Featured Post Today
print this page
Latest Post

WANAODAIWA KUWA NI WAVUVI HARAMU WAPOTEZA MIKONO, MACHO BAADA YA KULIPUKIWA NA MABOMU YAO WAKATI WAKIVUA

WANAODAIWA KUWA NI WAVUVI HARAMU WAPOTEZA MIKONO, MACHO BAADA YA KULIPUKIWA NA MABOMU YAO WAKATI WAKIVUA

Baadhi ya majeruhi waliolipukiwa na baruti jana wakati wakivua samaki kwa kutumia baruti katika Kisiwa cha Karange tarafa ya Pongwe wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo huku wakiwa wamepoteza baadhi ya viungo vikiwemo macho na mikono. (Picha na Elizabeth Kilindi)
 Baadhi ya majeruhi waliolipukiwa na baruti jana wakati wakivua samaki kwa kutumia baruti katika Kisiwa cha Karange tarafa ya Pongwe wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo huku wakiwa wamepoteza baadhi ya viungo vikiwemo macho na mikono.
 Baadhi ya majeruhi waliolipukiwa na barutiwakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo huku wakiwa wamepoteza baadhi ya viungo vikiwemo macho na mikono.
  Mmoja wa majeruhi waliolipukiwa na baruti wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo huku wakiwa wamepoteza baadhi ya viungo vikiwemo macho na mikono. 

Elizabeth Kilindi, Tanga
Wakazi wawili wa kata ya Tangasisi tarafa ya Pongwe wilayani Tanga wamejeruhiwa vibaya viungo mbalimbali vya mwili  kwa kulipukiwa na baruti wakati wakivua kwa kutumia dhana za uvuvi haramu kwenye kisiwa cha Karange.

Tukio hilo limetokea mnamo Novemba 12 mwaka huu majira ya saa nane mchana katika kisiwa  ambapo majeruhi hao wakiwa kwenye ngalawa yenye namab za usajili TTA 315 wakati wakijianda kutegesha baruti hizo ndipo zilipowalipukia.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga Freisse Kashai amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja majeruhi hao kuwa ni Hamis Omari ambaye amekatika mkono wa kulia na ameumia jicho la kulia, huku majeruhi mwingine Adamu Selemani amekatika mikoni yote miwili, pamoja na kupoteza macho yote mawili.

“Hali ya majeruhi wote wawili ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo ni mbaya hii inaonyesha ni kwa kiasi gani uvuvi haramu ulivyo na madhara makubwa kwa jamii pamoja na viumbe wa baharini “alisema Kamanda Kashai.

Kamanda Kashai alitumia fursa hiyo kuwa taka wakazi
wanaoishi maeneo ya bahari kutoa taarifa ya watu wanaojihusisha na uvuvi haramu ili kuweza kuwachukulia hatua mapema kabla ya kutokea kwa madhara zaidi.
0 comments

Upekee wa Hifadhi ya Saadani usiotangazwa

Upekee wa Hifadhi ya Saadani usiotangazwa


Kila hifadhi ya taifa ina upekee wake. Na hicho hukifanya kuwa kivutio kwa watalii. Hifadhi ya Taifa ya Saadani ina vivutio vya kihistoria kama vile wanyama, mito na bahari. Nadhani ni hifadhi pekee inayoweka pamoja vivutio vyote.
Kihistoria Hifadhi ya Saadani inapakana au kuhifadhi miji ya kihistoria kama Saadani wenywe, Utondwe, Kipumbwi na Mkwaja, Pangani, Buyuni Ukuu na Buyuni Kitopeni ambayo ingawa sasa haijulikani tena.
Katika zama zake ilikaribisha wageni wa kimataifa, au kuwa miji ya kibiashara (ya maliasili na watumwa) na kuwakaribisha wakoloni na kujenga miji.
Saadani ulikuwa mji mkubwa sana wakati wa ukoloni


 wa Wajerumani na pia kaburi la yule mmishenari maarufu aliyekuja kueneza Ukristo, hasa Mombasa, Tanga na Kilindi, Johannes Rebmann liko hapo hadi leo.
Hadi leo Kipumbwi bado ni bandari muhimu ya majahazi inayounganisha Wazanzibari na Watanganyika kwa kufanya safari kati ya kijiji hicho cha pwani na bandari kuu ya awali – Mkokotoni. Safari hizo ziko kila siku.
Miji ya Pangani, Bagamoyo na kijiji kilichopotea cha Utondwe vina mpatia fursa mtalii kuvifikia wakati anapotembelea hifadhi hiyo.
Utondwe unaandikwa na Wareno kama mji wa mashamba ya chumvi na askari wa Kizaramo wapiga mishale wazuri. Ushahidi ni msikiti wa kale uliopo hadi sasa huko Kitame, ingawa hautumiki.
Saadani ni hifadhi inayopakana na mito mitatu. Ruvu uko mbali lakini kuna Pangani na Wami. Mito hii mitatu kwa pamoja hukutana huko baharini na kutengeneza mkondo hatari wa Nungwi unaoleta vurugu katika majira fulani fulani.
Serikali ya Zanzibar kama ingekuwa na uwezo wa kifedha ungeweza kutengeneza bomba la kuvuta maji baridi kutoka kwenye kine kirefu cha Nungwi, yanayotokana na Ruvu, Wami na Pangani, mito mitatu inayopangana na hifadhi ya Saadani.
Pia, ndani ya mito hiyo unajifunza maisha na uhifadhi unaofanyika wa maisha ya majini na baharini ya wanyama na mimea.
Wakati ukiwa Mto Wami unajifunza maisha ya baharini na wanyama wake, Mto Pangani una hifadhi kubwa ya mapito ya kihistoria na biashara- utumwa, katani, mali ya asili, hasa meno ya tembo na nazi mbichi na mbata.
Ukisafiri katika Mto Pangani hadi huko ndani nchi kavu unakutana na vituo vya kihistoria ikiwamo mahali Bushiri bin Salim alipoishi, Matakani na Kijiji cha Bushiri.
- Mwananchi
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger