Featured Post Today
print this page
Latest Post

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA NCHI WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NGUO KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA (CAPA)

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA NCHI WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NGUO KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA (CAPA)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya Kinyago kutoka kwa Makamu wa Mwenyekiti wa CAPA wa Kanda ya Afrika Magharibi, Prof. Daniel Nyarko, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa nne kushoto), Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya CAPA,John Kondoro (kushoto kwa Makamu) na baadhi ya viongozi wa CAPA, wakifurahia kwa pamoja baada ya kuzindua rasmi Jarida la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal), wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakiwa makini kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akisoma hotuba ya ufunguzi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia burudani ya ngoma ya Kimasai, wakati akitoka kwenye Ukumbi wa AICC, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal)lililoanza leo katika jijini Arusha. Picha na OMR

0 comments

NAIBU WAZIRI UMMY MWALIMU APOKEA SHLLLINGI MILIONI 100 KWA NIABA YA TAYOA KUTOKA NBC KUSAIDIA VIJANA!!

NAIBU WAZIRI UMMY MWALIMU APOKEA SHLLLINGI MILIONI 100 KWA NIABA YA TAYOA KUTOKA NBC KUSAIDIA VIJANA!!


 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) akipokea mfano wa hundi ya shs milioni 100 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bi. Mizinga Melu kusaidia mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA). Hafla ilifanyika wakati wa tukio la uzinduzi wa mradi huo unaodhaminiwa na NBC jijini Dar es Salaam jana. Katikani ni Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika.
 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bi. Mizinga Melu (katikati) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Bi. Mwinda Kiula Mfugale wakionyesha vipeperushi kuashiria uzinduzi wa tofuti ya vijanatz.com ikiwa na habari kuhusu ajira (kazitz.com), fedha (fedhatz.com) na ujasiriamali (biasharatz.com). Hafla hiyo ilikwenda sambamba na uzinduzi wa mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana  wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA) unaodhaminiwa na NBC.
3: Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Mizinga Melu akishikana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika baada ya kukabidhi  mfano wa hundi ya shs milioni 100 zilitotolewa na benki hiyo kusaidia mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA). Hafla ilifanyika wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo unaodhaminiwa na NBC. Kushoto ni Naibu Waziri wa Maendeleo aya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu na kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula Mfugale.
 Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika (kushoto), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia), na Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa NBC, William Kallaghe wakibadilishana mawazo katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika (kushoto), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia), na Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa NBC, William Kallaghe wakibadilishana mawazo katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Mizinga Melu akizungumza na vijana na wageni wengine kuhusu huduma za kibenki na kuhusu mikakati ya benki kusaidia suala la ajira na ujasiriamali kwa vijana katika hafla hiyo.
Wasanii wakitoa burudani kusindikiza uzinduzi wa mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA) unaodhaminiwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jijini Dar es Salaam
0 comments

RAIS WA MALAWI JOYCE BANDA ASHITAKIWE UMOJA WA NCHI ZA AFRICA

RAIS WA MALAWI JOYCE BANDA ASHITAKIWE UMOJA WA NCHI ZA AFRICA

Taasisi isiyo ya kiserikali inayoshughulikia mambo ya utawala bora na maendeleo nchini (The Center for Good Governance and Development in Tanzania -CEGODETA), imeitaka Serikali ya Tanzania kumshtaki Rais wa Malawi, Joyce Banda Umoja wa Nchi za Afrika (AU).

Taarifa ya taasisi hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Thomas Ngawaiya ilisema uamuzi huo ni kutokana na kauli za dharau za Banda dhidi ya viongozi wanaoshughulikia mgogoro wa Ziwa Nyasa.

“Serikali imshtaki kiongozi huyo wa Malawi AU ili aulizwe ana dhamira gani kwa Tanzania na Afrika kabla hajaleta madhara makubwa kwa nchi yetu na Bara zima la Afrika.

Waswahili husema ‘Mchelea mwana kulia hulia yeye’ na ‘Mdharau mwiba mguu huota tende’, maana yake ni kuwa inawezekana huyu mtu ana mtandao mbaya sana tusioujua, tufanye uchunguzi kuubaini,” inasema taarifa hiyo.

Inasema kuwa, mara tu baada ya kuingia madarakani Rais Banda alidai kuwa Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi kwa asilimia 100 na Tanzania haina haki ya kulitumia ziwa hilo kwa njia yoyote ile.

Taarifa hiyo inasema kuwa, mgogoro huo kwa sasa uko kwenye jopo la usuluhishi la marais wastaafu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) chini ya Rais Mstaafu, Joachim Chissano wa Msumbiji.

0 comments

TANZANIA, CONGO NA BURUNDI WAUNDA MUUNGANO WAO BAADA YA KUTENGENGWA

TANZANIA, CONGO NA BURUNDI WAUNDA MUUNGANO WAO BAADA YA KUTENGENGWA

Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa `Umoja wa Walio Tayari’ , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao.
  
Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.

Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.
Mkutano wa ujirani mwema
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.
Alisema mkutano huo ulilenga kuboresha miundombinu ya usafiri katika Ziwa Tanganyika ambalo linaziunganisha Burundi Tanzania, DRC na Zambia.
Pia tumepanga kuendeleza reli ya kati kutoka eneo la Uvinza, Tanzania hadi Msongati, Burundi na pia kuunganisha Barabara ya Manyoni - Tabora - Kigoma kupitia Bujumbura hadi Kivu ya Kusini, DRC,” alisema Sitta.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Sitta pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Burundi, Leontine Nzeyimana na Waziri wa Uchukuzi wa DRC, Jack Lukeba.
Pia tulitembelea Bandari ya Kalindo iliyoko katika Ziwa Tanganyika upande wa Burundi kwani tunataka kuboresha bandari za ziwa hilo,” alisema Sitta.
Waziri huyo alisema Tanzania na Burundi zitaunganishwa na Barabara ya Manyoni – Tabora - Kigoma na Barabara ya Manyovu - Mgina, Mabanda - Bujumbura itakayounganishwa mpaka Kivu ya Kusini, DRC.
Kuhusu usafiri wa anga, Sitta alisema nchi hizo zinaangalia uwezekano wa kuanzisha safari za ndege za Dar es Salaam mpaka Bujumbura.

0 comments

PRINCESS OF SAUDI ARABIA VISIT TANAPA HEADQUATERS

PRINCESS OF SAUDI ARABIA VISIT TANAPA HEADQUATERS

aa_cb654.jpg
Princess Haifa Bin AbdulAziz of Saudi Arabia (far left) inspired by the statue of the Father of Nation the late Mwalimu Julius Nyerere at the reception of the TANAPA Headquarters in Arusha.In the middle with black suit is the Saudi Arabian Ambassador to Tanzania H.E. Hani Mominah while TANAPA's Public Relations Manager Pascal Shelutete (first right) is also looking on.
bb_c8353.jpg
Princess Haifa signing a visitors book at the office of the Director General of TANAPA.
cc_a058b.jpg
Princess Haifa (middle) in a talk with the Director General of TANAPA Allan Kijazi (far right) while the Ambassador Hani Mominah is paying attention.
dd_fafdc.jpg

Princess Haifa and her delegation in a discussion with the Management of TANAPA
PRINCESS OF SAUDI ARABIA VISIT TANAPA HEADQUARTERS
Princess Haifa Bin AbdulAzizi Mogrin of Saudi Arabia visited Tanzania National Parks Headquarters in Arusha yesterday and held talks with the Management of TANAPA regarding the forthcoming youth forum on Biodiversity Conservation scheduled for January next year in Arusha.
The Princess who is the coordinator of the forum, discussed with TANAPA on how best the forum can be conducted. The main theme of the forum is
"Construction and Implementation of the Regulatory Framework for Biodiversity Conservation" and will involve about 50 youths from both
Tanzania and Saudi Arabia who will have an opportunity to interact and discuss on the future of biodiversity conservation in the two countries.

TANAPA has been appointed by the Government of Saudi Arabia to host the forum in Arusha. The youth forum is an initiative by King Abdullah Bin Abdulazizi for dialogue among the forums worldwide under the program Saudi International Youth Dialogue Forums. These forums provide the platform for Saudi youth to interact with their peers from different countries, while adopting their creative initiatives and solutions under various themes.
The upcoming Saudi‑Tanzania Youth Dialogue Forum (STYF) will include a delegation of Saudi Youth who will be visiting Tanzania to learn about and
review, with their Tanzanian counterparts, the structural framework of various agencies or societies and their roles in addition to the implementation systems of regulatory framework for biodiversity conservation in the two countries. The objective of the forum is to develop initiatives to ensure more effective conservation practices locally and globally.

On his side, Director General TANAPA Allan Kijazi said TANAPA will do everything possible to ensure that the forum will bear fruitful results.
ISSUED BY PUBLIC RELATIONS DEPARTMENT
TANZANIA NATIONAL PARKS
28 TH NOVEMBER, 2013

0 comments

STARS YATOA SARE NA MABINGWA WA AFRIKA, KIWANGO CHA TIMU CHARIDHISHA

STARS YATOA SARE NA MABINGWA WA AFRIKA, KIWANGO CHA TIMU CHARIDHISHA

GOLI_LA_STARS_879d6.jpg

Mrisho Ngassa akishangilia baada ya Said Morad (hayupo pichani) kuisawazish Stars, huku kipa wa Zambia na mabeki wake wakiwa wameduwaa

Na Mahmoud Zubeiry, Machakos

TANZANIA Bara, Kilimanjaro Stars imeanza taratibu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kutoa sare ya 1-1 na mabingwa wa zamani wa Afrika, Zambia au Chipolopolo kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos, Kenya.

Katika mchezo huo wa Kundi B, Zambia ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Ronald Kampamba dakika ya 41, akiunganisha kwa kichwa krosi ya Felix Katongo.

Zambia walitawala zaidi mchezo huo kipindi cha kwanza na kutengeneza nafasi zaidi ya nne za kufunga, lakini sifa zimuendee kipa Ivon Philip Mapunda aliyeokoa michomo kadhaa ya hatari.
Kipindi cha pili, Stars ilibadilika mno kiuchezaji, japokuwa wachezaji waliomaliza kipindi cha kwanza ndiyo wote waliorejea kuanza ngwe hiyo ya lala salama.

Kutokana na mshambulizi mfululizo langoni mwa Zambia, Bara walipata kona dakika ya 48 ambayo ilikwenda kuchongwa na Salum Abubakar 'Sure Boy' na kuunganishwa nyavuni na Said Morad kwa kichwa.

Baada ya bao hilo, Zambia walianza kuutafuta mpira kwa tochi na kama si umahiri wa kipa wao, Nsabata Toaster kuokoa hatari nyingi, Stars wangeweza kuondoka na ushindi.
Kwa matokeo hayo, Burundi inaongoza kundi hilo baada ya kuifunga Somalia 2-0 katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo kwenye Uwanja huo.

Kikosi cha Stars kilikuwa; Ivo Mapunda, Himid Mao, Erasto Nyoni, Said Morad, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar 'Sure Boy'/Ramadhani Singano 'Messi' dk89, Hassan Dilunga/Athumani Iddi 'Chuji' dk85, Elias Maguri/Haroun Chanongo dk72, Amri Kiemba na Mrisho Ngassa.
 
Chipolopolo; Nsabata Toaster, Bronson Chama, Jimmy Chisenga/Kabaso Chongo dk67, Christopher Munthali, Rodrcik Kabwe, Stanley Nshimbi/Alex Nshimbi dk57, Sydney Kalume, Kondwani Mtonga, Felix Katongo/Salulani Phiri dk73, Ronald Kampamba na Festus Ndewe.
0 comments

Njia mpya ya Reli Afrika Mashariki

Njia mpya ya Reli Afrika Mashariki



Njia hii ya reli itaunganisha Kenya na kanda nzima ya Afrika Mashariki na eneo la maziwa makuu

Kenya imezindua rasmi ujenzi wa njia ya Reli itakayounganisha kanda ya Afrika Mashariki na eneo la maziwa makuu ujenzi utakaofadhiliwa na serikali ya China.

Reli hiyo itaunganisha Kenya na Sudan Kusini, DR Congo na Burundi.

Sehemu ya kwanza ya njia hiyo ya reli , itaunganisha bandari ya Mombasa na Mji mkuu Nairobi na kupunguza muda wa safari kati ya miji hiyo kutoka masaa 15 hadi masaa manne tu.

Huu bila shaka ndio utakuwa mradi mkubwa Zaidi kuwahi kujengwa tangu nchi hiyo kujipatia uhuru miaka 50 iliyopita.
Mradi huo utagharimu dola bilioni 5.2 kiasi kikubwa cha pesa hizo kikitolewa na Uchina.

Baadhi ya wakenya wanalalamika kuwa tenda hiyo imetolewa kwa kampuni ya kichina kwa njia isiyofaa.
Rais Uhuru Kenyatta katika hafla ya uzinduzi huo amesema kuwa mradi huu ndio utakuwa kumbukumbu kubwa ya utawala wake Kenya.
Mkataba wa ujenzi wa njia hiyo ya reli, ulifikiwa kati ya Rais Kenyatta na mwenzake wa China Xi Jinping mnamo mwezi Agosti mjini Beijing.

Pia kuna matumaini kuwa njia hiyo ya reli itapunguza msongamano mjini Mombasa moja ya bandari yenye shughuli chungu nzima barani Afrika.

Njia ya reli iliyoko sasa, ni ile iliyojengwa enzi za ukoloni.
Baada ya kukamilika kwa sehemu ya kwanza ya reli hiyo mjini Nairobi, mwaka 2017, itaendelezwa hadi Magharibi mwa DRC hususan mjini Kisangani, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini.

"Tunachokifanya hapa leo, kitaleta mageuzi makubwa sio nchini Kenya tu bali katika kanda nzima ya Afrika Mashariki,’’ alisema Rais Kenyatta akitaja mradi huo kama jambo la kihistoria.

Aliongeza kusema kuwa mradi huu ni moja ya miradi mikubwa katika maono yake ya maendeleo itimiapo mwaka 2030 kuboresha hali ya miundo msingi nchini humo.
0 comments

Magazeti ya leo November 29 2013

Magazeti ya leo November 29 2013,

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.


0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger