Featured Post Today
print this page
Latest Post

MAGEREZA MKOA WA TANGA YAANZA MAANDALIZI YA UKARABATI WA OFISI MPYA ZA UTAWALA, JIJINI TANGA

MAGEREZA MKOA WA TANGA YAANZA MAANDALIZI YA UKARABATI WA OFISI MPYA ZA UTAWALA, JIJINI TANGA

 Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya(wa pili kulia) akielezea hatua mbalimbali za Maandalizi ya ukarabati wa Jengo la Ofisi za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga(wa kwanza kulia) ni Afisa Habari wa Jeshi la Magereza, Mkaguzi wa Magereza Deodatus Kazinja alipotembelea kujionea hatua mbalimbali za ukarabati unaoendelea leo Februari 7, 2014 Jijini Tanga.
 Muonekano wa mbele wa Jengo la Kikoloni ambalo linalotarajiwa kukarabatiwa kwa ajili ya Ofisi za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga. Jengo hilo hapo awali lilitumika kama Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Tanga ambapo hivi sasa Jeshi la Magereza tayari limeanza ukarabati wa jengo hilo. Wa kwanza katika picha ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya akiwa ameongozana na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza leo Februari 07, 2014 Jijini Tanga.
 Tofali ambazo zimefyatuliwa kwa ajili ya ukarabati wa Jengo la Ofisi za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga. Ukarabati huo wa Ofisi mpya za Utawala unaanza hivi karibuni Jijini Tanga na utasimamia kwa karibu na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga.
 Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya akiongoza Kikao kazi Ofsini kwake pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wanaofanya kazi Ofisi ya Magereza Mkoa wa Tanga leo Februari 07, 2014 alipotembelewa Ofsini kwake na timu ya Maafisa Habari kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaaam(hawapo pichani)
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Naibu Kamishna wa Magereza Edither Malya(wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wanaofanya kazi Magereza Mkoa wa Tanga baada ya kutembelea sehemu mbalimbali ya maandalizi ya ukarabati wa Ofisi  Mpya za Utawala za Magereza Mkoa wa Tanga leo Februari 07, 2014(wa Nne kulia) ni Mnadhimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Augustino Mboje
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
0 comments

Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira yatembelea hifadhi ya Tarangire

Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira yatembelea hifadhi ya Tarangire

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya ardhi, maliasili na mazingira wakijiandaa kwa safari ya kuelekea katika hifadhi ya Tarangire, iliyoko wilayani Babati, mkoa wa Manyara.
Mbunge wa Luchoto, Dkt. Henry Daffa Shekifu (katikati) akisalimiana na askari muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kuelekea Hifadhi ya Tarangire, kushoto kwake ni Mkurugenzi mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira katika ofisi za hifadhi ya Tarangire, wakisikiliza taarifa ya uhuifadhi kutoka kwa Mhifadhi Mkuu, Stephano Kolli (hayupo pichani).
Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi, maliasili na mazingira, James Lembeli, akijadiliana jambo na Mkurugenzi mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi (aliyeinama).
Mhifadhi mkuu wa Tarangire, Stephano Kolli, akitoa taarifa ya hifadhi kwa kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliyotembelea Hifadhi hiyo.
Muda wa kuanza safari kuelekea katika eneo la mradi, mbele ni mhifadhi wa Tarangire, Stephanojumbe Kolli,wajumbe na waandishi wa habari.
0 comments

RC GALLAWA AWAFARIJI WANANCHI WALIEZULIWA NYUMBA ZAO KOROGWE NA MUHEZA

RC GALLAWA AWAFARIJI WANANCHI WALIEZULIWA NYUMBA ZAO KOROGWE NA MUHEZA

Picha namba 9274 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa
kushoto akitoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa Kijiji Lusanga kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe Thabiti Selemani mwenye kofia jinsi ya kuutumia msaada huo wa unga kwa wananchi walioathirika.
Afisa Rasilimali wa Kiwanda cha Unga jijini Tanga cha Pembe, Salele Masoudy kushoto akimkabidhi Msaada wa Unga kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Lusanga kata ya Mnyunzi,Thabiti Selemani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kushoto na Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo wakishuhudia makabidhiano hayo
MKUU wa Mkoa wa Taga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akisisitiza jambo kwa wananchi wa Kijiji cha Lusanga kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe  kilichokumbwa na maafa ya wananchi wake kuezuliwa mabati kwenye nyumba za kaya 83 wilayani humo uliotokana na upepo mkali ulioaambatana na mvua juzi ukushoto ni Afisa Rasilimali wa Kiwanda cha Unga cha Pembe jijini TangaSalele Masoudy  na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo
0 comments

ANATAFUTWA NA POLISI TANGA KWA KUMUUA MWENZAKE KTK UGOMVI WA WA KUGOMBEA SIGARA.

ANATAFUTWA NA POLISI TANGA KWA KUMUUA MWENZAKE KTK UGOMVI WA WA KUGOMBEA SIGARA.


Jeshi la polisi mkoa wa Tanga linamsaka  mtu mmoja  baada ya kumuuwa mwenzake wakiwa wanagombania sigara.
 kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Costantino  Masawe (pichani)amemtaja mtu huyo ambaye amefanya tukio hilo  kuwa ni Iddi mkono  mwenye umri wa miaka 30 mkazi wa kijiji cha kwamdolwa kata ya kwamdolwa wilayani Korogwe mkoani hapa ambaye alimkata mwenzake mkono kwa kutumia panga wakiwa wakigombania sigara na kumsababishia umauti.
Kamanda masawe amemtaja mtu aliyefariki kwa jina la Ramadhani Budalo 35 naye anaishi katika  kijiji cha kwamdolwa kata ya kwamdolwa wilayani Korogwe mkoani hapa,
Hata hivyo watu hawa walikuwa katika ugovi na kufikia atua ya kushikiana panga na mmoja akamuwahi mwenzie na kusababishia jeraha na ikawa ndiyo mwisho wake na aliye fanya unyama huo alitoroka ambapo jitihada za kumtafuta zinaendelea iliafikishwe kwenye vyombo vya sheria
Pia kamanda huyo akusita kutoa wito kwa wakazi wa mkoa wa tanga kujiepusha na ugovi,kutofanya maamuzi ya gafra na kujichukulia sheria mkononi kwani ni kofa pia inahatarisha amani ndani ya jamii.
0 comments

SOKO LA SAMAKI DEEP SEA KAMA LINAVYOONEKA IJUMAA YA LEO

SOKO LA SAMAKI, DEEP SEA KAMA LINAVYOONEKA IJUMAA YA LEO



Eneo maarufu jirani na bandari ya Tanga inayojulikana kwa jina la deep sea, eneo ambalo ni maarufu kwa uuzaji wa samaki wa aina mbalimbali, nalo ni miongoni mwa maeneo yaliyokumbwa na chungu ya msalagambo





Masalia ya vifaa vilivyokuwa vimetumika ktk ujenzi wa mabanda ya biashara ktk eneo hilo la deep sea






Ni zaidi ya miaka miwili au mitatu mpaka sasa halmashauri ya jiji  la  tanga linatekeleza na kuendeleza kampeni ya weka jiji katika hali ya usafi ambayo inatambulika na kila mmoja wa wakazi wa jiji la Tanga kwa kushiriki kufanya usafi katika mazingira wanayoishi na pia kujitoa kikamilifu  kufanikisha zoezi hilo lifanikiwe

Viongozi wa ngazi ya mkoa,wilaya,tarafa, kata kijiji hadi mtaa wameweka utaratibu wakuwafanya kila mmoja aweze kushiriki kikamilifu kutekeleza kampeni ya kuweka jiji katika haliya usafi ambayo imepewa jina la kalembo day abayo wakazi wanashiriki kwa pamoja kusafisha na kuzibua mitaro au kurekebisha sehemu kolofi ndani ya maeneo yao, yote kufanikisha kampeni hiyo.

Je,unajua kwanini kampeni hiyo imepewa jina la kalembo daya.imetokana na jina la aliyekuwa mkuu wa mkoa wa tanga said said kalembo alivyo shikiria kidete na kusimamia zoezi hilo kwani ilimlazimu kupita mitaani na kuamasisha usafi wa mazingira lifanikiwe, kwa upande mwengine zoezi hilo lilionekana kama na la watu wachache au  ubabe binafsi kwa viongozi tu,kumbe siyo sahii  bali  hiyo ni  la wote nakuweka afya ya wananchi kuwa bora.

Utaratibu uluwekwa kila jumamosi yakwanza ya mwezi zoezi hilo linafanyika kwa kila mmoja pia ililazimika kutolewe amri kila mfanya biashara mkubwa au mdogo kuto fungua biashara yake mpaka saa tatu asubihi, hali hiyo ilifanyika kila mwezi kwa umuhimu wajambo hilo viongozi waka onelea iendelee kwa kila wiki ili kuendeleza na kutekeleza zoezi hilo na limepiga hatua na mafanikio yanaonekana.

Baada ya kuondoka mkuu wa mkoa huyo utawala ulishikwa na luteni mstaafu bi chiku galawa ambaye amesima kidete kuendelea na kutekeleza kwa vikali swala hilo kwa kutoa mwanya kwa taasiai binafsi,mashirika,vyama vya siasa,vikundi mbalimbali,vyombo vya habari  na mtu mmoja mmoja kwanafasi yake kufanikisha kampeni ya msalagambi(kalembo day) cha kupendeza zaidi


wasani wa vikuni vya ngoma,maigizo na wale wa kizazi kipya wametumia vipajivya kwa kutunga na kuimba amakuigiza ili kufikisha ujumbe wa kufanya usafi wa jiji la Tanga.

Ila ukitaka maendeleo na afya bora nilazima maeneo yaani mazingira tunayoishi yawe masafi itafayanya kuimarisha upana wa mawazo wakufikiri na magonjwa yanayo sababishwa na uchafu yatapungua,kwani kwasasa jiji la tanga nitofauti na kipindi cha nyuma magonjwa kama kipindu pindu na magojwa mengine yanayo sabaisha yamepungua wa mujibu wa wakazi wa jiji hili

Kwa sasa hali ya usafi kwa jiji la tanga linavutia na kulizisha kwani wahenga walisema mwenye macho ambiwi tazama pia wakazi wa jiji hilo wanatama wageni siku baada siku na kwapamba kwa ule usemi wao usemao “waja leo waondoa leo” huu usemi unamaana kubwa sana hatakama ulikuja wawenyeji hao na kuaa mwezi wao wanaona ni muda mfupi basi wanazidi kuwapoke wageni mbalimbali baada ya kampeni hizo ambazo zina endele mpaka na mafanikio yanaoneka.

Hata hivyo hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Tanga Chiku Galawa alipokuwa akifungua mafunzo ya watafiti wa kutambua watu wenye uwezo wa kufanya kaziuliyo fanyika jiji hapa wa kanda ya masariki yaani Arusha,Kilimanjaro,manyara na tanga alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wageni hao kwakusema “jiji la tanga ni safi,mazingira mazury bustani za mapumziko na sehemu za burudani zipo za tosha muwe na amani karibuni tanga mkatangaze uzuri wetu”

Kwa pamoja tunaweza endapo tukishirikiana kwa pamoja kwani changamo ndani ya zoezi hilo zipo ila tujivunie matokeo tuliyo yapata tusiishie hapa tuwaunge mkono viongozi tunaweza. Vizuri vina higwa tuige mfano wajiji la tanga kwa kampeni yao ya kalembo day.  
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger