Featured Post Today
print this page
Latest Post

Bunge la Marekani lafikia makubaliano

Bunge la Marekani lafikia makubaliano

Serikali ya Marekani imefungua milango yake leo baada ya bunge kupitisha sheria inayomaliza kufungwa shughuli za serikali na kuepusha dakika za mwisho nchi hiyo kushindwa kulipa madeni yake. 

Obama hält Rede zur Lage der Nation. 
United States President Barack Obama delivers his State of the Union Address to a Joint Session of Congress in the U.S. Capitol in Washington, D.C. on Tuesday, January 25, 2011..Credit: Ron Sachs / CNP.(RESTRICTION: NO New York or New Jersey Newspapers or newspapers within a 75 mile radius of New York City) Bunge la Marekani 

Hata hivyo shirika la fedha la kimataifa IMF limeitolea mwito Marekani kufanyakazi zaidi kuweza kudhibiti matumizi ya serikali.
Baraza la seneti lilipiga kura kuidhinisha hatua hiyo kwa kura 81 za ndio na 18 zilizokataa na kulipeleka suala hilo katika baraza la wawakilishi ambalo linadhibitiwa na chama cha Republican , ambalo nalo liliidhinisha hatua hiyo usiku wa jana Jumatano kwa kura 285 dhidi ya 144. 

Speaker of the House John Boehner walks to the House floor during the vote on the fiscal deal in the U.S. Capitol in Washington October 16, 2013. The U.S. Congress on Wednesday approved an 11th-hour deal to end a partial government shutdown and pull the world�s biggest economy back from the brink of a historic debt default that could have threatened financial calamity. REUTERS/Kevin Lamarque (UNITED STATES - Tags: POLITICS BUSINESS)  
Spika wa baraza la wawakilishi kutoka chama cha Republican John Boehner 
 
Rais barack Obama alitia saini makubaliano hayo ambayo yamefuata masharti yale yale aliyoyatoa wakati matatizo hayo mawili yalipojitokeza zaidi ya wiki tatu zilizopita , muda mfupi baada ya usiku wa manane leo Alhamis. Bunge la Marekani lilikuwa linakabiliwa na muda wa mwisho hadi saa tano na dakika 59 usiku wa jana kuingia leo Alhamis kupandisha mamlaka ya serikali kuweza kukopa ama waliingize taifa hilo katika hatari ya kushindwa kutekeleza majukumu yake.
Mswada huo sasa unaifungua serikali hadi tarehe 15 mwezi Januari mwakani na unaruhusu wizara ya fedha kukopa hadi Februari 7 mwaka ujao ama huenda kwa muda wa mwezi mmoja zaidi.
Hatua hiyo haijumuishi chochote ambacho wabunge wa chama cha Republican walikidai wakitaka kufutwa ama kupunguzwa kwa mpango wa rais Obama wa kufanyia mageuzi mpango wake wa bima ya afya.
U.S. President Barack Obama speaks about the sequester after a meeting with congressional leaders at the White House in Washington March 1, 2013. Obama pressed the U.S. Congress on Friday to avoid a government shutdown when federal spending authority runs out on March 27, saying it is the right thing to do. REUTERS/Kevin Lamarque (UNITED STATES - Tags: BUSINESS POLITICS PROFILE TPX IMAGES OF THE DAY)  
Rais Barack Obama 
 
Spika wa baraza la wawakilishi la Marekani John Boehner amesema , "Tumepambana , lakini hatukushinda."
Marekani imekwisha wahi kuwa katika hali kama hiyo hapo kabla, ikisubiri kupata muafaka kuhusu suala la bajeti bila ya kuwa na matokeo ya uhakika. Lakini hii ilikuwa mara ya kwanza katika miaka 17 kwa serikali ya Marekani kufunga baadhi ya shughuli zake muhimu . Kiongozi wa wabunge wa chama cha Democratic katika baraza la wawakilishi Nancy Pelosi aliita hatua hiyo kuwa ni siku 16 za hatari ya kifahari ambayo imeugharimu uchumi wa Marekani karibu dola bilioni 24.
Spika wa baraza la seneti la Marekani Harry Reid wa chama cha Democratic amesema kuwa hiyo ni hatua muhimu kwa Marekani.
"Tumeona leo jinsi bunge lilivyofikia makubaliano ya kihistoria kwa vyama vyote, ili kuiwezesha serikali kufanya kazi zake tena na kuwezesha kulipa madeni yake."

  Wafanyakazi wa serikali ya Marekani wakiandamana
 
Mkwamo huo wa kibajeti ulitikisa masoko duniani na kutishia kuharibu hadhi ya deni la Marekani kama sehemu ambayo haileti hali ya wasi wasi kwa serikali na wawekezaji kuhifadhi fedha zao kwa matrilioni katika fedha za kigeni. Wachache waliitarajia Marekani kushindwa kulipa madeni yake lakini baadhi ya wawekezaji waliuza dhamana za serikali kwa kuhofu juu ya uwezekano wa kucheleweshewa malipo na kuacha kununua hisa ambazo zinaweza kuguswa na mporomoko wa uchumi nchini Marekani.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha la kimataifa IMF Christine Lagarde ameyakaribisha makubaliano hayo lakini amesema uchumi wa Marekani unaoyumba yumba unahitaji uimara wa muda mrefu wa bajeti yake.
China na Japan ambazo kila moja inamiliki kiasi cha dola trilioni moja katika hazina ya Marekani, ziliitolea mwito nchi hiyo hapo kabla kufikia makubaliano haraka.
0 comments

Taswira:Aliyemuua Mama Yake Mzazi Mwandishi wa habari wa ITV/Radio One, Ufoo Saro na Kumjeruhi Ufoo Saro Kisha Kujiua Mwenyewe Marehemu Anthery Mushi Aagwa Jijini Dar es Salaam

Waombolezaji wakipita kuaga mwili wa aliyekuwa mzazi mwenzake mwandishi wa habari wa ITV/Radio One, Ufoo Saro marehemu Anthery Mushi wakati wa ibada fupi ya kuaga mwili wake iliyofanyika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam Jana
Sehemu ya waombolezaji wakisikiliza kwa makini wasifu wa aliyekuwa mzazi mwenzake mwandishi wa habari wa ITV/Radio One, Ufoo Saro, marehemu Anthery Mushi, muda mfupi kabla ya kuagwa mwili wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam jana  Marehemu Anthery alisafirishwa Jana kuelekea Uru, Moshi kwa maziko yanaotarajiwa kufanyika LEO.Picha Zote na Mroki Mroki
0 comments

UKATILI WA KIJINSIA:Mume amkata mkewe mkono Kisa: Wivu wa mapenzi

UKATILI WA KIJINSIA:Mume amkata mkewe mkono Kisa: Wivu wa mapenzi

Leah Clement

Majeruhi Leah Clement (24), akiuguza jeraha lake wodini katika Hospitali Teule ya Wilaya Geita kwa madai ya kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe.(PICHA:RENATUS MASUGULIKO)

Mwanamke mkazi wa kijiji cha Nyamikoma Kata ya Bugarama Wilaya ya Geita, Leah Clement (24), anadaiwa kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe kutokana na wivu wa mapenzi.
Hivi sasa mwanamke huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akiendelea kupatiwa matibabu.
Aidha, mtuhumiwa wa ukatili huo, anadaiwa ametoroka na kwenda kujichimbia kwa `sangoma’ kwa imani kwamba hatakamatwa.
Tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu saa 1:30  usiku katika kijiji cha Chifufu kata ya Bugarama wilayani Geita.
Imeelezwa kwamba mtuhumiwa huyo alikwenda jikoni kwa mkewe na kukuta akisonga ugali kisha akamvamia na kumshambulia kwa panga lengo likiwa ni kumkata shingo yake.
Hata hivyo, mkewe aliwahi kujikinga shingoni kwa kutumia mkono wake wa kushoto na hivyo kusababisha ukatwe.
Akizungumza akiwa katika wodi alikolazwa majeruhi huyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie, aliapa kuwa vitendo vya aina hiyo haviwezi kuvumiliwa katika ya jamii kwani licha ya kuwa vya unyanyasaiji wa kijinsia, pia vinakiuka haki za binadamu na sheria za nchi.
Mangochie ameagiza mtuhumiwa huyo, Mussa Lutobeka (34), akamatwe mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Kadhalika, ameagiza mganga wa kienyeji anakodaiwa kukutwa mtuhumiwa amehifadhiwa, pia akamatwe.
Ofisa Mtendaji wa kata ya Bugarama, Juma Choma, alisema walimkamata mtuhumiwa huyo nyumbani kwa mganga wa kienyeji, Mashindeke Mwanzalima (47), akiwa amejificha chini ya uvungu wa kitanda.
Hata hivyo, Choma alisema walipokwenda nyumbani kwa mganga huyo wa kienyeji, alikana kuwapo kwa mtuhumiwa huyo.
Lakini alisema baada ya kumbana na kuipekua nyumba yake, walimkuta mtuhumiwa wa ukatili huo akiwa amejificha uvunguni mwa kitanda.
“Ndipo nilipoamuru mganga huyo naye akamatwe,” alisema.
Watuhumiwa wote wawili wanashikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo.
Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Leonard Paul, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na watuhumiwa kukamatwa.
Akizungumzia tukio hilo huku akibubujikwa machozi wodini likolazwa, Leah alisema kabla ya tukio hilo, mumewe ambaye ana wake wawili, alikuwa akimtishia kuwa siku moja atamuua kama hataondoka.
Mke mwingine wa mtuhumiwa huyo anadaiwa alikimbia.
Kutokana na vitisho hivyo, Leah alikwenda kutoa taarifa kwenye ofisi ya kijiji, lakini askari mgambo waliokwenda nyumbani, hawakumkuta mtuhumiwa baada ya kutoroka.
Leah alisema alilazimika kuondoka nyumbani kwa mumewe na kwenda wa baba yake mdogo hadi ufumbuzi utakapopatikana.
Kwa mujibu wa Leah, aliolewa na mume huyo mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 19 baada ya wazazi wake kupokea mahari ya Sh. 400,000 kati ya 500,000  alizokuwa amepangiwa kutoa.
Aidha, alisema wazazi wake (Leah), Clement Jading’wa na Rehema Rehema Kasabuku, walitengaba tangu mwaka 1995.
Leah anasema wakiwa na mume wake, wamebahatika kupata watoto wawili, Happiness Mussa (5) na Merciana Mussa (3).
Hata hivyo, alisema watoto hao kwa sasa wanaishi kwa baba yake mzazi tangu walipofarakana na mumewe.
Daktari wa zamu katika Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dk. Leah Kusalula, alisema ulemavu alioupata majeruhi huyo, ni wa kudumu na ni kitendo cha ukatili wa kutisha wa kijinsia ambao haupaswi kuvumiliwa.
CHANZO: NIPASHE
0 comments

ZITTO NOMA AWAKOMALIA CCM NA CHADEMA ASISITIZA KUSITISHWA KWA RUZUKU

ZITTO NOMA AWAKOMALIA CCM NA CHADEMA ASISITIZA KUSITISHWA KWA RUZUKU

Wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe akisisitiza kuwa hesabu za Chadema ni miongoni mwa ambazo hazijakaguliwa, chama hicho kimeishutumu kamati hiyo kwa kuagiza kusitishwa kwa ruzuku kwa vyama vya siasa na kusema hatua hiyo ni ubabe.

Wakati Chadema wakitoa kauli hiyo, jana Zitto alisema vyama vya siasa tisa vikiwamo Chadema, CCM na CUF vinatakiwa kufika mbele ya PAC Oktoba 25 mwaka huu, kwa ajili ya kujieleza na kwamba chama kitakachokaidi, sheria za Bunge zinaeleza wazi, kwamba wahusika wanaweza kufungwa jela siku saba.

Chadema kilisema kuwa PAC kabla ya kuchukua hatua, ilipaswa kuwapa nafasi ya kuwasikiliza viongozi wa vyama husika, kumhoji Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Msajili wa vyama vya Siasa ambao wameshindwa kutimiza wajibu wa kukagua hesabu hizo kwa miaka minne.

Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chadema, Anthony Komu alisema jana kuwa, uamuzi wa PAC utaviathiri vyama kwani bajeti zake zimezingatia kuwapo kwa ruzuku.

“Kuna vyama ambavyo vinategemea ruzuku kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, Chadema ingawa tuna vyanzo vingine vya mapato, tunaitegemea kukamilisha bajeti yetu kwa fedha za ruzuku ambazo zinatusaidia kwa asilimia 45. Ni tabia mbaya kuchukua uamuzi kwa kibabe na kuhukumu kabla ya kutusikiliza siyo haki hata kidogo,” alisema Komu.

Alitetea chama chake kwamba kimekuwa na utaratibu wa kuwasilisha hesabu zilizokaguliwa ambapo alitoa ushahidi wa barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa ya April 16, 2012 ikithibitisha kwamba hesabu zao zipo sawa baada ya kuziwasilisha katika ofisi hiyo.

“Chadema tunataka ukaguzi wa hesabu usijikite katika fedha za ruzuku pekee bali katika vyanzo vyote vya mapato ya vyama, tatizo CAG alitueleza kwamba anakabiliwa na upungufu wa rasilimali watu kwa hiyo PAC walipaswa kuliangalia tatizo hilo na kutafuta ufumbuzi,” alisema Komu.

Zitto juzi alikaririwa na vyombo vya habari akieleza kuwa Serikali ilitoa kiasi cha Sh67.7 bilioni kama ruzuku kwa vyama tisa vya siasa tangu mwaka 2009, lakini vyama hivyo havijawahi kuwasilisha taarifa za ukaguzi wa hesabu zake kwa msajili kama sheria inavyoagiza.

Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema), aliamuru Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kusimamisha utoaji wa ruzuku hadi hapo vitakapowasilisha ripoti ya ukaguzi na makatibu wake wakuu kuhojiwa.

Miongoni mwa vyama vilivyotajwa ni APPT-Maendeleo lakini jana Rais Mtendaji wa Chama hicho, Peter Mziray alisema chama chake hakijawahi kupewa kiasi cha Sh217 milioni kama inavyodaiwa na PAC.

Mziray alikiri walianza kupata ruzuku 2009 ila inasema ilikuwa kidogo kiasi cha Sh 50,000 kwa mwezi na baadae kupanda Sh 275,000 kwa mwezi.


Alisema kiasi walichopata kuanzia mwaka 2009 ni kiasi cha Sh12 milioni tu. “APPT-Maendeleo haina uwakilishi bungeni kwa hiyo haiwezi kupata kiasi hicho kikubwa cha fedha,” alisema Mziray.

Zitto akaza kamba

Jana Zitto alivitaka Chadema, CUF na CCM kuacha kupiga kelele katika vyombo vya habari na badala yake viwasilishe taarifa za ukaguzi wa matumizi yake katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

“Vyama hivi visilete ujanja ujanja, hizi ni fedha za umma lazima zikaguliwe. Tatizo la CCM, CUF na Chadema wanahusisha suala la kuwasilisha taarifa za ukaguzi na nafasi yangu ya Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, sifanyi kazi kwa niaba ya Chadema mimi nafuata sheria za Bunge na katika hili sitacheka na mtu,” alisema Zitto jana wakati akizungumza na wanahabari katika ofisi ndogo za bunge, Dar es Salaam.

Zitto alisema Kanuni za Bunge zinataka ukaguzi wa hesabu ya serikali huku akionya kuwa sio sahihi kwa vyama hivyo kulichukulia suala hilo kama jambo binafsi. Alisema chama husika kikishakaguliwa na ofisi ya CAG, na taarifa husika hupigwa muhuri wa ofisi hiyo ya mkaguzi.

Zitto alisema vyama hivyo vinatakiwa kuichukua taarifa hiyo na kuipeleka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye hutangaza taarifa hiyo katika gazeti la Serikali ili ijulikane wazi mapato ya vyama husika.

“Hilo ndio halijafanyika, waulizeni hao CCM, CUF na Chadema lini wamekaguliwa na kama wamekaguliwa mbona taarifa zao hazipo katika ofisi ya msajili, sisi tunatambua taarifa za ukaguzi wa vyama ambazo zipo ofisi ya msajili,” alisema Zitto na kuongeza:

“CCM na Chadema ndiyo wana kelele zaidi, hatuwezi kusimamia Serikali wakati sisi wenyewe ni wachafu, najua kila mtu alikuwa akiogopa kueleza ukweli kuhusu ukaguzi kwa vyama vya siasa, kuanzia CAG, Mwenyekiti aliyepita wa PAC hadi Msajili wa vyama.”

Alisema ruzuku za vyama hivyo ilitakiwa kusimamishwa tangu miaka mitatu iliyopita, kwa maelezo kuwa Sheria ya Vyama vya Siasa Ibara ya 14(4) inaeleza kuwa Ofisi ya Msajili wa Vyama ina uwezo wa kufungia ruzuku ya chama fulani, mpaka hapo kitakapowasilisha hesabu zake.

“Katika hili CAG na Msajili wa Vyama kila mtu atabeba mzigo wake, inaonekana kulikuwa na kuogopana lakini mimi nimekuwa Mwenyekiti wa PAC hivi karibuni lazima nisimamie sheria na hiyo ndiyo kawaida yangu,” alisema Zitto.

Msajili anena

Msajili wa Vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi alizungumza na gazeti dada la The Citizen juzi na kufafanua kuwa ofisi yake itayafanyia kazi maoni ya PAC na kuongeza kuwa uamuzi wowote utakaotolewa utafanyika kwa mujibu wa sheria za ofisi yake.


Alisema kuwa alipitia maoni yaliyotolewa na Zitto kuhusu vyama kufungiwa kupewa ruzuku na kwamba atayafanyia kazi licha ya kuwa pia alitoa maoni binafsi kuhusu suala hilo.
-Mwananchi
0 comments

CHANGUDOA AKIMBIA MTAANI UCHI BAADA YA KUONA MASHINE KUBWA YA MTEJA WAKE

CHANGUDOA AKIMBIA MTAANI UCHI BAADA YA KUONA MASHINE KUBWA YA MTEJA WAKE

Ushawahi kusikia mwanaume ana mguu wa mtoto ? basi haya ndio yamemkuta changudoa mmoja huko Mombasa baada ya kwenda na Mteja Gesti house...Inasema walivyofika Gesti walikubaliana malipo na baada ya hapo walivua ila msichana baada ya kuona maumbile makubwa ya jamaaaa ilibidi aombe Poo lakini jamaaa hakusikia kwa vile alishatoa hela ikabidi alazimishe ...Msichana alipata upenyo wa kutoroka na kutoka Gesti akiwa uchi huku akipiga yowe.....Baada ya kuulizwa nini alisema Jamaaa ana maumbile ya siri makubwa kama Mguu wa mtoto ...Watu walicheka tu na wasamaria wema wakamsitiri kwa kanga...Chezea Mombasa wewe
0 comments

USAFIRI KIKWAZO KITUO CHA KUTUNZIA WAZEE CHA MWANZANGE.


USAFIRI KIKWAZO KITUO CHA KUTUNZIA WAZEE CHA MWANZANGE.
 
Na Oscar Assenga,Tanga. 
UKOSEFU wa Usafiri katika makao kwa ajili ya kuwapeleka wazee sehemu mbalimbali ikiwemo hospitalini ni miongoni mwa changamoto zinazokikabili kituo cha kutunzia wazee cha Mwanzange jijini Tanga.
 
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Ustawi wa Jamii katika kituo hicho,Clara Kibanga wakati akisoma taarifa kwa mkuu wa mkoa wa Tanga ,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa ambaye alikwenda kituo hapo kukabidhi zawadi za sikuu ya Eid Al Hajj kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanga,Jakaya Mrisho Kikwete.

Kibanga licha ya kukabiliwa na changamoto hiyo lakini pia kuna ukosefu mkubwa wa madawa katika kituo hicho hasa pale wanapopata dharura kwa mgonjwa anayehitaji huduma ya haraka au dawa zinapokosekana katika hospitali za serikali na hivyo hulazimika kuzinunua.

Ameongeza kuwa changamoto nyingine ni uhaba wa vitanda kutokana na kuwa vilivyopo vimechakaa na ni vya muda mrefu.

Akizungumzia mafanikio ya kituo hicho,Kibanga amesema wamefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa ombaomba kwa wazee licha ya kutofanikiwa kulimaliza kabisa.

Kituo hicho cha kuwahudumia wazee Mwanzange  kilianzishwa mwaka 1950 na wakoloni wa kiingereza kwa ajili ya kuwatunza wazee ambao walikuwa wafanyakazi (manamba)katika mashamba ya mkonge na chai.

Na Oscar Assenga,Handeni.
MKAZI wa Kijiji cha Kwedichocho wilayani Handeni mkoani Tanga Aweso Athumani (38) amemuua mkewe Saumu Athumani (24) kwa risasi naye kujiua kwa kujipiga risasi kisongoni kwa kutumia bunduki aina ya Gobole tukio ambalo limeacha simanzi kwa wakazi wa eneo hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe alisema tukio hilo limetokea octoba 16 mwaka huu majira ya saa kumi na moja asubuhi wakati wakiwa nyumbani kwao ndipo alipofanya tukio hilo na kukimbilia msituni.
Massawe alisema baada ya kukimbia msituni na ndipo alipofanya tukio hilo la kujiua mwenyewe kwa kujipiga risasi shingoni na baadae wananchi walipokwenda eneo hilo waliuona mwili wake na kutoa taarifa kuhusu tukio hilo.
Kamanda Massawe alisema baada ya polisi kufika eneo la tukio wakauchukua mwili huo na kuufanyia uchunguzi wakagundua wamepigwa risasi na kuwakabidhi ndugu zao kwa ajili ya taratibu za mazishi.

WAHAMIAJI HARAMU 32 WAKAMATWA TANGA.

Na Oscar Assenga,Tanga.
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Tanga imewakamata wahamiaji haramu 32 ndani ya kipindi cha wiki mbili ambao waliingia mkoani hapa kinyume cha sheria
 

Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Sixtus Nyaki amesema tukio la kwanza lilitokea septemba 25 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili asubuhi wakati maafisa wa idara hiyo wakiwa kwenye doria walikamata wahamiaji haramu kumi raia wa Ethiopia.

Nyaki alisema raia hao walikamatiwa katika eneo la kange nje kidogo ya jiji la Tanga na kufanyiwa mahojiano ambapo ilibainika kwamba waethiopia hao waliingia nchini wakitokea nchi jirani ya Kenya na walisafiri kwa kutumia boti lililopita bahari ya hindi mpaka maeneo ya sahare jijini hapa.
 

Ofisa uhamiaji huyo aliwataja wahamiaji haramu hao kuwa ni Ayano Tamrat Shanko,Abraham Tafara Dobuse,Yonas Ayala Dolaso,Salamu Zalaka Wondu,Tamasgen Yohans Herano,Tasfahun Qalbiso Angore na Dababa Dante Handiso ambao wote kwa pamoja wanatuhumiwa kwa kosa la kuingia nchini kinyume na sheria ya uhamiaji.
 

Nyaki alisema uchunguzi bado unaendelea ili kubaini boti lililotumika na watu waliohusika kuwasaidia wahamiaji haramu kuingia nchini.

Hata hivyo alieleza taratibu za kuwafikisha mahakamani zitachukuliwa dhidi ya wahamiaji haramu waliokamatwa ambapo alisema zoezi hilo litakuwa endelevu na kutoa wito kwa wananchi na raia wema kutoa taarifa pindi wanapowaona au kuwatilia mashaka watu wa namna hiyo.
 

Alisema wahamiaji haramu wengine 22 walikamatwa Octoba 9 mwaka huu eneo la kisiwa cha kirui kilichopo kilomita 10 kutoka kijiji cha jasini wilayani Mkinga majira ya saa kumi na mbili jioni.

Alieleza wahamiaji haramu hao walitokea Mombasa, Kenya kwa kutumia njia ya majini wakiwa na lengo la kwenda Afrika kusini ambapo taratibu wa kuwafikisha mahakamani zinaendelea.
0 comments

DK MAGUFULI AANZISHA SAKATA LINGINE, SAFARI HII NI NDANI YA SERIKALI AKIWATAKA WATUMISHI WANAODAIWA MIKOPO YA NYUMBA KULIPA NDANI YA MWEZI MMOJA, ATAYESHINDWA KUPOKONYWA NYUMBA

Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal akikagua ujenzi wa nyumba 851 kwa ajili ya kuuzia wafanyakazi wa serikali baada a kuweka jiwe la msingi jana  katika eneo la Mabwe Pande Jijini la Dar es Salaam. . Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli. Picha na Salim Shao. 

DAR ES SALAAM.
WAZIRI  wa Ujenzi, Dk John Magufuli ametoa mwezi mmoja kwa watumishi wa Serikali ambao wanadaiwa mikopo ya nyumba kulipa madeni yao mara moja na kuonya kwamba ikiwa watashindwa kulipa, watany
ang’anywa nyumba hizo na watakopeshwa watu wengine.
Dk Magufuli ameibuka na hoja hiyo mpya, zikiwa ni siku chache tangu alipopigwa ‘stop’ na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutekeleza sheria ya kuondoa msamaha wa asilimia tano kwa mizigo inayozidi kwenye malori, hali ambayo ilizusha mvutano mkubwa baina ya Serikali na wasafirishaji wa mizigo nchini.
Akizungumza wakati wa kuweka jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa nyumba 851 za watumishi wa Serikali eneo la Mabwepande jijini Dar es Salaam, Dk Magufuli alisema watumishi 2500 hawajalipa mikopo ya nyumba walizonunua.
Dk Magufuli alionya kuwa atafuatilia suala hilo na kuhakikisha madeni hayo yanalipwa mara moja, huku akimwomba Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal kumuunga mkono kwenye jambo hilo, ambalo ni utekelezaji wa sheria za nchi.
“Naomba ifahamike kwamba tunapojenga nyumba kwa ajili ya kuwakopesha watumishi wa umma tunataka kuboresha makazi yao. Pia fedha tunazokusanya zinasaidia kujenga nyumba zaidi,” alisema Dk Magufuli. Hata hivyo alisema hadi sasa watumishi wa Serikali 4,900 ambao walikopa nyumba hizo tayari wamelipa madeni.
“Mimi nafanya kazi kwa kufuata sheria na kila mtumishi wa Serikali anafahamu jambo hilo, hivyo watu ambao wanajua tunawadai wakae kwa tahadhari, kwani ndani ya mwezi mmoja kama hawatalipa tutawachukulia hatua bila kupuuzia,” alionya Magufuli.
Hii siyo mara ya kwanza kwa Dk Magufuli kutangaza kunyang’anya nyumba hizo, kwani alifanya hivyo mwishoni mwa Machi mwaka jana pale alipouagiza uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kuwapa siku saba watu wote walionunua nyumba hizo kulipa madeni yao.
Dk Magufuli aliwataka TBA kutoa ilani ya maandishi inayowataka wahusika walipe fedha hizo ndani ya wiki moja vinginevyo wangenyang’anywa kwa maelezo kwamba wanachelewesha malengo ya TBA kujenga nyumba zaidi. 

Hata hivyo, hakuna taarifa zozote zilizowahi kutolewa kuhusu kutekelezwa kwa amri hiyo iliyotolewa zaidi ya miezi 18 iliyopita.
Jana, Makamu wa Rais, Dk Bilal alimuunga mkono Magufuli akisema: “Naunga mkono tamko la Waziri wa Ujenzi kwamba ni lazima watumishi wa Serikali ambao wanakopeshwa nyumba walipe haraka ili fedha hizo zisaidie kujenga nyumba nyingine.”
Dk Bilal alikuwa mgeni rasmi katika shughuli ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 851, kwenye eneo la Bunju ‘B’ Kinondoni, Dar es Salaam. Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga, alisema ujenzi huo unafanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza iligharimu Sh2 bilioni na awamu ya pili Sh1 bilioni.
“Nyumba 851 zinazojengwa Bunju B ni sehemu ya ujenzi wa nyumba 4,400 katika Mkoa wa Dar es Salaam na nyumba 10,000 kwa nchi nzima,” alisema Mwakalinga.
Hafla hiyo ilisimama takriban kwa dakika 10 wakati Dk Bilal akitaka kuhutubia baada ya jenereta kushindwa kufanya kazi, hivyo kumlazimu kurudi kuketi kwenye kiti hadi umeme uliporejea. 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alilazimika kwenda kufuatilia suala hilo na mafundi waliokuwapo walifanikiwa kuunganisha mashine za kipaza sauti na umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), hivyo Makamu wa Rais aliendelea kuhutubia. MWANANCHI
0 comments

MATOKEO YA AJABU: SIMBA YAPELEKA MAAFA JANGWANI 1977 (4)

MATOKEO YA AJABU: SIMBA YAPELEKA MAAFA JANGWANI 1977 (4)

simba_enzi_zao_3e490.jpg
Wachezaji wa Simba wakiwa 'wameulamba'.

Na Daniel Mbega
KATIKA mchezo wa soka kushinda ama kushindwa ni mambo ya kawaida, lakini vipo vipigo ambavyo timu hupata kiasi cha kujiuliza mara kumi kumi, kulikoni? Kama kuna kipigo ambacho kitabaki katika kumbukumbu za Yanga milele na milele ni kile cha mwaka 1977 cha magoli 6-0 (MNYAMA).
kutoka kwa watani wake wa jadi, Simba, kwenye mchezo wa Ligi ya Taifa.
Kwa waliokuwepo na waliopata simulizi baadaye, Jumanne ya Julai 19, 1977 ilikuwa siku yenye majonzi makubwa kwa mashabiki wa Yanga na furaha kubwa kwa wale wa Simba, ambayo kwa ushindi huo, mbali na kujihakikishia ubingwa wa Ligi ya Taifa kwa kuwa ilibakiza mechi moja tu dhidi ya Navy (sasa KMKM) ya Zanzibar iliyokuwa ya kukamilisha ratiba, pia ilikuwa imefanikiwa baada ya miaka tisa kulipa kisasi cha kufungwa magoli 5-0 na Yanga mwaka 1968.
Kati ya watu waliojihisi wenye furaha kupindukia walikuwa kocha wa Simba, Dimitier Samsarov wa Bulgaria ambaye alikuwa na muda mchache tu tokea akabidhiwe timu na nahodha Abdallah Kibadeni 'Mputa' ambaye siku hiyo 'alicheka' na nyavu mara tatu.
Ilikuwa hadithi ya kifo cha nyani miti yote huteleza, kwani pamoja na kukuru kakara zote za Yanga, ikiwemo kubadilisha wachezaji wawili dhidi ya mmoja wa Simba, ambaye alibadilishwa kufuatia mwenzake kuumia (Martin Kikwa ndiye aliyeumia na kumpisha Abbas Dilunga), mambo yalichacha na kuvunda kwa vijana wa Jangwani waliokuwa wakipokea mashambulizi mfululizo na kubaki wakitumia ujanja wa mtego wa kuotea (offside-trick), ambao hata hivyo, haukusaidia kitu.
Mwaka huo Yanga ilikuwa haijatulia baada ya mgogoro mkubwa wa mwaka 1976 uliopelekea karibu wachezaji 20 nyota kufukuzwa kwa madai ya kutokuwa wazalendo na kusababisha Yanga kupoteza taji lake la ubingwa wa soka Afrika Mashariki na Kati mjini Mombasa, Kenya mwaka huo. Wachezaji hao ni Gibson Sembuli, Leodgar Tenga, Sunday Manara, Boi Idd 'Wickens', Ally Yusuf, na wengineo ambao walikwenda kuunda timu ya Nyota Afrika ya Morogoro kabla ya kuanzisha Pan African ya Dar es Salaam.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger