Featured Post Today
print this page
Latest Post

ARSENAL RAHAAAAAAAA, WENGER ASHEREHEKEA MIAKA 17 KAZINI KWA USHINDI WA UGENINI LIGI KUU ENGLAND

ARSENAL RAHAAAAAAAA, WENGER ASHEREHEKEA MIAKA 17 KAZINI KWA USHINDI WA UGENINI LIGI KUU ENGLAND

Happy days: Arsenal youngster Serge Gnabry celebrates after breaking the deadlock at the Liberty Stadium
  Happy days: Arsenal youngster Serge Gnabry celebrates after breaking the deadlock at the Liberty Stadium
 
 MFARANSA Arsene Wenger amefurah miaka 17 ya kuwa kazini kama kocha wa Arsenal kwa ushindi wa mabao 2-1 katika Ligi Kuu ya England leo dhidi ya Swansea Uwanja wa Liberty.
Shukrani kwao, Aaron Ramsey na kinda Serge Gnabry waliofunga mabao hayo, huo ukiwe ushindi wa 12 mfululizo kwa Gunners katika mashindano yote.
Swansea ilipata bao lake kupitia kwa Ben Davies dakika ya 82, baada ya Gnabry kufunga dakika ya 58 na Ramsey dakika ya 62.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny; Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Ramsey, Gnabry/Arteta dk77, Ozil/Monreal dk88, Wilshere/Jenkinson dk90 na Giroud.
Swansea: Vorm, Tiendalli, Flores, Amat, Davies, Canas, De Guzman, Dyer, Shelvey/Bony dk60, Routledge/Pozuelo dk64 na Michu.
 
 
Drilled home: Aaron Ramsey rifled in the second goal from close range as Arsenal doubled their lead
Drilled home: Aaron Ramsey rifled in the second goal from close range as Arsenal doubled their lead
No entry: Mathieu Flamini (left) shoots past Jose Canas but can't find the net
No entry: Mathieu Flamini (left) shoots past Jose Canas but can't find the net
Hard graft: Michu flies in to a tackle with Flamini as the Swans worked hard
Hard graft: Michu flies in to a tackle with Flamini as the Swans worked hard
On target: Gnabry celebrates scoring his first Premier League goal for Arsenal
On target: Gnabry celebrates scoring his first Premier League goal for Arsenal
No! Michu is not happy with a refereeing decision and falls to his knees
No! Michu is not happy with a refereeing decision and falls to his knees
Roar of delight: Olivier Giroud and Jack Wilshere (left) celebrate with Gnabry (obscured, centre)
Roar of delight: Olivier Giroud and Jack Wilshere (left) celebrate with Gnabry (obscured, centre)
Steered home: Gnabry watched his shot fly past Michel Vorm and into the net
Steered home: Gnabry watched his shot fly past Michel Vorm and into the net
Height mismatch: Nathan Dyer tries to trick his way past Per Mertesacker
Height mismatch: Nathan Dyer tries to trick his way past Per Mertesacker
Hunted down: Olivier Giroud is tracked by Jonjo Shelvey as he tries to make progress
Hunted down: Olivier Giroud is tracked by Jonjo Shelvey as he tries to make progress
Top of the league: Arsene Wenger saw his charges usurp Tottenham at the head of the Premier League
Top of the league: Arsene Wenger saw his charges usurp Tottenham at the head of the Premier League
Artist: But Mesut Ozil was not at his best as Arsenal won the game
Artist: But Mesut Ozil was not at his best as Arsenal won the game
0 comments

Hapa ndio stend ya mabasi ya Handeni Mjini

Hapa ndio stend ya mabasi ya Handeni Mjini



Hapa ndio kituo cha mabasi cha Handeni Mjini kama kilivyopigwa picha hii juzi wilayani humo mkoani Tanga. Ni tofauti na kituo cha mabasi cha Korogwe Mjini, Handeni hali inaonekana kuwa tulivu na hakuna mkanyagano sana. Hii ni kwasababu Mabasi mengi yanayopitia hapo yakitoka Tanga, Dodoma, Dar es Salaam hivyo kukusanya watu wengi mno. Picha na Kambi Mbwana.
0 comments

DC RWEYMAM AWAPA SOMO WAZAZI TANGA.

DC RWEYMAM AWAPA SOMO WAZAZI TANGA.

NA OSCAR ASSENGA,TANGA
MKUU wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweymam amewataka wazazi na walezi Mkoani hapa kuchangia kupatikana kwa unywaji wa maziwa shuleni ili kulinda afya na uelewa wa wanafunzi darasani.

Akizungumza katika siku ya unywaji wa maziwa Duniani na kufanyika kitaifa Mkoani Tanga, Rweymam alisema kinywaji hicho ambacho pia ni chakula ni muhimu kwa faida ya wanafunzi hasa kujenga afya zao.

Alisema wazazi wako na wajibu wa kuona kwa dhati unywaji wa maziwa shuleni ni muhimu na hivyo kuwataka kuchangia ili kuwezesha upatikanaji wa maziwa sambamba na uji shuleni.

“Ni jukumu la wazazi na walezi kuona unywaji wa maziwa shuleni ni muhimu ---mimi nadhani ni jukumu letu sisi wazazi kuwezesha upatikanaji wa maziwa na tusiwe na uzioto wa jambo hilo” alisema Rweymam

Rweymam alisema kufanya hivyo kutawawezesha wanafunzi kuwa na afya nzuri na kuzidisha uelewa darasani lengo ni kuwa na vijana wenye vipaji ambao watakuwa msaada kwa taifa.

Akifunga maadhimisho hayo, Naibu Meya wa jiji la Tanga, Muzzamilu Shemdoe, aliwataka wanafunzi kujibidiisha na masomo yao darasani pamoja na kuacha utoro jambo ambalo linaweza kuwaathiri na maisha mbeleni.

Alisema kuna baadhi ya wanafunzi wamekuwa hawafiki mashuleni mbali ya kuondoka majumbani kwao kuaga kwenda shule hali ambayo baadhi ya shule imekuwa ikikabiliwa na changamoto hiyo.

“Leo ni siku ya unywaji wa maziwa Duniani na kitaifa ni hapa tulipo---sisi tuliopo tu we mabalozi wa elimu majumbani na mitaani kwetu na tuhakikishe kila mtoto anakwenda shule na kuacha utoro” alisema Shemdoe

Shemdoe alisema halmashauri ya jiji inatarajia kufanya kampeni ya kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule haki hiyo anaipata na kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka shule watoto wao na kupata elimu.

                 
0 comments

WANAWAKE SINGLE WAANDAMANA KUSHINIKIZA SEREKALI IWASAIDIA WAOLEWE.

WANAWAKE SINGLE WAANDAMANA KUSHINIKIZA SEREKALI IWASAIDIA WAOLEWE.

Amini usiamini Nigeria ina upungufu wa wanaume wa kuoa!! Kiasi kwamba wanawake wanaotamani kupata wenza na kutengeneza familia wameamua kuchukua hatua.Zaidi ya wanawake elfu 8 walio single jana wameandamana kutokana na upungufu wa wanaume wa kuwaoa.


Lengo la maandamano yao ni kuishinikiza serikali kuwasaidia waolewe, kivipi? (Ndio swali hata mimi nimejiuliza!)

Wanawake waliojikusanya na kuandamana ni mkusanyiko wa 5380 waliopewa talaka, 2200 ni wajane 1200 yatima, na 80 wengine. Wanawake hao wamedai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku kwa sababu hawana wanaume wa kuwasaidia ndio maana wanahitaji wanaume wa kuwaoa na kuwasaidia mahitaji yao.
0 comments

BABU WA LOLIONDO ATABIRI"HIVI KARIBUNI TANZANIA ITAKUWA KIOO CHA AFRIKA NA DUNIA"

BABU WA LOLIONDO ATABIRI"HIVI KARIBUNI TANZANIA ITAKUWA KIOO CHA AFRIKA NA DUNIA"

 
MCHUNGAJI mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapila ‘Babu wa Loliondo’ amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia.

 Ametoa kauli hiyo Septemba 24, mwaka huu mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha. 

Mchungaji Mstaafu Mwaisapila aliyesifika kwa tiba ya kikombe cha dawa, alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia na hayakutokea Israeli sasa yatafanyika Samunge. “Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nimeyaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa. 

Alisema katika mafunuo aliyopewa na Mungu ameonyeshwa kwamba watu wengi zaidi watafurika kijijini Samunge kuliko ilivyokuwa hapo awali. Alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa misaada iliyotoa wakati wa ‘kugawa kikombe’ ikiwemo mahema, maji na ulinzi. Pamoja na maono hayo aliyopewa Babu wa Loliondo, aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT), marehemu Moses Kulola alikuwa akimpiga waziwazi katika mahubiri yake akidai mwenendo wa tiba alizokuwa akizitoa hazifanani na mafundisho ya Mungu. 

Kama hiyo haitoshi, watumishi mbalimbali wa Mungu wamekuwa hawamuamini. Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe na Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ kwa nyakati tofauti waliwahi kunukuliwa wakisema hawana imani na tiba ya kikombe iliyokuwa ikitolewa na Babu wa Loliondo



0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger