Featured Post Today
print this page
Latest Post

NGASSA ALIVYOWASILISHA MILIONI 45 ZA SIMBA TFF SIKU YA IJUMAA JIONI

NGASSA ALIVYOWASILISHA MILIONI 45 ZA SIMBA TFF SIKU YA IJUMAA JIONI


Mshambuliaji wa Yanga SC, Mrisho Khalfan Ngassa (katikati) akiwa ameshika risiti ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kulipa Sh. Milioni 45, alizotakiwa kuilipia klabu ya Simba SC. Wengine kulia ni Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto na kushoto Mhasibu, Rose Msamila. Ngassa alifungiwa mechi sita za mashindano na TFF pamoja na kutakiwa kurejesha fedha za Simba Sh. Milioni 30 na fidia ya Sh. Milioni 15, baada ya kubainika alisaini timu mbili, Simba na Yanga alikoidhinishwa kuchezea msimu huu.

Ngassa akiwa ndani ya ofisi za TFF wakati anaandikiwa risiti baada ya kulipwa fedha

Ngassa akionyesha cheki alizokwenda kulipa TFF

Wapambe; Wanachama wa Yanga, Kaisi na Shamte kushoto walimsindikiza Ngassa leo

Risiti ya TFF

Cheki za Milioni 45
0 comments

Wengine wanasoma shule za gharama na wenzao wana choma mkaa, ajira za watoto zipo kwa wingi hapa nchini serikali ijitathimini upya kuhusu hili.

Wengine wanasoma shule za gharama na wenzao wana choma mkaa, ajira za watoto zipo kwa wingi hapa nchini serikali ijitathimini upya kuhusu hili.



Mtoto ambaye hajaweza kupatikana jina lake mara moja akijishughulisha na kazi ya uchomaji mkaa, kama alivyokutwa maeneo ya Kwachaga, wilayani Handeni mkoani Tanga. 
Mtoto kama huyu anastahili kutumia muda mwingi kusoma na sio kufanya kazi ya matanuri huku akiifanya kazi hiyo kwa kurithi kwa familia yake au sehemu nyingine ya jamii kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maisha yake ya kila siku. Picha na Kambi Mbwana.
0 comments

HIVI NDIO HALI YA JENGO LA WESTGATE BAADA LA SHAMBULIO LA AL-SHABAAB.

HIVI NDIO HALI YA JENGO LA WESTGATE BAADA LA SHAMBULIO LA AL-SHABAAB.

Picha za nje ya jengo la Westgate hazioneshi uhalisia wa hali iliyoko ndani ya jengo baada ya shambulio la kigaidi Jumamosi iliyopita jijini Nairobi, Kenya na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 70.

a7
Picha hizi zinatoa picha halisi ya jinsi jengo hilo lilivyoharibika vibaya kwa ndani baada ya ghorofa tatu za jengo hilo kudondoka baada ya kupigwa mabomu katika mchakato wa kukabiliana na magaidi. 
a6
Picha hizi pia zinaonesha jinsi magari yaliokuwepo eneo la maegesho ya magari katika jengo hilo yakiwa yameharibiwa kiasi kwamba kuna mengine ambayo huenda hata wamiliki wanaweza kushindwa kuyatambua.
a1
a2
a3
a4
a5
a8
0 comments

Sheikh Sharrif Ahmed; Rais Anayedhibiti Maeneo Jirani Na Ikulu..

Sheikh Sharrif Ahmed; Rais Anayedhibiti Maeneo Jirani Na Ikulu..

shehki_871e3.jpg
Ni Rais wa Somalia. Kwa hakika, kwa sasa ndiye Rais wa nchi ya Kiafrika mwenye wakati mgumu sana. Na katika shida zake, Sheikh Sharrif ameonekana, si mara moja, akitua Dar Es Salaam, kwenye Ikulu ya JK. Kwa Sheikh Sharrif aliye matatizoni, kufunga safari ya Dar kwa JK ni kama kwenda kwa Obama! Kuna tofauti kubwa na Mogadishu.
Kiukweli Sheikh Sharrif Ahmed hana eneo kubwa la nchi ambalo anaweza kusema kuwa analidhibiti. Kuna wakati ikasemwa, kuwa anadhibiti maeneo jirani tu na Ikulu yake ya Mogadishu. Huko kwengine kuna ' Mabwana wa Vita'.
Na sasa ni ' pasua' kichwa ya Al shabaab. Tofauti na inavyoonekana nje, Al shaabab hawajawa na nguvu za kutisha sana. Isipokuwa, wakiachwa wakue, ni ' pasua' kichwa si tu kwa Somalia, bali kwa nchi zetu hizi.

Shambulizi la Wastgate ni ishara za Al Shabaab wanaoanza kuota mapembe. Kuna mantiki ya Marais wa nchi jirani na Somalia ikiwamo Tanzania, chini ya mwevuli wa AU na UN, kufanya jitihada za kuungana katika kupanga mikakati ya kumsaidia Sheikh Sharrif Ahmed.
Wamsaidie ili Somalia itawalike. Na kwa kufanya hivyo, kutaharakisha vita ya kuisambaratisha Al Shabaab, ambayo kimsingi, haina sapoti ya Wasomalia wengi.
Wikiendi Njema.
Maggid.

0 comments

Nawashukuru kwa kuniombea:Awila Silla

Nawashukuru kwa kuniombea:Awila Silla

20130923_113144_187fa.png
20130923_113248_89d98.png
Mlinipenda, mkanijali na kunithamini sana katika taabu na mateso makali ya mapanga siku 17 zilizopita. Namshukuru kila mmoja aliyetaabika na kuamua kuteseka kwa sala kwa ajili yangu na katika kila hali, hakika Mungu amependezwa na kusikia. Mungu ni mwema naendelea vyema kama mnavyoniona. Sina cha kuwalipa Mungu awaone katika kila hitaji na hatua za maisha yenu.Na Awila Silla 


0 comments

meza ya magazeti leo jumamosi

0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger