Featured Post Today
print this page
Latest Post

ZAHIR ZORRO ALA SHAVU TUSKER PROJECT FAME, HAMMY B IS NO LONG A JUDGE.

ZAHIR ZORRO ALA SHAVU TUSKER PROJECT FAME, HAMMY B IS NO LONG A JUDGE.


Hii ni Message iliyoandikwa na kituo kikubwa cha TV huko nchini Kenya kuhusu Ali Zoro,,

“Tanzanian music legend Zahir Ali Zoro joins the #TPF6 judging team. He’ll be one of the judges alongside @IanMbugua and @JKanyomozi,” kimeandika kituo cha runingo cha Citizen TV cha Kenya kinachorusha mashindano hayo.
0 comments

WAJUE WASHIRIKI WANNE WANAO IWAKILISHA TANZANIA TUSKER PROJECT FAME.

WAJUE WASHIRIKI WANNE WANAO IWAKILISHA TANZANIA TUSKER PROJECT FAME.

Hatimae Washiriki watakao iwakilisha Tanzania katika Mashindano ya mziki yanayo andaliwa na kinjwaji cha Tusker ,Tusker Project Fame wamejulikana.


 Washiriki hao ni  Angel, 23 yrs, Hisia, 21 yrs Tanah, 21 yrs na Dubson, 25yrs. Washiriki hao watakaa katika Academy ya music huko Nairobi kwa kipindi fulani huku wakichuana kupata washindi.

Mashindano hayo ndio yamezaa wakali katika Bongo Flava kama Hemed na Peter Msechu.
Stay Tuned we will be Updating you on Their Progress.
0 comments

HUENDA HUDUMA ZA KUSAFIRISHA ABIRIA WA MIKOANI IKASITISHA NA CHAMA CHA WAMILIKI WA BASI YAENDAYO MIKOANI KESHO.

SAFARI ZA MIKOANI SASA UTATA...! MALORI NA MABASI FUL MGOMO... CHEKI HAPA.

Na Goodluck Hongo.
SIKU moja baada ya Chama cha Wamiliki wa Malori nchini (TATOA), kutangaza usimamish

aji huduma za kusafirisha mizigo ndani na nje ya nchi kuanzia leo, Chama cha Wamiliki wa Mabasi yaendayo Mikoani (TABOA), nacho kimetangaza usitishaji huduma zake (kusafirisha abiria), kuanzia kesho

. Awali TATOA kilidai, lengo la kusitisha huduma ni kupinga agizo la Serikali kupitia Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli kuondoa msamaha wa tozo ya uzito wa magari yaliyozidi asilimia tano ya uzito unaokubalika kisheria.

Msemaji wa TATOA, Bw. Elias Lukumay, alisema msamaha huo ulitolewa na Serikali mwaka 2006 baada ya kamati ambayo iliundwa na Serikali ikishirikisha kufanya ziara katika mizani na kubaini haziko sawa kwa maana ya kutofautiana vipimo vyake.
Sababu nyingine iliyosababisha Serikali kutoa msamaha huo ni ubovu wa barabara, matuta mengi yaliyosababisha kuyumba kwa mzigo na mizani kutofanyiwa matengenezo.
 
Alisema uamuzi huo wa Serikali haukuishirikisha TATOA kama ilivyofanya mwaka 2006 mbali ya umuhimu wa sekta hiyo nchini hivyo ili kuepusha mgogoro na Serikali pamoja na wafanyakazi wa mizani, wamekubaliana kupaki magari yao.
 
Wakati TATOA ikitoa msimamo huo ambao utekelezaji wake unaanza leo, TABOA nao wamemtaka Dkt. Magufuli kurudisha msamaha wa asilimia tano vinginevyo wanasitisha huduma za kusafirissha abiria kwenda mikoa mbalimbali nchini pamoja na nje ya nchi kuanzia kesho.
 
Akizungumza na Majira Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu, alisema kitendo cha kuondoa asilimia tano kutayafanya mabasi mengi kusafiri na abiria wachache hivyo wamiliki wake kuingia hasara.
 
Alisema tangu kutolewa kwa taarifa hiyo, kumekuwa na misururu mikubwa ya magari katika mizani hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa abiria na kumaliza safari zao muda mbaya.
 
"Tunamuomba Dkt. Magufuli arudishe msamaha wa asilimia tano aliouondoa, upo uwezekano mkubwa wa mabasi kusafiri na abiria wachache hivyo kuingia hasara," alisema.
 
Alimtaka Dkt. Magufuli na Waziri wa Uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe, kutafakari uamuzi huo kwa kina ili kutoka na jawabu la kurudisha msamaha huo kwani sekta hiyo inategemewa na wananchi wengi wanaosafiri kila siku.
 
"Tumekuwa hatushirikishwi katika masuala kama haya, kitendo cha Serikali kuyaruhusu magari aina ya Noah yenye thamani ndogo kubeba abiria zaidi ya uwezo wake pia hatukushirikishwa," alisema.
 
Wakati huo huo, Bw. Mrutu aliwataka wamiliki wote wa mabasi kufika katika Ofisi za TABOA ili kuchukua fomu kwa ajili ya kupunguziwa bima kwa asilimia tano.

Aliwataka na wamiliki ambao hawajajiunga na TABOA,wafanye hivyo sasa ili waweze kushirikiana katika mambo muhimu yanayohusu huduma wanayoitoa kwa abiria
Majira
0 comments

SERIKALI YATOA KAULI JUU YA MGOMO WA WASAFIRISHAJI.


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo kuhusu mgomo uliopangwa kufanywa na wadau wa usafirishaji nchini wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akifafanua sheria namba 30 ya mwaka 1973 ya usalama barabarani iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2001 inayohusu kiwango cha mwisho cha uzito wa magari, kulia ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam Kamishna Suleiman Kova akifuatilia kwa makini.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam Kamishna Suleiman Kova akieleza jinsi Jeshi la Polisi lilivyojipanga kulinda usalama ili watumiaji wa barabara wasiweze kupata usumbufu huku akisisitiza kuwa kabla ya Jeshi la polisi kuchukua hatua za kisheria ni vema vyombo vinavyosimamia usafirishaji vikachukua hatuaKushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.

Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Ujenzi na Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini maelezo toka kwa Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli. (Picha zote na Eliphace Marwa)
0 comments

NAPE AWAPIGA KIJEMBE CHADEMA "UCHAGUZI NDANI YA CHAMA CHA CHADEMA LINI?"

NAPE AWAPIGA KIJEMBE CHADEMA "UCHAGUZI NDANI YA CHAMA CHA CHADEMA LINI?"

"Nimekutana na kijana asub leo wakati natoka mazoezini akaniuliza;

"Kaka Nape mambo vipi? Mie mshabiki kufa wa Chadema lakini sijapata mtu wa kunijibu kwanini Chadema kila wakipanga maandamano wanapanga, Dar,Mwanza, Arusha na nimesikia wanakwenda Mbeya tar. 10. Kwanini hawapangi maandamano anakotoka muasisi wa Chadema Mzee Mtei?!!!"

Nikainama chini nikamuuliza uchaguzi ndani ya chama chenu lini?! Akastuka kidogo, akanambia hivi unatakiwa kuwa mwaka huu kweli!?!! "Mhhh hilo nalo swali! Lakini hivi tukifanya uchaguzi Chama chetu kitapona kweli?! Nadhani bora tusifanya uchaguzi mpaka tutakapokamata dola"! Alisisitiza kijana.


Nikamjibu "BWANA YESU KRISTO ASIFIWE" Says Nape

0 comments

TUNDU LISSU AMJIBU RAIS JK "HOTUBA YA RAIS IMEJAA MANENO YA KUAMBIWA"

TUNDU LISSU AMJIBU RAIS JK "HOTUBA YA RAIS IMEJAA MANENO YA KUAMBIWA"

Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amesema hotuba ya kila mwezi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa siku tatu zilizopita, imejaa maneno mengi ya kuambiwa hasa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, ikiwa ni pamoja na uteuzi alioufanya wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu wa Chadema, Lissu alisema kauli zilizotolewa na Rais za kumshutumu yeye (Lissu) kuzungumza uongo bungeni, kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba zilikuwa zakuambiwa, hazina ukweli wowote.

 “Pengine rais Kikwete angesoma hotuba yangu niliyoitoa bungeni asingezungumza vile kuhusu mimi.”

Katika hotuba yake, Rais Kikwete alimshutumu Lissu kwa kusema kwamba katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa  Rais hakuheshimu mawazo ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na  Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).

Rais Kikwete alisema kauli hiyo ya Lissu ni uzushi, uongo na uzandiki wa hali ya juu huku akisisitiza kuwa Lissu alitoa kauli hiyo ili kupotosha ukweli na pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wajumbe 166 wa Bunge Maalum la Katiba.

Katika maelezo yake ya jana, Lissu alisema kuwa alipinga Rais kuteua wajumbe wa Bunge la Katiba kwa sababu hata wakati akiteua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba baada ya kupelekewa majina na taasisi mbalimbali, alifanya uteuzi wa watu ambao hawakupendekezwa na taasisi mbalimbali, ikiwemo TEC na CCT.

Lissu ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala alisema kamati hiyo ilipokutana na wawakilishi wa TEC na CCT (majina yanahifadhiwa kwa kuwa hatukuwapata kuthibitisha hilo), wawakilishi hao walikiri wazi kuwa majina waliyoyapendekeza sio ya watu walioteuliwa na Rais.

“Sasa hapo uongo na uzandiki wangu ni nini, labda hao wawakilishi wa TEC na CCT walisema uongo, hata wawakilishi wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania nao waliieleza kamati kuwa majina waliyoyapendekeza, sio ambayo Rais aliteua” alisema Lissu.

Alisema kuwa Rais amemshutumu bila kuujua ukweli, kusisitiza kuwa kama angesoma hotuba yake aliyoisoma katika mkutano wa 12 wa Bunge, asingezungumza maneno hayo dhidi yake.


“Ndio maana katika hotuba yake rais Kikwete alikiri wazi kwa kusema, nimeambiwa, nimesikia, nimeelezwa ukweli ni kwamba wasaidizi wake wamemdanganya,” alisema Lissu.

Source:Mwananchi
Udaku Specially Blog
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger