

WILSHERE ATIKISA KIBERTIKI ARSENAL...ASEMA ATAONDOKA WENGER AKIFUKUZWA

WILSHERE ATIKISA KIBERTIKI ARSENAL...ASEMA ATAONDOKA WENGER AKIFUKUZWA.

Jack Wilshere
Arsene Wenger

 KIUNGO Jack Wilshere amkandia wanaomponda Arsene Wenger na kusema atafikiria mustakabali wake Arsenal iwapo Mfaransa huyo ataondoka klabuni.

Wenger amejikuta katika wakati mgumu The Gunners kwa kutosajili huku akiwakosa wachezaji aliowataka Gonzalo Higuain, Wayne Rooney, Luis Suarez na Luiz Gustavo.
Kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Aston Villa Jumamosi iliyopita kimesababisha mashabiki wa Arsenal, waitwao Supporters' Trust kusema kwamba itakuwa vibaya kwa bodi kumpa Mkataba mpya asiposajili hadi dirisha likafungwa.
 
Onyo: Jack Wilshere amesema ataangalia upya mustakabali wake Arsenal ikiwa Arsene Wenger ataondoka
 
Critics: Wilshere has also hit out at Wenger's critics, branding them 'ridiculous'
Mgogoro: Wilshere ameponda kulaumiwa kwa Wenger

Wilshere, pamoja na hayo amesema kwamba atalazimika kuondoka Uwanja wa Emirates kama Wenger akiondoka.
"Nataka kushinda vitu na Arsenal na ninataka kuwapo huko muda mrefu, lakini ikiwa kocha ataondoka, mambo yatabadilika," alisema Wilshere akizungumza na Zapsportz.com.
"Arsenal ipo moyoni mwangu wakati wote na kwa kusaini Mkataba kwa miaka mingine mitano inaonyesha ni jinsi gani nimeshikamana nao na ni wajibu wao kuniwekea kila kitu vizuri.
 
Preparation: Arsenal face Fulham at Craven Cottage at lunchtime on Saturday
 
Maandalizi: Arsenal itamenyana na Fulham Uwanja wa Craven Cottage mchana wa Jumamosi

"Arsene Wenger amekuwapo kwa miaka mingi na wakati wote ameshinda mataji. Sawa, tumeporomoka mno kwa miaka mitano au sita iliyopita, lakini ni kocha babu kubwa na watu ambao wanahoji uwezo wake ni wapuuzi.
"Amefuzu Ligi  ya Mabingwa kwa miaka 16, hivyo nafikiri ni mtu sahihi kazini,".alisema.
Wenger aliiongoza Arsenal Jumatano usiku kuichapa mabao 3-0 Fenerbahce nchini Uturuki, matokeo ambayo yanaiweka timu katika nafasi ya kufuzu kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.
Miaka nane imepita sasa tangu The Gunners imeshinda taji na Wilshere ameanzisha kampeni za kumkingia kifua kocha wake.
 
Another year: Arsenal's win in Turkey has virtually guaranteed their passage into the group stage of the Champions League for another year
 
Mwaka mwingine: Ushindi wa Arsenal Uturuki unaiweka timu katika nafasi ya kufuzu tena hatua ya makundi ya Lii ya Mabingwa

"Tumepoteza majina machache ya wachezaji wa nguvu miaka ya karibuni na hiyo ni ngumu kwa klabu yoyote,"alisema kiungo huyo mwenye umri wa miaka 21 wa England.
"Kwanza tulimpoteza Thierry Henry na kisha Cesc Fabregas, Samir Nasri na Robin van Persie. "Hiyo ni ngumu, hususan wakati Robin alipohamia kwa timu nyingine England, inatupa ugumu wa kushindana.
"Lakini sasa tumepata damu changa ya wachezaji wa England wanaoibuka na kama tutakaa pamoja na kujenga kitu, kisha tutashinda mataji katika miaka michache ijayo,".
 
Losses: Selling the likes of Robin van Persie, Cesc Fabregas and Thierry Henry has made it difficult for Arsenal, says Wilshere
Impoteza: Kuuza nyota kama Robin van Persie, Cesc Fabregas na Thierry Henry kumesababisha ugumu Arsenal, amesema Wilshere
0 comments

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AUGUST 24,2013

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AUGUST 24, 2013 

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

 

0 comments

USAJILI WA BALE: BAADA YA JANA KUANZA KUUZA JEZI ZAKE - LEO HII REAL MADRID WAANZA KUTENGENEZA JUKWAA LA KUMTAMBULISHA MCHEZAJI MPYA

USAJILI WA BALE: BAADA YA JANA KUANZA KUUZA JEZI ZAKE - LEO HII REAL MADRID WAANZA KUTENGENEZA JUKWAA LA KUMTAMBULISHA MCHEZAJI MPYA 

Gareth Bale anakaribia kutua Real Madrid
BSW25jqIgAAKTWM {Pictures} Real Madrid preparing stage for tomorrows presentation of Gareth Bale [AS]
Ujeniz wa jukwaa kubwa la kutambulishia wachezaji wakubwa wanaosajiliwa na Real Madrid ukiendelea mapema jana mchana. Inaaminika Real Madrid wapo katika hatua za mwisho za kumsajili Gareth Bale kwa ada ya uhamisho wa £94m ambayo itakuwa rekodi mpya ya dunia baada ya ile £80m waliyolipa Madrid kumsajili Cristiano Ronaldo kutoka Manchester United miaka minne iliyopita.
Miaka minne iliyopita Cristiano Ronaldo alikuwa mtu wa mwisho kupita juu ya jukwaa hili - na kama habari zilizopo ni za kuaminika basi Gareth Bale akiwa na jezi yake namba 11 atakuwa mchezaji mwingine kutoka ligi kuu ya Uingereza kupanda kwenye jukwaa ndani ya uwanja wa Santiago Bernabeu ndani ya siku chache zijazo

 Picha Kwa HIsani ya Shaffih Dauda Blog

0 comments

MAPOKEZI YA RAIS KIKWETE KWA AJILI YA MKUTANO WA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM MJINI DODOMA.

MAPOKEZI YA RAIS KIKWETE KWA AJILI YA MKUTANO WA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM MJINI DODOMA. 

 

 Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mjumbe wa Kamati Kuu Ndugu Adam Kimbisa.

 Mwenyekiti wa CCM Taifa , Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Khamis Sadifa Juma.



 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mtumishi wa Chama Cha Mapinduzi  ndugu Octavian Kimario .
 Watumishi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakishangilia kwa furaha ujio wa Mwenyekiti wa CCM Taifa , Rais Jakaya Mrisho Kikwete mara tu alipowasili Dodoma tayari kwa Mkutano wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu Taifa ya Chama.


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akibadilishina mawazo na Mjumbe wa Kamati Kuu Ndugu Stephen Wassira kabla ya Kikao cha Kamati kuanza leo Dodoma kwenye Ukumbi wa NEC.
 Wajumbe wa Kamati Kuu wakijadiliana jambo ndani ya ukumbi wa NEC kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu,Dodoma 23 Agosti 2013.
 Mjumbe wa NEC, Prof. Anna Tibaijuka akipitia Katiba ya Chama kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ndani ya ukumbi wa NEC.
Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete ,akifungua kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa CCM,Kushoto kwake ni Makamu wa CCM Zanzibar Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana.

 

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger