Featured Post Today
print this page
Latest Post

Mandela aendelea kupambana kitandani

Mandela aendelea kupambana kitandani

130626094927_nelson_mandela_304x171__nocredit_689ac.jpg
Rais wa kwanza mwaafrika wa Afrika Kusini, Nelson Mandela anaendelea kupambana na ugonjwa akiwa bado kitandani, binti yake Makaziwe Mandela amesema.

Bi Makaziwe ameliambia Shirika la Utangazaji la Afrika Kusini, SABC kuwa mpinzani huyo wa siasa za ubaguzi wa rangi, "bado yupo nasi, imara, na anatia moyo".
"Hata kwa kukosa neno zuri zaidi... Akiwa bado kitandani anatufundisha somo-somo la subira, upendo, uvumilivu," amesema, Makaziwe.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 95, anaendelea kupata huduma ya matibabu akiwa nyumbani kwake.

Aliruhusiwa kutoka hospitali mwezi Septemba mwaka huu baada ya kutibiwa kwa karibu miezi mitatu kufuatia maambukizi yanayojirudiarudia katika mapafu yake.

Bwana Mandela anaheshimika kwa kiasi kikubwa kutokana na namna alivyopambana dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini na baada ya kuachiliwa huru kutoka gerezani mwaka 1990 aliwasamehe wazungu wa zamani waliomkamata na kumfunga.
Alifungwa miaka 27 jela na alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini mwaka 1994.

Bwana Mandela mara baada ya kumaliza kipindi kimoja cha miaka mitano ya urais, hakutaka kugombea tena nafasi hiyo.

Mwezi uliopita mke wa zamani wa Bwana Mandela Winnie Madikizela-Mandela alisema Bwana Mandela hakuweza kuzungumza kwa sababu ya mipira iliyoko kinywani ili kuvuta maji maji yaliyoko katika mapafu.

Ofisi ya rais wa Afrika Kusini mara kwa mara imekuwa ikielezea hali ya Bwana Mandela kuwa ni mahututi lakini imara.
0 comments

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR

Jakaya-Mrisho-Kikwete_5bcd9.jpg
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Johari Masoud Sururu kuwa Kamishna mpya wa Uhamiaji Zanzibar.
Kabla ya uteuzi huu ambao unaanzia tarehe 24 Novemba, 2013 Bwana Sururu alikuwa Mwambata wa Uhamiaji katika Ubalozi wa Tanzania jijini Abu Dhabi, Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E).
Kufuatana na uteuzi huu, aliyekuwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Bwana Mwinchumu Hassan Salim sasa atapangiwa kazi nyingine.
Imetolewa na:
Isaac J. Nantanga
MSEMAJI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
04 Desemba, 2013
NB: Picha ya Bwana Sururu imetumwa kwa e-mail yenu.
0 comments

Mbunge Mch, Msigwa akanusha tuhuma dhidi yake.....

Mbunge Mch, Msigwa akanusha tuhuma dhidi yake.....

1454628_602438129803504_1373062112_n_ed4ef.jpg

Mbunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha CHADEMA Mch Peter Msigwa amekanusha kuhusiana na tuhuma zinazomkabili juu ya kutokabidhi rambirambi kiasi cha shilingi milioni moja kwa mjane wa aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi, ambazo zilitolewa na wanachama wa CHADEMA waliopo nchini Uingereza na kusema kuwa tuhuma hizo si za kweli, ni mambo ya uzushi na kwamba watu wanasema hivyo ili kumchafua.

akizungumza na kituo cha redio ya Nuru FM ya Iringa, kupitia kipindi cha sunrise power, Mh.Msingwa amesema kuwa ni kweli pesa hizo alipokea kupitia kwa MAJID MJENGWA na baada ya kupokea fedha hizo alichangisha tena fedha kwa wananchi wa jimbo la Iringa mjini kupitia mkutano, ambapo walichangia kiasi cha shilingi laki tatu pamoja na yeye mwenyewe aliongezea kiasi cha shilingi laki tano, hivyo kupelekea kufikia kiasi cha shilingi milioni moja na laki nane na sitini na nane na kumkabidhi mjane wa marehemu DAUDI MWANGOSI.

Msigwa amesema kuwa ni wanasiasa tu wanaojaribu kuwachafua baada ya kuona kuwa wameshindwa na tayari amewasiliana na uongozi wa chama chake ili kuweza kulichukulia hatua gazeti ambalo limeandika tuhuma hiyo.

0 comments

KINANA AICHANACHANA CHADEMA MBEYA, AMALIZA ZIARA KWA KISHINDO

KINANA AICHANACHANA CHADEMA MBEYA, AMALIZA ZIARA KWA KISHINDO

1

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda bajaji tayari kwa kuelekea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Luanda Nzovwe Mwanjelwa jijini Mbeya akitokea ofisi za CCM mkoa wa Mbeya, huku Nape Nnauye naye akijiandaa kuinga kwenye bajaji. Kinana akiongozana na Ujumbe wake pamoja na viongozi wa mkoa wa Mbeya na wilaya leo wametumia usafiri huo ili kuonyesha kwamba Chama hicho ni chama cha wananchi wa kawaida ambao ni wafanyakazi na wakulima tofauti na wenzetu wanaojifanya wanawatetea lakini wanakuja na Helikopta na kuwachangisha michango ya fedha kisha wanatokomea zao. Katika msafara huo pia yupo Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na Mbunge wa kuteuliwa.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MBEYA) 2
Msafara ukielekea kwenye mkutano
4Vijana wa Mwanjelwa wakiuzuia msafara wa Kinana wakati alipokuwa akielekea uwanja wa Luanda Nzovwe kwenye mkutano jambo lililofanya Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye watembeee kwa mguu(P.T)
7
Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye wakitembea kwa miguu katika eneo la Mwanjelwa huku vijana wakiwashangilia 8
Abdulrahman Kinana akiwa katika bajaji iliyomchukua
9Nape Nnauye akiwa katika Bajaji iliyombeba
10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi wakiwapungia mikono wananchi wakati wakielekea kwenye mkutano. 13
Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na Mbunge wa kuteuliwa akizungumza na wananchi katika mkutano huo. 14
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi wengine wakiwa katika meza kuu.
17Umati wa watu waliohudhuria katika mkutano huo.
18Kada wa CCM aliyejiunga na CCM hivi karibuni akitoka chama. cha CHADEMA Braison Mwasimba akiunguruma katika mkutano huo 19
Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akimwaga sumu katika mkutano huo.
20Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akiwaimbisha wananchi katika mkutano huo.
22Msanii wa muziki wa kizazi Kipya Michael Senka mashairi jukwaani wakati mkutano huo ukiendelea leo jioni.
24Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro akitolea ufafanuzi wa mbolea ya Minjingu ambayo imekataliwa na wananchi wa mkoa wa Mbeya huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisikiliza kwa makini

25Kada wa Chama cha Mapinduzi Tambwe Shitambala akizungumza katika mkutano huo.

0 comments

MTIKILA "KUNA CHADEMA MBILI-"CHADEMA CHUMBANI NA CHADEMA SEBULENI"

MTIKILA "KUNA CHADEMA MBILI-"CHADEMA CHUMBANI NA CHADEMA SEBULENI"

Mchungaji Christopher MTIKILA azidi kupiga msumali wa MOTO katika JENEZA la Chadema mashumbulizi yake yamuelekea Edwin MTEI.


"Amemtuhumu mmoja wa waanzilishi na m/kiti wa kwanza wa chadema Edwin MTEI, akidai kuwa ni muasisi wa dhana ya UKABILA na UKANDA katika chama hicho huku m/kiti wa sasa Freeman MBOWE na Katibu wake SLAA wakidaiwa kuboresha mfumo huo KISASA zaidi kwa kuweka NAKSH NAKSH"

Hata kinacho wafukuza Zitto na wenzake ktk Chadema ni matokeo ya kuota mizizi kwa mfumo wa UKABILA na UKANDA ambao hauruhusu mwanachama yoyote kuhoji mapato na matumizi ndai ya chama"

WATANZANIA waelewe Chadema si chama cha siasa na VIONGOZI wake si wanasiasa wa kweli, kwani hawana MAONO wala MALENGO ya kuwakomboa watanzania

KWA UJUMLA NI GENGE LA WALAJI TU!!!

Ndani ya chadema kuna kundi linaitwa "BIG EIGHT " ambalo linaudwa na wazee wa KICHAGA na kiongozi wao mkuu ni Edwin MTEI akisaidiwa na akina Mariale na Ndessamburo,

Hawa ndio wenye chadema yao ambapo moja ya MAJUKUMU yao ni kulinda maslahi ya kichaga ndani ya chama,Kuna Chadema mbili kuna chadema ya CHUMBANI na Chadema ya SEBULENI"
0 comments

JAMANI MADEMU WETU WA BONGO NDIVYO WALIVYO.EBU SOMA HAPA.NDIO MAANA NAWACHUKIA MIMI

JAMANI MADEMU WETU WA BONGO NDIVYO WALIVYO.EBU SOMA HAPA.NDIO MAANA NAWACHUKIA MIMI

Admin
Mimi ni Msichana wa Miaka 21 , Nasoma chuo kimoja hapa dar ..nimetokea mkoa niko mwaka wa Pili sasa , huko nilipotokea nina Boyfriend ambae nimekuwa nae kwa muda mrefu toka secondary ila swala mapenzi hatujawahi fanya kwa vile kabla ya kuja chuo nilikuwa Bikira ..


Baada ya kuja chuo naweza sema nimekutana na vijana wajanja na nadiriki kusema sina tena Bikira washaitoa ...Sasa nashindwa ni namna gani nimwambie boy wangu huyo wa mkoa ..Likizo nilienda nikamtega tufanye ili nijidai yeye ndio kaitoa lakini aliniambia tutafanya mapenzi siku ya ndoa ...Naombeni ushauri mie nataka nimwambie kwamba sina tena na tuwe tunafanya mapenzi ..Nitaanzia wapi ?
0 comments

INADAIWA WAYNE ROONEY AMEPOTEZA NGUVU ZA KIUME BAADA YA KUPANDIKIZA NYWELE BANDIA

INADAIWA WAYNE ROONEY AMEPOTEZA NGUVU ZA KIUME BAADA YA KUPANDIKIZA NYWELE BANDIA

Mchezaji nyota wa timu ya Manchester United na England, Wayne Rooney anadaiwa alipoteza nguvu zake za kiume baada ya upandikizaji wa nywele mwaka jana.

Kituo cha runinga cha KTN cha nchini Kenya, kimedai kuwa Rooney amekuwa akimsumbua doctor wake kumtaka amrudishie pesa zake baada ya kupata madhara ya kupoteza nguvu za kiume kutokana na kupandikizwa nywele bandia kwenye kipara chake,hali iliyopelekea kusababisha mgogoro mkubwa ndani ya familia ya mchezaji huyo.
0 comments

CHADEMA YAPANIA KUCHUKUA KATA ZOTE SITA KANDA YA KASKAZINI.

CHADEMA YAPANIA KUCHUKUA KATA ZOTE SITA KANDA YA KASKAZINI.



KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA KATIKAI AKIMKABIDHI VIFAA VYA AWALI MWENYEKITI  WA CHADEMA KATA YA SUNGA JIMBO LA MLALO EDWARD NGEREZA ANAYESHUHUHIA NI KATIBU WA CHADEMA MKOA WA TANGA,JONATHAN BAWEJE.



KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA KATIKATI AKISISITIZA JAMBO KABLA YA KUKABIDHI VIFAA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA KITONGOJI CHA LUANDE KATA YA KIOMONI  MWANAMTAMA BAKARI KUSHOTO NA KULIA NI KATIBU WA CHADEMA MKOA WA TANGA,JONATHAN BAHWEJE.

WANACHAMA WA CHAMA HICHO MKOANI TANGA WAKIMSIKILIZA KATIBU WA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AMBAYE HAYUPO PICHANI LEO

KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AKISISITIZA JAMBO LEO.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)kimesema kuwa licha ya kuwepo msuguano wa ndani lakini kimetamba kuwa kitachukua kata zote sita zilizopo kanda ya kaskazini katika uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni hapa nchini. 

Uchaguzi huo wa marudio unatokana na kata za Kiomoni,Mtae mkoani Tanga na Sombetini mkoani Arusha,Kiborolioni mkoani Kilimanjaro na Karachimbi Kiteto mkoani Manyara kutokuwa na madiwani wake kutokana na baadhi yao kujiuzulu na wengine kufariki dunia.

Tambo hizo zilitolewa na Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini,Amani Golugwa wakati akizungumza na viongozi wa chama hicho mkoani hapa kwenye mafunzo ya Chadema ni msingi ambayo yalikuwa na lengo la kuwajengea uwezo pamoja na kukabidhi vifaa vya awali vya kampeni kwa kata zinazokabiliwa na uchaguzi huo ambazo ni Kiomoni na Mtae

Golugwa alisema vifaa hivyo vimetolewa kwa awamu ambapo awamu ya pili watakabidhi pikipiki ili viongozi wa chama hicho waweze kutimiza wajibu wao ipasavyo na hatimaye kuweza kupata ushindi kwenye chaguzi hizo.

Alisema chama hicho kitaingia kwenye mchakato huo kwa kuangalia wanachama ambao watakao kuwa na uwezo wa kuipeperusha bendera yao kwa kuweka wagombea wanaokubalika kwa wananchi kwenye kata zao.

Katibu huyo alisema kuelekea kwenye mchakato huo aliwataka wanachama kuwa na mshikamano wa dhata ambao utakiwezesha chama hicho kupata ushindi na kuacha kutengeneza makundi yasiyo na tija.

   “Tunataka kutengeneza historia kwa madiwani wawili kwenye jimbo la Tanga na kata nyingine zilizopo mikoa ya kanda ya kaskazini “Alisema Golugwa.

Akizungumzia mafunzo hayo,Golugwa alisema mafunzo hayo ya siku mbili yana lengo la kuwajengea uwezo wanachama wake mkoani Tanga pamoja na kukiimarisha chama hicho kuelekea uchaguzi ujao.

Waliopokea vifaa hivyo ni Mwanamtama Bakari ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema kitongoji cha Luande kata ya Kiomoni Jimbo la Tanga na Edward Ngereza wa Kata ya Mtae Jimbo Mlalo wilayani Lushoto
0 comments

PAPA FRANCIS ADAIWA KUTOROKA USIKU MAKAO YA VATICAN

PAPA FRANCIS ADAIWA KUTOROKA USIKU MAKAO YA VATICAN

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amedaiwa kutoroka usiku Makao Vatican ili apate fursa ya kwenda kutoa misaada kwa walemavu na watu wasiojiweza.

Tetesi za Papa Francis kuwatembelea maskini hao usiku kwa kujificha zimekuja baada ya mahojiano yaliyofanywa na Askofu Mkuu, Konrad Krajewski ambaye kazi yake kubwa ni kukusanya fedha toka kwa wasamaria wema na kuwapelekea maskini.

Imeelezwa kuwa Askofu Krajewski amekuwa akiambatana na Papa Francis wakati mwingine na kwenda kuwapa misaada maskini maeneo ya vijiji, mjini Vatican.

Askofu Krajewski alisema tangu zamani alipokuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires, Papa Francis amekuwa akipenda kwenda mijini nyakati za usiku na kuwatembelea wenye shida mbalimbali.

“Amekuwa akionyesha dalili ya kupenda kunisindikiza kwenda kuwapa misaada maskini, pindi nikiondoka kwenda kufanya kazi hiyo,” alisema Padri Krajewski.

Hata hivyo, alipoulizwa iwapo Papa aliwahi kwenda naye nje ya mji kwa ajili hiyo, Askofu Krajewski, alisita kujibu swali hilo.

Wakati huohuo, gazeti la Huffington Post limeripoti kuwa walinzi wa Uswisi, wamethibitisha kuwa Papa amekuwa akizunguka maeneo mbalimbali usiku akiwa amevalia mavazi ya kawaida ya wachungaji na kuwapa misaada, wanaume na wanawake wenye shida mbalimbali.

Tangu kuteuliwa kwake, papa Francis amevipamba vichwa vya habari duniani baada ya kuonekana akijaribu kuvaa kofia za polisi wa zimamoto, kuwaruhusu vijana wadogo wa kiume kuibusu miguu yake na kuwapigia simu waumini wake na kuzungumza nao.

Hivi karibuni, aliripotiwa katika vyombo vya habari akiwabusu na kuwafariji waumini walemavu katika Kanisa la Mtakatifu Peter, huku taarifa nyingine zikionyesha kuwa ametuma fedha zake binafsi kwa wahamiaji na wanaohangaikia mafao yao.

Alipokuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires, Papa Francis alifahamika kwa kutoroka usiku na kuwatafuta watu, kuzungumza nao na wakati mwingine kuwanunulia chakula.

Mapapa wengine waliopita pia wametajwa kutoroka usiku, kwa mfano papa John wa X111 alikuwa na tabia ya kutoroka usiku na kwenda mitaa ya Rome kufurahia uzuri wa jiji hilo, wakati Papa Pius wa X11alivalia kama Mfaransa wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia na kwenda mipakani kuwasaidia Wayahudi wa Kirumi kisha kuwaweka katika sehemu salama.
0 comments

SINTAH AMUUNGA MKONO FLORA LYIMO KWA JINSI ANAVYOTANGAZA BIASHARA YAKE MTANDAONI

SINTAH AMUUNGA MKONO FLORA LYIMO KWA JINSI ANAVYOTANGAZA BIASHARA YAKE MTANDAONI

Alichokiandika Sinta Kuhusu Jinsi Flora lymo anavyotangaza Biashara online:
Biashara ni matangazo na inapendeza sana ukiitangaza mweyewe muhusika kwa mfano mie nauza wedding dresses kutwa natangaza humu na navaa pia, na yeye Flora anauza  mother's union  so mpeni deal masela akamate mahela na hii xmass inakuja anakusafirishia buree kabisa na fasta, Mother's union oyeahhh

biashara ni matangazo na na itakuzika wewe mwenyewe ukiitangaza na kutuonyesha mfano kama utapendezaje ukiivaa, sasa ushatangaziwa Mother's union sasa kazi ni kwako kuagiza white, pink or red light special.

ciao 


nipo busy ku advertise my business
wedding dresses
0 comments

SINEMA YA BABY MADAHA NA DIAMOND BADO INAENDELEA,DIAMOND NAE AFUNGUKA NA KUMPONDA BABY MADAHA

SINEMA YA BABY MADAHA NA DIAMOND BADO INAENDELEA,DIAMOND NAE AFUNGUKA NA KUMPONDA BABY MADAHA

ACHANA na mabifu yaliyotangulia, hili ni jipya kabisaa! Msanii wa sinema na Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ameingia kwenye bifu zito na Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kudai staa huyo wa Wimbo wa Number One ni mzinzi ‘fuska’, Amani lina mkanda mzima. 


Bila kumung’unya maneno, mapema wiki hii, Baby Madaha alimvaa Diamond ambaye ni Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB) akimtuhumu kuwa na tabia za kifuska.
Baby Madaha alidai hata muziki anaoufanya Diamond kamwe hauwezi kulingana na mafanikio makubwa ya jina lake zaidi ya kubebwa na skendo tu.

CHOKOCHOKO ZILIVYOANZA
Kupitia mitandao ya kijamii, ilivuja posti ambayo ilidaiwa kutoka kwa Baby Madaha ikimpaka Diamond kuwa siyo mwanamuziki kama ilivyo kwa wasanii wengine wenye uwezo mkubwa, akitolea mfano Elias Barnaba wa THT.
Sehemu ya posti hiyo ilionesha kuwa, Diamond si msanii wa muziki bali ni mzinzi f’lani hivi anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.

“Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapojitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond, huo ndiyo utakuwa mwisho wa maisha yake kimuziki kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaporomoka,” ilisomeka posti hiyo.
UKWELI NI UPI?
Baada ya ishu hiyo kugeuka habari ya mjini na kuibuka kwa makundi mawili yanayokinzana, Amani lilimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa posti hiyo ndipo akatiririka aya za kuthibitisha kuwa picha haziivi, hamkubali Diamond na kudai hata kimuziki hamkubali kwani anaamini wapo wanamuziki wanaofanya vema katika gemu kuliko yeye.

“…tuseme ukweli, Diamond ni mfanyabiashara siyo mwanamuziki. Kuhusu hiyo posti iwe ni mimi nimeandika au si mimi lakini kimsingi hayo maneno yanamstahili kabisa. Mzinzi tu.
“Diamond anabebwa na media (vyombo vya habari). Kuna wanamuziki wengi wazuri sembuse yeye? Ana nini haswa?” alihoji Baby.

AMANI LAMGEUKIA DIAMOND
Baada ya kusikia maelezo ya Baby kwa kifupi, Amani lilimuweka ‘pending’ kwa muda na kumwendea hewani Diamond ili liweze kujua upande wake analizungumziaje bifu hilo ambalo lilikuwa likienea mitandaoni kama moto wa kifuu.
Tofauti na matarajio ya mapaparazi wetu kwamba huenda angejibu mashambulizi makali kwa Madaha, Diamond au ‘Sukari ya Warembo’ aling’aka huku akimponda mwanadada huyo na kumshangaa:

DIAMOND SASA
“Daaah! Huko ni kunishusha…mimi na huyo (Baby) wapi kwa wapi kamwe huwezi kunilinganisha na mtu ambaye yupo chini yangu sana, nikijibizana naye nitajishusha tu. Ingekuwa ni mtu mkubwa mwenye levo yangu hapo ningesema natakiwa kusema neno.
“Hana lolote huyo anatafuta ‘kiki’ tu kupitia mimi, nipo na dili zangu za maana nipoteze muda kwake? Atafute wa levo yake na wala si mimi.”

UZINZI VIPI?
Alipoulizwa kuhusu suala la uzinzi ambalo Baby Madaha aliumaanisha katika posti yake, Diamond aliendelea kukazia kuwa hana muda wa kupoteza kwa mtu kama Baby Madaha ambaye kimsingi ni kama ardhi na mbingu.
“Huyo anatafuta kiki tu, aachane na mimi…mbona hatufanani kabisa mimi na yeye wapi kwa wapi?” alikazia Diamond a.k.a Weka Mbali na Watoto Wazuri wa Kike.

BABY AREJEA HEWANI
Wakati mapaparazi wetu wakimalizana na Diamond, kilongalonga kimoja cha paparazi wetu kilikuwa kikionesha kinaita, ilivyokatika ya Diamond, Baby akapanda hewani kwa mara nyingine.

Safari hii alimchana laivu: “Nimeisoma upya posti yenyewe, kilichopo humu ni ukweli mtupu. Hakuna hata tone la uongo, wewe utamlinganisha Diamond na mtu kama Barnaba? Huyu ni mfanyabiashara tu, hajui kuimba kwa kutumia vyombo kama mimi.
“Diamond hawezi kupiga chombo hata kimoja cha muziki atajiitaje mwanamuziki? Anastahili kabisa ujumbe huu.”

UFUSKA
Mapaparazi wetu walilazimika kumtwanga swali Baby Madaha kuhusiana na ufuska ambao ulikuwa umetajwa katika maelezo ya awali, kama endapo Diamond ni mzinzi au yeye ndiyo mzinzi.
Katika maelezo yake, Baby Madaha aliwashangaza mapaparazi wetu kwa kutaja namna gani anaweza kumuita Diamond mzinzi. Sikia:

Amani: “Umesema Diamond si mwanamuziki, je, suala la uzinzi ni nani analo kati yako na yeye?”
Baby: “Mimi si mzinzi. Diamond ndiyo mzinzi tena sana tu.”
Amani: “Uzinzi wake upo wapi?”
Baby: “Kitendo cha kubadilisha wanawake, kufumaniwa na Wema Sepetu akiwa na Jokate Mwegelo ndiyo uzinzi wenyewe huo.”

Amani: “Kwani wewe hujawahi kuwa na wanaume tofauti? Hujawahi kufumaniwa?”
Baby: “Mimi sijawahi, yeye amewahi na hakuwahi kukanusha hivyo inadhihirisha kuwa ni kweli. Kwangu mimi kila aliyetajwa kutoka na mimi kama haikuwa kweli, nilikanusha mara moja yeye mbona hakanushi?”
Amani: “Kwani Diamond alifumaniwa na nani?”
Baby: “Acha hizo, kwani hukumbuki kipindi cha Wema? Mara alinaswa na Aunt mara na… yule ndiyo mzinzi sasa.”

KWANI WALITONGOZANA?
Kuhusu suala la kutongozwa, Baby alisema Diamond hajawahi. Cha kushangaza zaidi, alisema hata kama ikitokea siku staa huyo akamtongoza kamwe hawezi kumkubalia kwani hawaendani hata kidogo.
Alisema yeye ni mtu wa kutembea na vigogo na si vitoto kama Diamond.

“Hana hela, kamwe siwezi kumkubalia. Ni mtu ambaye ana vihela mbuzi sasa mtu kama yeye mimi wa nini? Ndiyo maana aliwahi kukimbiwa na mwanamke kwa kuwa hana hela.
“Tena yule mwanamke akaenda kwa kigogo mwenye hela, mimi na yeye ni mbalimbali kabisa. Hata muziki ninaofanya hauwezi, mimi ninaimba RnB yeye anafanya Pop, tuko tofauti kabisa,” alisema Baby pasipo kumtaja mwanamke aliyemkimbia Diamond.

TUJIKUMBUSHE PANDE ZOTE
Diamond aliwahi kuripotiwa kutoka kimapenzi na ‘totoz’ kibao wakiwemo yule wa mwanzo aliyemzingua aitwaye Sarah, Rehema Fabian, Jacqueline Wolper, Upendo Mushi ‘Pendo wa Maisha Plus’, Wema Sepetu, Natasha (Video Queen wa Wimbo wa Moyo Wangu), Najma (aliwahi kuwa mpenzi wa Mr. Blue), Jokate Mwegelo, yule demu wa Kenya na aliyekuwa mwigizaji aliyefulia ambaye ni mke wa mtu.

Kwa upande wake Baby Madaha anayekimbiza na ngoma yake ya Summer Holiday
0 comments

Magazetini leo December 05 2013,

Magazetini leo December 05 2013,


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger