MAMLAKA YA MAJI SAFI NA MAJI TAKA MKOA WA TANGA YAPANIA KUBORESHA HUDUMA ZAKE



·       



 BWAWA LA MAJI MABAYANI AMBALO NDILO LINALOTEGEMEWA NA    WAKAZI WA JIJI LA TANGA.

Mamlaka ya maji safi na maji taka mkoa wa Tanga, Tanga UWASA inatarajia kuongeza mitandao ya usambazaji wa maji ktk baadhi ya maeneo ya jiji la Tanga, kwa lengo la kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo ya pembezoni mwa jiji la Tanga.
Hayo yamebainishwa hivi karibuni kwenye hafla ya kusimika bodi mpya ya mamlaka hiyo iliyofanyika hivi karibuni mkoani hapa na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na Serekali.
Maeneo yatakayonufaika kutokana na kuboreshwa kwa mitandao hiyo ya maji safi ni pamoja na Kange masiwani, Kange Mkurumuzi, Mwakidila C na baadhi ya maeneo ya mji wa Pongwe.
Kwa upande wa maji taka mamlaka imekwisha tenga fedha kwa ajili ya upanuzi ambao hadi sasa bomba la maji taka la barabara ya tano upo ktk hatua ya mwisho na pia ulazaji wa mabomba maeneo ya barabara ya Mnyanjani Lumumba kwa barabara ya 13 utafanyika mwaka huu wa fedha.
Mbali na maboresho hayo mamlaka hiyo pia inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji kupitia mpango wa maendeleo ya sekta ya maji ktk maeneo ya pembezoni mwa mji ambapo inatarajiwa ifikapo mwaka 2015, wakazi wote wa pembezoni mwa jiji la Tanga watakuwa wanapata maji safi na salama.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger