Featured Post Today
print this page
Latest Post

Chaneta Tanga yatoa semina kwa walimu wa mchezo huo

Chaneta Tanga yatoa semina kwa walimu wa mchezo huo

Na Safari Chuwa,Tanga.
 
CHAMA cha Mpira wa Pete Mkoa wa Tanga,(Chaneta)kimeanza kutoa semina ya walimu wa mchezo toka wilaya zote za mkoa wa Tanga lengo likiwa ni kuwaanda walimu hao kwa ajili ya kufundisha kwenye michezo ya Umitashumta na Umiseta mkoani Tanga.

Akizungumza jijini Tanga, Katibu wa chama hicho,Julieti Mndeme alisema semina hayo ina lengo ya kuwajengea uwezo washiriki na kuhamasisha mchezo huo ambayo yanaendeshwa na mkufunzi wa toka Chama hicho Taifa Anna Kibira.


Mndeme alisema semina hiyo itaendeshwa kwa muda wa siku kumi na moja  yalianza Januari 16 na  yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 27 mwaka huu na yanashirikisha wanawake na wanaume yakifanyika kwenye viwanja vya bandari mkoani hapa.

Katibu huyo alisema mikakati waliokuwa nayo katika kuuendelea mchezo  huo ni kuanzisha ligi za vijana wadogo na kuweka msukumu kwenye mashindano mbalimbali yakiwemo ya wilaya na mkoa ili kuupa maendeleo mchezo huo.

Mndeme alisema kuwa ni matumaini yake mpaka mashindano hayo
yatakapomalizika watapatikana walimu wazuri ambao watakuwa ni chachu ya kukuza maendeleo ya mchezo huo kwenye wilaya wanazotoka na mkoa kwa ujumla.
0 comments

MAMIA WASHIRIKI MAZISHI YA MAMA WA MZEE MAKAMBA

MAMIA WASHIRIKI MAZISHI YA MAMA WA MZEE MAKAMBA

 
Mzee Yusufu Makamba akishauriana jambo na mwanae January Makamba wakati wa shughuli za mazishi zikiendelea.
Mzee Yusufu Makamba amefiwa na mama yake mzazi aliyefahamika kama Mariam Masau Kivugo  kilichotokea tarehe 21 January 2014.
Mzee Yusufu Makamba akiwa na mwanae January Makamba wakitafakari jambo baada ya kupata msiba mkubwa  wa kufiwa na Mama mzazi wa Mzee Yusufu Makamba, Mariam Kivugo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ndugu Abdallah Majura Bulembo akitoa salaam za pole kwa wafiwa wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Masau Kivugo.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa salaam za pole kwa niaba ya Chama  kwa Mzee Yusufu Makamba na Familia yake wakati wa mazishi ya Mama wa Mzee Yusufu Makamba.
 Mamia ya watu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Ndugu January Makamba wakati akitoa salaama za shukrani kwa niaba ya familia kwa wananchi wote waliojitokeza kwenye mazishi ya Bibi yake Marehemu Mariam Masau Kivugo yaliofnyika Mehazangulu,Tanga.(P.T)

 Mwili wa Marehemu Mariam Kivugo ukipelekwa msikitini kwa ajili ya kuombewa kabla ya kuelekea makaburini.
 Watu wakiwa kwenye nyuso za huzuni wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Kivugo ambaye pia ni mama wa Mzee Yusufu Makamba.
 :
Katibu wa NEC itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kuweka udongo kwenye kaburi la mama wa Mzee Yusuf Makamba aliyefariki tarehe 20 Januari 2014.
0 comments

MAMA KIKWETE ASISITIZA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO

MAMA KIKWETE ASISITIZA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO

img_0858_04a5f.jpg
Na Magreth Kinabo – Maelezo

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka Watanzania kuongeza juhudi za kuzuia maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi(VVU) kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ili katika Tanzania iweze kuwa na kizazi kisichokuwa na VVU na ugonjwa wa Ukimwi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) wakati akifungua mkutano wa kitaifa wa wadau wa kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Aidha mama Kikwete aliwataka Watanzania kuchangia sh. 100 katika kupambana na tatizo kwa mchango utawapa nguvu wadau wengine kuwaunga mkono.

Aliwataka wadau wamaendeleo kuendele kuunga mkno katika juhudi za kuondokana na tatizo hilo.

" Lazima juhudi za makusudi zifanyike bila kuchoka kwa maeneo yote Serikali, NGO's, taasisi za dini mashirika ya kiraia na watu binafsi . Hii itasaidia kunusuru kizazi chetu na kuwa na nguvu kazi iliyobora, kizazi kisichokuwa na maambukizi na VVU na Ukimwi," alisema Mama Kikwete huku akisisitiza Tanzania bila Ukimwi inawezekana.

Aliongeza kuwa mikakati imara na endelevu ni lazima iwepo kama vile kutoa huduma za kuzuia maambukizi ya VVU na Ukimwi kwa kushirikisha jamii na kutoa tiba kikamilifu zinaweza kupunguza maambukizi hayo.


Alisema asilimia 98 ya wakina mama wajawazito wanahudhuria kiliniki angalau mara moja na asilimia 43 mara nne wakati wa ujauzito kati ya hao, asilimia 81 wanapimwa VVU.

Aliwataka wakina mama wajazito kuhudhuria kiliniki wakati wa ujauzito kuanzia siku ya kwanza hadi watakapoajifungua ili idadi ya wanahudhuria kiliniki iweze kufikia asilimia 100.

Naye Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid alisema hivi sasa Tanzania imefanikiwa kupunguza maambukizi hayo kwa asilimia 15 mwaka 2012 kutoka asilimia 19 mwaka 2011 na lengo ni kufikia asilimia 5 ifikapo mwaka 2015.

Alisema asilimia 90 ya wakina mama wajawazito wamepimwa VVU kati yao asilimia 64 wamegundulika wanaishi na VVU , pia asilimia 55 ya watoto wanapatiwa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo.(ARV's).

Kaimu Mkurugenzi wa Kinga kutoka wizara hiyo , Dk .Neema Rusibamayilla alisema alisema awamu ya pili ya kupambana na tatizo hilo itaanza Januari mwaka huu katika mikoa mingine 16.
Mratibu wa huduma hiyo kutoka Malawi, Dk. Michael Eliya alisema ni muhimu kuweza katika utoaji wa huduma, kuboresha miundombinu ,ikiwemo rasilimali fedha na watu katika kufanikisha malengo hayo.
Mwisho.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger