Featured Post Today
print this page
Latest Post

ANGALIA PICHA YA MFUNGWA ALIYETAKA KUTOROKA KWA KUTOBOA UKUTA

ANGALIA PICHA YA MFUNGWA ALIYETAKA KUTOROKA KWA KUTOBOA UKUTA

An overweight inmate who tried to escape a Brazilian jail through a hole smashed through a prison wall had to be rescued by firemen after he got stuck halfway through.
16-stone Rafael Valadao is surrounded by giggling guards after getting stuck in his escape hole
Rafael Valadão, the well-built tattooed convict, tried to follow one of his smaller fellow prisoners
who had already made a bid for freedom through the gap.
But he was left screaming for help when he became wedged while others tried to force him through the hole they had made with a metal shower pipe.
“He has a very large physique and is also very tall,” said Lieutenant Tiago Costa, of the local fire brigade.
“The other prisoners tried to push him but he stayed stuck in the wall. He started screaming in pain, and that was when the prison guards were alerted.”
The prisoner tried to break free late on Monday night at a prison in Ceres, near Goiania, according to Jornal Populacional.
0 comments

Q-CHILA "NIMEOTESHWA NDOTO YA USHINDI KUWA PAPII KOCHA ATARUDI URAIANI"

Q-CHILA "NIMEOTESHWA NDOTO YA USHINDI KUWA PAPII KOCHA ATARUDI URAIANI"

Muimbaji wa Beautiful, Q-Chilla amesema ameota ndoto kuwa Papii Kocha na baba yake Nguza Viking aka Babu Seya wataachiwa huru.

Leo, Jumatano, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani nchini Tanzania limeipitia upya hukumu yao.

“Nimeota ndoto ya ushindi, nimemuona Papii Kocha Sinza anakatiza barabara. Naotaga mara chache sana na huwa vitu vinatokea. Iko wazi kaka yangu anarudi uraiani. Nimemuona, welcome home, dunia ilikumiss, vita imekwisha,” Q-Chilla ameimbia Bongo5.

“Let the world know that the beloved kid is coming home.”

Katika rufaa hiyo leo wakili wa Babu Seya na Papii Kocha ameiomba mahakama hiyo ifute ushahidi na waachiwe huru lakini serikali imepinga. Kutokana na hatua hiyo, leo mahakama ya rufaa haijafanya uamuzi wowote imewapiga kalenda.

Nguza Viking na Papii Kocha wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya msingi.
0 comments

Saini zakusanywa kumng’oa Spika wa Bunge Anna Makinda.

Saini zakusanywa kumng’oa Spika wa Bunge Anna Makinda.

Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangalla, (CCM), leo anatarajiwa kuanza kukusanya saini za wabunge akitafuta kuungwa mkono katika hoja ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa madai kwamba amekuwa akikiuka kanuni za Bunge.
Dk Kigwangalla aliibua hoja ya kutokuwa na imani na Spika katika kikao cha wabunge wote cha kuelezea shughuli zitakazofanywa na Bunge katika mkutano wa 13, kilichofanyika juzi jioni kwenye ukumbi wa Pius Msekwa.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, jana alithibitisha kuwapo kwa mjadala huo katika kikao cha wabunge, lakini hakuwa tayari kueleza kwa undani na badala yake alisema kwamba leo ataanza kukusanya saini za wabunge kwa ajili ya kukamilisha hoja ya kutokuwa na imani na Spika Makinda.
Chanzo chetu kutoka katika kikao hicho cha wabunge kilibainisha kuwa Kigwangalla alihoji kuhusiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge (CCM-Bariadi Magharibi) kuteuliwa na Spika wakati katika kamati nyingine wenyeviti na makamu huchaguliwa na wajumbe wa kamati husika.
Pia Dk Kigwangala alisema Spika Makinda alivunja kanuni kwa kuwapa posho ya Sh430,000 kwa siku wajumbe wa kamati inayoongozwa na Chenge wakati wajumbe wa kamati nyingine wamekuwa wakipewa Sh130,000.
“Anachokifanya Spika ni matumizi mabaya ya fedha za umma, inakuwaje wengine wafanye kazi hata bila posho lakini wao (Kamati ya Bajeti), walipwe posho ya Sh430,000 kwa siku?” chanzo hicho kilimkariri Dk Kigwangalla akihoji. Hata hivyo, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah akizungumza na gazeti hili jana alisema mazingira ya kamati fulani kupata malipo ya ziada tofauti na viwango vya kawaida hutokea pale uongozi wa kamati husika unapoomba kwa Spika.
“Si kweli kwamba Kamati ya Bajeti inalipwa fedha za ziada kila wakati, hapana, ni pale tu wanapoomba malipo hayo kutokana na sababu ambazo lazima Spika aridhike nazo. Ieleweke kuwa siyo kamati hiyo tu, kwa sasa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ambayo inachambua miswada mingi nayo imekuwa ikiomba na baada ya Spika kuridhia basi nao wanapewa,” alisema Dk Kashililah.
Katibu huyo wa Bunge alieleza kuwa zaidi ya kamati nane zimewahi kuomba malipo ya ziada kwa maana ya kutaka posho zaidi, ulinzi, usafiri na hata chakula, ikiwa zinakabiliwa na majukumu ya ziada pia katika mazingira tofauti nje ya utaratibu wa kawaida.
“Kimsingi, kamati nyingi zinapewa malipo tofauti, watu wanaweza kuwa na kazi mpaka saa saba au nane usiku, au wanakwenda kufanya kazi katika mazingira yasiyokuwa ya kawaida, taratibu zinamruhusu Spika kama akiridhika na maelezo ya kazi husika, basi anaruhusu kutekelezwa kwa maombi hayo,” alisema Dk Kashililah.
Kuhusu Serukamba
Aidha, Dk Kigwangalla alinukuliwa akisema Spika amekiuka kanuni kwa kumchagua Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, Peter Serukamba (Kigoma Mjini-CCM), kuwa mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti.
“Hakuna mbunge yeyote aliyepo katika kamati mbili lakini hata kungekuwa na sababu maalumu basi wa kuteuliwa angekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara, Mahmoud Mgimwa (Mufindi Kaskazini-CCM) ambaye TRA (Mamlaka ya Mapato Nchini) ipo chini ya kamati yake,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kilisema Dk Kigwangalla alisema badala ya kumweka karibu katika ushiriki, Mgimwa alipokwenda katika kamati hiyo aliambulia kufukuzwa.
Akizungumzia suala hilo, Dk Kashililah alisema Serukamba pamoja na wabunge wengine kadhaa waliteuliwa na Spika kwa ajili ya kuongeza nguvu katika kamati hiyo wakati wa kipindi cha Bajeti Kuu ya Serikali.
Aliwataja wabunge wengine walioteuliwa kushiriki katika Kamati ya Bunge ya Bajeti kuwa ni John Cheyo (Bariadi Mashariki-UDP), Salahe Pamba (Pangani - CCM) na Hamadi Rashid Mohamed (Wawi - CUF).
Kanuni za Bunge
Kwa mujibu wa kanuni za Bunge katika toleo la mwaka 2007, kifungu cha 137(1), ili kumwondoa Spika madarakani, mbunge anayetaka kuwasilisha hoja hiyo atatakiwa kuwasilisha taarifa ya maandishi ya kusudio hilo kwa Katibu, akieleza sababu kamili ya kutaka kuleta hoja hiyo.
Kifungu kidogo cha pili kinasema baada ya kupokea taarifa ya maandishi ya kusudio la kumwondoa Spika kwenye madaraka, Katibu atapeleka taarifa hiyo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kujadiliwa.
Kifungu cha tatu kinabainisha kuwa endapo kamati hiyo itaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Spika zinazohusu uvunjaji wa masharti ya ibara husika za Katiba, sheria au kanuni zinazoongoza shughuli za Bunge, basi kamati hiyo itaidhinisha hoja hiyo ipelekwe bungeni ili iamuliwe.

Kanuni zinasema Naibu Spika, atakalia Kiti cha Spika wakati wa kujadili hoja ya kutaka kumwondoa Spika madarakani na Spika atakuwa na haki ya kujitetea wakati wa mjadala na kwamba ili kumwondoa zinahitajika kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya wabunge wote.

source:Mwananchi.
0 comments

N/WAZIRI MAKAMBA AVIPA CHANGAMOTO VIWANDA VYA CHAI BUMBULI.

N/WAZIRI MAKAMBA AVIPA CHANGAMOTO VIWANDA VYA CHAI BUMBULI.

Na Raisa Said, Bumbuli.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba amevipa changamoto  viwanda vya chai vya Hekulu na Dindira kuongeza uzalishaji ili kuweza kuchukua majani ya chai kutoka kwa wakulima wa zao la chai wa Bumbuli ambao walikuwa wakihudumiwa na Kiwanda cha Mponde.

Hatua hiyo inatokana na kiwanda cha chai cha Mponde kufungwa kutokana na mgogoro baina yawakulima wa chai na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (UTEGA) na mwekezaji.

Makamba, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Bumbuli aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na wakulima katika kijiji cha Tamota, kilichopo kata ya Tamota jimboni hapo, alisema hatua hiyo ni muhimu kwa kiwanda cha Mponde kilivyofungwa na viwanda hivyo viwili vikiongeza uzalishaji wakulima watapata mahali pa kuuzia majani ya chai na kujipatia kipato.

Alisema kuwa hivi sasa majani ya chai ni mengi hivyo hatua ya viwanda hivyo kuongeza uzalishaji ni nafuu kwa wakulima ikiwemo kuchangia kasi ya maendeleo kwa wananchi wa maeneo hayo.

Makamba alisema kuwa alikwisha kuzungumza na menejimenti za viwanda hivyo ili viongeze uzalishaji na vifaa vya kusafirishia chai kutoka mashambani hadi kwenye viwanda.

Alisema kuwa atavishauri viwanda hivyo kuweka utaratibu wa kuchukua majani ya chai mara tatu kila wiki kwa wakulima hao ili kukabiliana ongezeko hilo la majaniya chai.

Aliwataka wakulima kuwa wavumilivu wakati huu ambapo kuna mpango wa kuweka menejimenti ya muda kama ilivyokubaliwa na serikali ili kiwanda hicho kianze kazi ya kusindika majani ya chai.

Aliwataka viongozi wa UTEGA kuacha kuwatisha wakulima kwa kuwaambia kuwa watawakomesha kipindi hiki cha majani mengi ya chai na kwamba watahakikisha wanawapigia magoti ili kiwanda kifunguliwe.
0 comments

A MOSQUE AND 16 HOUSES TORCHED IN VIOLENT STRICKE

A MOSQUE AND 16 HOUSES TORCHED IN VIOLENT STRICKE

By Paskal Mbunga, Kilindi    October 30, 2013
AN unknown number of angry residents in Lulago village in Kilindi district have burned down a mosque used by an armed assailants who had tiraken refuge in the forests after killing a militia man last week.

A group of Tanga based journalists who toured the troubled area early this week were informed by the Chairman of Lulago village, Mohamed Waziri Mwariko that all the assailants were of the Ansar Sunni sect and that apart from torching down their mosque, but also 16 houses belonging to the assailants were completely burned to ashes.

The village chairman confirmed that the security atmosphere  was still tense because the main culprits were still at large, though the police has apprehended 18 of them.

Mwariko said there were three main ring leaders in the gang namely, Ayub Idd/a.k.a. Master and his lietnant, known by only one name, Jumanne. He named the third as Yusuf Said.

According to the village chairman, the torching down of the mosque belonging to the Ansar Sunni sect had nothing to do with religion strife or conflict but it was rather they (assailants) to blame for failing to live up according to the law of the land.

‘Let me clarify to you journalists that the torching of the mosque and the burned houses had no connection with religion strife”. 
He said and added that there is no christianity driven agenda or government intervention. It was the Ansar Sunni members whose open agenda was to disobey the government, calling it a kafir one.

The moslem population here is 99.5 per cent against other believers, he said adding that there are two mosques, apart from the torched one which belonged to the Ansar Sunni sect.   

According to residents of the village who talked to reporters, the Ansar Sunni members settled in the village in 20o9 without the consent of the village government. 
 Athumani Bakari and Mariam Abdallah said since they settled in the village, there has more chaos rather than peace in the village.

Another villager,  Mganga Kilimo said after their arrival in two buses  from Dar es Salaam, they singled out themselves from other villagers, saying that they cannot mingle with kafirs.
0 comments

UKUMBI WA MAZOEZI KIKWAZO NGUMI ZA RIDHAA TANGA.

UKUMBI WA MAZOEZI KIKWAZO NGUMI ZA RIDHAA TANGA.

Na Oscar Assenga,Tanga.
CHAMA cha Ngumi za Ridhaa mkoa wa Tanga(TBA)kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutokuwa na ukumbi wa kufanya mazoezi kwa mabondia kitendo ambacho kinawapa wakati mgumu mabondia wakati wa kufanya mazoezi.


Mwenyekiti wa Chama hicho,Mansour Soud Semfyoa aliiambia Tanga Raha kuwa hali hiyo inawafanya mabondia hao kushindwa kutimiza ndoto zao na kuziomba mamlaka husika ikiwemo uongozi wa serikali ya wilaya kuwasaidia ili kuweza kupatikana ukumbi wa mazoezi.

Soud alisema suala lengine ambalo linawapa changamoto ni uhaba wa vifaa vya kufanyia mazoezi kwa mabondia waliopo mkoani hapa hivyo kuwaomba wadau kuwasaidia ili viweze kupatikana.

MWENYEKITI WA CHAMA CHA NGUMU ZA RIDHAA MKOA WA TANGA,MANSOUR SOUD SEMFYOA
Mwenyekiti huyo alisema chama hicho kimefanya jitihada mbalimbali ili kuweza kupatikana ukumbi wa Tangamano ambapo uongozi wa chama hicho  tayari umeshaandika barua kwenda kwa mkurugenzi wa Jiji lengo likiwa ni kumuomba wautumia ukumbi wa Tangamano.

Alisema majibu ya barua hiyo iliwajibu wamekubaliwa katika ukumbi wa Communite Centre Makorora ambapo wataungana na vikundi vyengine na kuelezwa kuwa wanatakiwa walipie sh.elfu hamsini ili waweze kupewa eneo hilo.

Aidha alisema mikakati waliokuwa nayo hivi sasa ni kuuendeleza mchezo wa ngumi ambao unaonekana kupotea mkoani hapa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali lengo likiwa ni kupata mabondia wazuri ambao watautangaza mkoa huu.

Aliongeza kuwa wanampango wa kuupeleka mchezo huo mashuleni ambapo kwa kuanzia wataanzia katika shule za msingi na sekondari na baadae vyuo vikuu lengo ni kuwapa vijana hao uelewa kuhusu mchezo huo.

Soud alisema pia wanatarajia kuanzisha miradi ambayo itakisaidia chama hicho kujiendesha chenyewe kuliko kutegemea misaada ambao wakati mwengine inaweza kukwamisha malengo yao waliojiwekea.    

CHAMA CHA NGUMI ZA RIDHAA TANGA WALILIA UKUMBI WA MAZOEZI

MABONDIA WA MKOA WA TANGA WAKIFANYA MAZOEZI KATIKA UWANJA WA VALLEYBALL MKWAKWANI KUTOKANA NA KUKOSA UKUMBI MAALUMU




0 comments

wapinzani kusimamisha mgombea mmoja 2015

wapinzani kusimamisha mgombea mmoja 2015

mbatia-k1 596f0
UPEPO wa mabadiliko ya kisiasa unaovuma kuelekea kambi ya upinzani, sasa unaonekana kuwaamsha viongozi wa vyama hivyo baada ya kutolewa kwa taarifa kuwa wanafikiria kusimamisha mgombea mmoja wa urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. (HM)

Taarifa zilizolifikia gazeti hili kabla ya kuthibitishwa na mmoja wa viongozi hao, zilieleza kuwa hatua ya vyama hivyo imekuja baada ya ushirika wao waliouunda kupinga upungufu uliokuwemo kwenye Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kuzaa matunda.
Pamoja na hilo, inaelezwa kuwa maamuzi hayo magumu ya wapinzani yametiwa chachu na kauli aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete ya hivi karibuni ya kukitabiria anguko Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi wa mwaka 2015 au ule wa 2020, kutokana na kile alichodai kuwa viongozi wa chama hicho kuendekeza rushwa.
Mmoja wa viongozi wanaounda ushirika huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alithibitisha taarifa hizo huku akisisitiza kuwa nia ya kufanya hivyo ni kuhakikisha wanaiondoa madarakani CCM mwaka 2015.
Kwa mujibu wa Mbatia, walichokifanya kwenye Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba si nguvu ya soda na badala yake wataendeleza hadi kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Mbatia alisema kuwa uongozi wa vyama vya upinzani unatarajia kuungana na kumsimamisha mgombea mmoja, ili kuhakikisha wanaiondoa madarakani CCM.
Mbatia ambaye alikuwa akizungumza katika mahojiano maalumu na RAI Jumatano, alisema hatua hiyo pamoja na ushirika wao unalenga kudumisha amani na uzalendo kwa kuweka utaifa mbele.
Alisema umoja wanaoendelea kuuonyesha kwenye mchakato wa Katiba Mpya, ambao unalenga kuweka mbele maslahi ya Taifa ili kuhakikisha inapatikana Katiba bora yenye kushirikisha Watanzania wote, wataufanya pia kwenye chaguzi mbalimbali.
"Ili jambo lolote litokee lazima kuwepo na chanzo, mwanzo wetu wa ushirikiano ulioanza Septemba mwaka huu ndani ya ukumbi wa Bunge, tutauendeleza.
"Tupo kwenye maridhiano zaidi, hata muungano wetu wa Tanzania bara na Zanzibar si wa kisheria, viongozi wetu Nyerere na Mzee Karume walikaa na kuzungumza, hata sisi tunafanya hivyo, tunatakiwa kuzungumza kwa maslahi ya nchi," alisisitiza Mbatia.
Alisema vyama vyao viliamua kuwa na ushirikiano wa pamoja kutokana na kubaini kwamba, bila umoja hakuna kitakachofanikiwa.
"Tumeshaanza kuzungumza kwa mapana juu ya ushirikiano wetu, ukweli ni kwamba kuna mwelekeo mzuri," alisema.
Alisema hatua ya vyama kujadili kwa pamoja mchakato wa Katiba ni dalili njema za kuelekea kwenye mafanikio na ndio maana wanaona ipo haja ya kuuendeleza ushirika huo hadi kwenye chaguzi mbalimbali nchini.
"Tunapaswa kuvifanya vyama vyetu viwe vya maslahi mapana kwa taifa, ili visionekane vipo kwa ajili ya maslahi ya viongozi.
"Kwa kuwa tumeweka maslahi ya taifa mbele kwenye suala la Katiba, tumeona tuwe na mfumo ambao utalisaidia taifa, ndio maana hata tulipotoka Ikulu tumekubaliana kuwa Tanzania kwanza vyama baadaye, naamini kwa nia njema hata ule ushirikiano wetu utaendelea mbele zaidi kwa maslahi mapana ya taifa letu, tunategemea hivyo... tuna mategemeo mazuri, lazima tufikirie chanya," alisema Mbatia.
Kauli ya Mbatia imeungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Julius Mtatiro ambaye ameeleza kuwa chama chao hakina tatizo kwenye suala la kumsimamisha mgombea mmoja na wako tayari kwa sababu ushirikiano ni suala la msingi na lenye maana.
"Kulingana na upepo wa kisiasa ulivyo sasa, ni dhahiri tunahitaji kushirikiana ili kukiondoa chama tawala madarakani, kwa sababu mahali tulipo sasa ni pagumu.
"Tunachosubiri sasa ili kukamilisha muungano wetu ni tamko la pamoja kutoka kwa viongozi wa juu wa vyama vyote, lakini naamini nia ya kusimamisha mgombea mmoja itakubalika bila kupingwa," alisema Mtatiro.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Habari kutoka Chadema, John Mnyika, alisema ushirikiano kwa sasa umejikita kwenye suala la kunusuru mchakato wa Katiba na kuwezesha nchi kupata Katiba bora.
Alisema ushirikiano katika masuala mengine ikiwamo pendekezo la kushirikiana katika uchaguzi, litatafakariwa kwa kuzingatia mafanikio katika ushirikiano kwenye suala la mchakato wa Katiba Mpya ambao tunaendelea nao kwa sasa.
"Huu ndio msimamo ambao naamini pia viongozi wote wanao.
"Kwa kuzingatia kauli zilizotolewa na wenyeviti wote watatu Septemba 15 mwaka huu kwenye mkutano na waandishi wa habari, wakati wa kutoa tamko la pamoja la ushirikiano," alisema.
Hata hivyo, mchambuzi wa masuala ya siasa nchini, Dk. Benson Bana ameukosoa uamuzi huo kwa kudai kuwa hawawezi kuungana kwa sababu hawana kiwango cha kuing'oa CCM madarakani.
Dk. Bana aliweka wazi kwamba, hadhani kama vyama hivyo vitafaulu kuitoa CCM madarakani, kwa sababu havina mtaji wa kutosha wa wanachama.
Alieleza kuwa vyama vyote vitatu vinavyojiona vinaisumbua CCM, ambavyo ni CUF, Chadema na NCCR-Mageuzi, havijafanya utafiti wa kutosha kubaini mtaji wa wapiga kura walio nao.
Alisema Chadema ina nguvu ndogo Bara hasa kwenye maeneo ya mijini, CUF ina nguvu Zanzibar na NCCR-Mageuzi haina nguvu ya aina yoyote jambo linaloashiria udhaifu wa vyama hivyo, ambapo alivitaka kujipa muda wa kujipanga kabla ya kufikiria kuing'oa CCM.
Wenye mtazamo tofauti na huo wanasema kuwa endapo hatua hiyo ya vyama vya upinzani itafanikiwa, ni wazi itathibitisha kauli ya Mwenyekiti wa CCM kwamba chama hicho kijiandae kung'oka mwaka 2015 au 2020.
Hata hivyo bado kuna shaka juu ya maamuzi hayo ya vyama vya upinzani, kutokana na yale ambayo yamepata kushuhudiwa katika chaguzi nyingine zilizotangulia hususani zile za viti vya ubunge.
Imeshuhudiwa katika chaguzi kadhaa vyama hivyo vikisigana kufikia maamuzi ya kuachiana maeneo ya kusimamisha wagombea wenye nguvu.
Mwaka 2010 kwenye uchaguzi Mkuu, CUF kilikitaka Chadema kutosimamisha mgombea kwenye Jimbo la Tunduru kutokana chama chao kuwa na nguvu, hata hivyo wenzao walikataa.
Hali hiyo pia ilijitokeza kwenye Jimbo la Kiteto, Chadema iliitaka CUF kutosimamisha mgombea jambo ambalo halikutekelezwa. Chanzo: mtanzania
0 comments

M23 yachakazwa, viongozi watimka

M23 yachakazwa, viongozi watimka

mejakomba_edffb.jpg

Kuna ripoti kwamba Kundi la Waasi la M23 ambalo limekuwa likisababisha mapigano katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), limesambaratishwa katika operesheni kali iliyoendeshwa kwa ushirikiano baina ya vikosi vya nchi hiyo na vile vya Umoja wa Mataifa.

Taarifa za kusambaratishwa kwa kundi hilo zimekuja siku chache baada ya kuzuka mapigano makali yaliyosababisha kuuawa kwa askari mmoja wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Rajab Ahmed Mlima aliyeuawa kwa kupigwa risasi akiwa katika operesheni ya kuwaokoa raia, waliokuwa wamenasa kwenye eneo la mapigano.

Wanajeshi wa Tanzania ni sehemu ya vikosi vya Umoja wa Mataifa vya Kulinda Amani huko Congo (Monusco) vyenye askari pia kutoka Afrika Kusini na Malawi, vikiwa na kazi ya kupambana na kupokonya silaha za vikundi vya waasi wanaopigana kwenye nchi hiyo.

Mkuu wa Vikosi vya Monusco, Martin Kobler alithibitisha taarifa za kusambaratika kwa kundi hilo la M23 na kuongeza kuwa vikosi vya Serikali na vile vya UN vilikuwa vikiendesha doria katika maeneo yaliyokuwa yakidhibitiwa.

Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) liliripoti jana kuwa Kiongozi wa M23, Bertrand Bisimwa amekimbia mashambulizi kwa kuvuka mpaka na kuingia Uganda wakati majeshi ya Congo yalipokuwa yanakaribia ngome yao.
Katika taarifa yake aliyoitoa mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juzi, Kobler alisema Kundi la M23 limepoteza mwelekeo.

"Ninachoweza kusema sasa tumefanikiwa kuwasambaratisha waasi na sasa vikosi vyetu kwa kushirikiana na vile vya DRC Congo vinadhibiti maeneo yote," alisema Kobler.

Hata hivyo, Msemaji wa JWTZ, Meja Eric Komba alisema asingeweza kutoa maelezo ya kina kuhusiana na taarifa za kusambaratishwa kwa kundi hilo la waasi, kwa vile wazungumzaji wakuu wa suala hilo ni Umoja wa Mataifa.

"Kama mnavyojua sisi tumekwenda DRC Congo kwa ridhaa ya Umoja wa Mataifa, hivyo kufanikiwa ama kushindwa kwa operesheni yoyote iko chini ya Umoja wa Mataifa wenyewe. Tanzania haiwezi kusema kwamba vikosi vyetu vimewasambaratisha waasi wakati mwenye jukumu la mwisho kutoa tamko hilo ni UN wenyewe," alisema Meja Komba.
Wakati hali ikiripotiwa kuwa hivyo, taarifa zinasema kuwa kundi hilo la M23 limemeguka mara mbili na kuzaliwa kundi jingine linalojiita M18. Maofisa wa Serikali ya Uganda wamesema kuwa kujitokeza kwa kundi hilo jipya kunaashiria kifo cha Kundi la M23 ambalo kwa miaka mingi limekuwa likidhibiti maeneo yanayotajwa kuwa na utajiri wa madini.

Kundi hilo la waasi ambalo limekuwa likidaiwa kupata msaada wa kijeshi kutoka kwa mataifa ya Rwanda na Uganda, limeelezwa kuelemewa nguvu na limesalimu amri katika maeneo liliyokuwa likishikilia.

Vikosi hivyo vya M23 vilianzisha upya mapigano hayo na kufanikiwa kuteka baadhi ya miji muhimu baada ya kuvunjika kwa mazungumzo ya amani yaliyokuwa yakiendelea Kampala, Uganda.
Waasi wakimbilia porini

Baada ya kutorokwa na viongozi wao, kuna taarifa askari wa kawaida wa Kundi la M23 wamejificha kwenye misitu ya mpaka wa DRC Congo na nchi za Rwanda na Uganda.

Msemaji la Jeshi la DRC, Olivier Hamuli aliliambia Shirika la Habari la Uingereza (Reuters) katika eneo la mapigano karibu na Goma kuwa Kundi la M23 limedhoofika baada ya kukimbiwa na askari wapatao 40, ambao wamejificha kwenye milima ya karibu na mpaka wa Rwanda.

"Kuna kundi dogo la M23 linapigana karibu na milima ya Rwanda," alisema. "Nadhani Rwanda watapaswa kufanya uungwana na kuwakamata."

Kundi la M23 lilianzisha vita mwaka 2012 baada ya baadhi ya askari wa Jeshi la DRC Congo kuasi baada ya kutoridhishwa na utekelezaji wa mkataba wa amani wa mwaka 2009, uliosainiwa na waasi hao wanaoaminika kusaidiwa na Rwanda.
DRC waandaa dua

Habari zaidi kutoka DRC Congo zinasema kuwa wafuasi wa dini ya Kiislamu katika mji wa Goma walifanya swala maalumu kwa ajili ya kuwaombea askari wa nchi hiyo na wale wa Umoja wa Mataifa waliofariki dunia kwenye operesheni hiyo.
Pia waliahidi kuandaa maandamano makubwa kwa ajili ya kushinikiza kuondoka kwa raia kutoka India na wale kutoka nchi za Ulaya kwani wanaamini ndio wamekuwa wakiwasaidia waasi kifedha.

Chanzo:Mwananchi
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger