Featured Post Today
print this page
Latest Post

WABUNGE WA TANZANIA NAO WASUSIA KIKAO CHA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI.

WABUNGE WA TANZANIA NAO WASUSIA KIKAO CHA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI.

Kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (EALA), jana kilivunjika kwa mara ya pili baada ya Wabunge wa Tanzania, kutoka ndani ya ukumbi wakipinga kanuni kuvunjwa juzi. 

  
Baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje, Spika wa Bunge hilo, Margareth Zziwa aliahirisha Bunge kwa dakika 15 ili kuweka mambo sawa, lakini jitihada za kuwashawishi ziligonga mwamba na kuamua kuahirisha Bunge hadi leo.
 
 Hata hivyo, Mbunge wa Tanzania, Makongoro Nyerere hakuungana na wenzake kugoma kwani alibakia ukumbini na kuungana na wabunge 32 wa Burundi, Kenya, Uganda na Rwanda.
 
Awali, Mbunge Abdullah Ali Hassan Mwinyi alitoa msimamo wa wabunge wa Tanzania kuwa walitoka, kupinga kitendo cha wabunge wengine kudharau kiti cha Spika juzi na kutoka nje ili kushinikiza hoja yao.
Mwinyi alisema ili kushinikiza kuheshimiwa kiti cha Spika, wameamua kutoka nje ya ukumbi huo kwa kuonyesha hawaungi mkono, tabia ya baadhi ya wabunge kushinikiza hoja zao, kujadiliwa na Bunge hata kwa kukiuka kanuni na taratibu.
 
“Jana(juzi) ilikuwa ni mara ya pili wenzetu, kudharau kiti cha Spika na kutaka kutoa hoja na kujadiliwa bila kufuata kanuni, sasa tumeona ni vizuri na sisi kwa kupinga kuvunjwa kanuni, tutoke ili kuonyesha tunapinga mchezo huu,” alisema Mwinyi.
 
Mwinyi alisema kitendo cha wabunge wenzao kutoka nje ya ukumbi kwa kukataliwa kuvunja taratibu, kinadhalilisha kiti cha Spika na hata wabunge wenyewe.
 
Mbunge mwingine wa Tanzania, Twaha Taslima alisema kanuni zipo wazi kuwa kama mbunge ana hoja na kutaka Bunge lijadili mambo ambayo si ya dharura ni lazima aiwasilishe saa 24 kabla kwa Spika.
“Sasa jana(juzi), Mbunge wa Kenya, Peter Mathuki alitaka hoja yake ya kutaka utaratibu wa kufanyika bunge kwa mzunguko ijadiliwe kitu ambacho hakikuwa sahihi,” alisema Taslima.
 
Muthuki, juzi aliungwa mkono na nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), isipokuwa Tanzania.
 
Jana aliwasilisha hoja hiyo kwa kufuata utaratibu lakini haikujadiliwa baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje. 
Katika hoja hiyo, msimamo wa wabunge wa Tanzania na Kamati ya Uongozi ya Bunge ni kuwa vikao vyote vifanyike katika ukumbi wa Bunge, Arusha baada ya kukamilika.
Wabunge wa Tanzania ambao jana walitoka ni Shyrose Bhanji, Profesa Nderakindo Kessy na Taslima. Wabunge wanne hawakuwapo.
 
Kwa mujibu wa kanuni za Bunge hilo, kama wabunge watatu wa nchi moja, wakitoka nje kupinga jambo lolote basi kikao kinaahirishwa kwa dakika 15 na wasiporejea bunge linaahirishwa.
 
Akizungumzia mgogoro huo, Ofisa Habari wa EALA, Bobi Odiko alisema kilichotokea jana si ukiukwaji wa taratibu na kuongeza kuwa ana imani mambo yatakuwa sawa na vikao vitaendelea leo kwa amani.
0 comments

Mtoto ang'olewa macho yote mawili na Mama katili.

Mtoto ang'olewa macho yote mawili na Mama katili.

Polisi nchini Uchina imetangaza kuwa itatoa zawadi kwa yeyote atakayetoa habari zitakazowasaidia kumkamata mama mmoja ambaye anashukiwa kumng'oa macho mvulana mwenye umri wa miaka sita.
0 comments

CHEKI KIZAAZAA CHA KUSHINDWA KWA WAZIRI ''WILLIAM LUKUVI'' KUWATAJA WABUNGE WANAOJISHUHULISHA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA, YAWAKERA WABUNGE BUNGENI MJINI DODOMA. SOMA HAPA

CHEKI KIZAAZAA CHA KUSHINDWA KWA WAZIRI ''WILLIAM LUKUVI'' KUWATAJA WABUNGE WANAOJISHUHULISHA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA, YAWAKERA WABUNGE BUNGENI MJINI DODOMA. SOMA HAPA

 
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2012/06/cocaine.jpgWAZIRI wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi amelazimika kufafanua kauli aliyoitoa juzi ya kuhusisha wabunge na dawa za kulevya, kwa kusema hakumaanisha kwamba wabunge wote ni
wafanyabiashara wa dawa hizo.
 
Lukuvi ambaye jana alisisitiza kuwa Serikali haiko tayari kutaja majina ya wafanyabiashara wa dawa hizo, aliliambia Bunge kwamba alimaanisha ipo orodha kubwa kutoka kwenye vyanzo mbalimbali, yakiwemo magazeti, vyenye majina na kwamba Serikali haiko tayari, kwa kuwa inahesh
imu utawala wa sheria na mgawanyo wa majukumu.

Ufafanuzi huo aliutoa baada ya Mbunge wa Simanjiro , Christopher ole Sendeka (CCM) kumtaka kutaja majina ya watuhumiwa, wakiwemo wabunge, kama wapo, vinginevyo afute kauli yake, aliyoitoa bungeni juzi.


Akiomba mwongozo baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni, Sendeka alisema kauli iliyotolewa na Lukuvi juzi, kwamba akitaja majina ya wafanyabiashara ya unga, hakuna mbunge atakayepona ni ya kulidhalilisha Bunge kwa kuwa Watanzania kwa kauli hiyo, wanawachukulia wabunge kama wafanyabiashara hiyo.


“Naomba Mheshimiwa Waziri ataje majina hayo ili kuondoa mkanganyiko kwetu wabunge mbele ya Watanzania, vinginevyo kauli hiyo inaweza kuchukuliwa kwamba kila mbunge ni mfanyabiashara hii la sivyo afute kauli yake ya jana (juzi) aliyotoa hapa bungeni,” alisema Sendeka.


Lukuvi alisema, “Serikali inaheshimu mihimili mingine ikiwemo Polisi na Mahakama, hivyo si kazi ya Serikali kutaja tu majina kutoka kwenye orodha ya watuhumiwa. Na hilo ndilo nililosema hapa bungeni jana (juzi).


Sikuamanisha kwamba wabunge ni wafanyabiashara ya madawa ya kulevya bali nilisema katika orodha hiyo ndefu kutoka vyanzo mbalimbali, hata wabunge waliomo humu ndani ya Bunge hili hawawezi kupona kutajwa,” alisisitiza.


Kauli hiyo ya juzi ilitokana na swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Catherine Magige aliyetaka kufahamu sababu za biashara ya dawa hizo kukithiri nchini, huku vijana wengine wa Kitanzania wakiendelea kukamatwa kwenye viwanja vya ndege ndani na nje ya nchi.
Chanzo; gazeti la habari leo

0 comments

BREAKING NEWS: MAJAMBAZI WALIOVALIA SARE YA JESHI LA POLISI HABIB AFRICAN BANK JIJINI DAR ES SALAAM.

BREAKING NEWS: MAJAMBAZI WALIOVALIA SARE YA JESHI LA POLISI HABIB AFRICAN BANK JIJINI DAR ES SALAAM.

 

WATU wanaodhaniwa kuwa ni Majambazi wamevalia sare za Jeshi la Polisi wamevamia Habib Afriican Ban
k Kariakoo DSM na kupora kiasi kikubwa cha Fedha. 

Jeshi la polisi kanda maalum wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo. Endelea kufuatilia taarifa zetu za habari. chanzo ITV

 

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger