Featured Post Today
print this page
Latest Post

SIMBA SC WAZUIWA KUCHEZA NA ASHANTI KESHO HADI WALIPE MILIONI 25, ‘MPIGANAJI’ RAGE AINGIA MSITUNI KUINUSURU KLABU

SIMBA SC WAZUIWA KUCHEZA NA ASHANTI KESHO HADI WALIPE MILIONI 25, ‘MPIGANAJI’ RAGE AINGIA MSITUNI KUINUSURU KLABU

Na Mahmoud Zubeiry, Posta
SIMBA SC imetakiwa kulipa Sh. Milioni 25 kama gharama za uharibifu wa viti katika vurugu ambazo mashabiki wa timu yake walifanya timu yao ikimenyana na Kagera Sugar, Oktoba 31, mwaka huu Uwanja wa taifa, Dar es Salaam na kutoka sare ya 1-1.
Adhabu hiyo imetolewa na Bodi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na tayari Simba SC wamekabidhiwa barua- na wameambiwa hawataruhusiwa kukanyaga nyasi za Uwanja wa Taifa kesho kumenyana na Ashanti United kabla ya kulipa fedha hizo.
Ustadh umeiponza timu kulimwa faini ya Sh. Milioni 25, unaisaidiaje sasa?

Lakini Simba SC wameistaajabu barua waliyopewa wakisema ina mapungufu kwa sababu haina mchanganuo wowote na mbaya zaidi muda uliobaki ni mchache kuelekea mechi ya kesho- maana yake hautatoa fursa ya mjadala.
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage sasa anataka kutumia kipaumbele chake cha kuwa Mbunge (Tabora Mjini CCM) akiwa na uwezo wa kuzungumza moja kwa moja na Mawaziri, kujaribu kuifanya adhabu hiyo isifanye kazi kesho hadi hapo mijadala itakapochukua nafasi.
Kikubwa Simba SC wanasema barua haina michanganuo na hata wakitafakari uharibifu ulitokea wanaona hauendani na gharama wanayotakiwa kulipa. BIN ZUBEIRY inafahamu Simba SC haina nia ya kuepuka adhabu, bali inataka mchanganuo ili kujiridhisha.
Rage anapambana adhabu isifanye kazi kesho


Pamoja na hayo, Simba SC wanalalamika kupewa adhabu mara mbili- kwanza wanachama wake wamekamatwa na sasa wapo Rumande kutokana na vurugu hizo, na wakati huo huo wanatakiwa kulipa gharama za uharibifu.
Simba SC wenyewe wanaamini hii ni sawa na kuadhibiwa mara mbili, jambo ambalo wanasema ni kinyume cha sheria.
Baada ya Kagera kusawazisha bao dakika ya pili ya muda wa nyongeza baada ya kutimia kwa dakika 90 na kupata sare ya 1-1, Uwanja wa Taifa, uligeuka eneo la vita baina ya Polisi mashabiki wa Simba SC.
Baada ya Salum Kanoni kukwamisha nyavuni mkwaju wake wa penalti, mashabiki wa Simba waliokuwa viti vya Rangi ya Bluu na Chungwa, walianza kung’oa viti na kuvitupia uwanjani.
Lakini hakuna wasiwasi, ikishindikana mwenye Simba yake, Zacharia Hans Poppe atalipa, Milioni 25 kitu bwana!

Malalamiko ya Simba SC ni kwamba, mchezaji aliyesababisha penalti ya Kagera aliuingiza mpira kwa mkono katika eneo la hatari na akajiangusha- lakini refa akatoa penalti. Na katika mchezo huo huo refa huyo huyo aliwanyima penalti Simba SC baada ya beki wa Kagera kuushika mpira kwenye eneo la hatari.
Mara baada ya viti kuanza kurushwa, Polisi walianza kupambana na mashabiki hao kwa kuwatupia mabomu ya machozi, ndipo wakaanza kukimbia. Makocha na wachezaji wa Simba kwa pamoja waliwafuata waamuzi kuwalalamikia- hali ambayo ilifanya watolewe kwa kusindikizwa na Polisi.
Bao la Simba lilifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amisi Tambwe dakika ya 45 baada ya kupokea pasi nzuri ya Betram Mombeki na kumpiga chenga beki Salum Kanoni, kabla ya kumchambua kipa Hannington Kalyesebula.
Wakati Simba inatozwa faini ya Sh. Milioni 25, yenyewe ilipata mgawo wa Sh. 7,242,252.45 kutokana na jumla ya Sh. 32,726,000 zilizopatikana kwenye mechi hiyo.
Ligi Kuu inatarajiwa kuendelea kesho kwa JKT Ruvu kumenyana na Coastal Union, Ashanti United na Simba, Kagera Sugar na Mgambo Shooting, na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar, wakati keshokutwa Azam itacheza na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons hizo zikiwa mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza.
0 comments

MWENYEKITI CCM WILAYA YA TANGA AWAAGIZA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KWA UKARIBU.

MWENYEKITI CCM WILAYA YA TANGA AWAAGIZA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KWA UKARIBU.

Na Amina Omari,Mzizima.
Mwenyekiti wa Chama Chama Mapinduzi Wilaya ya TangaKassim Mbuguni amewaagiza watendaji wa mitaa,vitongoji na kata kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo kwa ukaribu katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama hicho  na kama wakishidwa waachei ngazi.

Agizo hilo alilitoa wakati wa uzinduzi wa shina la Vijana wa nguvu

kazi wa  Chama Cha Mapinduzi UVCCM kata ya  Mzizima mwishoni mwa wiki ambapo alisema kuwa haiwezekani kuwa na watendaji ambao hawasimami wa kutekekeleza ilani ya chama.

Alisema kuwa ifike mahali ni lazima tuwe na watendaji ambao

tunaendanao kwenye maamuzi yetu sio kuwa na ambao wanatupinga na kurudisha nyuma maendeleo pamoja na kasi katika kuwasogezea huduma wananchi.

“Salamu nazitoa kwa watendaji ambao watashindwa kusimamia na

kutekeleza miradi wajitoe wenyewe,Ni aibu kwa mtendaji wa mtaa
kushindwa kusimamia mradi mdogo wa darasa moja la shule halafu
unajiita mtendaji hutufai katika mbio zetu za kuleta maendeleo jitoe
mapema kabla hatujakutoa kwa nguvu”Mbuguni.

Pia aliwashauri watendaji hao kuacha kukaa ofisi pekee na kusubiri

taarifa kwenye makaratasi bali wahakikishe wanashuka hadi katika ngazi za chini za wananchi na kusikiliza kero zinazowakabili ili kuzitafutia ufumbuzi wa haraka .

Aliongeza kuwa sifa ya kiongozi bora aliyechaguliwa na wananchi ni
kuhakikisha anawasikiliza na kuwatatulia kero zao wanazokabilianazo waliomchangua na sio kusubi maamuzi kutoka ngazi za juu pekee.

“Nawapa taarifa nitaanza kupita kuanzia ngazi za mitaa,kata na

vitongoji katika Jiji hili na  kukagua maendeleo na changamoto
zilizopo Na jinsi zilivyotatuliwa na viongozi wa serikali nitakapo
baini mapungufu hatabaki mtu nitamtoa kwa aibu “alisisitiza Mbuguni.


Katika Hatua nyingine alimuagiza Diwani wa Kata hiyo Daniel Mgaza
  kuhakikisha na maliza kabisa changamoto ya ukosefu wa maji na umeme katika kata hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ili wananchi hao wasiendelea kuteseka na kero hizo.

Alisema kuwa diwani ni ndio msimamiaji sera na ndiuo aetetea wananchi
katika kata yake hivyo tatizo la maji na umeme kuikabili kata hiyo tena ipo mjini ni jambo la aibu hivyo ni vemna ahakikishea ameimaliza mapema kero hiyo.
0 comments

HANDENI WATAKIWA KULITUMIA VEMA TAMASHA LA HANDENI KWA KUTAFUTA FURSA.

HANDENI WATAKIWA KULITUMIA VEMA TAMASHA LA HANDENI KWA KUTAFUTA FURSA.

Na  Mwandishi Wetu, Handeni.

MKUU wa wilaya Handeni, DC Muhingo Rweyemamu, amewataka wananchi wa Handeni, mkoani Tanga kulitumia Tamasha la Handeni kwa ajili ya kutafuta fursa za kimaendeleo.

Akizungumza jana mjini Handeni, Muhingo alisema kutokana na tamasha hilo kufanyika mwisho wa mwaka, Desemba 14, itakuwa chachu ya kuwaunganisha watu wote, sanjari na kujadili changamoto zinazoikabiri Handeni na Tanzania kwa ujumla.

Muhingo alisema kuwa tamasha hilo lina umuhimu mkubwa kutokana na kuandaliwa maalum kwa ajili ya Watanzania kwa ajili ya kuangalia ngoma na matukio mbalimbali ya kijamii.

“Wakati napongeza kwa dhati kuandaliwa kwa tamasha hili wilayani hapa, pia nawaomba watu waje kwa wingi kushuhudia namna gani Handeni imepiga hatua kimaendeleo na kuangalia namna gani wanaweza kusonga mbele.

“Naamini tutafikia hatua nzuri kwa kushirikiana na wadau wote, hivyo wale wanaoishi mbali na Handeni pia ni wakati wao kurudi nyumbani mwishoni mwa mwaka kujifunza mambo ya utamaduni wao, sanjari na kufanya juhudi za kupiga hatua kimaendeleo,” alisema.

Tamasha hilo linaloandaliwa na Mratibu wake Kambi Mbwana, hadi sasa limedhamiwa na Phed Trans, Clouds Media Group, Grace Products, Screen Masters na mtandao wao wa Saluti5.com, Dullah Tiles & Construction Ltd, Katomu Solar Specialist, PLAN B SOLUTIONS (T) LTD, Country Business Directory (CBD) na Michuzi Media Group.

Wengine ni duka la mavazi la Chichi Local Ware, Smart Mind & Arters chini ya Anesa Company Ltd, ikidhamini kwa kupitia kitabu chao cha ‘Ni Wakati Wako wa Kung’aa’, Lukaza Blog, Kajunason Blog, Jiachie Blog na Taifa Letu.com, huku likipangwa kuanza saa 2 za asubuhi hadi saa 12 za jioni.
0 comments

JK kulihutubia Bunge kesho

JK kulihutubia Bunge kesho



                            Rais Jakaya Kikwete.  (PICHA|MAKTABA)
 

Dodoma na Dar.

Rais Jakaya Kikwete, kesho anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Habari zilizopatikana Mjini Dodoma jana na kuthibitishwa na uongozi wa Bunge pamoja na Ikulu, Dar es Salaam zinasema atahutubia mchana.
Kutokana na ujio huo, Serikali imewaelekeza Mawaziri na Manaibu Waziri kutotoka nje ya Dodoma hadi hapo Rais atakapokuwa amehutubia Bunge. Kadhalika safari zote za Kamati za Bunge ambazo zilikuwa katika mchakato wa kutekelezwa zimeahirishwa hadi baada ya kesho, ili kutoa fursa kwa wabunge wote kuwapo wakati wa hotuba hiyo.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana kuwa hata yeye amesikia taarifa kuwa Rais atazungumza bungeni lakini hajui atazungumza kitu gani… “Hata mimi nimesikia kuwa atazungumza lakini sijui atazungumza jambo gani kwa kuwa siyo miongoni mwa watu wanaomwandalia hotuba,” alisema Balozi Sefue.
Kadhalika, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alithibitisha kuwa Rais Kikwete atalihutubia Bunge, Alhamisi… “Nathibitisha ni kweli, ila kwa taarifa nyingine watafuteni watendaji wa Bunge, kama Katibu wa Bunge nadhani wana taarifa zaidi.”
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alithibitisha jana katika Viwanja vya Bunge Dodoma kuwapo kwa ratiba ya Rais Kikwete kulihutubia Bunge na kwamba taarifa rasmi ingetolewa jana jioni kwa wabunge.
“Ni kweli Rais anatarajiwa kuja kulihutubia Bunge na leo (jana) jioni, tutatoa taarifa rasmi bungeni,” alisema Dk Kashililah.
Mara ya mwisho Rais Kikwete alilihutubia Bunge wakati akifungua rasmi Bunge la Kumi, Novemba 18, 2010 alipoeleza vipaumbele vya Serikali yake katika awamu ya pili ya uongozi wake. Rais Kikwete analihutubia Bunge wakati likisubiri kujadili mapendekezo ya marekebisho katika Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 2013 ambayo ilipitishwa katika mkutano uliopita.
Tayari Muswada wa Marekebisho unaopendekezwa umewasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa Bunge chini ya hati ya dharura na leo utajadiliwa katika Kikao cha Kamati ya Uongozi ili kupata kibali cha kuingizwa ndani ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala na baadaye Bungeni.
Dk Kashililah alisema amepokea muswada huo na kwamba uamuzi wa lini utafikishwa bungeni utafanywa na Kamati ya Uongozi ya Bunge ambayo itakutana na leo.
Kamati hiyo ndiyo yenye mamlaka ya kuifanyia marekebisho ratiba ya vikao vya Bunge na kuruhusu mambo yanayopaswa kuingizwa bungeni kujadiliwa.
Muswada huo ni matokeo ya majadiliano baina ya Serikali kwa upande mmoja na vyama vya siasa vyenye wabunge chini ya uratibu wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kwa upande mwingine, baada ya vyama vya siasa kutoridhishwa na muswada ulipitishwa katika mkutano wa Bunge uliopita.
0 comments

Naibu Meya na diwani wa kata ya Kiboriloni, Vicent Rimoy afariki Dunia

Naibu Meya na diwani wa kata ya Kiboriloni, Vicent Rimoy afariki Dunia

BREAKING NEWS:NAIBU MEYA MANISPAA YA MOSHI AMEFARIKI DUNIA....

Diwani Rimoy
Mwandishi Wetu, Kilimanjaro
NAIBU Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, (Chadema), Mhe. Vincent Rimoy (pichani), ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kiboriloni(chadema) amefariki dunia Ghafla Leo, majira ya saa 11:30 asubuhi akiwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC kupata matibabu.


Akizungumzia kifo hicho, Meya wa Manispaa ya Moshi, na  Mstahiki Jaffari Michael, alithibitisha taarifa za kifo hicho ambapo  alisema Mhe. Rimoy alifariki wakati akikimbizwa hospitali baada ya kudondoka akiwa shambani kwake eneo la Mandaka, wilaya ya Moshi.


“Ni kweli amefariki na muda siyo mrefu jamaa zake tayari wameshakwenda  kuuhifdhi mwili wa marehemu katika chumba cha kuhifadhia maiti cha  hospitali ya Rufaa ya KCMC”, alisema Meya huyo ambae pia ni Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Moshi Mjini.

 

Rimoy ambaye alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la Damu, alikutwa na umauti huo baada ya awali kufikishwa katika Zahanati ya Jaffar ambako alipewa huduma ya kwanza na Daktari wa Zahanati hiyo
ambaye hata hivyo alishauri apelekwe katika Hospitali ya KCMC kwa matibabu zaidi.

 

Kwa mujibu wa mmoja wa wafanyakazi wake ambaye hakutaka jina lake litajwe, Mhe. Rimoy aliamka asubuhi na kwenda shambani kwake baada ya kutoka safari ya Dar es Salaam juzi.
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger