Featured Post Today
print this page
Latest Post

STENDI YA MABASI MKOANI DODOMA

STENDI YA MABASI MKOANI DODOMA.



0 comments

PILIKAPILIKA ZA KIBIASHARA NDANI YA STENDI YA MABASI DODOMA.

PILIKAPILIKA ZA KIBIASHARA NDANI YA STENDI YA MABASI DODOMA.


                    DODOMA INAVYOONEKANA ASUBUHI YA LEO.






0 comments

Magazeti ya leo Jumapili December 01 2013

Magazeti ya leo Jumapili December 01 2013

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments

CHADEMA YATOA UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA

CHADEMA YATOA UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA

c1_24e5d.jpg
UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA YA NDUGU ALI O. CHITANDA
Kutokana na kuwepo kwa taarifa ya Ndugu Ali Omari. Chitanda, huku pia waandishi wa habari wakitaka kujua na kupata ukweli kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, tunapenda kutoa ufafanuzi mfupi;
Kwanza suala la maamuzi ya Kamati Kuu ya kuwavua uongozi ndani ya chama, Ndugu Zitto Kabwe na Dkt. Kitila Mkumbo, chama kimeshafunga mjadala kwenye vyombo vya habari kwa kuheshimu na kuzingatia taratibu za kikatiba za ndani ya chama kuendelea.
Pili kuhusu suala la restructuring ya Makao Makuu ya Chama. Chitanda ametoa taarifa akiwataja wakurugenzi wafuatao, kuwa ni wapya;
1.Mkurugenzi wa Oganaizesheni Mhe. Singo Kigaila Benson.
2. Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano ya ndani Mhe. John Mnyika
3. Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji Mhe. Anthony Komu.
4. Mkurugenzi wa Bunge na Halmashuri Mhe. John Mrema.
5. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama Mhe. Wilfred Lwakatale.

Wakurugenzi wote aliowataja si wapya. Mkurugenzi pekee ambaye uteuzi wake ni mpya na umefanyika hivi karibuni na kuthibitishwa ni Mwanasheria Peter Kibatala, atakayesimamia Kurugenzi ya Sheria na Haki za Binadamu.
Kama ni suala la kuangalia mtu anatokea wapi (ambalo halijawahi wala haliwezi kuwa moja ya vigezo), ili kuonesha ukweli na kubainisha uongo wa watu wanaojaribu kufanya kazi ya CCM wakisema wao ni wanaCHADEMA, kwa kutumia propaganda zile zile na kuzifanya kuwa ni kete zao za kisiasa ndani ya chama, tunaweza kutaja maeneo ya wanakotoka au asili yao kama ifuatavyo;(P.T)
Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji, Antony Komu- Kilimanjaro.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama, Wilfred Lwakatare- Kagera.
Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni, Benson Kigaila- Dodoma.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John John Mnyika- Mwanza
Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri, John Mrema- Kilimanjar.o
Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu, Peter Kibatala- Morogoro.
Hadi sasa uteuzi wa kurugenzi za Makao Makuu ya CHADEMA haujakamilika. Bado kuna nafasi zinazotakiwa kujazwa kwa kufuata taratibu za chama.
Hii ni kwa sababu maboresho yanayofanyika ndani ya chama, hadi sasa yanaendelea katika ngazi ya Makao Makuu na kanda, kisha itaendelea kwa ngazi za mikoa, wilaya, majimbo, kata, kijiji na hatimaye kitongoji.
Katika maboresho hayo, kwa nafasi za uteuzi, yanayoendelea sasa ambayo yanakwenda hatua kwa hatua, hadi kuwa na makatibu wa kuajiriwa ngazi ya chini ya chama, chama kinazingatia uwezo, uadilifu na utayari wa mtu katika kutoa utumishi bora kwa wanaCHADEMA na Watanzania wote katika nafasi husika.
Suala la maslahi ya watumishi wa CHADEMA ni utaratibu wa chama ambao unajadiliwa, kufikiwa uamuzi na kisha kuridhiwa kwenye vikao vya chama, kama ilivyofanyika kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichoketi karibuni.
Katika suala hili la maslahi ya watumishi wanaojitolea Makao Makuu ya CHADEMA ambayo si siri, Ndugu Chitanda amesema uongo mkubwa. Kusema kwamba Ofisa Mwandamizi anaweza kulipwa posho kubwa kuliko Mkurugenzi wa kurugenzi husika, ni uongo unaovuka mipaka.
Ndugu huyo anadhihirisha uongo huo yeye mwenyewe kwa kuandika hivi; "800,000/= za awali na sasa itakuwa ni kuanzia Tshs. 1,500,000-2,500,000/= kwa Mkurugenzi na kutoka Tshs.6,800,000/= kwa Afisa Mwandamizi na sasa ni Tshs.1,000,000-1,500,000/=".
Pia si kweli kuwa kila mtumishi anayejitolea Makao Makuu analipwa. Mathalani, wakurugenzi wenye nafasi za ubunge, hawalipwi hata shilingi moja kwa kazi zote wanazokitumikia chama na Watanzania kwa ujumla.
Kwa maelezo hayo ya kutengeneza, ni kwamba hadi sasa Ofisa Mwandamizi anapokea posho kubwa kuliko Mkurugenzi na hata baada ya maboresho atapata posho kulingana na Mkurugenzi. Anapaswa kuwa mkweli. Mtu anayetaka kuonekana muungwana, anapaswa kujiweka mbali na uongo pamoja, maneno ya kutunga pamoja na upotoshaji wa makusudi.
Kama ilivyoelezwa hapo juu, restructuring inaendelea. Ni hatua kwa hatua. Itafika ngazi za chini kama Baraza Kuu lilivyoagiza. Kwa sababu hiyo hadi sasa uteuzi wa Makatibu wa Mikoa na Wilaya haujafanyika.
Hata hivyo ruzuku imekuwa ikipelekwa kila kanda, mkoa, wilaya na jimbo kama ilivyoridhiwa na Kamati Kuu. Na hii ni zaidi ya pikipiki, kompyuta na magari yaliyopelekwa kila kanda. Angelikuwa mkweli, nagelisema na hili pia.
Ndugu Chitanda anajichanganya sana katika taarifa yake yote. Hii ni moja ya sifa ya kukosa hoja hivyo mtu anaamua kuibua viroja au kutunga maneno kwa sababu ya kujaribu kuukana ukweli anaoujua moyoni. Tutatoa mfano mmoja;
Kupitia taarifa yake, anasema alikuwa mtu aliyeaminiwa hadi kuwa katika vikao muhimu, lakini wakati huo huo anasema kuna ubaguzi! Tunapaswa kumhurumia kwa kushindwa kuunganisha hata mawazo yake na kupata mtiririko wa hoja zenye mantiki! Angelikuwa mkweli angesema katika vikao vya sekretarieti na CC, aliingiaje kama kuna ubaguzi wa dini!
Kwa sababu anazozijua yeye, Ndugu Chitanda ameamua kujipachika cheo ambacho hajawahi kuwa nacho. Amejiita kuwa ni Katibu wa Sekretarieti ya Makao Makuu.
Ndani ya CHADEMA pamoja na kwamba nafasi hiyo imetajwa ndani ya Katiba ya Chama, hakuna mtu ambaye ameteuliwa kutumikia nafasi hiyo. Kama anaweza athibitishe kwa kutoa barua ya uteuzi kutoka kwa Katibu Mkuu.
Mahali pengine amejitambulisha kuwa ni Katibu Ofisi ya Katibu Mkuu. Ofisi hiyo ina Katibu Mtendaji mmoja ambaye ni Mzee Victor Kimesera, mmoja wa waasisi wa CHADEMA.
Operesheni ya Chama inayoendelea nchi nzima kwenye majimbo 103, si suala la siri wala lengo bovu kama anavyotaka umma uamini.
Ni mwendelezo wa mpango mkakati wa chama kupitia progamu za Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), unaotekelezwa kwa hatua mbalimbali na kwa mbinu tofauti tofauti pamoja na dhana ya CHADEMA ni msingi.
Operesheni hiyo ambayo ni mwendelezo wa nyingi za namna hiyo zinazokwenda ngazi za chini kabisa za chama, zikilenga kuimarisha taasisi na mifumo, imeanza wiki hii na ilitangazwa mbele ya waandishi wa habari.
Tungependa kumalizia ufafanuzi huu mfupi kwa kutoa tahadhari kwa umma kuwa makini na matamko ya watu wa namna hii. Maana tunajua kwa uhakika yako mengi ya namna hii yataandaliwa na kutolewa kadri ambavyo Watanzania wanakaribia kuona na kuishi matumaini ya mabadiliko ya kiutawala na mfumo ndani ya nchi yao.
Mathalani katika taarifa yake, Ndugu Ali Chitanda amedhihirisha na kuonesha kuwa ni aina ya watu ambao wanaCHADEMA na Watanzania kwa ujumla wanapaswa kuwaangalia kwa macho ya kuhoji na tahadhari ya hali ya juu, anasema hivi;
"Kwa kuwa siamini kwamba kuvuliwa nyadhifa kwa Zitto Kabwe na Dkt Kitila Mkumbo ni kwa sababu ya waraka wa ushindi, bali ninaamini kuvuliwa kwao ni kutokana na hofu ya uchaguzi, ubaguzi wa kikabila na kikanda."
Aya hiyo pekee inayotumia lugha wanayotumia mahasimu wa CHADEMA, wakiongozwa na viongozi waaandamizi wa CCM, wanaohangaika kutokana na Watanzania kuwakataa, wakijiandaa kuwaondoa madarakani kwa sababu sera zao zimeshindwa, inatosha kuonesha uhalisia wa yeye mwenyewe (mtoa taarifa) alivyo.
Ni kauli za namna hii (kuwatisha na kutaka kuwatenganisha Watanzania) ambazo zimekuwa zikitumiwa na watawala kama njia pekee ya kutaka kuzuia upepo wa mabadiliko unaovuma nchi nzima, zimekuwa zikiwaunganisha zaidi Watanzania kuiunga mkono CHADEMA bega kwa bega, ili kupata haki na matumaini ya wanyonge, katika mapambano ya awamu ya pili, kuelekea uhuru wa kweli.
Imetolewa leo Novemba 30, 2013, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari- CHADEMA
0 comments

ARSENAL HAIKAMATIKI, YAWAFUMUA CARDIFF 3-0 BARAZANI KWAO...LUKAKU NI HATARI

ARSENAL HAIKAMATIKI, YAWAFUMUA CARDIFF 3-0 BARAZANI KWAO...LUKAKU NI HATARI

ramsey_4f6c3.jpg
Ramsey hakutaka kushangilia baada ya kuifunga timu yake ya zamani

ARSENAL imezidi kijichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya England, baada ya kuilaza mabao 3-0 Cardiff City, kwenye Uwanja wa Cardiff jioni hii.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Aaron Ramsey dakika ya 29 akimalizia pasi ya Mesut Ozil na 90 pasi ya Theo Walcott na Mathieu Flamini dakika ya 86 pasi ya Ozil tena.
Ushindi huo, unaifanya Arsenal itemize pointi 31 baada ya kucheza mechi 13, ikiizidi Liverpool iliyo katika nafasi ya pili kwa pointi saba.

lukaku_53cf1.jpg
Lukaku akishangilia bao lake leo

Katika mechi nyingine za Ligi Kuu England leo,
Everton imeichapa 4-0 Stoke City Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, mabao ya Gerard Deulofeu dakika ya 45, pasi ya Gareth Barry, Seamus Coleman dakika ya 49 pasi ya Barry tena, Bryan Oviedo dakika ya 58, pasi ya Gerard Deulofeu na Romelu Lukaku dakika ya 79 pasi ya Oviedo.
Bao pekee la Gary Hooper dakika ya 30 limeipa Norwich ushindi wa 1-0 dhidi ya Crystal Palace Uwanja wa Carrow Road, Norwich, Norfolk.

West HamUnited imeifunga 3-0 Fulham Uwanja wa Boleyn Ground, London mabao ya Mohamed Diame dakika ya 47, Carlton Michael Cole Okirie dakika ya 82 na Joe Cole dakika ya 88.
Aston Villa imetoka sare ya bila kufungana na Sunderland Uwanja wa Villa Park na mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu England, Newcastle United imeifunga West Bromwich 2-1.

0 comments

KOCHA WA CAMEROON ASAINI MIAKA MWILI AZAM

KOCHA MCAMEROON ASAINI MIAKA MWILI AZAM

Kocha mpya wa Azam FC. Joseph Marius Omog (katikati) akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kusaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.


KLABU ya Azam inapenda kuufahamisha umma hususan wapenzi wa mpira wa miguu kuwa imeingia mkataba na kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon kwa kipindi cha miaka miwili (2) kuanzia leo.

Kocha Omog ni bingwa kwani anakuja kuifundisha Azam akiwa ametoka kuiongoza klabu ya A.C Leopards ya Jamhuri ya Kongo (Brazaville) kutwaa ubingwa wa ligi ya nchi hiyo kwa misimu miwili mfululizo (2012 na 2013).

Timu hii ilikuwa haijatwaa ubingwa wa ligi kwa zaidi ya miaka 30. Kwa mwaka huu wametwaa ubingwa wakiwaacha wapinzani wao, Diables Noirs kwa pengo la pointi kumi (10) wakikusanya pointi 87 katika ligi yenye timu 18.

Pia ni mwaka jana tu (2012) aliiwezesha A.C Leopards kunyakua ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika kwa kuzipiga kumbo timu ngumu na zenye uzoefu mkubwa kama vile Mas de Fes ya Morocco, Heartlands ya Nigeria na Sfaxien ya Tunisia.

Mafanikio hayo ya kutwaa ubingwa wa Afrika yalifikiwa baada ya miaka 38 tangu klabu ya Jamhuri yas Kongo ifanye hivyo, na kumfanya kocha Omog kuwa moja ya makocha wa kupigiwa mfano barani Afrika.
0 comments

LAAC WAIAGIZA HALMASHAURI HANDENI KUPELEKA ZAIDI YA MILI 105 KWA VIJIJI RUZUKU YA SERIKALI.

LAAC WAIAGIZA HALMASHAURI HANDENI KUPELEKA ZAIDI YA MILI 105 KWA VIJIJI RUZUKU YA SERIKALI.

MWENYEKITI wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajabu Mbaruku imeiagiza Halmashauri ya wilaya ya Handeni kuhakikisha kwamba inapeleka kiasi cha sh.milioni 105,779,260 kwa vijiji vilivyostahili kuzipata ikiwa ni michango ya lazima ya asilimia 20 ya ruzuku ya serikakali kuu kwa ajili ya maendelo vijijini,

Kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo ilitokana na halmashauri hiyo kushindwa kuzipeleka vijijini fedha za ruzuku ya serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo hali ambayo inapelekea kuchangia kudhorotesha kasi yao katika shughuli mbalimbali.
Licha ya kutoa agizo hilo pia aliiagiza halmashauri hiyo kuandaa mchanganuo wa madeni inayodai na kudaiwa kwa kuonyesha majina ya wadai na wadaiwa ikiwemo kuchukua hatua za makusudi za kupatikana kwa fedha zinazodaiwa.

Mwenyekiti huyo alisema katika mchanganuo huo wadai wa halmashauri unaonyesha ni kiasi cha sh.milioni 736,302,302 ambapo katika hilo mchanganuo wa wadaiwa hao haukuonyesha kitendo ambacho kinaleta mashaka hasa katika utendaji wake.
Aidha pia kamati hiyo iliagiza mchanganuo wa matumizi ya mabati 466 yaliyotumika kujengea vyumba 8 vya madarasa katika shule ya sekondari Segera uandaliwe na kupelekwa kwa mkaguzi mkazi kwa ajili ya uhakiki zaidi.
Aliitaka halmashauri hiyo kuzingatia vipimo na vigezo vya ubora katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ambapo agizo hilo lilitokana na kubainika kwa kiwango duni kwa madarasa manne yaliyojengwa kwa sh.milioni 14 katika shule ya sekondari Komnyang’anyo.
Hata hiyo waliitaka halmashauri hiyo kuongeza bidii katika kudai kiasi cha sh.,milioni 133,391,724 ambazo inadai kutoka kwa wadaiwa ambao ni pamoja na MSD sh.milioni 39,310,646,State Business sh.milioni 14,690,000,HADECO sh.milioni 10,200,000, Hazina (15% LAPF) sh.milioni 44,059,300, Hazina(Salaries)sh.milioni 19.806,278 na mfuko wa wanawake ni sh.milioni 5,025,500.
0 comments

Kigoda: Kamanda wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM)

Kigoda: Kamanda wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM)

WAZIRI wa Biashara na Viwanda nchini, Dr.Abdalla Kigoda ameteuliwa kuwa kamanda wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM) katika uteuzi ambao ulifanywa na kamati ya utekelezaji Taifa chini ya Mwenyekiti wao Sadifa Juma.

Akizungumza na Tanga Raha, katika ofisi za Umoja huo mkoani hapa, Mwenyekiti wa Umoja huo, Abdi Makange alisema mchakato huo ulianzia ngazi ya mkoa ambapo wao waliamua kumpendekeza Kigoda na hatimaye kupata baraka kutoka kamati ya utekelezaji na kumuidhinisha kwa kumpitisha.

Makange alisema hatua yao ya kumpendekeza ilitokana na mchango wake mkubwa aliokuwa ukitolewa na kiongozi huo kwa vijana wa mkoa wa Tanga kitendo ambacho kimewapa wigo katika ufanisi wao.

   “Naishukuru sana kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa kuridhia mapendekezo hayo na sasa tunakwenda kufungua ukurasa mpya wa mafaniko ndani yetu “Alisema Makange.

Alisema umoja huo unatarajiwa kuandaa taratibu za kumsimika rasmi kiongozi huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Handeni mkoani Tanga lengo likiwa ni kuhakikisha wanatimiza malengo yao waliojiwekea.
0 comments

Harufu ya ufisadi yabainika halmashauri za Tanga

Harufu ya ufisadi yabainika halmashauri za Tanga

 
Jiji la Tanga
 
Kamati  ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa( LAAC) imeagiza kuchukliwa hatua kali  na kusimamishwa kazi Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Korogwe, Sadiki Kallaghe, kwa tuhuma za kusaini mkataba  wa kumpa tenda ya kukusanya ushuru wa halmashauri  mzabuni bila kumshirikisha mwanasheria wala mkurugenzi wa halmashauri hiyo.
Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa LAAC, Rajabu Mbarok, katika majumuisho ya ziara yao katika ofisi za mkuu wa mkoa  wa Tanga na kushirikisha wakuu wa idara, wakurugenzi, wenyeviti wa halmashauri, mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya.

Mbarok  alimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Bendkito Ole Kuyani, kuunda kamati ya kuchunguza suala hilo huku akitaka mwenyekiti huyo asimamishwe kazi ili kuepuka kuharibu uchunguzi.

Mbarok alisema wametembelea miradi sita katika halmashauri hiyo ikiwamo soko la kimataifa linalojengwa maeneo ya Makuyuni na kwamba miradi hiyo hairidhishi na kutolea mfano choo kilichojengwa kwa thamani ya Sh. milioni saba ambacho hakilingani na thamani halisi ya fedha.

Alisema halmashauri ya Korogwe imekuwa ikipata hati chafu kwa muda wa miaka mitano sasa na zaidi ya Sh. bilioni moja hazikutumika.

Kuhusu halmashauri ya Mji Mdogo wa Korogwe, alisema walikagua miradi mitano, lakini miradi yenye nafuu ni miwili tu hiyo mingine ipo chini ya viwango huku akimpa onyo mkurugenzi wa mji wa Korogwe kwa kuikimbia kamati hiyo na kwenda kujificha na kuwa wamekaidi agizo la  mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa hawawapandishi vyeo walimu na kuwaongezea mishahara mpaka sasa.

Katika Jiji la Tanga alisema walikagua mradi wa bwawa la umwagiliaji liliyopo Mabaayani lakini aligundua ufisadi mkubwa na kusema kuwa mradi huo ni wa watendaji na sio wananchi kwani mpaka sasa zaidi ya MSh. mlioni 300katika mradi huo zimeliwa na wajanja.
0 comments

Tanga sasa hatarini kupoteza hadhi ya Jiji

Tanga sasa hatarini kupoteza hadhi ya Jiji

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Chiku Gallawa 

Halmashauri  ya Jiji la Tanga inaweza kushushwa hadhi kuwa manispaa kutokana na kushindwa kukusanya mapato.
Hayo yalibainishwa jana na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) wakati wa majumuisho ya ziara yao.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Rajabu Mbaruk, alisema kamati inakwenda kuishauri serikali kushusha hadhi ya kuwa jiji na kurudi katika hadhi ya manispaa kwa kuwa imeshindwa kukusanya mapato.

Alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Tanga inatia aibu kwani inakusanya mapato ya Sh. bilioni 3.5 kwa mwaka ambayo ni madogo kulinganisha na ya Jiji la Mwanza ambalo linakusanya Sh. bilioni 10 kwa mwaka.

Alisema cha kusangaza, Halmashauri ya Jiji la Tanga ina vyanzo vingi vya mapato, lakini mapato hayakusanywi na kusema kuwa hiyo ni aibu na haifai kuwa na hadhi ya jiji.

Mbarok alisema kuwa madiwani na watendaji hawana uchungu na halmashauri ya jiji la Tanga. “Sasa kamati inakwenda kuishauri serikali kushusha hadhi jiji la Tanga kuwa manispaa kama zamani,” alisema.

Alisema kuwa Mkoa wa Tanga una wilaya tisa, lakini cha kushangaza ni kuwa mkoa mzima wanakusanya Sh. bilioni nane tu na kuzidiwa na Jiji la Mwanza.

Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa kiasi cha Sh. bilioni mbili za mapato zimepotea kutokana na jiji hilo kutokuwa na uwezo wa kutunza vizuri kumbukumbu za mahesabu.

Alipoulizwa na NIPASHE kuhusiana na lini LAAC itakutana na serikali ili kuwasilisha pendekezo la kulishusha hadhi Jiji la Tanga, alisema  kamati yake inaandaa taarifa ya mapendekezo na ili kuipeleka  Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi).
 
CHANZO: NIPASHE
0 comments

Waziri Kigoda mgeni rasmi tamasha la Handeni Kwetu 2013



Waziri Kigoda mgeni rasmi tamasha la Handeni Kwetu 2013



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
 
WAZIRI wa Viwanda na Biashara ambaye pia ndio mbunge wa Handeni, Dkt Abdallah Kigoda, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Utamaduni, lililopangwa kufanyika Katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni mkoani Tanga, Desemba 14 mwaka huu.
 
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt Abdallah Kigoda, pichani.
Tamasha hilo linafanyika kwa mara ya kwanza wilayani hapa, huku likitarajiwa kuwa la aina yake kutokana na maandalizi yanayoendelea kushika kasi.
Akizungumza jana mjini Handeni, Mratibu wa Tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema maandalizi yamezidi kushika kasi kwa kuangalia mazoezi ya vikundi kadhaa vitakavyotoa burudani katika tukio hilo.
“Tunashukuru Mungu kuona mambo yanazidi kuwa mazuri kwa kuhakikisha kuwa Desemba 14 mwaka huu tunafanya tamasha lenye mguso na kila mmoja wetu kufaidishwa.

“Huu ni wakati wa kila mtu kujipanga ili aje kushiriki kwa namna moja ama nyingine, ukizingatia kuwa juhudi hizi zote zipo kwa ajili ya kujenga ushirikiano kwa watu wote,” alisema Mbwana.
Wadhamini katika tamasha hilo ni pamoja na gazeti la Mwananchi, Clouds Media Group, ni Phed Trans, Clouds Media Group, Grace Products, Screen Masters na mtandao wao wa Saluti5.com, Dullah Tiles & Construction Ltd, Katomu Solar Specialist, PLAN B SOLUTIONS (T) LTD, Country Business Directory (CBD) na Michuzi Media Group duka la mavazi la Chichi Local Ware, Smart Mind & Arters chini ya Anesa Company Ltd, ikidhamini kwa kupitia kitabu chao cha ‘Ni Wakati Wako wa Kung’aa’, Lukaza Blog, Kajunason Blog, Jiachie Blog na Taifa Letu.com, huku likipangwa kuanza saa 2 za asubuhi hadi saa 12 za jioni.
0 comments

CHADEMA TANGA YAPONGEZA UAMUZI WA KUVULIWA UONGOZI KATIBU MSAIDIZI

CHADEMA TANGA YAPONGEZA UAMUZI WA KUVULIWA UONGOZI KATIBU MSAIDIZI

Na Oscar Assenga, Tanga
SIKU Chache baada ya Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Taifa (Chadema) kuamua kumvua uongozi ndani ya chama hicho aliyekuwa katibu Msaidizi Zitto Kabwe chama hicho mkoani hapa kimeipongeza hatua hiyo kwa kusema italeta umakini mkubwa kwa viongozi waliobaki.
Uamuzi huo ulitolewa kwa mujibu ibara ya 7.7.16 kifungu (V) ambayo inaeleza kuwa kamati hiyo ina mamlaka ya kumwachisha ujumbe wa kamati kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume cha katiba, kanuni na maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake.
Akizungumza na Tanga Raha,Katibu wa Chadema Mkoa wa Tanga,Jonathan Bahweje alisema suala hilo lilipaswa kufanywa na kamati hiyo kwa sababu ni sahihi kwa mtu yoyote anayekiuka kanuni na taratibu za uongozi ndani ya chama hicho.
Bahweje alisema hatua ya Zitto kukiri kuwa alikosea na kupewa adhabu ya siku kumi na nne kujitetea kwa kamati kuu ya chama hicho alitumia busara kubwa sana na kuwataka wanachama kuwa na utulivu wakati mchakato huo ukiendelea.
  “Maamuzi ya kamati kuu yaliyofanywa sidhani kama yanaweza kuingiliwa na upande mwengine hivyo napenda kuwaasa viongozi wa ngazi za chini kuacha kuingilia suala hilo kwani tayari limeshapata muafaka “Alisema Bahweje.
Alisema wanaiomba kamati kuu ya chama hicho kumaliza mgogoro uliopo huo mapema ili kuweza kujiandaa na uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa mwaka 2014  kwani wamedhamiri kuhakikisha wanashinda katika chaguzi hizo.
Katibu huyo aliitaka kamati hiyo kukemea viongozi ambao wanapiga maamuzi yao kwani wao ndio chombo cha mwisho ambacho kinauwezo wa kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuleta mgawanyiko ndani ya chama hicho.
   “Naishauri kamati kutumia nafasi yao kuwaonya viongozi kuanzia ngazi za chini na kuweza kuleta mshikamano wa pamoja ambao utaweza kuleta mafanikio katika chama chetu kwani uongozi imara ndio utakiwezesha kuwatumikia wananchi “Alisema Bahweje
0 comments

PANGANI YAZINDUA UTARATIBU WA UTOAJI VIBALI SHUGHULI ZA UFUGAJI MDOGO

PANGANI YAZINDUA UTARATIBU WA UTOAJI VIBALI SHUGHULI ZA UFUGAJI MDOGO

Na Burhan Yakub,Pangani.

Wilaya ya Pangani imezindua rasmi cha kitabu cha utaratibu wa
utoaji wa vibali vya shughuli za ufugaji mdogo wa viumbebahari ambao utawawezesha wakazi wa mwambao wa pwani kufanya shughuli za uzalishaji mali bila kuathiri mazingira.

Kitabu hicho  kilichozinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Hafsa Mtasiwa hivi karibuni kikiwa kimeandaliwa na mradi ujulikanao “Pwani Project”kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Pangani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho,Mkurugenzi wa mradi wa Pwani,Baraka Kalangahe alisema yaliyoandikwa ni hali halisi ya sasa ya ufugaji mdogo wa viumbebahari na matatizo yanayoikabili tasnia ya maendeleo ya ufugaji mdogo wa viumbe bahari katika Wilaya ya Pangani.

Mengine yaliyoandikwa ni taarifa muhimu za maeneo yanayofaa kwa ufugaji mdogo wa viumbebahari katika Wilaya ya Pangani, maeneo yanayofaa kwa vijiji vya Buyuni, Mkwaja, Mikocheni, Sange,Kipumbwi, Mikinguni,Stahabu,Ushongo Bweni , Mkwajuni,  Pangani Magharibi, Mwembeni,Msaraza na   Kigurusimba.

Mkurugenzi huo pia alisema Kitabu hicho kinatoa mwongozo wa utoaji wa vibali, ufuatiliaji na udhibiti.

Akizungumza baada ya kuzindua kitabu hicho,Mkuu wa Wilaya alisema mradi huu utasaidia kuongeza thamani ya bahari nakuonya kuwa mtendaji atakayesababisha kuzorota katika eneo lake atamuwajibisha.
0 comments

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA NCHI WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NGUO KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA (CAPA)

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA NCHI WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NGUO KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA (CAPA)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya Kinyago kutoka kwa Makamu wa Mwenyekiti wa CAPA wa Kanda ya Afrika Magharibi, Prof. Daniel Nyarko, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa nne kushoto), Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya CAPA,John Kondoro (kushoto kwa Makamu) na baadhi ya viongozi wa CAPA, wakifurahia kwa pamoja baada ya kuzindua rasmi Jarida la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal), wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakiwa makini kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akisoma hotuba ya ufunguzi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia burudani ya ngoma ya Kimasai, wakati akitoka kwenye Ukumbi wa AICC, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal)lililoanza leo katika jijini Arusha. Picha na OMR

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger