Featured Post Today
print this page
Latest Post

KAZI IMEANZA, SIMBA SC YASAINI BEKI LA TAIFA STARS MIAKA MITATU...YANGA NA MAGAZETI YAO

KAZI IMEANZA, SIMBA SC YASAINI BEKI LA TAIFA STARS MIAKA MITATU...YANGA NA MAGAZETI YAO

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
KAZI imeanza. Simba SC imesajili mchezaji wa kwanza kabisa kwa ajili ya msimu ujao, ambaye ni chipukizi wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars Joram Nason Mgeveke.
Mchezaji huyo chipukizi pekee kutoka kikosi cha maboresho aliyebaki Taifa Stars chini ya kocha Mholanzi Mart Nooij, amesaini Mkataba wa miaka mitatu leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, Joram amesaini mjini Iringa na rasmi sasa ni mchezaji wa Simba SC.

Kifaa cha kwanza 2014-2015; Joram Mgeveke akipeana mikono na Hans Poppe baada ya kusiani Mkataba wa miaka mitatu na Simba SC. Chini anasaini.


“Tuna muda mfupi sana kwa ajili ya kufanya usajili, sasa tuna orodha ya wachezaji waliopendekezwa, kwa hiyo tunaanza kuwapandia ndege kuwafuata na kumalizana nao, ndani na nje ya nchi. Tumeanza na Joram, kwa sababu yuko Taifa Stars ambayo inakwenda kambini Botswana,”alisema Poppe.   
Poppe amewahakikishia wana Simba SC kwamba safari hii watasajili wachezaji bora ambao watarejesha heshima ya klabu hiyo msimu ujao.
Kwa upande wake, beki huyo mwenye misuli anayecheza nafasi za kati za ulinzi, amesema kwamba amefurahi mno kujiunga na Simba SC kwa sababu ni timu kubwa, ambayo anaamini itainua kiwango chake na kumfungulia milango zaidi ya mafanikio.
Joram Mgeveke wa pili kutoka kushoto waliosimama akiwa kikosini Stars dhidi ya Malawi

“Kwa kweli nimefurahi sana kujiunga na Simba SC, ni timu kubwa na ya kihistoria hapa Tanzania ambayo wamepita wachezaji wengi wazuri, ambao na mimi ningependea kufuata nyayo zao,”amesema.
Beki huyo alicheza kwa dakika 75 mechi ya kirafiki ya Tanzania na Malawi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambayo bao pekee la Amri Kiemba wa Simba SC liliipa Taifa Stars ushindi wa 1-0 kabla ya kumpisha Kevin Yondan wa Yanga.
Tangu hapo amekuwemo kwenye orodha ya wachezaji 18 walioshiriki mechi zote za Stars dhidi ya Zimbabwe kufuzu Mataifa ya Afrika kama mchezaji wa akiba.
Nyota Njema ndiyo iliyomuibua kinda huyo mwenye umri wa miaka 22, baadaye akachezea Polisi na Lipuli zote za Iringa, kabla ya kuchukuliwa timu ya mkoa, ambayo ilimfungulia milango ya kuingia Taifa Stars kupitia mpango wa maboresho. Katibu wa Lipuli, Willy Chikweo ametoa baraka zake zote juu ya usajili huo. “Kuanzia sasa, Joram ni wa Simba SC, kwa roho safi kabisa na tunamtakia kila la heri,”amesema katibu huyo.
Wakati Simba SC inafanikisha usajili wa mchezaji wa kwanza wa msimu ujao, watani wa jadi Yanga SC wanaendelea kupamba kurasa za magazeti kwa majina ya wachezaji tofauti ambao inadaiwa wanataka kuwasajili kutoka sehemu mbalimbali duniani.
Na wakati dirisha la usajili linafungwa mwishoni mwa mwezi huu, hakuna mchezaji hata mmoja ambaye hadi asa Yanga SC imesema rasmi imemsainisha Mkataba, huku ikiwa tayari imewapoteza Frank Domayo na Mrundi Didier Kavumbangu waliohamia Azam FC.
0 comments

MGIMWA ATUMIA USAFIRI WA BAISKELI KUWATEMBELEA WANANCHI



Mbunge wa  jimbo la Kalenga mkoani Iringa Godfrey Mgimwa akitumia usafiri wa Baiskeli kuwafikia wapiga kura wake katika kijiji cha Kivalali kata ya Ifunda baada ya gari lake  kupata pacha  wakati wa ziara hiyo hivyo kulazimika kutafuta baiskeli ili kufika haraka mkutanoni kusikiliza kero za  wananchi wake.(picha na Francis Godwin Blog) (P.T)
0 comments

KIINGLISHI KILIVYOWAGOMBANISHA ASKARI POLISI NA ASKARI WA MANISPAA YA MOSHI

KIINGLISHI KILIVYOWAGOMBANISHA ASKARI POLISI NA ASKARI WA MANISPAA YA MOSHI

Baada ya kuzunguka kwa muda mrefu raia huyu wa kigeni ambaye haikufahamika mara moja anatoka nchi gani aliketi katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi kisha akatoa Mkate huku akiulainisha na Jam na kuanza kula.
Alikula Silesi kadhaa lakini alionekana mwingi wa mawazo kila alipotafuna mkate .
Baadae akasukumia mkate na Maji ya Kilimanjaro.
Akafunga maji yake akayarudisha ndani ya begi lake.
Akaendelea kutafuna Mkate.
Akamuuliza mtu aliyekuwa jirani yake vipi unahitaji na wewe nikupatie kidogo na hii ilikuwa ni silesi ya mwisho.
Baada ya kupita muda mgeni huyo aliamua kuondoka eneo alilokuwa ameketi akipata mkate wake wa kila siku.
Ghafla nyuma yake akajitokeza askari wa manispaa ya Moshi (Mwenye t-shirt nyeupe) ambaye ana jukumu la kusimamia maswala ya mazingira.
Baada ya kufuatilia kwa kina ,ikagundulika kuwa askari huyo alikuwa anamfuatilia mgeni huyo akitaka kumtia mikononi kwa kosa la kutupa taka ambazo ni vipande vya mikate na kopo la Jam na kama unavyofahamu sheria za usafi kwa manispaa yetu ya Moshi.
Globu ya jamii ikabahatika kuona vipande vya mikate lakini ilipomuuliza askari huyo ni vipi mbona hajamkamata na kumpeleka kunako husika kama wafanyavyo kwa wabongo wenzao ,askari huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja alisema anataka kumkamata lakini hawaelewani lugha huku akidai kuwa yeye kimombo hakipandi akalazimika kwenda kuomba msaada kwa asakri polisi kata aliyekuwa katika kituo hicho cha mabasi.
Raia huyo wa kigeni akaondoka zake.
Kumbe askari yule wa mazingira aliyeenda kuomba msaada kwa askari polisi aliyekuwa katika kituo hicho cha mabasi alikutana na zahama nyingine wakati akiomba msaada kwa askari huyu anayeonekana hapa ya kupigwa makofi kwa madai aligoma kwenda kutoa msaada wa kumkamata yule raia wa kigeni kwa kuwa hajui "Kizungu",na hapa askari huyo aliamua kumueleza mwenzake (mwenye t-shirt nyeupe)aliyetambulika kwa jina la Mkude kuhusu tukio hilo ndipo Mkude kwa ghadhabu ya hali ya juu akaenda kuwakamata askari hao wa mazingira.
Wakati asakari hao wa mazingira wakifanya utaratibu wa kumakamata raia huyo wa kigeni ghafla walidakwa na Mkude wote wawili .
Kisha safari ya kwenda Kituoni ikaanza.
Ghafla Mkude baada ya kuona kamera ya globu ya jamii inammulika alimuamuru askari mwenzake kuikamata ,alakini hata hivyo askari yule alifahamu kuwa Globu ya jamii pia iko kazini kama walivyo wao.
Mzobe mzobe ukaendelea kupita katikati ya kituo kikuu cha mabasi huku mbinje za kutosha toka kwa wakatisha tiketi na wapiga debe zikirindima.
Askari Polisi.Mkude akafanikiwa kuwatia mikononi askari wa manispaa ya Moshi wanaoshughulika na mazingira hadi kituoni.Globu ya jamii ilifika hadi kituoni licha ya kwamba asakri wa kata aliyekuwa amevalia sare kudai kuwa yeye aliwasamehe lakini Mkude akiwa kituoni alisimamia msimamo wa kufunguliwa kwa kesi dhidi ya sakari hao.Hata hivyo baadae raia wa kigeni alionekana katika eneo la stendi akiranda randa.Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.
0 comments

DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOANGUSHA BONGE LA KAMUZI JIJINI BRUSSEL

DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOANGUSHA BONGE LA KAMUZI JIJINI BRUSSEL

 Diamond Platnumz akifanya mavituzz ukumbini na wacheza show wake wakiwa wanaendeleza manjonjo
 Waaaawwwoohh..ni umati haswaaa..kweli Diamond anapedwa
 Diamond Platnuz kijana mdogo mwenye mafanikio katika mziki na kimaisha akiimba wimbo wa nimpende nani
 V.I.P. table ilijumlishwa na viongozi mbalimbali,pichani ni mke wa Mh: wa Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi bwana Kamala aliyevalia nguo ya mizungo miyeusi na miyeupe
 Hapo sasa..Diamond Plutnumz akiendelea kukonga nyoyo za waliofika kumshughudia show yake
 Sema naeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..!! warembo toka Tz wakishangilia show ya Diamond ikiendelea.
                                                              OOOooyoooooooooooh
 Ooooooiiihhh!!! Ni peace n' Love toka kwa watoto wa nyumbani
 Umati wa watu wakiendelea kupata burudani ya muziki toka kwa msanii Diamond Platnumz
Ngololo aai ngololo mama  ngololo...... and show me how they do ngololo ngololo ni Saidi Biboze na dada yake Zuhra Biboze wakijiachia kwa raha zao.
 (Picha zote na Maganga One Blogger)
 (Picha zote na Maganga One Blogger)
0 comments
 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger